Kama Dhahabu ni pesa, kwanini tupokee mgao wa makaratasi Badala ya Dhahabu?

Kama Dhahabu ni pesa, kwanini tupokee mgao wa makaratasi Badala ya Dhahabu?

Hujaelewa. Dhahabu kwa sasa ni Tsh 150,000 kwa gram. Serikali haina uhaba wa Tsh. Inaweza kwenda kununua kwa wachimbaji wadogo kwa 160,000. Au kwa hiyo 150,000 lakini bila kodi hivyo mchimbaji anapata pesa nzuri. Yenyewe unaenda kuiuza kwa bei ya dunia kama ni dola 60 kwa gram na kupata dola inazozihitaji sana. Inaweza fanya arrangement hii na wauzaji wa dhahabu ili kupata dola inazohitaji sana. Kifupi itakubali kuingiliwa ili ipate dola. Na

Hili linafanana na wanachofanya sasa NFRA. Wanajumua mahindi kwa bei nzuri kwa kutumia Tsh. Wanataka mtu kutoka nje ananunue kwao kwa pesa za kigeni, dola.

Hili likifanyika, serikali ikanunua labda 30% ya dhahabu za wachimbaji wadogo kwa mtindo huo, litaongeza sana dola nchini.
Nimekupata, wazo zuri.
 
Sana tena sana.

Serikali inafanyia kazi mengi sana inayoshauriwa yenye kueleweka. Asiye na macho haambiwi tazama.
Kama mambo ya serikali inayoongoza hadi wasiokuwa na macho hayaonekani kwa wenye macho basi hapo kuna tatizo
 
Habari njema, serikali ya Tanzania yaangalia uwezekano wa mali-kwa-mali kwa wawekezaji kubakiza mgao wa dhahabu badala ya kusubiri iuzwe nje ndiyo serikali ipate mgao wa fedha za kigeni kama kampuni itapata faida :

[Latest Updates]: Dkt. Kiruswa Autaka Mgodi wa Buckreef Kutenga Dhahabu ya Kusafishwa, Kuuzwa Ndani ya Nchi​

Tarehe : Nov. 13, 2023, 8:28 p.m.
Geita, Tanzania

left

DKT. KIRUSWA AUTAKA MGODI WA BUCKREEF KUTENGA DHAHABU YA KUSAFISHWA, KUUZWA NDANI YA NCHI

#Autaka Mgodi wa Buckreef kutengeneza miradi endelevu kwa ajili ya wananchi

#Mgodi unazalisha dhahabu yenye thamani ya shilingi bilioni 8 kwa mwezi

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameutaka Mgodi wa Dhahabu wa Buckreef kuhakikisha unatenga kiasi cha dhahabu kwa ajili ya kusafisha kwenye viwanda vya ndani au kuuza katika masoko ya ndani ikiwemo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambayo imeanza kununua dhahabu kwa ajili ya akiba.
Ametoa rai hiyo leo Novemba 13, 2023 mkoani Geita alipotembelea mgodi huo kukagua maendeleo ya shughuli za uzalishaji pamoja na kuzungumza na kusikiliza changamoto zinazoukabili mradi huo.

Dkt. Kiruswa amesema kuwa Serikali imeamua kutumia dhahabu inayozalishwa hapa nchini ili kuimarisha akiba ya fedha za kigeni kwa kuhakikisha Benki Kuu ya Tanzania inakuwa na akiba ya dhahabu lakini pia dhahabu inayozalishwa hapa nchini inasafishwa katika Viwanda vya kusafisha madini hayo hapa nchini.

