Noti bandia
JF-Expert Member
- May 3, 2020
- 2,684
- 4,315
Kwa hiyo unaamini kabisa Waziri wa Ardhi Ridhwani Kikwete yuko kwa ajili ya na ana uwezo wa kusimamia mipango miji ?
Kwani uongo?Madarasa elfu 12 kwa miezi mitatu.
Huu ni uongo.
Viwanda vilianza kujengwa kipindi cha magufuli? Vingapi?1. Tanzania ya viwanda
2. Nchi kujitegemea
3. Miundombinu ya kuunganisha nchi
4. Umeme nafuu ila usaidie uzalishaji mpaka kwa mtanzania wa hali ya chini
5. Na mengine mengi
Umesema Kweli kabisaKinachonisikitisha ni maeneo mapya ya ujenzi kuendelea kujengwa kihilela miaka hii. Tuanzie hapa tulipo kwa maeneo mapya yote yajengwe kisasa. Tukitaka kufanikiwa tuwe na mipango alafu wajinga wachache wasiojali ni kuvunja tu nyumba kadhaa kama JPM alivyofanya hapo kimara mbezi tuone kama watu hawatabadilika
Asante sana ndugu! Watu wengi sana tumeliongelea sana hili jambo humu! Ni wakati sasa kwa serikali kulifanyia kazi kwa kulipa kipaumbele maalum!Naungana na mtoa hoja. Hili Jambo nilikwisha liongelea siku moja humu jukwaani. Pitia hiyo link hapo juu.Uzi maalum kwako waziri Lukuvi na watendaji wa Wizara ya Ardhi kwa ujumla
Kwanza kabisa napenda nikupongeze kwa juhudi zako za kutatua migogoro ya ardhi nchini. Pamoja na pongezi hizo, naomba utilie mkazo suala la upimaji ardhi kwa nchi nzima, na udhibiti wa makazi holela. Niseme tu wazi kuwa ujenzi holela na mpangilio mbovu wa makazi katika miji yote nchini ni...www.jamiiforums.com
Nilishatoa wazu siku nyingi kwamba Serikali ianzishe wakala wa kujitegemea kwa ajili ya kuratibu matumizi ya ardhi na mipango miji na wawe na pesa zao ndio tutapata suluhisho.Nilichojifunza hapa Tanzania, ukidhamiria kufanya jambo fulani, ukalipa jitihada za kutosha na fedha , lazima jambo hilo lifanikiwe.
Kwenye moja ya sehemu ambayo kwa macho yangu nimeshuhudia hilo ni ujenzi wa madarasa zaidi ya 12,000 tena kwa viwango vizuri sana uliofanyika kipindi hiki cha Awamu ya Sita. Ndani ya miezi 3 tu, taifa limeshuhudia operesheni yenye mafanikio zaidi ya asilimia 95 ya ujenzi wa madaraka kwa ajiri ya watoto wetu kwenye viwango vya juu kabisa vya ubora!
Moja ya maeneo ambayo kwa Awamu zote 5 za nyuma Taifa hili tumekwama ni suala la kupima na kupanga miji na maeneo yetu
Jambo hili limekuwa likifanya Taifa letu kuonekana la hovyo kutokana na watu kujilimia na kujenga hovyo kila kukicha!
Leo hii ukitoka Manyara kwenda Arusha maeneo ya Tarangire unashuhudia ujenzi holela wa nyumba hadi kwenye eneo ambalo ndo yalikuwa mapito ya wanyama. Kilimo pia kinafanyika kwa kasi kwenye maeneo haya.
Leo hii ukienda Mwanza, Iringa, Mbeya, Kilimanjaro, Songwe, Tanga, Dar es Salaam, Morogoro na mikoa mingi unaona Jinsi watu wanavyozidi kujenga kila siku bila mpangilio, Wengine wanajenga hadi maeneo ya hifadhi jambo litakaloleta hatari kubwa sana huko mbeleni maana kwa Jinsi watu wanavyozidi kuongezeka Tanzania, itafika wakati Taifa zima litakuwa squatters
Naomba serikali ya Awamu ya 6 ijiondoe kwenye dhambi hii! Watanzania wa sasa wana uwezo wa kujenga nyumba Nzuri tena sana na hili limeonekana hadi maeneo ya Dodoma yaliyopangwa na kupimwa vizuri. Kinachotakiwa kufanyika kuanzia sasa ni Serikali kuweka nguvu kubwa sana kwenye kupima na kuyapanga, maeneo yote na miji yote ya nchi hii na Kuhakikisha kila sehemu inaendelezwa na kulimwa kimpangilio.
