Kama kuna mwanafunzi anasoma tahasusi CBG na HGE imekula kwake. NECTA yazifuta rasmi

Kama kuna mwanafunzi anasoma tahasusi CBG na HGE imekula kwake. NECTA yazifuta rasmi

Cbg wanaweza kuwa waalimu,wanaweza soma a.griculure,food and bioprocess eng food science,kimsingi kufuta hizo kombi ni kukurupuka
Nashindwa kuacha kushangaa hata mimi mkuu.
Nimesoma maoni ya watu wengi humu, kuhusu combination ya cbg, nimegundua waTanzania wengi niwavivu wa kusoma na ufuatiliaji wa mambo wengi mnafikiria ndani ya kile mlichofundishwa tu , cbg inampa mwanafunzi uwanda mpana sana, kuanzia mambo ya aquatic science,environmental science, zoology, botanic science, microbiology, labaratory technology, biotechnology, agricultural science, agribusiness, chemistry, geology and so forth, food science, food processing engineering, kwa kifupi hii ni combination maarufu duniani kote na katika nchi nyingi zilizoendelea watu hawa pia kama wanaufaulu mzuri wa physics o level wanasoma medicine bila shida, tatizo wengi wenu humu mnaenda kama manyumbu, Elimu ina uwanda mpana sana nje ya combination, somo moja tu la natural science mfano biology, chemistry, physics likisimama lenyewe bado linampa mwanafunzi mwangaza mzuri kiutaalamu tofauti na hesabu, historia, so as long as CBG iko na two natural science subjects ni upuuzi wa hali ya juu kuifuta hii combination [emoji108]
Yaani mkuu ndio maana viongozi waropakaji na wakurupukaji km akina Chalamila wataonekana viongozi makini sana nchi hii kwani watoa maoni wengi hasa wanaotetea uamzi huo wanaonekana wamefungiwa ktk kisiwa flani cha mafichoni na wamenyimwa mawasiliano.

Sijui wao wanadhani wale zoologist wamesoma masomo gani sasa wakati ndio wanaochukua mpunga wa kutosha huko TANAPA,maafisa mifugo,uvuvi na kilimo.

Wanaenda mbali zaidi wanasema wanaosoma CBG wanaenda kuwa walimu,sasa unajiuliza kwani kusomea ualimu ni dhambi au huwa wana walazimisha?
 
Umechanganya na CBA (Chemistry, Biology , Agriculture) ndugu. CBG inahusu nutrition
CBN ndio nutrition bhana....... CBG ipo kivyake vyake tuu na nilisoma hiyo. Kuna watu ni ma nurse, kuna watu ni mabwana afya na wengine wapo kwenye mambo ya kilimo.
 
Hapa ndio naelewa kwann watu wana vyeti wamefaulu vizuri lakini ajira hawana.

kumbe shida sio wanafunzi tatizo ni Elimu yetu inaandaa watu kupata vyeti tu lakini uhalisia wa Kazi ZIROOO.

Tutaendelea kuwa na Wahitimu wengi wasio na ajira kwa hii elimu yetu, hadi tutakapofika Level ya ADvance Level kufutwa ndio watu watakua profitable mitaani ila saivi tunasoma Tu graduate.
 
Daah mkosi wa CBG ulianza tangu Ndalichako aliporudishwa wizara ya elimu na jiwe.
TCU ikawaondelea privileges walizokuwa nazo za kusoma fani mbali mbali vyuoni kama BVM(SUA), Medical lab na vitu kama hizo.
Sasa hizi tahasusi zilianzishwa kwa siasa au Lah, kwasababu wanafunzi uzichagua kwa kuwa zipo katika machaguo.
 
Kama ni kweli;
wamekurupuka, wamekurupuka, wamekurupuka, wamekurupuka, wamekurupuka, wamekurupuka, wamekurupuka..........!!!
 
Back
Top Bottom