Kama Dhahabu ni pesa, kwanini tupokee mgao wa makaratasi Badala ya Dhahabu?

Kama Dhahabu ni pesa, kwanini tupokee mgao wa makaratasi Badala ya Dhahabu?

Upi sahihi migodi mipya mikataba yake iwe ya magao wa mali kwa mali ya vitofali vya dhahabu


MJADALA WA BIASHARA YA DHAHABU KWA MAFUTA WAPAMBA MOTO NCHINI 🇬🇭

Mjumbe wa kamati ya migodi na nishati ya Bunge nchini Ghana, Dr. Kwabena Donkor amesema hizi ni sarakasi zinazochezwa na serikali ambazo ni kiini macho kwani haziwezi kutekelezeka.

Kujaribu biashara ya mali-kwa-mali (barter trade) ya kubadilisha dhahabu kwa mafuta ya petroli / dizeli kimataifa ni dalili ya serikali kushindwa kusimamia uchumi anasisitiza mbunge na mjumbe huyo wa kamati ya bunge Dr. Kwabena Donkor ambaye aliwahi kufanya kazi ktk sekta ya petroli.


Dr. Kwabena Donkor akishiriki ndani ya mjadala exclusive wa kituo cha JoyNews amekwenda ndani zaidi kwa kuhoji ni nani anayemiliki migodi hiyo, na inajulikana ni makampuni makubwa ya kigeni hivyo watawalipa nini wenye migodi je ni kwa pesa za madafu yaani sarafu ya cedis ya Ghana au dollars za Kimarekani ambazo serikali ya Ghana haina fedha hizo za kigeni.

Anaongeza hoja Dr. Kwabena Donkor, pia kama serikali italenga kununua kwa wachimbaji wadogo wadogo itaweza kushindana na bei ya dhahabu ya soko la dunia? Maana itapelekea wachimbaji hao wadogo kutorosha dhahabu kupitia njia za panya za mipakani.

Hii ni kutokana na serikali itashindwa kuwalipa bei nzuri wachimbaji wadogo au kuwalipa kwa dollar za marekani wachimbaji wadogo kulingana na bei ya soko la dunia kwani serikali haina hifadhi ya kutosha ya fedha za kigeni.

Kimsingi katika mada hii moto ya kituo cha TV JoyNews pia mtendaji mkuu (CEO) wa chemba ya migodi ya Ghana, Dr. Sulemanu Koney naye ktk mahojiano ametoa kauli juu ya changamoto ya jinsi ya uhalisia wa uwezekano wa sera hiyo mpya ya biashara ya mali-kwa-mali kuweza kutekelezeka, kwani kuna mengi ya kuyafanya kabla ya sera hiyo kuweza kutekelezeka ingawa chemba hiyo milango yake ipo wazi kwa majadiliano na serikali ya Ghana.

View: https://m.youtube.com/watch?v=idU-ZxmfIMU
Source : JoyNews

Ni Kweli kabisa ndugu bagamoyo,

Serikali Haina uwezo wa kuwalipa pesa nyingi zaidi ya wanayopata huko wanakopeleka sasa,

Wakijaribu njia hiyo, Yale ya korosho yanaweza Kutokea.
 
Niwaambie ili tufike hapo 50/50 ni lazima tukomae Tuwe nchi ya Uchumi wa kati,kiukweli Magufuli alikuwa mtu mhimu mno,in fact ukiwa uchumi wa kati kuna profile inapanda katika nyanja za uchumi,watesi wakala kichwa
Ndugu Magu alitufumbua macho na kutuaminisha kuwa inawezekana kukata minyororo ya unyonyaji inayodidimiza Africa katika Umaskini.

Magu mmoja amekufa, Bado tupo watz zaidi ya 60 ml ambao tunaweza kufanya zaidi ya alivyofanya Magu.

Mungu atusaidie.
 
Zimbabwe imetengeneza sarafu ya Dhahabu yenye thamani sawa na USD 900 baada ya pesa Yao kutoimarika.

