Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

NA BUNGE LIVUNJWE TURUDI KWENYE UCHAGUZI.
KWA TUME ILE ILE YA UCHAGUZI?
IMG-20210409-WA0000.jpg
 
Unaandika mithili ya layman. Kwani kuwa mpinzani lazima ujinasibishe na wapinzani unaowaita wamepotea?

Wewe binafsi ume compromise nafsi yako kwakua wengine wamepotea? Really?

Hivi misimamo na ideology za mtu huwa kwa wengine au wewe binafsi?

Kwahiyo huko nyuma ulifanya upinzani kwakua wengine walifanya?

Au kauli na matendo yako yanadhihirisha ulifanya mambo kwa chuki binafsi, chuki za kimaslahi, kikanda, kidini na kirangi? Seriously mtu mwenye upinzani wa Moyoni unaweza sema nilishindwa fanya upinzani maana sikumjua mpinzani wa kweli?

Seriously mtu wa kariba yako ulikuja kuwa simply brainwashed na siasa za watu aina ya akina Magufuli really?

Kunywa chochote hapo kwa Mangi nakuja kulipa! Huyu mzee nilimuovarate huko nyuma, sikujua kama ni kiazi kwa kiwango hiki. Mahaba niue yake kwa Magufuli yamemshusha kiwango vibaya sana.
 
Ukisoma mitandao ya kijamii hasa twitter utafikiri kweli hii nchi imeibiwa kila kitu na hakuna kitu kimeachwa, kumbe sio kweli.

Watu wanajifanya kushangaa ATCL kupata hasara, hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kushangaa atcl kupata hasara? By the way, ni shirika gani la serikali linalopata faida? Lipi? Mashirika yote ni hasara kila mwaka kuanzia Tanesco, TPDC, TTCL, ATCL, NHC na mengine yote, kwa nini shida iwe kwa ATCL?

Halafu watu wanataka kusema Magufuli ange eliminate rushwa ama wizi wa mali za umma 100%, hilo jambo halipo Duniani. Duniani kote, kuanzia China ambapo kosa la rushwa unaweza kuuwawa ama Marekani ambapo mifumo iko strong bado watu wanaiba na kula rushwa, tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag
Kama leo unaona sio ajabu kwa ATCL kupata hasara.. mbona miaka yote hatukuambiwa. Na kwanini mwaka jana walidanganya wamepata faida na wakatoa gawio kwa serikali la B 23? Kwanini Magu alikuwa anaongopa? Kwanini ofisi ya CAG ilipunguziwa bajeti yake ili isifanye kazi ya kuchimba madudu na Profesa Assad akafukuzwa?
 
Kama Mheshimiwa Magufuli kaacha jeshi kubwa nyuma, basi jeshi hilo linapaswa lipokee ripoti ya CAG inayobainisha mapungufu makubwa katika matumizi ya pesa za Umma na kuyafanyia kazi ili kuendeleza legacy ya JPM na Serikali yake.

Nimesema kwamba kufanya miradi ya maendeleo hakumpi Kiongozi yeyote haki ya kufanya ama kuruhusu ufisadi. Mheshimiwa Magufuli kaacha alama 4 kubwa katika maendeleo ya Taifa hili, hilo halina ubishi, lkn hii haiondoi ukweli kwamba kuna wizi mkubwa umefanyika katika awamu yake lkn alizuia umma usiambiwe.

Kuikosoa taarifa ya ukaguzi uliofanywa na CAG ni ujinga mkubwa.

Ni aibu kujiita Mzalendo huku unatetea wizi wa mali ya Umma.
Nguvu kubwa mnayotumia kufuta legacy ya JPM ina ajenda nyuma yake na tumeshawastukia. Kama mna lengo jema, na nia yenu si ovu, si muiwajibishe serikali ya JPM kuanzia waziri mkuu wake, makamu wake wa rais, mawaziri na watendaji wake wote? Mbona bado wapo wapo serikalini? Ni uhuni tu, na bado muendelee kusisitizwa, JPM kaacha jeshi kubwa nyuma. Furaha yenu ni ya muda tu.
 
