Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Nimesoma lakini sijaelewa unataka kufikisha ujumbe gani.
uyo anamtetea Magufuli, na pia anasema turudi kwenye uchaguzi mkuu,SAMIA asigombee, asimamishwe msukuma yoyote kama Chenge, ili wasukuma washike tena hatamu, Tatizo ni uraisi wa Samia hapo,,, mwendazake alikuwa fisadi mkuu
 
Sidhani kama huu CAG ni mkweli.Yani kaaamua kwa makusudi kununulika Kuiua CCM na Tanzania .ni aibu kwa kweli.Tunarudi nyuma kwa kasi ya ajabu.
Kama Mwanakijiji alivyosema kuna kitu kinaundwa.Ajabu Spika hajui kinachoundwa.in short CCM is finished ,Tanzania is finished.
CCM haipo, bali inalindwa na jeshi la polisi pale kwenye box la kura
 
Nimekuelewa..lkn unapaswa ujiulize jambo moja, kama Mheshimiwa Magufuli alikuwa na nia njema na Nchi hii kwa nini alizuia sauti mbadala zisiingie Bungeni?
Kwa nini alichukizwa na taarifa za ufisadi wa Serikali yake? Kwa nini alizuia vyombo vya habari kufanya kazi zao kwa uhuru? Kwa nini alizuia Bunge live kwa kisingizio cha kubana matumizi lkn yeye akionyeshwa live hata kwenye shughuli za kuzindua soko?
Huko Bungeni unakokusemea kumejaa watu wengi ambao ni wezi na mafisadi wakubwa kwenye Nchi hii. Wao hutazama maslahi yao tu. Wapo tayari kufanya kazi na yeyote ilimradi ufisadi wao unadumu.
Waliokataa ujenzi wa Bagamoyo leo wanaupigia debe. Walioshangilia ununuzi wa ndege leo wanahoji uendelee ama ukome. Walio apa kumwongezea muda wa kutawala leo wanatetea udhaifu na wizi mkubwa kwenye taasisi za Umma.
Mfumo unaozalisha ufisadi kamwe hauwezi kuondoa ufisadi hata kama ataletwa Malaika kutawala.
Wewe unatazama upande mmoja wa ripoti ya CAG, mimi ninatazama pia pande zingine kuanzia bungeni (tuendelee kununua ndege au tuache..?) na kauli kadha wa kadha za viongozi serikalini. Ninachokisoma ni mpango kabambe uliopangwa wa kutaka kufuta legacy ya JPM na kuirudisha nchi kuzimu. Kwani mara ngapi JPM mwenyewe amekuwa akisema kwamba nchi hii inachezewa sana, akiwa rais? Yeye mwenyewe hao aliokuwa akiwatumbua mara kwa mara ilikuwa ni kwa sababu gani kama sio kwa ufisadi? Suala si kufumbia macho ufisadi, suala ni watu waovu sana, mafisadi wa kiwango cha juu kabisa, wanaotaka kupaint picha kwamba JPM mwenyewe alikuwa fisadi nyuma ya pazia. Hilo si kweli na it wont work.
 
Kunywa chochote hapo kwa Mangi nakuja kulipa! Huyu mzee nilimuovarate huko nyuma, sikujua kama ni kiazi kwa kiwango hiki. Mahaba niue yake kwa Magufuli yamemshusha kiwango vibaya sana.
MI MWENYEWE SIAMINI KAMA JAMAA MAHABA NIUE UTAFIKIRI HUU UFISADI WAMEFANYA UPINZANI ATAKUWA MSUKUMA HUYU TU UPIGE BIL 3 MZEE ASIJUE MNALETA UTANI NYIE MWIZI NI MWIZI TU HATA UMTETE VIP NDO MAANA ALIBANA UHURU WA VYOMBO VYA HABAR ALIJUA ATAGUNDULIKA WIZI WAKE NA KWA MWENDO HUU JAMMA ALIKUWA HATOKI IKULU
 
Usimwamini NDUNGAI MNAFIKI na huyu Mama ambae hana anachojua zaidi ya mipasho na taarab
Kwa huyu mama bado ni mapema sana ku judge direction anayoenda,tumpe muda kidogo ili tuweze kupata tathmini ya utendaji kazi wake...
 
uyo anamtetea Magufuli, na pia anasema turudi kwenye uchaguzi mkuu,SAMIA asigombee, asimamishwe msukuma yoyote kama Chenge, ili wasukuma washike tena hatamu, Tatizo ni uraisi wa Samia hapo,,, mwendazake alikuwa fisadi mkuu
Aaah wapi..!