Sie Watanzania tumebinafsisha migodi yetu, wachimbe pesa Kisha kutupa mgao wa makaratasi, tena Kwa makadirio na wakati mwingine wanatangaza HASARA na kubadili Majina Ili kukwepa Kodi mf Kutoka Barrick kwenda Acacia 😳

Ikumbukwe kuwa tangu kuumbwa Kwa Dunia, Dhahabu haijawahi tetereka katika soko la Dunia.

Kununua Dhahabu Kutoka wachimbaji WADOGO Bado uzalishaji uko chini kutokana na uwekezaji wa Serikali chini ya Mamlaka husika kuzalisha na kuongeza ubora Kwa viwango vya kidunia.

Hivyo kuwaelekeza wafanyabiashara huko kununua Dhahabu Ili waende kuuza kupata dollar za kuagizia mafuta na bidhaa adimu, ni kukosa vision.

Botswana ni Nchi IPO hapa hapa Africa, wao wamebinafsiaha Dhahabu Yao Kwa wageni Kwa kupewa hisa ya 50%.

Sie Watanzania tunapewa mrabaha wa chini ya 20%, na mbaya zaidi tunalipwa cash Dhahabu inaenda.

Ikiwa kama Nchi tunaona uelekeo sahihi ni kununua Dhahabu Kwa wachimbaji wa ndani, kwanini tusianze na makampuni tuloyabinafsishia migodi Ili yatulipe mrabaha in terms of Gold na Si pesa cash?

Pia kwanini tusirudi mezani na kuhakikisha tunapata share ya 50+1% sababu sisi ndo wamiliki wa raslimali?

Na hiyo 50+1% Inatakiwa tupewe in terms of Gold iliyozalishwa Kwa ubora wa juu katika gold bars(vitofali).

Yaani tunaweka wazalendo kwenye Kila mgodi pale jikoni vinapitengenezwa vitofali yaani gold bars, moja letu, moja lao mwanzo mwisho.

Kwa kufanya hivyo, Nchi ingepata vitofali vingapi Kwa siku? Ni Dhahabu kiasi Gani inapelekwa nje ukizingatia wanafanya KAZI day and night?

Stamico kwanini haisitishi vibali vya utafiti na uchimbaji madini yetu Kwa makampuni ya nje Ili yenyewe iunde na kusimamia migodi itayochimba Dhahabu yetu na tukapata share kubwa zaidi?

Kwanini Benki kuu isianzishe SARAFU ya Dhahabu yenye ubora wa kimataifa Ili kuimarisha currency yetu ya Tshs?

Kwani madini yetu Mungu alitupa tuwagawie majirani au tulipewa yatutajirishe?

Watoto wanakaa chini wakati Dhahabu yetu inaenda kutajirisha wageni ambao hawakujaliwa raslimali hizo!!

Wazalendo wa Nchi wapo wapi?

Karibuni🙏
Cc Faiza fox, Meneja wa makampuni, Lord Denim, Kalamu.
Faiza yuko busy na bwana zake wa Walodi sidhani kama anaweze kutinga hapa
 
Niliwahi kuandika haya kuhusu dhahabu yetu:
Ndugu bagamoyo ametoa HOJA muhimu hapa, kwamba:

1.Serikali inazo pesa za kununua Dhahabu ya wachimbaji WADOGO?

2. Na ikiwa inazo pesa, je inaweza Kutoa Bei ya juu kuliko huko wanakopeleka sasa wafanyabiashara WADOGO?

3. Na ikiwa itaamua kununua Kutoka makampuni makubwa Kutoka nje kama GGM au Acacia ,Je makampuni hayo yatakubali kupokea pesa za madafu kubadilishana na gold bars?

4. Pia naongezea, wafanyabiashara wa mafuta ikiwa watataka kununua Dhahabu Kutoka Acaccia au GGM, Serikali imeweka Utaratibu Gani Ili jambo Hilo liwezekane?

Karibu.
 
1 July 2023

Under the new deal announced on Friday, Botswana gets a bigger share of rough stones from their joint venture, Debswana.

Botswana and mining company De Beers have announced a new diamond sales deal.
View attachment 2709249
The new deal, concluded on Friday, gives Botswana a bigger share of rough stones from their joint venture.

Debswana, a joint venture between Anglo American unit De Beers and Botswana's government, sells 75% of its output to De Beers, with the balance taken up by state-owned Okavango Diamond Co.

