Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 31,913
- 65,514
Acha hype za ukichaa basi🤓😂, we mwenyewe huja wahi fika.Safi kabisa, karibu tena Tanga.
Ukifika nitakupakia kwa daladala ninayopigia debe maana tuna utaratibu mzuri kweli, utafurahia zaidi ya awali.
Wivu na stress zitakuua.Acha hype za ukichaa basi🤓😂, we mwenyewe huja wahi fika.
Ila una Anza kuni karibisha tena 😂🤣
CHAIIjue Tanga Mjini Na Maajabu Yake.
Katika maisha yako jitahidi sana walau siku moja ufike Tanga, utakuja kunishukuru… Haya jionee maajab ya jiji la Tanga
1. Ikifika Saa 3 usiku Hakuna Daladala Utaona Barabarani.
2. Jiji Lina Watu 390K Lakini Ifikapo Saa 4 Huoni Watu Nje Usiulize Kwanini Jiongeze.
3. Ugali Wa 1500 Unapata Mboga 7 Usisahau Uono (Dagaa Mchele) Buree.
4. Tanga Ndio Jiji Pekee Kuna Baiskeli Za Kukodi Yaani Kama Bodaboda Vile Zina Kiti Chenye Sponge Hadi Raha.
5. Club Za Tanga Zinapiga Taarabu Unashangaa Shauri Yako.
6. Self Tanga Ni 50K Chumba Kikubwa Na Choo Ndani Tena Vimenakshiwa Vizuri Kabisa.
7. Wakazi Wa Tanga Hawapandi Boxer,TVS Wanapikipiki Zao Special Zinaitwa "Huoniao" AKA Kibao Mbuzi.
8. Breakfast Ya 1000 Tanga Unashiba Vizuri Kabisa Kifupi Ukila Mchana Kisa Njaa Ujue Una Minyoo Au Ulafi.
9. Ndio Jiji Lisilo Na Kelele Wala Vurugu Pako Kimyaaa Hadi Raha.
Kijana Wa Tanga Akishakuwa Na Uhakika Wa Kula Na Sehemu Ya Kukaa Anawaza Kuongeza Mke Sio Biashara Wala Kuwekeza Hayo Mtajua Wenyewe.
10. Ukitaka Binti Wa Kitanga Aje Geto Mwambie Apande Pikipiki Utamlipa Boda Halafu Akifika Mnunulie Chips Yai Na Soda Broo Umemaliza Kazi.
11. Tanga Ndio Jiji Lenye Soda Au Tuseme Juice Ya Kipekee Inayoitwa "Healtho" Au "Anjari" Ni Tamu Sana Zipo Aina Kama 5 Hivi Huko Bakhresa,Mo,Coca,Pepsi Hata Hawasikiki Sana.
12. Ukiwa Tanga Jaribu Kuishi Na Watu Vizuri Kuoa Na Kuolewa Usipate Shida Wao Ndio Watakutafutia.
13. Raskazone,Donge,Tanga Beach Ndio Ushuani Huko Wanaishi Vigogo AKA Mafogo.
14. Tanga Mjini Kuna Super Market 1 Tu Inaitwa Mkwabi 🤣🤣 (Labda Kama Zimeongezeka)
15. Wasambaa Ndio Kabila Linaloheshimika Zaidi Tanga Mjini Na Ndio Kabila Superior.
16. Kuhusu maji ya kunywa hapo usiseme kule huna haja ya kununua maji dukani maana maji ya bomba tu yanatosha kukata kiu yako kifupi hayana shida kabisa hadi raha.
17. Ukiwa na binti wa kitanga uwe na pumzi ipasavyo usipoangalia utatolewa jasho mwanaume alaa.
18. Tanga Kuna Traffic Light sehemu 2 Tu Pale Toyota Kuelekea Bombo na Maeneo ya Mkwakwani.
19. Tanga hakuna Bolt, Uber Wala Farasi ni Mwendo Wakuita Kibao Mbuzi au Upande Daladala.
2o. Daladala Ipo Radhi Imsubiri Mtu Tena Ikibidi Ipige Reverse Imfwate Alipo.
Sema katika yote Tanga ni jiji lililopangika vizuri kuanzia uswahilini, mjini kati mpaka huko kwa matajiri!!
#VisitTanga
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Wagosi wa tanga mjini wajinga sana[emoji16]
Wanabagua hata wenzao wanaoishi wilayani wanawaita wakuja
Karibu Sana mkuu😂😂Nitakuja unipeleke huko mkuu
Week end hii nikutafute twende au twende zetu kwenye sikukuu ya Idd Baby[emoji3526]na wish mtu anipeleke tanga nipajue [emoji8]
Twende nyerere day honeyWeek end hii nikutafute twende au twende zetu kwenye sikukuu ya Idd Baby
Namba 3 iyo shule inaitwa hegongo hollycross ipo mpaka leoJE WAJUA HAYA KUHUSU TANGA?