Wasukuma Tena??wasahau nchi hii,kama ni gundu,jamaa yao ameshawatia gundu...

RAIS,ni mama SAMIA had 2030..!!
 
Nimekuelewa..lkn unapaswa ujiulize jambo moja, kama Mheshimiwa Magufuli alikuwa na nia njema na Nchi hii kwa nini alizuia sauti mbadala zisiingie Bungeni?
Kwa nini alichukizwa na taarifa za ufisadi wa Serikali yake? Kwa nini alizuia vyombo vya habari kufanya kazi zao kwa uhuru? Kwa nini alizuia Bunge live kwa kisingizio cha kubana matumizi lkn yeye akionyeshwa live hata kwenye shughuli za kuzindua soko?
Huko Bungeni unakokusemea kumejaa watu wengi ambao ni wezi na mafisadi wakubwa kwenye Nchi hii. Wao hutazama maslahi yao tu. Wapo tayari kufanya kazi na yeyote ilimradi ufisadi wao unadumu.
Waliokataa ujenzi wa Bagamoyo leo wanaupigia debe. Walioshangilia ununuzi wa ndege leo wanahoji uendelee ama ukome. Walio apa kumwongezea muda wa kutawala leo wanatetea udhaifu na wizi mkubwa kwenye taasisi za Umma.
Mfumo unaozalisha ufisadi kamwe hauwezi kuondoa ufisadi hata kama ataletwa Malaika kutawala.
Nimekuelewa pia. Sijawahi kusema popote kwamba JPM hakuwa na kasoro zake na miongoni mwa kasoro zake ilikuwa uwezo wake mdogo wa kuhimili kelele kinzani. Kwa nini hakuwa na uwezo huo siwezi kujua, pengine ni kwa sababu high performance individuals hupenda kufanya mambo bila bugudha, bila kelele kinzani. Lakini kasoro yake hiyo haiwezi kutufanya tusione nchi aliikuta wapi na ameifikisha wapi, uthubutu wake, ufanisi wake, na matokeo yake.

Kama kuna tunachoweza kujifunza kupitia kasoro na mazuri ya JPM ni kwamba tumuombe Mungu kama nchi atuibulie mtu visionary, mzalendo, na results oriented anayeweza kuhimili vishindo vya sauti kinzani. Kitu tusichotamani kitokee tena ni kumpata kiongozi mediocre atakayetaka kumfurahisha kila mtu ikiwemo vyombo vya habari, huku mambo ya msingi ya nchi yanaharibika.
 
Nime note kitu kimoja kutoka kwako nayo ni 'wapinzani' kumbe ulishajiweka tawi la watawala?

Ok ni haki yako lakini kwa binadamu kamili angehoji je, kwanini aliyeninasibu kuwa msafi mithili ya sufi apende kufanya mambo gizani kiasi kile?

Kweli mtu msafi ajiondoe kwenye mikataba ya uwazi?

Kwanini mtu msafi hakuitaji transparency ili umma umsaidie kuwa msafi?

Mnachofanya sasa ni nafsi zinawasuta, mmeachwa kwenye tope msijue nani atawachomoa, mli compromise nafsi zenu kwa vitu vya kipuuzi na kishenzi.

Kinachowauma zaidi mlizoea kuuza maneno sasa hakuna atakaewaamini tena.

Kwa tuliomfahamu Magufuli tangu enzi hatukua tayari kuuza nafsi zetu kwa sifa za kipuuzi na kijumla jumla namna ile.
Pole sana mtafute kazi ya kufanya sasa.
[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Hii ripoyo imekuja strategically ili kutoa option badala ya restriction ndiyo maana kuna mtu nimesikia akisema .....tuendelee au..!.
Wananchi tunatak kazi iendele ova!...
 
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amepewa mwangaza wa kuanzia. CAG kaweka hadharani changamoto katika usimamizi na matumizi ya pesa za Umma.

Anapaswa sasa arekebishe kasoro zilizopo. Wale wote waliotajwa kwenye ufisadi huu wawajibishwe kisiasa na kisheria.
Miradi yote iliyoanzishwa na Mheshimiwa Magufuli inapaswa iendelee..hasa ile yenye tija kwa Taifa kama Bwawa la Umeme, Ujenzi wa reli ya kisasa, Elimu bure, Ujenzi wa daraja la Busisi, upelekaji wa umeme vijijjini na miradi mingine.

Miradi isiyo na tija kwa sasa inapaswa isimame. Mfano wa miradi isiyo ni pamoja na ununuzi wa Ndege. Zilizonunulia zinatosha, zisimamiwe vizuri, ufanyike utaratibu wa kuongeza mauzo ya ticket za ndege hasa kwa safari za ndani kwa kupunguza ukubwa wa nauli uliopo na pia kuanzisha route mpya ndani ya Nchi.