The new agreement covers a 10-year sales deal for Debswana rough diamond production through to 2033 and 25-year Debswana mining licences.

In the run-up to Friday's deal, Botswana President Mokgweetsi Masisi, who is expected to seek re-election next year, had pushed De Beers for a bigger share of Debswana's output.

In March, Botswana announced it would take a 24% stake in Belgian gem processing firm HB Antwerp in a move seen as designed to loosen De Beers' grip on the country's gems.

Botswana supplies 70% of De Beers' rough diamonds
Wazo zuri
 
Faiza yuko busy na bwana zake wa Walodi sidhani kama anaweze kutinga hapa
Swali muhimu ni kuwa, Je inawezekana wafanya biashara wakubwa wa mafuta kutinga pale Acacia au GGM kununua Dhahabu Kwa pesa za madafu na ikawezekana?

Maana Kuna thread aliandika faizafox na Meneja wa makampuni wakishauri wafanyabiashara na Serikali kununua Dhahabu ya ndani!!
 
Swali muhimu ni kuwa, Je inawezekana wafanya biashara wakubwa wa mafuta kutinga pale Acacia au GGM kununua Dhahabu Kwa pesa za madafu na ikawezekana?

Maana Kuna thread aliandika faizafox na Meneja wa makampuni wakishauri wafanyabiashara na Serikali kununua Dhahabu ya ndani!!
Huwezi kufanya terms of reference na mtu hajasomea economics ....its an insult bwana
 
Ndugu bagamoyo ametoa HOJA muhimu hapa, kwamba:

1.Serikali inazo pesa za kununua Dhahabu ya wachimbaji WADOGO?

2. Na ikiwa inazo pesa, je inaweza Kutoa Bei ya juu kuliko huko wanakopeleka sasa wafanyabiashara WADOGO?

3. Na ikiwa itaamua kununua Kutoka makampuni makubwa Kutoka nje kama GGM au Acacia ,Je makampuni hayo yatakubali kupokea pesa za madafu kubadilishana na gold bars?

4. Pia naongezea, wafanyabiashara wa mafuta ikiwa watataka kununua Dhahabu Kutoka Acaccia au GGM, Serikali imeweka Utaratibu Gani Ili jambo Hilo liwezekane?

Karibu.
Biashara inatakiwa iwe "fair and square". Tusitake kuunda kanuni mpya za biashara.
 
Botswana na Tanzania ni tofauti kama mjamzito na tasa! Very very different experience!

Hivi hiyo ccm yenu inayapokea haya maoni??
Sana tena sana.

Serikali inafanyia kazi mengi sana inayoshauriwa yenye kueleweka. Asiye na macho haambiwi tazama.
 
Mabeberu wameidhibiti dhahabu ndiyo maana hatufurukuti nayo...
 
Mabeberu wameidhibiti dhahabu ndiyo maana hatufurukuti nayo...
Basi tupige MARUFUKU vibali vipya vya uchimbaji.

Kampuni zetu chini ya stamico viwezeshwe, kikope kununua mashine za kisasa,

Sirikali ipata mgao wake, pia inunue na kutunza reserve.
 
Asante Kwa kujazia nyama,

Dhahabu ni pesa, hivyo tukisubiri kugawana baada ya hesabu watatupiga,

Tubadili SHERIA, tugawane GOLD BARS(VITOFALI).

Wazalendo wa Nchi hii tuamke, tukifanya hivyo, hatutashangilia tena kukopeshwa 1.5 trillion kujengea madarasa na vyoo!!
Kwa Tanzania na jinsi tulivyo tunahitaji Rais mjeuri kama botswana wameweza sisi tunaongozwa na NG'OMBE au wasomi?
 
Basi tupige MARUFUKU vibali vipya vya uchimbaji.

Kampuni zetu chini ya stamico viwezeshwe, kikope kununua mashine za kisasa,

Sirikali ipata mgao wake, pia inunue na kutunza reserve.
Kuna vibali vinahusisha mabeberu ili uweze kua kwenye soko, tutakwama...

Mashine za kisasa na vipuli vyake vinatoka kwa hao mabeberu, tutakwama...

