LGE2024 Kama lile ndio Daftari la kujiandikisha kupiga kura, Professor Assad yuko Sahihi kuwa hatapiga kura

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Huyo mgombea angejipanga sehenu ngapi? Firia mbunge ukubwa wa jibu au hata tu diwani. Unakuta Kata moja ina vijijini ht vinne na viko mbalimbali kuunda hiyi Kata je huyo mgombea ataenda kusimama wapi ili wananchi wakajipange mbele yake?
Zina pritiwa picha kubwa za wagombea Waubunge, udiwani, na Hata uRais. Zinawekwa sehemu maalumu za kupigia kura. Ni Rahisi tu!
 
Vishikwambi vingefaa kwenye Hili zoezi, mtu unakuja na namba Yako ya NIDA wanaingiza then details zako zinakuja unajaza na kwenye register Yao Ile, mtu akijiandikisha mara mbili namba ya NIDA Ile inatakiwa kuonesha.
 
Aheri hata wangeuliza namba ya nyumba!
Mimi nilimuuliza huyo mundikishaji ndio tayari! Yaani jina umri na sain!
Halafu kazi ndogo namna hii ndio watoe siku nyingi kiasi hicho za kuanfikisha!
 
Vipi kuhusu watu wanaojulikana mitaa tofauti na wakajiandikisha kote.
Wakati wa kupiga kura Kuna alama unapewa na haifutiki kirahisi ndi ya masaa 24. Kwa hiyo itakuwa vigumu kufanya kitendo hicho kiovu
 
Huyo mgombea angejipanga sehenu ngapi? Firia mbunge ukubwa wa jibu au hata tu diwani. Unakuta Kata moja ina vijijini ht vinne na viko mbalimbali kuunda hiyi Kata je huyo mgombea ataenda kusimama wapi ili wananchi wakajipange mbele yake?
Kila chama kiwe na box lake wapiga kula wanakwenda kwa chama wanacho taka kutumbukiza kula chamsingi wapiga kula wawe sahihi pasiwe na mapandikizi wala kula za pembeni
 
Ukipitia comments za baadhi yetu humu ndani unagundua watu wanashindwa kutofautisha kati ya uchaguzi wa serikali za mitaa ambao uandikishaji wa wapiga kura ndo unaondelea sasa na unasimamiwa na Tamisemi na uchaguzi mkuu (wa madiwani, wabunge na Rais) unaosomamiwa na Tume "huru"
ya uchaguzi ambao mchakato wake ni hapo mwakani
 
Sijapiga kura kuanzia mwaka 2020 baada ya uchafuzi wa Magufuli ule mwaka. Sijioni nikipiga kura tena nchi hii, sitaki kuingia kwenye takwimu za kuhalalisha uchafuzi.

Serikali na CCM hawana mpango wa kuwapa wananchi haki ya kuchagua viongozi wanaowataka. Tunapoteza muda tu na hizi chaguzi
 
Kukiwa na mfumo madhubuti ni vyema kupiga Kura ila kwa upumbavu huu? Ni wastage of time and resources wala hata tusidanganyane. Ninachoshangaa, yaani Huko Serikalini hakuna MTU mwenye akili hata mmoja akashauri mambo ya msingi?
Hayo ya msingi yakishauriwa hayawezi kufuatwa maana itabomoa himaya inayoendelea kulindwa
 
Nilipowasikia chadema wanasema wamekubali kushiriki chaguzi hizi nikajisemea kimoyomoyo kuwa kumbe hii nchi ina wapinzani wajinga Sana!
 
Unakwenda kupiga kura sehemu unapojulikana! Tunajuana Mtaani!
Ulitaka utumike utaratibu upi?
Njia Rahisi na uhakika ni kujipanga mbele ya mgombea unayemtaka! Kwanza hiyo, ingepunguza gharama nyingi za uchaguzi!
Labda kwenye kitongoji chako, kuna wengine tukijulikana sana labda nyumba ya pili tena kwa sura tu.

Pili, tunatakiwa kujiandikisha vituo vingapi? Jitihada gani zimefanyika kuona watu hawajiandikishi zaidi ya mara moja?

Kwa kuangalia sura unaweza jua kwa usahihi kiasi gani kati ya mtu wa miaka 17 na 18?

Leo nikijiandikalisha Juma nikakaa siku tatu nikaenda nikajiandikisha kama John? inakuaje hapo?
 
Hata mimi siwezi kupiga kura kwa daftari kama lile naona limekaa kimizengwe sana mara aakwenda nalo mwandikishaji nyumbani mara linaachwa kwenye kibanda cha mlinzi😀
 
JANA NILIKUWA WILAYA YA MKINGA TANGA KIJIJI CHA DARUNI WALIKUJA KWENYE MIGODI YA MADINI WAKIHAMASISHA WATU KUJIANDIKISHA WANASEMA HATA UKITOKEA MANYARA AU TABORA HAKUNA SHDA WW JIANDIKISHE.KUMBUKA HUO MGODI UNA KM MIEZ 2
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…