Ni dhahiri pia Serikali inao uwezo wa kutoa ajira mpya kwa vijana wengi waliomaliza masomo yao na kukosa ajira, hata kama ni kwa hatua. Kiasi cha pesa kinachopotea kwa kuibiwa ama kusimamiwa vibaya ni kielelezo Serikali inao uwezo wa kutoa ajira mpya.
Uzalendo ni pamoja na kukosoa pale penye matatizo. Kushauri na kuelekeza yaliyo sahihi. Uzalendo sio kuwazuia wakosoaji wako. Wote tunajenga Taifa hili... Tunahitaji kukubaliana hata kama mengine yanatufedhehesha.
 
Babu Kuna sehemu CAG kasema miundombinu haikujengwa !?
CAG kafichua uchafu na uvundo wa Mungu, soory Yesu jiwe ....!
Ila nakupongeza kwa kuokoteza hoja za kumantain 'status quo!
Ila nguo mnavuliwa sebuleni, kabla hata hamjafikishwa chumbani
20210409_075024.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Hivi ulimsikiliza Magufuli wakati anamwapisha Kichere kuwa CAG? Zile bit alikuwa anampiga kuwa asiende kuanzisha mhimili wake ilikuwa kuweka mazingira ya kumtisha CAG asije akafunua maovu ya serikali.

Prof Assad alisema kuna wizi lakini huyu huyu Ndugai alitishia kutofanya naye kazi na kumdhalilisha bungeni kwa kumvua viatu na mkanda hii yote ilikuwa kumtisha.

Magufuli alikuwa corrupt to the core ila alichofanikiwa ni kuwanyamazisha wabaya wake ili uovu wake usijulikane. Na huyu mtu asingelitoka madarakani kwa amani. Ama angeweka mtu wake baada yake au angetawala milele atake asitake kama walivyotuambia kina Ndugai.

Baada ya huu ufisadi wa Serikali ya Magufuli subiri sasa utakuja kusikia wa yeye binafsi. Hapo ndipo mtachoka kabisa nyie wafuasi wa kiongozi wa malaika
 
Umezungumza jambo zuri sana. Changamoto ni hii, je mfumo huu wa kulindana unaweza kuacha nafasi ya Taifa kupata mtu mwenye sifa ulizoziainisha?
Nimekuelewa pia. Sijawahi kusema popote kwamba JPM hakuwa na kasoro zake na miongoni mwa kasoro zake ilikuwa uwezo wake mdogo wa kuhimili kelele kinzani. Kwa nini hakuwa na uwezo huo siwezi kujua, pengine ni kwa sababu high performance individuals hupenda kufanya mambo bila bugudha, bila kelele kinzani. Lakini kasoro yake hiyo haiwezi kutufanya tusione nchi aliikuta wapi na ameifikisha wapi, uthubutu wake, ufanisi wake, na matokeo yake.

Kama kuna tunachoweza kujifunza kupitia kasoro na mazuri ya JPM ni kwamba tumuombe Mungu kama nchi atuibulie mtu visionary, mzalendo, na results oriented anayeweza kuhimili vishindo vya sauti kinzani. Kitu tusichotamani kitokee tena ni kumpata kiongozi mediocre atakayetaka kumfurahisha kila mtu ikiwemo vyombo vya habari, huku mambo ya msingi ya nchi yanaharibika.
 
Ukisoma mitandao ya kijamii hasa twitter utafikiri kweli hii nchi imeibiwa kila kitu na hakuna kitu kimeachwa, kumbe sio kweli.

Watu wanajifanya kushangaa ATCL kupata hasara, hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kushangaa atcl kupata hasara? By the way, ni shirika gani la serikali linalopata faida? Lipi? Mashirika yote ni hasara kila mwaka kuanzia Tanesco, TPDC, TTCL, ATCL, NHC na mengine yote, kwa nini shida iwe kwa ATCL?

Halafu watu wanataka kusema Magufuli ange eliminate rushwa ama wizi wa mali za umma 100%, hilo jambo halipo Duniani. Duniani kote, kuanzia China ambapo kosa la rushwa unaweza kuuwawa ama Marekani ambapo mifumo iko strong bado watu wanaiba na kula rushwa, tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag

Mkuu Hakimu Mfawidhi heshima kwako. Naomba unisaidie kidogo mkuu, hivi "Gawio" huwa linalipwa serikalini kutokana na Mapato "Ghafi" au "Faida"?

Ahsante
 
Back
Top Bottom