Kama DPP haondolewi ofisini mpaka afanye makosa au awe na tatizo la kiafya, Rais kamuondoa katika mazingira gani?

Nimesoma mtandaoni kuhusu taratibu za kisheria zinazotakiwa kufuata ili kumuondoa DPP ofisini, ambapo sheria imetamka wazi kuwa DPP hapaswi kuondolewa ofisini isipokuwa tu kama ana tatizo la kiafya(illness) au amekwenda kinyume na maadili ya kazi
...
kashafanya makosa mengi tu mbona hata na hivyo maza kamtoa kistaarabu sana
 
Magufuli ashavunja sheria mara ngapi? Magufuli ndio kapitisha izo sheria mbovu kuwalinda wakwapuzi wake
 
Nimesoma mtandaoni kuhusu taratibu za kisheria zinazotakiwa kufuata ili kumuondoa DPP ofisini, ambapo sheria imetamka wazi kuwa DPP hapaswi kuondolewa ofisini isipokuwa tu kama ana tatizo la kiafya(illness) au amekwenda kinyume na maadili ya kazi...
Yote yako sahihi. Mh. Rais amemuondoa kwa kumpandisha cheo. Hilo halina tatizo. Ndivyo pia mwenda zake alivyobmuondoa Felesh.
 
Masheria ya kipumbavu yaliyoletwa na mwendazake yafutwe yanasababishwa contradictions
Siyo mwenda zake alileta hizi sheria bali bunge la Ccm. Kila kitu ndiyoooo.

Hata juzi tumeshuhudia Ndugai akiropoka mbele ya wabunge wa Ccm kuhusu covid 19 huku wabunge wa Ccm wana mpigia makofi wakati Ndugai ana vunja sheria na kanuni walizo pitisha wenyewe. Shidaaaa.
 
Hata mimi naelewa Jiwe ndio alikuwa chanzo, ila na wao wanapaswa kuwajibila vinginevyo huu utakuwa ni mfano mbaya kwa watawala na wateuliwe wajao otherwise wangejiuzu.
 
Hata katika hili la kwenda kinyume na maadili ya kazi/ professional yake, Raisi atapaswa kuunda tribunal kumchunguza kabla ya kumuondoa.

Sasa kama haya yana ukweli, Raisi Samia amemuon
Labda rais katafuta convenience kwa kumpa u-jaji, badala ya mlolongo wa kuunda tribunal ili kumng'oa..
 
Kwaiyo ni Bora angeendelea kumuacha,, kipi afadhali,kwaiyo angefuata sheria aendelee kumuacha mtu ambae hata nyinyi na sisi tunajua kwamba DPP biswalo hakuwa msafi!!?
Kama inajulikana si Msafi kwanini ampeleke kua Jaji? Huoni kama huyu anaeteua na kutengua nae ana shida?
 
Nimesoma mitandao ya jamii yote maarufu katika mambo ya kitaifa na kisiasa jana. Ni Jaji mmoja tu Biswalo Mganga aliyelalamikiwa kuwa siyo uteuzi "safi" na wanasema Mama "kakosea". Biswalo ana tuhuma nyingi za kubamnikiza watu makosa ya uhujumu uchumi na kujipatia fedha yeye binafsi kupitia kichochoro cha "plea bargain".

Rais Samia Suluhu Hassan ashauriwe kuunda Tribunal Maalum kwa ajili ya kumchunguza Biswalo Mganga kwa vitendo vyake kama DPP kuanzia mwaka 2016 hadi 2021.

Sheria ya National Prosecution Services Namba 27 ya 2008, kifungu 3-8, imetoa mwongozo wa namna ya kumuondoa DPP
 

Angekuwa na akili, angejitengua mwenyewe asisubiri kuapishwa, angekuwa amelinda heshima yake kama kweli anayo
 
Huyu mazaa amefeli mapema sn ndiyo maana amepoteza mvuto mapema sn
Alafu Cha ajabu Watumishi wengi wa Umma ndiyo hawampendi sana! Wanamuektia na Sasa ndiyo huko ma officini ndiyo hawatumiki kabisa wame relax wanamuangalia Mama!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…