CAG ni kiongozi wa idara ambaye ana technical team, vijana wake wamefanya kazi wanayopaswa ! Labda niulize tunadhani CAG anaweza kuandika vitu ambavyo havipo kwa faida ya nani?
Wana sukuma gang wanachohitaji ni REPORT INAYO MSIFIA MWENDAZAKE KUWA HAJAWAHI KUONEKANA KIONGOZI KAMA YEYE.
 
Tatizo hii nchi yetu Bado inasumbuliwa na ukosefu wa VIONGOZI/WATENDAJI WAADILIFU.

lakini pia kuna udhaifu Mkubwa kwa viongozi wetu walio pewa dhamana ya kusimamia walio chini yao. haya ni matokeo ya usimamizi mbovu matokeo yake ni ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi.

Nitashangaa sana kama hatua hazito chukuliwa kwa viongozi wa taasisi au idara zilizo hushishwa na ubadhirifu kwa namna moja au nyingine.

NASISIYIZA HATUA KALI ZIVHUKULIWE KWA WOTE ILI IWE FUNDISHO KWA WENGINE.
Bila katiba mpya hakuna kitu utamwajibishaje mwizi ingali wanajua mfumo wao wa kuiba ukoje na njia zake

Kuiba pesa za uma ni mfumo uliopo juu mpaka chini sasa nani wa kumfunga paka kengele ?

-Ukichunguza utajua hii aliyeiba kwenye shirika ameoa kwenye ukoo wa ndugai

Hapo unaanzaje kumkamata mwizi?
 
Binafsi huyu CAG simuamini kamwe.
Usipomuamini CAG utakuwa unafanya makosa makubwa sana. CAG yuko sahihi na ana nia njema sana, lakini pia Hayati JPM naye alikuwa yuko sahihi na akiwa na nia njema sana vile vile, isipokuwa baadhi ya wasaidizi wa JPM ndiyo hawakuwa sahihi na hawakuwa na nia njema!
 
Ukisoma mitandao ya kijamii hasa twitter utafikiri kweli hii nchi imeibiwa kila kitu na hakuna kitu kimeachwa, kumbe sio kweli.

Watu wanajifanya kushangaa ATCL kupata hasara, hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kushangaa atcl kupata hasara? By the way, ni shirika gani la serikali linalopata faida? Lipi? Mashirika yote ni hasara kila mwaka kuanzia Tanesco, TPDC, TTCL, ATCL, NHC na mengine yote, kwa nini shida iwe kwa ATCL?

Halafu watu wanataka kusema Magufuli ange eliminate rushwa ama wizi wa mali za umma 100%, hilo jambo halipo Duniani. Duniani kote, kuanzia China ambapo kosa la rushwa unaweza kuuwawa ama Marekani ambapo mifumo iko strong bado watu wanaiba na kula rushwa, tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag

Kwani tulipokuwa tunawalaumu wakoloni kwa kuiba raslimali zetu, ni kuwa waliiba zote? Naona umeishiwa na hoja za utetezi.
 
Subiri uone kama kuna mtu anaweza kutetea mtu dhalimu. Kama aliweza kunajisi uchaguzi kwa kiwango kile, ni nani unataka kumletea hekaya zako? Hakuwa mtu muadilifu hilo halina mjadala, ndio maana hata waliomzunguka ukiacha uoga waliokuwa nao, wameweza kumgeuka haraka sana. Naona umejaribu kutaja miradi mingi katika hali ya upotoshaji, kama vile wote wanasema hakuna kilichofanyika. Acha kuleta hoja ulizochanganya na upotoshaji, ili kuficha ukweli wa kinachozungumzwa sasa. Ni hivi, hakuwa muadilifu hata kama kuna vitu kadhaa vimefanyika.
Ni hivi, mtu dhalimu hawezi kuliliwa kiasi hicho tulichokishuhudia. Hajageukwa na wote waliomzunguka, hiyo ni tafsiri yako. Ni kwa vile tu umesikia kelele na mayowe ya matapeli wanaotaka kutumia kipindi hiki cha mpito kama fursa ya kumchanganya mama afuate nia zao ovu. Uimara wa mama utapimwa hapa.
 
