Kuna hoja ipo kuwa pale ilipo Israel kwa Sasa si Ardhi ya waisrael bali wapalestina.
Binafsi nakubaliana na hoja hiyo. Lakini swali la kujiuliza ni kwamba, kama ilipo Israel kwa Sasa siyo nchi ya waisrael, jee pale Mashariki ya kati, waisrael wanastahili kuwepo kwenye nchi Gani?
Quran na Biblia zina hadithi kuhusu wayahudi. Hao wayahudi wanaotajwa kwenye Quran na Biblia, zama hizo walikuwa wanaishi kwenye nchi gani ambayo kwa sasa haipo?
Kwao ni maeneo yote wanayoishi sasa pamoja na maeneo ya Westbank, Gollan heights waliyoikalia kimabavu, maeneo ya kusini mwa Lebanon, Gaza na maeneo ya Sinai Misri ukigoogle utaona.
Kusema walipo si kwao ni maneno ya kisiasa tu.
Ukisoma 'the history of Israel' katika wikipedia ama google utaona mtawala wa mwisho katika ufalme wa Israel alikuwa ni nani na baadaye kufuatia tawala za mataifa mbalimbali yakiwemo Assirians, Romans, Shirazzi, Egypty hadi Ottoman empare nk nk.
Katika tawala zote hizo ziliwakandamiza sana, kuwahamisha kwa nguvu katika maeneo yao pamoja na kuchukuliwa mateka na wengine kutawanyika katika mataifa mbali mbali ya Ulaya, Marekani, Asia, Africa na kwingineko duniani.
Uyahudi ni kabila, dini na utamaduni vilivyofungamana, hivyo popote walipoenda walitambulika hivyo.
Kwa utambulisho huo, ndiyomaana walivyopata uhuru wengi wao waliamua kurudi kwao.
Historia ni ndefu kidogo ni vizuri ukatafuta vyanzo ukasoma mwenyewe utaelewa vizuri zaidi.