Kama hii tweet ni kweli basi Air Tanzania ni ya kuhurumiwa

Kama hii tweet ni kweli basi Air Tanzania ni ya kuhurumiwa

Hee Manitoba to New Yorke kumbe imesitishwa.?
Hizi ni changamoto za biashara japokuwa ni ngumu kutoa maamuzi kwa kutumia flight moja.Je ni kila siku hakuna wateja au ni siku hiyo tuu?Na jee ilivyokua inarudi Entebe Kilimanjaro, hali ilikua hivyo hivyo?

Niliwahi kushuhudia Egypt Air Airbus 320 from Cairo to DSM ikiwa na abiria 20.

So hizi ni changamoto na ninaamini wahusika wakiona route hailipi wataifuta kama KQ walivyositisha NBO to New York.
 
IMESHABUMAA MZEE...!! Yani huyu mzee ataacha nchi ina madeni makubwa ambayo hayalipiki kabisa...Ngoja uoneee[emoji35][emoji35][emoji35]
Hii biashara ya ndege mmekurupuka itabuma tu subiri kidogo
 
Hata basi za Modern kutoka Mwanza kwenda Nairobi mara nyingine huwa zinabeba hadi watu 15 kwenda Nairobi. Biashara kuna kupata na kukosa.
Watu hawafanyi biashara za kubahatisha siku hizi haya mambo ya kusema biashara kuna kupata na kukosa mmebaki nayo nyie waswahili tu.
 
Hizo ndege mtazipaki vijana wa Lumumba wapigie picha
 
Pia ukumbuke kuwa hata uendeshaji wa mradi mdogo wa BRT umekuwa balaa kubwa!
 
Jamaa kila siku yeye ni kutafuta na kufurahia mapungufu tu.
Kama alikosekana kwenye kutumbuliwa sababu ya utendaji mbovu wa kazi, upigaji dili basi hawezi kukosekana katika kumwaga unga kwa vyeti feki au ni ndugu yake ndiye atayekuwa amehusika katika hayo, so anaamua kupinga kila atendalo Raisi ili apunguze maumivu aliyonayo rohoni.

Maana si kwa chuki hizo Mkuu, yani kila siku yeye ni Malaika tu na haoneshagi baadhi ya mazuri ya Mkuu wa nchi zaidi ya kukosoa kila kitu.

Sasa hapo utamkuta kakaa vijiweni na kudai kuwa ananyimwa uhuru wa kuongea, he anapataje muda wa kukaa chini na kutafuta mapungufu tu ya Raisi wetu badala ya kutafuta na mazuri yake?
 
Hizi ni changamoto za biashara japokuwa ni ngumu kutoa maamuzi kwa kutumia flight moja.Je ni kila siku hakuna wateja au ni siku hiyo tuu?Na jee ilivyokua inarudi Entebe Kilimanjaro, hali ilikua hivyo hivyo?

Niliwahi kushuhudia Egypt Air Airbus 320 from Cairo to DSM ikiwa na abiria 20.

So hizi ni changamoto na ninaamini wahusika wakiona route hailipi wataifuta au kupunguza idadi ya safari kama KQ walivyofanya route ya NBO to New York.
WAZO ZURI SANA LISILO NA UKAKASI WA UPENDELEO UPANDE WOWOTE ZAIDI YA KUBEBA HOJA YA KIMANTIKI PEKEE.
 
Air Tanzania Haifi Tena Hata Ikipakia Abiria Mmoja Inaleta Faida Tu
Mbona Tumenunua Korosho Bila Tatizo
 
Minitu kama nyie ndio sawa na wale wana wa israel wametoka utumwani wanafika jangwani wanatamani tena kurudi utumwani kwa sababu kule wameaacha masufuria ya nyama na pilau!

Hivi hao walioweza waliaanzaje? Unafikiri waliibuka tu?
SAFI SAAAAAAAANA....NAKAZIA KUWA HATA INDIA NI WATAALAMU SANA KATIKA FANI YA UTABIBU LAKINI IMETOKANA NA KUKUMBWA NA AINA YA MAGONJWA MENGI SANA YA AJABU AJABU, NDIPO WALIPOWEZA KUUMIZWA VICHWA ZAIDI KATIKA KUTAFITI TIBA NA DAWA ZA KUKAVILIANA NA HAYO MAGONJWA.

NAMAANISHA HAKUNA KIZURI DUNIANI KINACHOKUJA KIRAHISI RAHISI NA NDIYOMAANA HATA UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

MIJITU YA BONGO NI MILAINI SANA YA KUKOSA UVUMILIVU KATIKA MAISHA, PIA HUWA INAPENDA SANA SHORT CUT WAY YO SUCCESS/NJIA FUPI ZA MAFANIKIO BILA YA KUPAMBANA NA MAISHA KWA KUWA NA BIDII KATIKA SHUGHULI MBALI MBALI NA IMANI THABITI.

MUNGU ATUSAIDIE ILI TUSIWE KAMA WANA WA ISRAEL WALIVYOKUWA WAKIONGOZWA NA MUSA.
 
Unajua ubishani huja mtu asipojua fikra za mwenzake.
Mimi najua biashara kwa shirika lililofufuliwa is next to national identity.
Sasa mtu asipojua hilo ni kila siku kuleta habar hasi.
What a sadist generation!
Kweli kabisa umenena vyema Mkuu
 
Hiyo mbona walitangaza officially kuistisha hadi mwakani?tatizo letu sisi hatutaki kuutangazia umma juu ya matatizo tunayo kutana nayo
Utangaziwe li iweje na unufaike na kipi hasa?

Tanzania ndiyo nchi pekee ambayo kila kinachotendwa na serikali yake basi Raia wake atataka akifahamu tu hata kama hausiki nacho.

Kizazi cha laana sana hiki, hivi hata pale nyumbani kwenu ulipolelewa ulikuwa unaelezwa kila kitu kilichokuwa kinatokea baina ya Wazazi wako halisi haijalishi kwa uzuri au kwa ubaya uliojitokeza kwa inahu za Wazazi wako?
 
If you don't plan you are planning to fail.

Kuna failures zingine ni za kujitakia, shirika linaanzaje biashara sensitive kama hii bila kufanya research na kuwa na business plan, matokeo yake ni kurupuka kupeleka ndege Entebe bila kujua flow ya abiria kwa kutafuta kiki za kisiasa.
Wewe hilo somo la plani za biashara ulipata ngapi vile?

Kila plani inayofanywa na Serikali haina faida yoyote kwako?

Serikali zilizotangulia hazikuwa na business plani na zilikufikisha wapi hasa kimafanikio katika mambo ya ukuaji wa uchumi wa nchi yako kimataifa?
 
Back
Top Bottom