Kama hila ya Wazungu kupitia chanjo ni kutumaliza, basi tusitie kiburi leo, tumechelewa, tangu utotoni tumechanjwa sana na chanjo zao

Kama hila ya Wazungu kupitia chanjo ni kutumaliza, basi tusitie kiburi leo, tumechelewa, tangu utotoni tumechanjwa sana na chanjo zao

Kididimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2016
Posts
4,153
Reaction score
3,800
Polio, ndui, kifaduro, pepopunda, TB, nk ni chanjo ambazo wengi wetu tumechanjwa utotoni. Na huenda kupitia chanjo hizo ndiyo sababu ya kuwa hai hadi leo tunapotunisha misuli majukwaani.

Halikadhalika ukienda kwa upande wa Mifugo,kuna chanjo nyingi mifugo yetu huchanjwa kukinga magonjwa mbalimbali. Hivyo chanjo ni kitu muhimu kwa binadamu na wanyama hasa kwa magojwa yale yasiyotibika kwa tiba za kawaida.

Kwa uelewa wangu,zaidi ya 99% ya chanjo hizo za binadamu zimetengenezwa nje ya nchi( hasa ulaya) kupitia uangalizi wa Unicef na WHO. Ni nani aliwahi kuhoji kuhusu usalama wake? Na kama alihoji,ni hatua ,zipi za Serikali zilichukuliwa kupata mbadala wake? Na je, viongozi wa awamu zilizopita wangeamua kusitisha kuziingiza nchini, nini kingetokea?

Tumesikia kwenye vyombo vya habari kuhusu ligi inayoendelea kuhusu chanjo ya Covid- 19 hasa kwa nchi zetu changa kupanga kuikataa. Kuna taarifa zisizo rasmi kuwa, kwa nchi changa, hofu siyo aina ya chanjo bali ni gharama kubwa za chanjo hiyo. Na yawezekana, ingetolewa kama msaada kama zile za Unicef kwa chanjo za watoto tusingesikia haya yote.

Kama ndiyo hivyo yaani kuogopa gharama,viongozi wetu wanapaswa kufahamu kuwa kipaumbele cha serikali yeyote ile kwa watu wake ni kulinda maisha yao! Kenya na baadhi ya nchi zinazotuzunguka wameshashaagiza au kuweka mipango ya kupata chanjo hiyo. Ni rai yangu kuwa,,nasi tuwe kwenye mstari wa pamoja na jirani zetu.

Na kama ipo agenda inayolenga kufafanua madhara yake,tucampaign kwa pamoja kuikataa. Mwl. Nyerere alipogundua IMF inayumbisha nchi maskini, alihamasisha na kuungana na nchi nyingi kuyakataa masharti ya IMF wakiwemo Nigeria ya kina Sani Abacha w, Zambia ya Mzee Kaunda
nk.

Hiyo approach ilifanya Wenye IMF kutikisika na kuanza kufuta baadhi ya misaada. Naamini hata viongozi wetu wa nchi hizi changa wanapaswa kutumia technique hiyo ya umoja pale wanapogundua kuna genuine reason ya kukataa jambo,na hapohapo wawe na mbadala. Covid-19 au 21 ni janga zito na siyo la kuisha leo wala kesho.

Siyo jambo la afya sana viongozi wa nchi zetu changa kuanza matamko ya kukinzana na juhudi yeyote ya awali ya kukabili tatizo la covid kama chanjo kwa staili ya majukwaa mepesimepesi.
 
Kwanza unahis n msaada, huna uhakika kuwa n msaada

Pili siyo kisa ulikuw unalishwa kinyes ukigundua au kuhis unatakiwa kuendelea kula kisa tuu unakulaga na babu zako walikulaga Sanaa.

Tatu .. Tz saiz imeamka, ukiwa umelala huwez kuwa na adui maana anajua anakuja anachukua anachohitaj maana unakoroma tuu kwenye blanket zitoo na umelewa, ila saiz wapo Watz wapo macho hawatak kulala ili waibiwe, unahis wazungu watachukuaje v2, bila kuwafanya wasinzie, think twice usilete mihemuko ya kisiasa, weka Utanzania mbele
 
Cerelac (food stuff) , yellow fever, measles, ARVs, condoms etc

Lakini wanaoipinga hii chanjo ya COVID sio kwamba hawaitaki kabisa ila wanahoji uharaka wake. Testing & approval processes zimekuwa fasttracked kwa speed ya ajabu na hakuna mwenye uhakika kama hakuna potential long term effects. Harafu zile note kama “not to be used in USA & Canada” zimetisha sana.