Dawa

Wasukuma huwawezi wewe tafuta mlo wako tu, ukiongelea uchumi wa nchi hii unaongelea usukumani ukiongelea ziwa kubwa liko usukumani na samaki wataaaaamu. Kaa kimya ulishwe upate mlo, ningetaja umaskini wa eneo lako lisilo hata na chembe ya madini ya kusingiziwa. Tanzania ni nchi ya pili afrika kwa mifugo na wafugaji ni wasukuma na wamasai. Madini yanayochimbwa nchii kwa sasa yako usukumani na umasaini. KAA KIMYA achana na sukuma gang
😀😀😀😀 Endelea kuota ata Marekani anachota mafuta hapo Libya na uarabuni
Kaa Kwa kutulia 💺tuku fundisheni ile ikitokea bahati mbaya ingine akili ziwe zime komaa!
Unafikiria USUKUMA wakati sisi tuna fidia kwenda kuwekeza Kongo na sehemu nyinginezo!
Tambua kwa Asilia flani vinasaba vyangu vina USUKUMA pia ila me sio mshamba
 
Ni hivi, mtu dhalimu hawezi kuliliwa kiasi hicho tulichokishuhudia. Hajageukwa na wote waliomzunguka, hiyo ni tafsiri yako. Ni kwa vile tu umesikia kelele na mayowe ya matapeli wanaotaka kutumia kipindi hiki cha mpito kama fursa ya kumchanganya mama afuate nia zao ovu. Uimara wa mama utapimwa hapa.

Hata Kaburu Pieter Botha wa Afrika kusini naye kuna waliomlilia. Kwa taarifa yako hata majambazi wanaouwawa kwenye wizi, kuna watu huwa wanawalilia sana.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli. Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea. Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufidadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Nadhani hoja yako ni kulalamika kuwa ndugu yako Magufuli amesalitiwa baada ya kufariki , kwamba alipokuwa hai mbona ufisadi huu haukusemwa ? mbona akina Mkapa na wengine walisemwa wakiwa madarakani ?

Ni hivi , kabla ya Utawala wa Magufuli vyama vya siasa vilikuwa na uhuru wa kufanya mikutano ya hadhara , kwenye mikutano hiyo uchafu wote wa watawala ulianikwa , Magazeti yalikuwa na Uhuru wa kuandika na kufichua uozo wote uliofanywa kwenye miradi , wewe umekuwa mwandishi wa MwanaHalisi kwa miaka yote hiyo na hukuwahi kufikishwa Mahakamani wala hukuwahi kutekwa , kulikuwa angalau na uhuru wa kutoa maoni .

Kabla ya kufanya atakavyo , Magufuli alipiga marufuku mikutano ya hadhara pamoja na harakati zote za kisiasa ili mambo yake yasifahamike , Vyombo vya habari visivyomtukuza vilidhibitiwa , waliojitolea kuokoa nchi kwa kusema uchafu wake hadharani walipigwa risasi , walitekwa na kutupwa kwenye mapori na baharini bila huruma yoyote , akajipa Uungu Mtu , Sasa muda wa kumsema ni huu , na ndio maana unaona alipokuwa hai watu walimsifu kinafiki , hakuandikwa vibaya kwa vile alidhibiti vyombo vya Habari kwa kuwatumia wapambe wake akiwemo Hassan Abbass , tungewezaje kufichua uovu ? Akataka kudhibiti hata hii JF , kamata Melo na kumtia korokoroni , unatarajia watu wangesemea wapi ?