“Mmesema hapa kuwa mmeingia mkataba wa manunuzi ya dhahabu na kampuni ya kigeni, hakikisheni mnatenga kiasi cha dhahabu kwa ajili ya kuuza au kusafisha katika viwanda vya ndani, ni kwasabbu ili tuwe na akiba ya kutosha ya fedha kigeni, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza nchi iwe na akiba ya dhahabu inayozalishwa hapa nchini na tayari Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iko kwenye mchakato wa kuweka akiba ya dhahabu kiasi kisichopungua tani 6 kwa mwaka, na hiyo dhahabu itatoka kwa wachimbaji wakubwa, Kati na wadogo na nyie mnaweza kuuza kwao" amesema Dkt. Kiruswa.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kiruswa ameutaka mgodi huo kusaidia wananchi wanaozunguka mradi huo kupitia Wajibu wa Kampuni kwa Jamii kujenga miradi endelevu ili hata pale shughuli za uchimbaji zitakapofikia ukomo wakazi hao waendelee kunufaika na miradi hio endelevu.

“Nimesikia hapa kuwa mmetoa zaidi ya shilingi milioni 400 kwenye miradi kama CSR, niwahimize mtengeneze miradi endelevu ili hawa wananchi waliopisha mradi wenu wapate kuona manufaa ya uwepo wa rasilimali hii, nafahamu mmesaidia upande wa huduma za kijamii kama elimu na afya, nawapongeza kwa hilo lakini pia hili la miradi endelevu mlichukue mkalifayie kazi mtengeneze hizo fursa ili manufaa ya mgodi yabaki kwa mud mrefu” amesema Dkt. Kiruswa.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Mgodi huo, Gaston Mjwahuzi amesema kuwa Mgodi umepokea maelekezo ya Naibu Waziri Dkt. Kiruswa na kwamba watatekeleza kwa kuwa ni manufaa ya taifa na uchumi kwa ujumla.

Akizungumzia maendeleo ya mradi huo, Mjwahuzi amesema kuwa hivi sasa mgodi unazalisha wakia tani 1700 hadi 2000 kwa mwezi ambako wanazalisha dhahabu yenye thamani ya shilingi bilioni 8 kwa mwezi.
Naye, Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya Geita Kara Magaro ameushukuru mgodi huo kwa kujenga miradi ya huduma za kijamii yakiwemo madarasa na zahanati ambako tangu mradi huo uanze tayari kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 400 zimetolewa na mgodi kama Wajibu wa Kampuni kwa Jamii (CSR) na kusaidia kupunguza adha ya uhaba na uchakavu wa miundombinu katika sekta ya elimu na afya katika Halmashauri hiyo.
Source : https://www.madini.go.tz/page/
 
14 November 2023
Geita, Tanzania

Kiruswa apiga marufuku dhahabu ya Buckreef kuuzwa moja kwa moja nje ya nchi


View: https://m.youtube.com/watch?v=1qnf76NZIZg

Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa ameuagiza mgodi wa dhahabu wa Buckreef uliopo wilayani Geita kutouza dhahabu nje ya nchi badala yake wauze Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ili kuongeza akiba ya madini kama mbadala wa fedha za kigeni.Dkt. Kiruswa ameyasema hayo ziarani kwenye mgodi ambao una ubia wa Serikali kupitia shirika la STAMICO na mwekezaji kutoka Canada.
 
TRX Gold Corporation - Buckreef Gold Operation - November 2022


View: https://m.youtube.com/watch?v=ap5X21s-C6k

TRX Gold is rapidly advancing the Buckreef Gold Project. Anchored by a Mineral Resource published in May 2020, the project currently hosts an NI43-101 Measured and Indicated Mineral Resource of 35.88 MT at 1.77 g/t gold containing 2,036,280 oz of gold and an Inferred Mineral Resource of 17.8 MT at 1.11g/t gold for 635,540 oz of gold.

The leadership team is focused on creating both near-term and long-term shareholder value by increasing gold production to generate positive cash flow. The positive cash flow will be utilized for exploratory drilling with the goal of increasing the current gold Resource base and advancing the Sulphide Ore Project which represents 90% of current gold Resources.

