Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Hawatakuelewa, watu wako bize kummezea mate mlegeza macho kwa udini. Wanapiga nae pambio mnafiki namba moja wa taifa, limbukeni wa madaraka mkojoa kwa kukaa yule. Bullshit.
Mkojoa kwa kukaa Yule [emoji850]SAWA
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Msome vizuri CAG bila hasira. Hajasema hakuna kilichofanyika, wala hajasema kuna uchafu pote. Tena kasema zaidi ya 80% ya taasisi zina hati safi! Lakini zilizobaki ndizo chafu au zenue mashaka. Bahati mbaya ni kuwa hata miradi yetu kipenzi mingine ina kasoro, ikiwemo shirika la ndege. Sisi wengine tulijua toka mwanzo kuwa ndege hazitatengeneza faida. Ni mashirika machache sana ya ndege yanayotengeneza faida. Kwetu ndiyo kabisa, maana wasafiri na viwanja vyetu vya ndani havitoshi kwa ndege zile, Nje si rahisi kwenda au kushindana, na lilipoongezeka zuio la usafiri kutokana na korona tukaisha kabisa! Ilitakiwa tuambiwe ukweli tu, tungeshazoea. Tulizoea kusifu pasipo sifa, tukiambiwa ukweli huo sasa tunakaidi tu kuupokea.
 
Magufuli alikuwa waziri kwa miaka mingapi kabla ya kuwa Raisi? Mbona hakujuuzulu kwa ufisadi uliofanyika akiwa waziri na badala yake akasubiri awe Raisi na kuanza kushambulia ufisadi uliopita huku akificha kwa mtutu wa bunduki ufisadi wa serikali ambayo yeye ni Raisi.
Tunasafari ndefu sana tena sana
 
Ukisoma mitandao ya kijamii hasa twitter utafikiri kweli hii nchi imeibiwa kila kitu na hakuna kitu kimeachwa, kumbe sio kweli.

Watu wanajifanya kushangaa ATCL kupata hasara, hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kushangaa atcl kupata hasara? By the way, ni shirika gani la serikali linalopata faida? Lipi? Mashirika yote ni hasara kila mwaka kuanzia Tanesco, TPDC, TTCL, ATCL, NHC na mengine yote, kwa nini shida iwe kwa ATCL?

Halafu watu wanataka kusema Magufuli ange eliminate rushwa ama wizi wa mali za umma 100%, hilo jambo halipo Duniani. Duniani kote, kuanzia China ambapo kosa la rushwa unaweza kuuwawa ama Marekani ambapo mifumo iko strong bado watu wanaiba na kula rushwa, tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag
Na hii ndio shida yenu mnaona waTZ wajinga sana..... Eti kikundi kimelipwa? Kwamba hakuna mtu mwenye uwezo wa kukosoa au kufikiri mpaka alipwe? Hvi CCM mnajiona mnamiliki mawazo yetu kisa propaganda zenu.

1. JPM 2019 alidai ATCL imeingiza mabillion hadi ikatoa gawio sasa leo watu wakiona hasara miaka 5 yote wasicharuke

2. SGR haikukaguliwa sasa leo imegundulika ndani ya 35% za pesa iliyolipwa ilitumia infkated exchange rate na haikua ya siku ya malipo wala ya BOT. Rate ya benki za kibiashara. Sasa hya tungejua bila CAG?

3. Tunaambiwa SGR wafanyakazi wa kigeni hawakuwa na vibali hivyo kukosesha nchi mabillion ya fedha. Furthermore interest rate ilikua inakua kubwa kutokana na fedha kucheleweshwa makusudi.

4. Nyerere Dam ilitumia feasibility/EIA ya mwaka 70 na 80 ila haikufanyila harmonisation kwa standards na sheria za Tanzania za sasa ikiwemo sustainability ya flow ya maji kwa miaka tajwa. Haya yangejulikana lini kama sio CAG kutufungu macho?

5. TGFA iliwahi kukaguliwa? Imegundulika na wao ni liability na hakuna mwenye utaalam na uzoefu kwenye aviation industry. Hya tungeyajua bila CAG?

