Kama ilipo Israel siyo Israel, Wayahudi wanaotajwa kwenye Quran na Biblia walikuwa wanaishi wapi?

Hizi hadithi zote inawezekana kupatikana kwenye Quran?
Kila kitu kipo, hayo yoote yapo tena kila walicho pewa na Allah ametuelezea maana ijapokuwa walipewa hiyo adhabu ya kutembea miaka 40 bila ya kufika tena jangwani pakavu kabisa lakini Allah aliwapa chakula na kinywaji pia aka wakinga, Quran imeeleza ili tusije tuka potea
 
Wayahudi ni kabila miongoni mwa watu waliokuwa wanaishi palestina ila siyo hawa wazungu wazungu waliotoka ulaya kisa wanajua kuongea kiebrania.
sasa hao wayahudi unaowazungumzia wewe wanaishi nchi Gani Kwa sasa? kama hawapo twambie waliishia wapi?
 
Kwa hiyo mnawaonea wivu ?
 
Allah hahusiki na wayahudi bali waarabu tu
 
Utapigwa fixes za kutosha kwa hayo maswali.Bado utaambiwa hao waizraeli waliopo leo siyo wenyewe.Hao ni "ashkenaz" tu.Utachanganywa hadi uimbe "Ndiyena ndiyena"!
 
Waliishi Israel, Palestina, Syria, Lebanon, Jordan na Misri.
 
Ugomvi uliopo ni wa kidini. Sio wayahud na waarabu. Waislam wanajua lile eneo ni la wayahud ila wakikubali inamaanisha ule msikiti utabid uvunjwe lijengwe hekalu. Lakin wanajua lile eneo walipewa jews
 
Kama nimekuelewa vizuri ni kwamba, hata wewe una amini kwamba pale ndio kwao ila hupenzwi tu na tabia zao za kibinafsi, right?
 
Sasa hivi. Wanakwambia hawa wa sasa sio jews ni wazungu .. wanasema Jews wenyewe hawapo tena.
 
Ugomvi uliopo ni wa kidini. Sio wayahud na waarabu. Waislam wanajua lile eneo ni la wayahud ila wakikubali inamaanisha ule msikiti utabid uvunjwe lijengwe hekalu. Lakin wanajua lile eneo walipewa jews
Acheni ujinga,uwezi kusumbua watu kwa kisingizio Cha eti kudai eneo lako kwa kutumia ushahidi wa stori za miaka elf2 iliyopita. Miaka elfu2 wewe unawajua walioishi hapo unapojivunia kua ni kwako? Je akijitokeza Leo na yeye akatumia ushahidi wa miaka 2000 iliyopita kupadai hapo unapoishi wewe utamwelewa? Wewe unawajua waliokua wanaushi USA miaka 2000iliyopita? Wakijitokeza kupadai kwa kutumia ushahidi huwohuwo wa miaka zaidi ya 2000 iliyopita kama wanavyofanya hao mayahudi,we unafikili wale wanaoishi sasa pale USA watawaelewa watu hao? Au hata wewe tu ukiwasikia watu hao utawaelewa na utawasaport kama munavyofanya kwa hawa wayahudi Leo?
 
Wayahudi hawajawahi ondoka israel,kilichofanyika nibaada ya wengi wao kutawanyika kukimbilia uhamishoni,kuamua kurejea na kuunda upya taifa lao kwa kushirikiana na wale wachache waliobakia,kasome kuhusu zionist movement utaelewa.
 
Ukiacha wayahud waliotokea ulaya palikuwepo wayahud asilia hapo chief. Sio kwamba waliokuja ndio pekee waliodai eneo lao.
 
Wenyewe wana ndoto yao inaitwa "GREATER ISRAEL ".
●GREATER ISRAEL itazichukua hadi Syria +iraq+Lebanon hadi kuja kupakana na Turkey.
●Huku wakiichukua Gaza yote +Westbank hadi sinai peninsula.
●Hiyo GREATER ISRAEL inayosemwa naona kama ni myths maana jirani anaotarajia kuwa conquer ni most enemies.
 
Ao wapo apo kitambo sana na wanajuana na mpaka waarabu wanawatambua vizuri wazayuni.
Isipokuwa wamechukuliwa utumwani mara kadhaa na wakarudi
 
Ao wapo apo kitambo sana na wanajuana na mpaka waarabu wanawatambua vizuri wazayuni.
Isipokuwa wamechukuliwa utumwani mara kadhaa na wakarudi
Hujajibu swali ndugu yangu.

Tukubaliane kwamba Taifa la Israel ya Sasa, Lilianzishwa mwaka 1948. Kabla ya hapo hakukuwa na Taifa la Israel ya Sasa.

Sasa kabla ya mwaka 1948, Waisraeli wanaotajwa kwenye Biblia na Quran walikuwa wanaishi wapi?

Isije kuwa Waisraeli wa zama hizo za Biblia na Quran ni wamakonde wa Leo!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…