Nakuhakikishia kwamba Magufuli ndio atakayekuwa rais wa hovyo zaidi kuwahi kutokea Tanzania milele na hatakumbukwa kwa wema wowote huko ccm wala Tanzania , Naihurumia familia yake
 
Ukisoma mitandao ya kijamii hasa twitter utafikiri kweli hii nchi imeibiwa kila kitu na hakuna kitu kimeachwa, kumbe sio kweli.

Watu wanajifanya kushangaa ATCL kupata hasara, hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kushangaa atcl kupata hasara? By the way, ni shirika gani la serikali linalopata faida? Lipi? Mashirika yote ni hasara kila mwaka kuanzia Tanesco, TPDC, TTCL, ATCL, NHC na mengine yote, kwa nini shida iwe kwa ATCL?

Halafu watu wanataka kusema Magufuli ange eliminate rushwa ama wizi wa mali za umma 100%, hilo jambo halipo Duniani. Duniani kote, kuanzia China ambapo kosa la rushwa unaweza kuuwawa ama Marekani ambapo mifumo iko strong bado watu wanaiba na kula rushwa, tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag
Assad alimchafua Magufuli, kichere nae anamchafua Magufuli, hivi ninyi mnaakili sawa sawa?
 
Kama Mheshimiwa Magufuli kaacha jeshi kubwa nyuma, basi jeshi hilo linapaswa lipokee ripoti ya CAG inayobainisha mapungufu makubwa katika matumizi ya pesa za Umma na kuyafanyia kazi ili kuendeleza legacy ya JPM na Serikali yake.

Nimesema kwamba kufanya miradi ya maendeleo hakumpi Kiongozi yeyote haki ya kufanya ama kuruhusu ufisadi. Mheshimiwa Magufuli kaacha alama 4 kubwa katika maendeleo ya Taifa hili, hilo halina ubishi, lkn hii haiondoi ukweli kwamba kuna wizi mkubwa umefanyika katika awamu yake lkn alizuia umma usiambiwe.

Kuikosoa taarifa ya ukaguzi uliofanywa na CAG ni ujinga mkubwa.

Ni aibu kujiita Mzalendo huku unatetea wizi wa mali ya Umma.
Wewe unatazama upande mmoja wa ripoti ya CAG, mimi ninatazama pia pande zingine kuanzia bungeni (tuendelee kununua ndege au tuache..?) na kauli kadha wa kadha za viongozi serikalini. Ninachokisoma ni mpango kabambe uliopangwa wa kutaka kufuta legacy ya JPM na kuirudisha nchi kuzimu. Kwani mara ngapi JPM mwenyewe amekuwa akisema kwamba nchi hii inachezewa sana, akiwa rais? Yeye mwenyewe hao aliokuwa akiwatumbua mara kwa mara ilikuwa ni kwa sababu gani kama sio kwa ufisadi? Suala si kufumbia macho ufisadi, suala ni watu waovu sana, mafisadi wa kiwango cha juu kabisa, wanaotaka kupaint picha kwamba JPM mwenyewe alikuwa fisadi nyuma ya pazia. Hilo si kweli na it wont work.
 
Hata Kaburu Pieter Botha wa Afrika kusini naye kuna waliomlilia. Kwa taarifa yako hata majambazi wanaouwawa kwenye wizi, kuna watu huwa wanawalilia sana.
Sasa ieleweke kwako kwamba JPM alililiwa na taifa zima, na bara zima la Afrika. Huyu si mtu wa kumfuta kirahisi.
 
Wapigaji wamerudi kwa kasi ili mambo yao yaende kazi ni moja kuua legacy yote ya mwendazake alafu waanze kupiga kama ilivyoada

Wapigaji hawajarud,walikuwepo tuh,

Infact hawakuwahi kuondoka,ni meko tuh aliamua kuminya uhuru wa habar na ukweli kusemwa,ukweli ndiyo huo unasemwa sasa,yeye si alikuwa hataki kuambiwa ukweli?
 
Back
Top Bottom