TRX Gold’s actions are led by the highest ESG standards, evidenced by the relationships and programs that the Company has developed during its nearly two decades of presence in Geita Region, Tanzania
 
03 November 2023

TRX Gold CEO Stephen Mullowney Sits with Matthew Gordon of Crux Investors


View: https://m.youtube.com/watch?v=XGhbXEMfiPg

TRX Gold Chief Executive Officer Stephen Mullowney, was interviewed by Matthew Gordon of Crux Investors recently while in London for the Canadian Mining and Investment Symposium. The two took a close look at TRX Gold’s current activities at the Buckreef Gold Project, about the Company’s future growth plans as well as what it takes to operate a successful publicly-trading mining business in todays capital markets . An hour well spent and some great insight for shareholders and investors wanting to learn more about gold mining and investing.TRXGold.com
 
Waziri wa Uvuvi Mh. Abdallah Ulega na mkataba wa maliasili samaki wa bahari kuu ya Tanzania


View: https://m.youtube.com/watch?v=5nr6DfbvHvw

Meli ya kampuni ya Albacora ya Spain inayokwenda kwa jina la MV Pacific Star inavua samaki wa aina ya Tuna katika bahari kuu ya Tanzania na kukubali kuchakata samaki ktk eneo la Tanga jiji...

MV Pacific star ya uvuvi inamilikiwa na kampuni ya Albacora ya Spain na inapeperusha bendera ya Tanzania. Ina uwezo wa kubeba tani 1,950 za samaki iliyowavua baharini.

Leo imefika bandarini Dar es Salaam na kushusha tani 50 za samaki mchanganyiko ambao siyo aina ya tuna / jodari.

Samaki wa jodari / tuna wanatakiwa sana katika soko la dunia. Kwa mujibu wa mkataba Tanzania kwa ujumla itapata tani 300 za jodari / tuna na tani 100 za samaki wengine mchanganyiko kwa mwaka.

1700763483866.png

Her carrying capacity is 1905 t DWT and her current draught is reported to be 7 meters. Her length overall (LOA) is 105 meters and her width is 16.8 meters. PACIFIC STAR (IMO: 8716837) is a Fishing Vessel that was built in 1990 (33 years ago) and is sailing under the flag of Tanzania
 
Na Baharini tena!!

Maliasili inayovunwa baharini katika maji makuu yaliyo ndani ya mipaka ya Tanzania kupitia vibali maalum vinavyotolewa na wizara ya mifugo na uvuvi ya Tanzania


More info :

TANZANIA will for the first time start reaping from its Exclusive Economic Zones (EEZ) after launching a large fishing vessel registered in the country.

Speaking at a launching ceremony held in Dar es Salaam on Monday evening, Minister for Livestock and Fisheries, Mashimba Ndaki said under the deal, licensing revenue will be $400,000 (approximately 927.6m/-) annually After being registered in the country, the Pacific Star fishing vessel, owned by Spanish based Albacora family company, will be sailing under a Tanzanian flag.

At the event attended by officials from both Mainland and Isles, the Minister said other benefits of the concluded deal was that Tanzania will get a portion of 300 tonnes of targeted tuna fish and other related species amounting to 100 tonnes per year
 
Samaki wa jodari / tuna wanatakiwa sana katika soko la dunia. Kwa mujibu wa mkataba Tanzania kwa ujumla itapata tani 300 za jodari / tuna na tani 100 za samaki wengine mchanganyiko kwa mwaka.

Siku ya samaki Jodari duniani : UN​

Samaki Jodari wanaweza kuishi katika maji yenye baridi sana ikiwemo kwenye ghuba ya Mexico na bahari ya Mediterranea

Mfuko wa kimataifa wa chakula endelevu cha samaki (ISSF) Fabien Forget
Samaki Jodari wanaweza kuishi katika maji yenye baridi sana ikiwemo kwenye ghuba ya Mexico na bahari ya Mediterranea

2 Mei 2021Masuala ya UM
Zaidi ya tani milioni 6 za samaki Jodari huvuliwa kila mwaka ulimwenguni na aina hii ya samaki inachukua asilimia 20 ya ujazo wa Samaki wote wanaovuliwa wa baharini zinazouzwa duniani umesema Umoja wa Mataifa leo katika siku ya Samaki jodari duniani.