Hao wazungu hawasemi kama ukishachanjwa tu then huna haja ya kuvaa barakoa tena na kwamba hutopata tena COVID19

37251355-BF87-47BB-80B8-AB0B588C4002.png
 
Jiwe anatuharibia nchi. Huwa anasema kabla ya kufikiri.

Au anataka tupigike kiafya kama alivyotufanya tupigike kifedha.
 
Kwanza unahis n msaada, huna uhakika kuwa n msaada
Pili siyo kisa ulikuw unalishwa kinyes ukigundua au kuhis unatakiwa kuendelea kula kisa tuu unakulaga na babu zako walikulaga Sanaa.
Tatu .. Tz saiz imeamka, ukiwa umelala huwez kuwa na adui maana anajua anakuja anachukua anachohitaj maana unakoroma tuu kwenye blanket zitoo na umelewa, ila saiz wapo Watz wapo macho hawatak kulala ili waibiwe, unahis wazungu watachukuaje v2, bila kuwafanya wasinzie, think twice usilete mihemuko ya kisiasa, weka Utanzania mbele
Maccm akili mnaweka wapi?/yaani unalinganisha vaccine na kinyeshi? Mwambieni polepole awarudishie ubongo
 
Kwanza unahis n msaada, huna uhakika kuwa n msaada
Pili siyo kisa ulikuw unalishwa kinyes ukigundua au kuhis unatakiwa kuendelea kula kisa tuu unakulaga na babu zako walikulaga Sanaa.
Tatu .. Tz saiz imeamka, ukiwa umelala huwez kuwa na adui maana anajua anakuja anachukua anachohitaj maana unakoroma tuu kwenye blanket zitoo na umelewa, ila saiz wapo Watz wapo macho hawatak kulala ili waibiwe, unahis wazungu watachukuaje v2, bila kuwafanya wasinzie, think twice usilete mihemuko ya kisiasa, weka Utanzania mbele
Well said!
Akili yakuendelea kutegemea wazungu kw kila kitu ni upumbavu. Kwa hao watafiti wanaograduate vyuoni wanasomeaga nini vibofu vya panya. Kwa nini msitafiti chanzo zetu
 
Maccm akili mnaweka wapi?/yaani unalinganisha vaccine na kinyeshi? Mwambieni polepole awarudishie ubongo
Hiyo n lugha ya Sanaa😂😂, bas pole Kama uwezo wa kufikiria n mdgo, nilijua Jf n ya great thinkers kumbe Kuna had vichwa tikiti humu 🙈🙈
 
Well said!
Akili yakuendelea kutegemea wazungu kw kila kitu ni upumbavu. Kwa hao watafiti wanaograduate vyuoni wanasomeaga nini vibofu vya panya. Kwa nini msitafiti chanzo zetu
Saiz wanajitahid at least wameonesha matumain
 
Kwanza unahis n msaada, huna uhakika kuwa n msaada
Pili siyo kisa ulikuw unalishwa kinyes ukigundua au kuhis unatakiwa kuendelea kula kisa tuu unakulaga na babu zako walikulaga Sanaa.
Tatu .. Tz saiz imeamka, ukiwa umelala huwez kuwa na adui maana anajua anakuja anachukua anachohitaj maana unakoroma tuu kwenye blanket zitoo na umelewa, ila saiz wapo Watz wapo macho hawatak kulala ili waibiwe, unahis wazungu watachukuaje v2, bila kuwafanya wasinzie, think twice usilete mihemuko ya kisiasa, weka Utanzania mbele
"Wazungu watachukuaje v2"
Hii kauli ni hopless. Why?
Sababu kwanza sisi wenyewe ndio tunawapa, tunawabatiza majina "wawekezaji" tena private sector ambayo inaongoza kwa kuingizia serikali mapato makubwa ni wao wameishikilia kwa asilimia kubwa.