1. Reli ya Kwanza Tanzania Bara - Tanga 1893.
2. Shule ya kwanza ya Sekondari- Tanga 1890 (Tanga Old School).
3. Shule ya Kwanza (Anglikana) Tanzania 1848 - Tanga Magila Muheza.
4. Taasisi ya Kwanza ya Utafiti wa Malaria Duniani - Tanga Muheza, Ubwari 1949.
5. Hospitali ya Kwanza (1st Modern Hospital) - Tanga, Cliff Block 1895
6. Hoteli ya Kwanza ya Kisasa Tanzania - Tanga, Kaiserhof Hotel 1906.
7. Upandaji wa Mkonge wa Kwanza Afrika - Tanga, Pangani 1900.
8. Nembo ya Benki Kuu ya Tanzania ni msukumo kutoka kwa Kiwanda cha Mkonge Tanga kwani kilichangia zaidi ya asilimia 60 ya Pato la Taifa.
9. Tanga lilikuwa jiji la kwanza kuwa Manispaa mwaka 1891.
10. Tanga ilikuwa na Soko la kwanza la kisasa nchini Tanzania - 1903 Soko la Uzunguni.
11. Risasi ya kwanza ya Vita Kuu ya Kwanza ya Afrika ilipigwa Tanga - Novemba 1914.
12. Tanga ilikuwa na kanisa la kwanza Tanzania - Magila Msalabani Muheza - 1840s.
13. Tanga ilitoa padre mzaliwa wa kwanza (Mlutheri) nchini Tanzania, Jacob Lumwe (1880 - 1970).
14. Zaidi ya 95% ya Kata za Jiji la Tanga zina maji ya kutosha, hivyo kuwa jiji pekee nchini.
15. Tanga ina mfumo wa maji taka kongwe na unaofanya kazi Afrika Mashariki.
16. Tanga inashikilia rekodi ya jiji lenye mpangilio mzuri zaidi Afrika Mashariki.
17. Tanga inashikilia rekodi ya kuwa na maktaba ya kwanza ya umma nchini Tanzania miaka ya 1950.
18. Tanga ina mtambo wa kwanza wa kufua umeme nchini Tanzania tangu mwaka 1905 huko Muheza Amani.
19. Bandari ya Tanga ndiyo bandari inayohudumu kwa muda mrefu zaidi Afrika Mashariki (Rejelea Mtandao wa Bandari ya Tanga).
20. Tanga ina mnara wa saa kongwe zaidi nchini Tanzania (pengine Afrika) 1901
LA MWISHO KABISA:
Tanga ina KARIBU haina KWAHERI.🤣💕👍✌🏽💋
Mateja ni wengi sana Tanga. Uvutaji wa bangi na madawa ya kulevya unafanyika kwa wingi sana. Jamaa wanakula Mirungi utadhani mbuzi bila kusahau tambuu. Kwa uvivu ndio wenyewe na kila nyumba ina mkeka au kochi au kiti kibarazani.Umesahau, mateja na mashoga.
Hizo hadithi tu mkuu.Vipi ishu za uchawi. Naskia unaweza ukachezewa tu bila kua na tatizo na mtu wala nini
Hahaaaaa kwa njeka ni kweli wanakula mirungi. Tulikuwa tunaangalia mpira huko ni mirungi tu kwa kwenda mbele.Mbona mkokaa na Mirungi sisikii ikitajwa.
Mida hii vijana mitaa ya usagara,kwa njeka wanatafuna majani kama Mbuzi wa Bwana Kheri
Ile hostel sijui nani alishauri ikae city center kabisa. Si Wagalanos tulikuwa tunakimbia mchakamchaka na tunapita hapo kuwatukana tu kwa ajili ya kumunua ugomvi mkawa mnatuogopa. Ila kimsingi tulikuwa tunawaonea wivu.Umenikubusha usagara sec advance,ugali wa kukoboa na maharage unchanganya na uono,mbilimbi chachu na top layer!!aiseh one of my best meals ever!!!
Halafu pale mzimuni ,unacheki madem.wakisubiri daladala Kwa dirishani!!ilikua burudani sana!!wakati.Organic chemistry ikiniumiza pole pole enzi zile!!
Zipo nyingi tu za namna hiyo Tanga.Tanga ni mji ninaoupenda sana. Ukitaka kufaidi jiji la Tanga nenda wakati huu wa Ramadhan. Pale town usiku kama uko uarabuni ni uislamu mtupu. Kilichonikera ni kuna hotel moja iko katikati ya mji kwamba ukienda na demu lazima muonyeshe cheti cha ndoa. Kama sikosei inaitwa Khayrat au jina linalofanania hivyo.
Hahaaaaaaa ni kweli tulikuwa tunawaonea wivu ndio maana siku ya Jumamosi tukikimbia mchakamchaka tunaambiana toka Galanos tupite pale Hostel yenu City Centre tuwatukane tu.Tanga nimesoma usagara pale wale wanangu wa chichi pale club lakassa tume enjoy sana.....enzi hizo boys wa galanos wanatuonea gere watoto wetu wao wapo maporini.
Likizo napanda zangu Ratco. Kweli Tanga raha....
Hahaaaa tulikuwa na wivu mkuu. Mi nimesoma Galanos A Level. Tulikuwa tukizinguliwa na St.Christina hasira zetu tunaenda malizia kwao. Tulikuwa tunaambiana kabisa tupite pale wakati wa mchakamchaka tukawatukane tu hasira zipoe.Nani kasema tulikuwa tunawaonea wivu,watu mnalala barabarani pale hostel[emoji3]
Wapo [emoji12][emoji12][emoji12]sijawahi kuona demu wa kisambaa mwenye chura. ni flat screen kwa kwenda mbele [emoji51]