Katika siku hii inayoadhimishwa kila mwaka Mei 2 Umoja wa Mataifa unasema matumizi ya chakula cha bei rahisi cha samaki wa makopo imekua sana duniani kote mwaka 2020.

Na uhitaji wa samaki waliohifadhiwa pia umeongezeka. Umoja wa Mataifa unakumbusha kwamba Samaki jodari na aina zingine za Samaki ni chanzo muhimu cha protini katika lishe ya watu wengi ulimwenguni.

Umeongeza kuwa, uvuvi wa jodari una jukumu kubwa katika uchumi wa nchi zinazoendelea na zilizoendelea pia.
Siku ya samaki Jodari duniani, iliyoanzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2016, ni fursa ya kukuza ufahamu wa hitaji la kuhakikisha bahari bora, uvuvi endelevu na uzalishaji bora wa chakula wa Samaki jodari.

Katika sekta ya chakula cha makopo, Samaki Jodari na nyama nyeupe hutumiwana hasa jodari wa aina ya manjano.

Wakati wa kuandaa mlo wa Kijapan aina ya sushi au sahani za chakula aina ya sashimi, hutumia aina zenye mafuta mengi kama vile jodari wa bluu au wenye nyama nyekundu hutumiwa na kiasi kikubwa cha monofu ya jodari wa blu hupelekwa Japan.

Kwa mujibu wa shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), biashara ya Samaki jodari imekua mara 14 katika kipindi cha miaka 30 iliyopita hadi karibu dola bilioni 12 kwa mwaka.

Uhitaji mkubwa wa samaki, pamoja na idadi kubwa ya meli za uvuvi, vimesababisha kupungua kwa kasi kwa akiba ya samaki jodari.

Umoja wa Mataifa unafuatilia kwa karibu uvuvi wa baharini na unachukua hatua zinazohitajika kulinda na kuhifadhi rasilimali muhimu za bahari.
 
Leo 23 November 2023 meli ya uvuvi ya MV Pacific Star imefika bandarini Dar es Salaam na kushusha tani 50 za samaki mchanganyiko ambao siyo aina ya tuna / jodari.

Toka Maktaba :

ZANZIBAR WATAKA MGAO WA SAMAKI JODARI / TUNA​

November 25, 2009 · by zanzibarkwetu · Bookmark the permalink. ·
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema haina taarifa zozote kuhusiana na kupata mgao wa samaki waliovuliwa na meli ya Kigeni katika bahari Kuu ya Tanzania (Samaki wa Magufuli) mwaka huu.

Samaki hao walitarajiwa kugaiwa hivi karibuni baada ya Waziri wa Uvuvi na Maendeleo ya Mifugo, John Pombe Magufuli kutangaza katika vyombo vya habari Mjini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Afisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, alisema kuwa Serikali haijui lolote kuhusiana na kufaidika na mgao wa samaki unaogaiwa huko Tanzania Bara.

Kwa mujibu wa Waziri Magufuli tani 296.32 za samaki aina ya jodari zilizokamatwa zikivuliwa na wavuvi kutoka nje katika bahari ya Tanzania kwenye Ukanda wa Uchumi wa bahari Kuu nchini watagaiwa katika taasisi 115, zilizopitishiwa maombi yao kupata kitoweo hicho.

Zanzibar imekuwa na wasi wasi juu ya kupata mgao huo wa kupata samaki baada ya serikali kukiri kuwa hakuna tarifa yoyote iliyopokelewa kutoka serikali ya Muungano inayoeleza kuhusu mgao wa samaki hao na namna Zanzibar itakavyofaidika nao.

Waziri Hamza alisema kwamba taarifa walizozipata kuhusu samaki hao ni kupitia matangazo ya magazeti yanayotaka taasisi zinazohitaji samaki hao kuomba, lakini serikali haina taarifa rasmi kutoka serikali ya Muungano inayoelezea hilo wala hakuna barua yoyote iliyopokea.