Hakuna gharama kwenye kupima na kupanga miji yetu na Tanzania nzuri Kama Dubai , Texas, New York inawezekana
Naomba kuwasilisha!
Huu ni ujinga mwingine,kwamba kwa sasa mafundi ni wachache na wanatusua Sana sio?Veta KILA kata ndio mkombozi wa tatizo la ajira nchini
Kweli kabisa! Nimejaribu kufuatilia humu if watu wengi sana wameandika sana kuhusu serikali kujikita rasmi kwenye suala la mipango miji. Ni wakati sasa serikali kufanyia kazi Masuala hayaNilishatoa wazu siku nyingi kwamba Serikali ianzishe wakala wa kujitegemea kwa ajili ya kuratibu matumizi ya ardhi na mipango miji na wawe na pesa zao ndio tutapata suluhisho.
Humu jukwaani hakuna viongozi wa serikali au?Kweli kabisa! Nimejaribu kufuatilia humu if watu wengi sana wameandika sana kuhusu serikali kujikita rasmi kwenye suala la mipango miji. Ni wakati sasa serikali kufanyia kazi Masuala haya
Kuna hii nyingine niliikuta!
Niko njiani natoka Mwanza naenda Dar, nchi tusiposhituka miji yote Tanzania itakuwa kama Tandale
Hamna mipango watu wanajenga jenga hovyo tu bila mpangilio, huu ni uzembe na utaigharimu nchi miaka mingi ijayowww.jamiiforums.com
Wapo wengi sana! Nashindwa kuelewa kigugumizi kwenye hili kinatoka wapi?Humu jukwaani hakuna viongozi wa serikali au?
Vijana ni masikini sababu hawana ujuzi,lengo la veta ni kuwapa ujuzi kupitia ujuzi wataziona fursa.Shida sio tatizo la ajira shida ni uelewa Mdogo kuhusu fursa zinazokuzunguka.Tafsiri ya nenoHuu ni ujinga mwingine,kwamba kwa sasa mafundi ni wachache na wanatusua Sana sio?
We bwana wee,soko la ajira ni kama tuu soko la bidhaa zingine,more supply less demand.Vijana ni masikini sababu hawana ujuzi,lengo la veta ni kuwapa ujuzi kupitia ujuzi wataziona fursa.Shida sio tatizo la ajira shida ni uelewa Mdogo kuhusu fursa zinazokuzunguka.Tafsiri ya neno
Umasikini ni ukosefu wa mbinu ya kuchukua pesa toka kwa watu. Watu wanazo pesa unazichukuaje sasa Ili zije kwako, hio ndio inaitwa skills, wape bidhaa, wape huduma, wape connection, nk wao watakupa pesa umasikini kwako utatoweka kupitia ujasiliamali.
Unakuwa masikini sababu umekosa mbinu za kuchukua pesa toka kwa watu,
Ina maana watu awali,awanywi,wameacha kuvaa,awanunui sukari,chumvi, sabuni,mafuta, mboga,matofali,mkaa,mafuta ya kula,nk hizi zote ni fursa kwa vijana ndo maana ya VETA kutoa ujuzi wa uzalishaji.We bwana wee,soko la ajira ni kama tuu soko la bidhaa zingine,more supply less demand.
Saizi tuu huko mitaani hao hao vijana wachache waliopo wanafanya wanachofanya lakini demand ni ndogo.
Tukienda unavyosema itafika tuu mahali inakuwa kama sasa ambavyo degree ziko kibao Kazi hakuna.
Kila kitu kiwe regulated ndio kitaleta maana.
Hawajali hili kwa Sasa, ila baadae zikianza lawama za wanyama kuvamia raia wa hapo ndio utasikia hao raia wamejenga kwenye mapito ya wanyama hivyo wavunjiwe.Leo hii ukitoka Manyara kwenda Arusha maeneo ya Tarangire unashuhudia ujenzi holela wa nyumba hadi kwenye eneo ambalo ndo yalikuwa mapito ya wanyama. Kilimo pia kinafanyika kwa kasi kwenye maeneo haya.