"Kisa ulikuwa unalishwa kinyesi ukagundua"
Yes ni kweli but bado baadhi ya chajo tunaendelea kuzipokea.
Hii dhana wazungu hivi wazungu vile.. wangeamua tungeshaenda siku nyingi sana.
And still asilimia kubwa ya madawa bado tunachukua kwao.
Vifaa vya mahospitalini tunachukua kwao..
Technologia za mawasiliano.. ulinzi kwao..
Technologia za ujenzi na usafiri kwao..

No offence naipenda nchi yangu. Lakin hizi fikra za kitoto za kusema sijui wazungu hivi.. wakat sisi wenyewe hatuna technologia ambazo zitatufanya tuachike na utegemezi wa technologia zao.
 
Mabeberu wanawivu kwa sababu tupo Uchumi wa kati
Wakiona Midege hewani roho zinawauma sana
Tanzanian ya Magufuli inawaumiza sana maana shule bure
Huduma za afya bure
Nchi hii ni tajiri sana hatuhitaji pesa za mabeberu
 
Cerelac (good stuff) , yellow fever, measles, ARVs, condoms etc

Lakini wanaoipinga hii chanjo ya COVID sio kwamba hawaitaki kabisa ila wanahoji uharaka wake. Testing & approval processes zimekuwa fasttracked kwa speed ya ajabu na hakuna mwenye uhakika kama kuna potential long term effects. Harafu zile note kama “not to be used in USA & Canada” zimetisha sana.

Hao wazungu hawasemi kama ukishachanjwa tu then huna haja ya kuvaa barakoa tena na kwamba hutopata tena COVID19
Ninakubaliana na wewe. Halikathalika tujue fasttracking inatokana na kind of virulence na morbidity ya covid. Death tolls kwa wenzetu wazungu kwa siku zinatisha.
 
"Wazungu watachukuaje v2"
Hii kauli ni hopless. Why?
Sababu kwanza sisi wenyewe ndio tunawapa, tunawabatiza majina "wawekezaji" tena private sector ambayo inaongoza kwa kuingizia serikali mapato makubwa ni wao wameishikilia kwa asilimia kubwa.

"Kisa ulikuwa unalishwa kinyesi ukagundua"
Yes ni kweli but bado baadhi ya chajo tunaendelea kuzipokea.
Hii dhana wazungu hivi wazungu vile.. wangeamua tungeshaenda siku nyingi sana.
And still asilimia kubwa ya madawa bado tunachukua kwao.
Vifaa vya mahospitalini tunachukua kwao..
Technologia za mawasiliano.. ulinzi kwao..
Technologia za ujenzi na usafiri kwao..

No offence naipenda nchi yangu. Lakin hizi fikra za kitoto za kusema sijui wazungu hivi.. wakat sisi wenyewe hatuna technologia ambazo zitatufanya tuachike na utegemezi wa technologia zao.
Yes tunawapatia ss wenyew kwa kusain mikataba huku tumesinzia, unahis mtu kutoka kusain mkataba wa 85%/15 had 50/50 anajisikiaje, anaona tumeamka, halafu chanjo hi ndo itaweza chukua almost Watz wotee, so ukitaka kuharbu generation it is a right time, halafu garama n kubwa, wanahitaj tukope kwao ili watuwekee mishert kibaoo, coz Tz n more than Tsh 100+ trion
 
Kwanza unahis n msaada, huna uhakika kuwa n msaada
Pili siyo kisa ulikuw unalishwa kinyes ukigundua au kuhis unatakiwa kuendelea kula kisa tuu unakulaga na babu zako walikulaga Sanaa.
Tatu .. Tz saiz imeamka, ukiwa umelala huwez kuwa na adui maana anajua anakuja anachukua anachohitaj maana unakoroma tuu kwenye blanket zitoo na umelewa, ila saiz wapo Watz wapo macho hawatak kulala ili waibiwe, unahis wazungu watachukuaje v2, bila kuwafanya wasinzie, think twice usilete mihemuko ya kisiasa, weka Utanzania mbele
Mkuu NATO wakitaka chochote hapa Tanzania wala hawahitaji tulale

Saa nane mchana jua la utosi wakitaka watachukua kila kitu
Tanzanian hatuna silaha za kivita kupambana na NATO kashindwa Gaddafi na Sadam pamoja na maScud yake yote

Hawa mabeberu inatakiwa tuishi nao kwa akili sana
 
Back
Top Bottom