Hata hivyo alisema zaidi suala hilo limefikishwa kwa Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Mazingira, ili lifanyiwe kazi kwa vile Wizara hiyo
ina vikao vya ushirikiano kisekta.

Suala la uvuvi wa Bahari Kuu ni miongoni mwa mambo yaliomo katika orodha ya mambo ya Muungano huku Zanzibar ikiwa ndio Makao Makuu ya Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu ambapo majengo yake yanatarajiwa kujengwa Fumba Wilaya ya Magharibi Unguja.

Awali ziliwahi kuzuka hoja kadhaa kuhusu samaki hao ndani ya vikao vya Baraza la Wawakilishi vilivyopita, na wajumbe wengi waliulizia hatma ya Zanzibar kupata samaki hao ikiwa ndio Makao Makuu ya Mamlaka hayo.

Wajumbe wa baraza la wawakilishi katika kikao kilichomalizika mwezi huu walitaka kupatika mgao wao wa samaki kwa kuwa wao ni wadau wakuu katika suala hilo na kuiomba serikali iweke wazi juu ya gawio lake ambalo linatakiwa kupatiwa wazanzibari.

Waziri Hamza, alisema Zanzibar inashindwa kufahamu kwamba inatakiwa iombe mgao wa samaki hao kama utaratibu alioutangaza Waziri Magufuli kwa kuwa suala la Bahari Kuu kisheria ni kupata mgao wa mapato ya asilimia 40 na asilimia 60 ni ya Tanzania Bara yanayotokana na Bahari Kuu.

Alisema kwa hali hiyo, Zanzibar ilipaswa itengewe tani zake za asilimia 40 kwa mujibu wa sheria ya usimamizi wa matumizi ya Bahari Kuu na sio kutakiwa vikosi na vyuo kuomba msaada kwa samaki hao kama ilivyoelezwa.

“Ilitakiwa serikali ya Muungano kutoa mgao huu ni wa Zanzibar na hapo Zanzibar ijue namna ya kuugawa baada ya kukabidhiwa chao, sio suala la Idara zetu ziombe” alisema Waziri huyo.

Waziri alisema haiwezekani kwa taasisi za Zanzibar, kuomba samaki hao moja kwa moja katika Wizara ya Uvuvi ya Tanzania Bara, bila ya maombi husika kupitia katika Wizara inayosimamia shughuli za uvuvi wa Bahari Kuu hapa Zanzibar.

“Zanzibar ina Wizara yake ilitakiwa Wizara ya Uvuvi na Maendeleo ya Mifugo yaTanzania Bara, izungumze na mwenzake kwani wanavyo vikao vya mahusiano ya kisekta, hasa suala hili ni mambo ya Muungano, haiwezekani Idara za Zanzibar, zikurupuke ziende kuomba bara, bila ya maombi yao kupitia Wizara husika hapa Zanzibar” alisema Waziri huyo.

Alisema kiutaratibu taasisi za Zanzibar zingeweza kuomba samaki hao baada ya serikali ya Zanzibar kukabidhiwa mgao wake kutoka serikali ya Muungano kupitia Wizara husika.
 
2022
MAMLAKA YA UVUVI KATIKA BAHARI YA KINA KIREFU TANZANIA / The Deep Sea Fishing Authority (DSFA)
Ilivyojizatiti kusimamia maliasili katika bahari kuu, kupitia kujiongezea uwezo na weledi wa rasilimali watu wafanyakazi wa mamlaka hiyo n.k


View: https://m.youtube.com/watch?v=vsJVwMM3dfg&

2023
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu, Dkt. Emmanuel Andrew Sweke.......

TANZANIA KUVUNA DOLA MILIONI 2.1 KUPITIA UVUVI WA BAHARI KUU​


GFDSFD.jpg

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Kuu (DSFA) zinatarajia kuvuna takribani Dola Milioni 2.1 kupitia mauzo ya leseni 45 za uvuvi wa bahari kuu zilizonunuliwa na wawekezaji kutoka nchi za China na Hispania.

