Kama alivyotuvusha kwenye janga la Corona, na hili la MAFUTA Magufuli angetuvusha!

Ni kweli na bila shaka angalifanya hivi:

1. Angejenga oil refinery kubwa ambalo lingalitosheleza mahitaji yetu na nchi jirani ambao tungaliwauzia. Hii ingalipunguza sana bei ya mafuta kwani badala ya kununua refined oil tungalinunua crude oil, including ile ya itakayotoka Uganda.

2. Mafuta ambayo yalishagunduliwa kuwepo Tanzania, kwa kushirikiana na wale watalaam wa Museveni, yangalianza kuchimbwa mara moja.

3. Katika kipindi hiki cha vita ya Russia vs Ukraine ambayo imesababisha mafuta kutoka Saudi Arabia na OPEC kupanda sana bei na yale ya kutoka Russia kushuka sana bei, tungalinunua kutoka Russia bila woga wo wote hata kama ni kwa rubles. Russia ni marafiki zetu na tungaliimarisha biashara kati yetu. China na India ambayo ni mataifa makubwa yenye watu billioni tatu, yanafanya hivyo.

4. Tungalipunguza idadi ya tozo za serikali kutoka idadi ya tozo 15 za sasa na kubaki na tatu tu za VAT, Tanroad na Tarura. Mapungufu ya bajeti ya serikali yatakayotokana na kupunguzwa kwa tozo hizi, yangalifidiwa kwa kubana sana matumizi ya serikali yasiyo ya lazima hususani safari za ndani na nje ya nchi, washa, semina na posho zisizokuwa za msingi eg seating allowance (posho ya kukaa) n.k.
 
Magufuli hayupo Chato, baba yetu yupo mioyoni mwa kila mtanzania.

Kipindi kama hiki uwa tunamkumbuka sana sababu ya uwezo wake wa kuchukua maamuzi ya kusaidia watu wa chini.
Si yupo moyoni mwako, vipi hajakwambia cha kufanya?
 
Aliwavusha kutoka wapi kwenda wapi?

Kwa hiyo aliwavusha nyingi kwa corona afu yeye akashindwa kujivusha au? 😂😂😂..

Kwa hili la mafuta limefanyaje? Mtahangaika Sana na waliooza .
 
Mkwere atuonee huruma jamani[emoji25]
 
Angewanyang'anya wauza mafuta Ka kawaida yake, mabavu na nguvu nyingi, maarifa, busara na hekima kiduchu!

Mafuta yamepanda duniani kote! Na Ile misafara yake ya Dar Chato Kwa barabara, kila baada ya miezi mitatu; Angeifilisi nchi!
 

PUMBAVU. Corona hii hii iliyomuondoa ama??

Labda angetuvusha kwenye hili janga la mafuta kwa kwenda kukopa. Nonsese
 
Sikuzote mwanamke hana plan B.... humtegemea mwanaume
 
Bado mambo ni yale yale apo ishu sio kuagiza kwani hata hayo mafuta Still tunaagiza eti, au mliskia kutakua hakuna mafuta tena yanayoingia nchini!
Punguza mahaba ya kijinga kwenye maswala ya muhimi... swala ni kusaidia wananchi kupata kwa bei yenye unafuu iwe kwa kutoa ruzuku ama kufanya maamuzi ya kiuwanaume kununua toka kwenye source yenye vikwazo... India imenunua mapipa 150k kwa bei ya US$ 25 toka Urusi kwa pipa wakati sisi tunanunua kwa bei ya US$ 108 mpaka 118..mafuta ghafi... China nao wamenunua kwa wingi tu tena kwa currency ya Russia wameachana Pertodollar kwakuwa sisi hiyo akili hatuna tunawaza zinduzi na teuzi tu
 
Hard work doesn't always pay.

Kwa wakristu wajifunze kwa Wana wa Israel baada ya Yusufu kufa kilicho wapata. Walihenyeshwa hasa na Wamisri wakawa watumwa kutoka katika Neema kuu aliyo waacha nayo Yusufu mpaka pale Mungu aliposikia kilio chao akaingilia kati. Ukiwa umetembelwa na Neema ni rahisi sana kumuona aliyeko kwenye dhiki/shida ni mjinga, mvivu, hana akili nk.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…