Kilicho pelekea haya yote ni TRANSPARENCY kutoweka. Kama mambo yangekuwa wazi unadhani kuna mtu angeshtuka? so sad Mzee Mwanakijiji nao wanageuka conspiracy theorists wkt facts zipo mezani
 
uwizi upi? makusanyo Tandahimba stand ambayo hayakupelekwa bank inakuwaje kosa la JPM!!!

haya JPM kaondoka, kaacha serikali yake sio? aliyemtua CAG si ni huyo huyo JPM!!

aisee
Ile trillion 1.5 iliyoliwa na Magufuli na CAG Prof Assad aliiandika kwenye ripot iko wapi
 
Mkuu serikalini ukishafanya matumizi ya fedha bila kufuata taratibu za manunuzi zilizopo kisheria, huo ni mwanya mkubwa wa upigaji. Ukisoma Ripoti ya CAG upotevu mkubwa wa fedha za umma umetokana na mwanya huo.
Hakuna Tender, hakuna Tender evaluation, Contract negotiations hakuna, Contracts hakuna, certificate hakuna wala risiti. Ni maagizo tu, matokeo yake ukiagiza watoe bilioni moja wao wanatoa bilioni 3.
Au unakuta client pia ni consultant na pengine pia ni contractor pia, kwa tu ni taasisi ya serikali.
Pamoja na urasimu hizi taratibu za kibajeti na manunuzi zinasaidia sana kudhibiti ubadhirifu.
KAZI IENDELEE-NENO HILI UKILITAZAMA KWA JICHO LA 3 NI NENO PANA SANA
IMG-20210408-WA0100.jpg
 
Jf ni great thinkers kweli au baadhi wanaendeshwa na midundo ya ngoma?
Mtu anauliza angewepo Magu report hii angekabidhiwa?
Ishu hapa siyo kukabidhiwa au la bali je report ya CAG ni sahihi na kama ya kupika hizo ofisi zijitokeze kujitetea.
Ifike wakati tukubali kuwa kuna watu walishindwa kuzungumza kwa kuwa:-

1.Hofu ya kupoteza kazi zao.

2.Kuawa au kuwekwa vilema vya maisha.

3.Kupoteza urafiki au undugu na

4.Kupigwa nyundo za uhujumu uchumi,kufungiwa biashara zao au kupotezewa uraia.

Mwisho tukubali kuwa Magufuli alifanya mazuri mengi tu lakini pia alikosea mengi pia ila vyombo vya habari vilimbeba.
 
Kwangu mimi ukimlinganisha mkapa , kikwete na Magufuli bado Magufuli ni best ever na amewaacha mbali hao Marais wengine, Rais anatoa dira na kuanzisha miradi yenye kuliletea faida taifa, katika miradi hiyo kuna chain ndefu ya usimamizi, Rais peke yake hawezi maliza tatizo za rushwa ni lazima team yote uhusike na I we na dira moja katika kupambana na rushwa, kwani Magufuli ni mara ngapi ana msema Jacob kuwa halimashauri bado kuna wizi? mara ngapi kaenda bandari kufufua madudu? ni Magufuli huyo huyo ndie alie zuia ndege isiende nje kupakwa rangi, shida iliyopo Tz ni watu tuna hulka ya wizi na kuoneana huruma, Rais akiwatumbua sisi wananchi tulalamika na kusema Rais anaonea ni mbaguzi, hivyo wezi kupata support na huruma ya wananchi, Magufuli kapigana sana na ufisadi a uwajibikaji kushinda awamu zote zilizopita, tulimuita majina yote mabaya akipigana na ufisadi roho mbaya, tengua tengua , ana pendelea, mkabila hii aina ya kulia lia watanzania we have stop kama tuko serious na nchi.

Na kipindi cha Magufuli tundio tumeona miradi ya maana na yenye pesa mingi , chukulia tu miradi ya kikwete terminal 3 na mwendo kasi phase 1 , udom, mloganzila hizo ni just one project of Magufuli ya upanuzi wa bandari ya Dar ambayo Imegharimu trillion 1.2, hapo hujagusa tril 1.2 miradi ya maji, Radar nne katika airports zetu , anga letu lilikuwa ni giza, sasa miradi kama ya maji kama wizara husika aifuatilii kwa karibu lazima ufisadi utakuwepo tu.
 
