Kaka unasafilisha mali ya asili - Julius Nyerere International Airport -Yamenikuta ya ajabu na kweli

Wakati huohuo TWIGA walipitishwa hapo hapo JKNIA kwa kupandishwa ndege na kusafirishwa nje, ila hatusikii wakikamata wasafirishaji wa hizo nyara muhimu za serikali, nchi ina vituko sana hii.
Twiga ni huko KIA
 
Kuna nchi zao lolote haiingii. Ati mchele, ndizi nanasi etc
 
Tusiwe tunapoteza muda kwa mambo ya hovyo, kama tumeshindwa kuzuia madini ndio tuje tukomae na mbegu za mibuyu? nchi nyingi za Afrika zina mibuyu na wala haiwasadii chochote.
Hoja siyo mibuyu haiwasaidii kitu chochote, bali hoja ya msingi hapa ni kwamba wenzetu nchi zingine wanajali sana kuhusu suala la usalama wa Watu wao. Hizo mbegu za mbuyu unazowapelekea huko huenda unaweza kwenda kusababisha tatizo fulani la kiafya kwa Watu wao, Ila wewe msafirishaji wa mbegu hizo yawezekana haujui Hilo.
 
"Na niambia kama kuna Mtanzania aliepanda mbegu za ubuyu tokea tupate uhuru ?"

Hii kauli imeniacha hoi sna
 
Alitaka rushwa ila aliona una msimamo
Hongera
 
Kwa maelezo aliyoyatoa shida wala sio huko anakoelekea au usalama wa hizo mbegu, bali ni mali asili.
 
Kuna nchi zao lolote haiingii. Ati mchele, ndizi nanasi etc
Yes, hawataki kabisa kusikia Habari hizo. Tena Maafisa wa Afya na Udhibiti Ubora wa Vyakula waliopo kwenye Viwanja vyao vya ndege wako very serious kuhusu suala hili, wanasema wazi kabisa kwamba "Security of our people must be given the Top and Foremost Priority, strictly no food transmission without permit."
 
Kweli ni mali asili. Pili kuna nchi hawataki uingie na exotic plants au mbegu zake, zisije kuwa invasive species. Huyo mkaguzi alikuwa sahihi. Na kwa vile wabongo hawapandi mibuyu basi haimaanishi wengine hawapandi.
 
Ungemwambia kuna tembo na twiga wanasafirishwa KIA je analijua hilo?
 
Ila kuna regularions za kusafirisha vyakula. Hukawii kwenda kunyang'anywa huko unapoenda usiviingize kwenye hiyo nchi.

Watakuambia ni threat kwa health na safety ya walaji wa huko.
 
Jaman ww kaka umekuja mpaka huku? Si nlikua nakujarbu tuu nione kama unaweza kuniachia walau msimbazi !!!
 
Mimi niliambiwa mihogo mali asili lazima kibali, mihogo yenyewe nimepewa zawadi haifiki hata alfu 10 labda wakaanza kuniomba pesa sijui laki nikawaambia sitoi hata cent moja na mihogo waitupe tu au waichukue sina shida nayo, wakaona aibu na kuniachia
 
Alikua anataka akutingishe umpe kahela,, wengine hapo njaa tu wanakutafutia kasababu kokote tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…