Mhe. Ulega amebainisha kuwa eneo la bahari linalomilikiwa na Tanzania bara na Zanzibar lina uwezo wa kuhimili mpaka meli 100 hivyo ametoa rai kwa wawekezaji wengine wenye nia ya kuwekeza kwenye Uvuvi wa bahari kuu kufanya hivyo ambapo amewahakikishia hali ya usalama na mazingira rafiki ya kufanya shughuli zao wakati wote.

Akizungumza katika hafla ya kusaini mikataba ya mauzo ya leseni hizo Jjini Dar-es-Salaam, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa eneo la bahari kuu kwa upande wa Tanzania bara na Zanzibar lina ukubwa wa takribani Kilomita za mraba 220,000 ambazo kwa muda mrefu zimekuwa hazitumiki ipasavyo.

“Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ana imani kubwa sana kwetu hivyo ni lazima tuwe wabunifu katika utekelezaji wa maelekezo yake ambayo amekuwa akitutaka tuhakikishe rasilimali hii ya maji ya bahari inatumika kikamilifu kuwanufaisha Watanzania wote” Amesema Mhe. Ulega.

Kwa upande wake Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi kutoka Zanzibar, Mhe. Suleiman Makame amewahakikishia wawekezaji hao kuwa Wizara yake kupitia mamlaka ya usimamizi wa Uvuvi wa bahari kuu (DSFA) itasimamia na kutekeleza vipengele vyote vilivyopo kwenye leseni hizo.

Hatua hiyo ni miongoni mwa jitihada zinazochukuliwa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha eneo la bahari kuu linatumika vizuri ili kuongeza upatikanaji wa fedha za kigeni hapa nchini
 
Thamani ya mchango wa sekta ya uvuvi nchini Morocco kwa uchumi ni kiasi cha 11 billion Moroccan dirhams (1.13 billion U.S. dollars huku kiasi cha samaki wanaovuliwa kwa mwaka ni tani zipatazo 1.4 million metric tons

Value of sea fishing production in Morocco 2020, by type​

Published by
Saifaddin Galal,
Apr 26, 2023
In 2020, the value of the sea fishing production in Morocco amounted to around 11 billion Moroccan dirhams (1.13 billion U.S. dollars). Coastal and artisanal fishing contributed the highest value, corresponding to roughly 6.6 billion Moroccan dirhams (680 million U.S. dollars). As of the same year, sea fishing production in the country added up to 1.4 million metric tons.

Read more : MOROCCAN FISHERIES A SUPPLY OVERVIEW by Hmida Atmani.
 
Waziri wa Uvuvi Mh. Abdallah Ulega na mkataba wa maliasili samaki wa bahari kuu ya Tanzania


View: https://m.youtube.com/watch?v=5nr6DfbvHvw

Meli ya kampuni ya Albacora ya Spain inayokwenda kwa jina la MV Pacific Star inavua samaki wa aina ya Tuna katika bahari kuu ya Tanzania na kukubali kuchakata samaki ktk eneo la Tanga jiji...

MV Pacific star ya uvuvi inamilikiwa na kampuni ya Albacora ya Spain na inapeperusha bendera ya Tanzania. Ina uwezo wa kubeba tani 1,950 za samaki iliyowavua baharini.

Leo imefika bandarini Dar es Salaam na kushusha tani 50 za samaki mchanganyiko ambao siyo aina ya tuna / jodari.

Samaki wa jodari / tuna wanatakiwa sana katika soko la dunia. Kwa mujibu wa mkataba Tanzania kwa ujumla itapata tani 300 za jodari / tuna na tani 100 za samaki wengine mchanganyiko kwa mwaka.

View attachment 2822687
Her carrying capacity is 1905 t DWT and her current draught is reported to be 7 meters. Her length overall (LOA) is 105 meters and her width is 16.8 meters. PACIFIC STAR (IMO: 8716837) is a Fishing Vessel that was built in 1990 (33 years ago) and is sailing under the flag of Tanzania


28 November 2023
Dar es Salaam, Tanzania


Waziri Abdallah Ulega akabidhi boti kwa wavuvi Dar es Salaam

1701207581053.png

Waziri Abdallah Ulega amekabidhi boti 11 zenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.85 kwa wavuvi wanaofanya shughuli zao kwenye ukanda wa pwani hususani Dar es Saalaam.Boti hizo ambazo ni mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TaDB) zimetolewa Kigamboni jijini Dar es Salaam leo Novemba 28, 2023.