Yani we jamaa ni kama mchawi aliyekutwa na ungo uchi wa mnyama katikati ya uwanja wa shule za Kayumba.

Ndo hali yako sa hiz.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!

Mkuu labda kwa kukusaidia na kwa akili ya kawaida tu

Kama wengine wanavyoita ‘Mwendazake’ ( Nafikiri sio neno la kubeza) alijaribu sana kuonyesha mafanikio ya serikali yake (na ambacho sio kitu kibaya) na kuna muda mpaka aliponda tawala zilizopita kwamba zilikuwa wapi kuona mauchafu yote yale aliyoyaona yeye

Ubaya unakuja ni kudhibiti kabisa vyanzo vyovyote vya taarifa kuhusu mapungufu ya serikali yake ukiachia mbali mikutano yake akiwa na msafara kusimamisha watu ili awatatulie shida zao ( ni kujiimarisha kisiasa zaidi hapa) lkn hakukuwa na njia rasmi kama vyombo vya habari / bunge au hata ripoti ya uwazi kama hizi kutoka kwa CAG kuonyesha matatizo ya uongozi na uadilifu (Rushwa, wizi) kwenye ofisi za umma

Hakuna ripoti yoyote itakayo kuja kuwa safi sana ktk awamu hii na zilizopita na zitakazo kuja sema tofauti moja ya msingi kuna awamu wananchi/watu walikuwa wanajua wanapigwa ( hata kama hawana namna) maana taarifa zilikuwa zinatoka hata kabla ya ripoti maalumu ya CAG kutoka na vyanzo ni kuanzia bungeni, vyombo vya habari lkn kwa kama mnavyomwita Mwendazake hakukuwa na taarifa zozote zaidi ya anazotaka/zinazotakiwa kutoka na hapa ndo tofauti ipo kubwa na inafanya watu wawe na hamasa kutoa maoni yao hasi au chanya kwa ripoti hii ya CAG baada ya so called Mwendazake kwenda

Na hili ndo limefanya ripoti hii iwe na msisimko maana kuna dhana ilijengwa kwamba utawala ni msafi na msimamizi yupo makini lkn kwa ujumla sio issue ya mtu mmoja tu hii kubwa kama jamii tunatakiwa tuanze kuona kwamba wizi, rushwa ni tabia mbaya kutoka mioyoni kwetu sio kwa sababu mtu mmoja na kwa kipindi kifupi tu katuaminisha kwamba tabia zetu hizi mbaya kama jamii eti zimekwisha/ zilikwisha
 
Umeandika kitu hapa, ninavyofahamu madudu ya ofisi za huko serikalini huwa yapo kila awamu, japo sasa tunaaminishwa yamezidi kwa awamu iliyopita, ningedhani pia kwa uelewa wangu wapinzani sasa waje na solution nini cha kufanya ili kuepuka hiyo situation mbele ya safari, badala yake naona wapinzani wameungana na lile kundi jingine la CCM kumshambulia mwendazake, hapa mwenye akili timamu lazima ujiulize, hawa wapinzani wa sampuli hii lengo lao ni nini hasa?

Wamejisahau wanamshangilia huyu mama tokea aingie ikulu, hata madudu yake yaliyotokea hivi karibuni bado hawajayaona, wao ni kushangilia tu kwa hali hii kwanini tusiendelee kutawaliwa na CCM miaka yote? hii ni kwasababu watu wameacha kufuata akili zao wanafuata za viongozi wao wa mitandaoni ndio maana.

CCM ni wale wale, kulindana kuko pale pale lakini watu wanashangilia tu kwa ufupi wa kumbukumbu zao, baada ya siku kadhaa akili zitawarudia waanze kulia tena, just a matter of time.
Wapinzani wanahusika vp na ripot ya CAG? Mbona mnashindwa kuficha ujinga wenu?
 
