Mimi nami niongezee hapo kwenye hayo maswali, japo najua kabisa hakuna mwenye majibu zaidi ya talalila;
Kama kweli Mungu anatupenda kama tunavyoaminishwa, kwanini baada ya shetani kuasi akaamua tena kumtupa DUNIANI ambako alijua kabisa kuna viumbe vyake pendwa (sisi) na alijua kabisa huyu jamaa atakuja kutusumbua na kutupotosha? Kwanini hakumtupa hata PLUTO huko au VENUS, JUPITER nk ambako hakuna kiumbe kinachoishi? Yaani ni sawa na wewe upambane na nyoka huko nje, ushindwe kumuua halafu umtupie chumbani kwa watoto! Inaingia akilini?
Halafu huyo nyoka akiwauma watoto, unaanza kuwalaumu tena wale watoto. Kwamba kwanini wamekubali kuumwa na nyoka, unawalaani wao na vizazi vyao vyote, unawaambia waombe msamaha kwako kwa kuumwa na nyoka uliewatupia wewe, la sivyo wakifa utawachoma moto MILELE!!!
Hapa kuna mawili tu;
AMA hizi hadithi za kwenye biblia ni za UONGO kama alfu lela ulela, AU huyo Mungu muweza yote alietuumba na anaetupenda SIO HUYO wa kwenye maandiko!
Usikute hata haya maandiko ni mpango wa shetani kututenganisha na Mungu wa kweli? 🤔 Eeh manake shetani tunaambiwa ana akili sana na yeye ndio mfalme wa dunia so anaweza kufanya chochote.