Gavana
JF-Expert Member
- Jul 19, 2008
- 33,637
- 8,947
ACHA KUMSINGIAZIA YESU ,ACHA KUMZULIA UONGO
YESU alikataa kwamba alikuja kuzitangua sheria za Mungu ikiwemo Sabato,
Mathayo.5:17,18 “msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie.”
Yesu alisema hata mbingu zitakapoondoka nukta ya amri zake haitaondoka.
Mitume nao wakiongozwa na Paulo baada ya kufa na kufufuka kwa Yesu walikuwa na Desturi kama ya Yesu ya kupumzika siku ya Sabato, Matendo.17:2 “Na Paulo kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko Sabato tatu,” Hivyo hapa tunaona Paulo akiwa na desturi kama ya Yesu kwenda katika nyumba ya ibada siku ya Jumamosi, akitoa hoja toka katika neno la MUNGU Matemdo.18:4. Biblia inasema pia, Matendo.16:13 “Siku ya Sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale.” Mafungu haya yanaonesha Sabato ilivyotunzwa baada ya kufa na kufufuka kwa Yesu (Luk.23:54-56, Matendo.13:14,27,43-44; 15:21; 18:4)
Kwa hivyo haya maneno ya Paulo yote ni uzushi na ni uongo
Collosians2
16 Kwa hiyo msimruhusu mtu awahukumu kuhusu chakula au kiny waji, au juu ya kuadhimisha sherehe za dini, sikukuu ya mwezi mpya au siku ya sabato. 17 Maana hizi zilikuwa ni kanuni za muda tu au vivuli vya yale mambo ambayo yangekuja; lakini hakika ya mambo yenyewe ni Kristo