Sambamba na ugawaji wa boti hizo Waziri Ulega pia aliamuru kuondolewa katika nafasi ya ukaimu ukurugenzi wa uvuvi Stephen Lukanga kwa kushindwa kupanga na kutekeleza mikakati thabiti ya kukomesha uvuvi haramu nchini


View: https://m.youtube.com/watch?v=aIy5BECGvro
 
Waziri wa Uvuvi na Mifugo Mh. Abdallah Ulega amtumbua mkurugenzi

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega ameelekeza kuondolewa katika nafasi yake Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi, Bw. Stephen Lukanga baada ya kushindwa kupanga na kutekeleza mikakati thabiti ya kukomesha uvuvi haramu nchini.

Waziri Ulega ametoa maamuzi hayo wakati akikabidhi maboti (11) yenye thamani ya Shilingi ya Bilioni 1. 85 yaliyotolewa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) kwa mkopo kwa wavuvi wa Mkoa wa Dar es Salaam leo Novemba 28, 2023.
1701220498943.png

Waziri Ulega amefika maamuzi hayo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wadau wa Uvuvi Mkoani Dar es Salaam ya kukithiri kwa vitendo vya Uvuvi haramu katika ukanda Pwani hususani Dar es Salaam.

Oktoba 4, 2023 akiwa mkoani Mwanza katika Soko la Lumumba, Waziri Ulega alimtaka Kaimu Mkurugenzi huyo kuwa ndani ya Mwezi mmoja kuhakikisha anapanga na kutekeleza mikakati thabiti ya kukomesha uvuvi haramu nchini ambao kwa muda umekuwa ni kikwazo kwa maendeleo ya sekta ya uvuvi.

Kufuatia kushindwa kutekeleza mikakati hiyo, Waziri Ulega ameamua kumuondoa katika nafasi hiyo na kuelekeza nafasi hiyo apewe aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani, Prof. Mohamed Sheikh.
 
28 November 2023
Dar es Salaam, Tanzania


Waziri Abdallah Ulega akabidhi boti kwa wavuvi Dar es Salaam

View attachment 2828101
Waziri Abdallah Ulega amekabidhi boti 11 zenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.85 kwa wavuvi wanaofanya shughuli zao kwenye ukanda wa pwani hususani Dar es Saalaam.Boti hizo ambazo ni mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TaDB) zimetolewa Kigamboni jijini Dar es Salaam leo Novemba 28, 2023.

Sambamba na ugawaji wa boti hizo Waziri Ulega pia aliamuru kuondolewa katika nafasi ya ukaimu ukurugenzi wa uvuvi Stephen Lukanga kwa kushindwa kupanga na kutekeleza mikakati thabiti ya kukomesha uvuvi haramu nchini


View: https://m.youtube.com/watch?v=aIy5BECGvro

Ni jambo jema, ingawa sijaziona boti za uvuvi,

Hatua ingine, ziwe boti Hasa kama Ile aloikamata Magu ikivua samaki deep sea.
 
ingawa sijaziona boti za uvuvi,

Naona wameona ni aibu kuonesha mashua /boti zilivyo ndogo na haziwezi kwenda bahari ya maji makuu kama meli aliyokamata Magufuli au MV Pacific Star ya kampuni ya Albacora iliyoteremsha tani 50 za jodari / tuna juzi kati.

1701272498161.png

Mv Pacific Star ya uvuvi inamilikiwa na kampuni ya Albacora ya Spain na inapeperusha bendera ya Tanzania. Ina uwezo wa kubeba tani 1,950 za samaki iliyowavua baharini.
 
Back
Top Bottom