Kwenye mgao, tunapangiwa na mabebru, sababu mambo mengi ni kutoka kwao, hata soko la dunia la dhahabu wanaliendsha wao...
 
Ndugu bagamoyo ametoa HOJA muhimu hapa, kwamba:

1.Serikali inazo pesa za kununua Dhahabu ya wachimbaji WADOGO?

2. Na ikiwa inazo pesa, je inaweza Kutoa Bei ya juu kuliko huko wanakopeleka sasa wafanyabiashara WADOGO?

3. Na ikiwa itaamua kununua Kutoka makampuni makubwa Kutoka nje kama GGM au Acacia ,Je makampuni hayo yatakubali kupokea pesa za madafu kubadilishana na gold bars?

4. Pia naongezea, wafanyabiashara wa mafuta ikiwa watataka kununua Dhahabu Kutoka Acaccia au GGM, Serikali imeweka Utaratibu Gani Ili jambo Hilo liwezekane?

Karibu.
Kwa wachimbaji wadogo kwa kutumia madafu inaweza hata kununua kwa bei ya zaidi ya soko. Serikali haina shida wala uhaba wa madafu.
 
Kwa wachimbaji wadogo kwa kutumia madafu inaweza hata kununua kwa bei ya zaidi ya soko. Serikali haina shida wala uhaba wa madafu.
NB:Neno madafu limetumila kumaanisha pesa ya madafu au pesa ya Tshss. Pesa ya ndani.

Na ikinunua Kwa Bei ya juu kuliko huko duniani hiyo gold itakuwa ghali hivyo kukosa wa kumuuzia.

Balance inahitajika.
 
NB:Neno madafu limetumila kumaanisha pesa ya madafu au pesa ya Tshss. Pesa ya ndani.

Na ikinunua Kwa Bei ya juu kuliko huko duniani hiyo gold itakuwa ghali hivyo kukosa wa kumuuzia.

Balance inahitajika.
Kwa pesa ya ndani unaweza nunua kwa bei ya juu. Huko si unapata dola. Serikali haina shida wala uhaba na Tsh. Na si mpaka uongeze bei. Unaweza kutoa kodi.
 
Kwa pesa ya ndani unaweza nunua kwa bei ya juu. Huko si unapata dola. Serikali haina shida wala uhaba na Tsh. Na si mpaka uongeze bei. Unaweza kutoa kodi.
Ndo nasema, ukinunua Kwa Bei ya juu, Dhahabu hiyo itakuwa na gharama kubwa, hivyo ukitaka kuiuza nje ukakuta unapewa Bei ya offer ndogo kuliko gharama uliyonunulia Kwa kulinganisha na thamani ya dollar itakuwa HASARA na hutapata mteja, na ukimpata atakupa dollar chache.
 
Ndo nasema, ukinunua Kwa Bei ya juu, Dhahabu hiyo itakuwa na gharama kubwa, hivyo ukitaka kuiuza nje ukakuta unapewa Bei ya offer ndogo kuliko gharama uliyonunulia Kwa kulinganisha na thamani ya dollar itakuwa HASARA na hutapata mteja, na ukimpata atakupa dollar chache.
Hujaelewa. Dhahabu kwa sasa ni Tsh 150,000 kwa gram. Serikali haina uhaba wa Tsh. Inaweza kwenda kununua kwa wachimbaji wadogo kwa 160,000. Au kwa hiyo 150,000 lakini bila kodi hivyo mchimbaji anapata pesa nzuri. Yenyewe unaenda kuiuza kwa bei ya dunia kama ni dola 60 kwa gram na kupata dola inazozihitaji sana. Inaweza fanya arrangement hii na wauzaji wa dhahabu ili kupata dola inazohitaji sana. Kifupi itakubali kuingiliwa ili ipate dola. Na

Hili linafanana na wanachofanya sasa NFRA. Wanajumua mahindi kwa bei nzuri kwa kutumia Tsh. Wanataka mtu kutoka nje ananunue kwao kwa pesa za kigeni, dola.

Hili likifanyika, serikali ikanunua labda 30% ya dhahabu za wachimbaji wadogo kwa mtindo huo, litaongeza sana dola nchini.
 
Back
Top Bottom