Upinzani uko kwenye damu yangu; ila sasa hivi naona kama umepotea maana sijui ni nani amebakia upinzani kweli. Labda tuunde upya kabisa... maana upinzani umekubali jukumu lisilo lao...
Huna upinzani wowote. Hakuna. Wewe opportunist kama hao wengine. Mpinzani hayumbi hivyo uyumbavyo. Consistency hukujaliwa. Flexibility hata kwa mpinzani ipo. Ndio inayoonekana leo na ukasema upinzani umepotea. Jema halipingwi. Kipingwacho ni njia ya kulipata. Kodi ni njema. Ya mabavu hapana. Wenzetu wana vijitabu vya kodi. Kitu, bidhaa na huduma ipi inalipiwa kodi. Formula ni wazi kwa kila kilipiwacho. Unatoka nyumbani na kiasi sahihi cha kulipa. Hakuna mizengwe. Compliance iko juu sana. CAG naye anatufahamisha kodi yetu ilivyotumika kwa usahihi. Sio hayo mambo yako ya kishamba ya kutia shaka ripoti ya CAG.
CAG anakagua na kudhibiti tu mapato na na matumizi ya serkali. Kuna mwenye serkali. CAG sio mhimili. Hata baada ya mwaka mmoja waweza tumbuliwa. Maneno ya busara na hekima yaliyomkaribisha CAG. Mtangulizi wake hakutakiwa na serkali hata na spika aliyemtuma kukagua. Trln 1.5 zikazaa jambo!
 
Hawatakuelewa, watu wako bize kummezea mate mlegeza macho kwa udini. Wanapiga nae pambio mnafiki namba moja wa taifa, limbukeni wa madaraka mkojoa kwa kukaa yule. Bullshit.
kwani wewe mama yako mzazi huwa anasimamaga wakt wakukojoa?

huyo ambaye siyo mnafik na mzalendo, CAG anasemaje juu ya utawala wake?
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Mkuu kama kujiuzuru si Majaliwa tu hata aliyekuwa makamu wa raisi,wote walikuwa ni timu moja huwezi ukasema sili nyama bali nakunywa mchuzi wa nyama na kwa mpango hata wa kule Zanzibar nae ajiuzuru si ndio wote walikuwa wakisema HAPA KAZI TU hadi akina Ndugai nao waondoke. Hakika nimejifunza kwamba Watanzania si watu wa kuwaamini,kama viongozi wanakuwa vigeugeu namna hii sijui mwananchi wa kawaida hali ikoje kwa maana haelewi kama kweli awaamini viongozi waliopo madarakani au asiwaamini.
 
Ni note kitu kwamba ufisadi kama huu ungelikuwa unafanyika tokea kipindi cha Mkapa hadi JK basi Tanzania ingekuwa mbali sana.
 
Umezungumza jambo zuri sana. Changamoto ni hii, je mfumo huu wa kulindana unaweza kuacha nafasi ya Taifa kupata mtu mwenye sifa ulizoziainisha?
Kwa sasa sidhani kama kuna mfumo unaoweza kutusaidia kumpata kiongozi wa sifa nilizoziainisha. Sidhani kama inawezekana, hata kwa nchi zenye mifumo imara ya uchaguzi, kama Marekani, kumpata kiongozi mwenye haiba fulani consistently. Ndio maana hata wao wanaweza kumuibua Obama awamu fulani, na kumuibua Trump awamu nyingine. Kitu kinachowezekanika kabisa ni kuweka malengo ya nini tunataka kiongozi afanye katika awamu yake ya uongozi, na kufanikiwa au kufeli kwake tumpime kwa malengo hayo. Style yake ya kufikia hayo malengo kama nalo ni miongoni mwa malengo tuliyoyaweka, basi tumwambie in advance. Kama kumbukumbu zangu zipo sawa hivyo ndivyo namna tulivyofanikiwa kumpata JPM. Wananchi tulichoka na ufisadi na uzembe uliokithiri hadi sauti zikasikika, hadi kutoka upinzani, za tunamtaka rais dikteta asiyetizama sura ya mtu.
 
Back
Top Bottom