Kama mbinguni Kuna utakatifu na hakuna dhambi Ibilisi(Shetani) alidanganywa na nani Hadi akaasi?

Kama mbinguni Kuna utakatifu na hakuna dhambi Ibilisi(Shetani) alidanganywa na nani Hadi akaasi?

Haya mambo ni pasua kichwa.Huenda kulikuwa na maisha(pre-creation civilization) kabla ya uumbaji wa mwanadamu kwa sura ya Mungu.Huenda huko ndo shetani alikokuwa anatawala kwa niaba ya Mungu badae akaona aabudiwe yeye kuliko Mungu-(Probably Jeremiah 4 :21....).Nadhani kuna mambo mengi ambayo huenda yalifichwa au Mungu hataki tuyajue,mojawapo ni re-incarnation/re-birth.
Nikweli kabisa maana Kila jibu la mtu anayetaka kukujibu linazalisha maswali mengine mengi!
 
Hilo ni swali zuri linaloibua tafakari ya kiroho na maadili. Katika imani nyingi za dini, mbinguni huchukuliwa kama mahali pa utimilifu wa furaha, utukufu, na usafi wa moyo.

Ikiwa tunashikilia mafundisho haya, tamaa, wivu, au maovu ya kidunia hayawezi kuwapo kwa sababu tabia na hisia hizo hazihusiani na hali ya ukamilifu.

Hivyo, yeyote mwenye tamaa ya namna hiyo hawezi kuwako kwenye sehemu hiyo ya wakamilifu wasio na dhambi.

Ova
Sahihi mkuu. Na hapo ndo yanaibuka maswali mengi sana kuhusu huo ukamilifu wa utakatifu sana hukohuko ndo ulikoanzia uasi unachanganya sana.
 
Umetolea mfano
Mimi nami niongezee hapo kwenye hayo maswali, japo najua kabisa hakuna mwenye majibu zaidi ya talalila;

Kama kweli Mungu anatupenda kama tunavyoaminishwa, kwanini baada ya shetani kuasi akaamua tena kumtupa DUNIANI ambako alijua kabisa kuna viumbe vyake pendwa (sisi) na alijua kabisa huyu jamaa atakuja kutusumbua na kutupotosha? Kwanini hakumtupa hata PLUTO huko au VENUS, JUPITER nk ambako hakuna kiumbe kinachoishi? Yaani ni sawa na wewe upambane na nyoka huko nje, ushindwe kumuua halafu umtupie chumbani kwa watoto! Inaingia akilini?

Halafu huyo nyoka akiwauma watoto, unaanza kuwalaumu tena wale watoto. Kwamba kwanini wamekubali kuumwa na nyoka, unawalaani wao na vizazi vyao vyote, unawaambia waombe msamaha kwako kwa kuumwa na nyoka uliewatupia wewe, la sivyo wakifa utawachoma moto MILELE!!!

Hapa kuna mawili tu;

AMA hizi hadithi za kwenye biblia ni za UONGO kama alfu lela ulela, AU huyo Mungu muweza yote alietuumba na anaetupenda SIO HUYO wa kwenye maandiko!

Usikute hata haya maandiko ni mpango wa shetani kututenganisha na Mungu wa kweli? 🤔 Eeh manake shetani tunaambiwa ana akili sana na yeye ndio mfalme wa dunia so anaweza kufanya chochote.
Konki sana asee sidhani kama tutapa majibu ya kina hapa!
 
Mimi naamini chanzo cha dhambi ni hamu ya kufahamu mambo mengi (elimu) elimu ni chanzo kikuu cha dhambi.

Embu fikiria, Eva aliponzwa na hamu ya kutaka kufahamu mema na mabaya (elimu) akadanganyika na akamshawishi Adamu wakala tunda la ujyzi na hapo hapo booom!! dhambi ikaanza.

Shetani naye hivyo hivyo tu ujuzi (elimu) wa mambo mengi zaidi ya wenzake ulimponza.

Hadi leo tunaamuni watoto hawana dhambi sababu hawana ujuzi wa mambo hayo bado ni elimu tu tatizo na wakiishaipata tu wanaanza kutenda dhambi.

Hata kwenye mausha ya jawaida waalufu wengi ni watu wenye maarifa juu ya jambo fulani na wakaamua kulitumia kwa maslahi yao. Bado ni elimu tu.
 
Umetolea mfano

Konki sana asee sidhani kama tutapa majibu ya kina hapa!
Wakati Mungu anaumba mbingu na nchi inaonekana maji yalikuwepo(huenda aliumba nchi kavu tu),maana anasema akayatemga maji yaliyo juu na yaliyo chini.Ikumbukwe siku moja kwa Mungu ni sawa na miaka elfu moja.Inavoonekana kabla ya kuumba mbingu na nchi shetani alikuwepo tayari Duniani.Nadhani kuna viumbe wengine tofaiti na wanadamu wenye sura ya Mingu ambao walikuwepo kwenye Sayari nyingine.Kabla ya Mwanzo moja nadhani kuna mambo ambayo tumefichwa wanadamu.Siku moja nilimsikiliza mtu mmoja (alikuwa mwabudi shetani) akasema;kabla ya kitabu cha mwanzo kulikuwa na civilization ambayo ilikuwa more advamced ambako shetani alikuwa kiongozi kama malaika nuru kwa kushirikiana na malaika wengine wa nuru kuoongoza hao viumbe kumwabudu Mungu.Badae kiburi kikachipuka ili aabudiwe kuliko Mungu ndipo vita ikapigawa.Mbinguni na Duniani umbali wake ni 'kufumba na kufumbua'.Ndipo Mungu akafutilia mbali hao viumbe na shetwani akatupwa Duniani ana Mungu akaanza upya uumbaji wa mtu wa kufanana nae.......Hakuna mwenye uhakika kwa haya.
 
Wakati Mungu anaumba mbingu na nchi inaonekana maji yalikuwepo(huenda aliumba nchi kavu tu),maana anasema akayatemga maji yaliyo juu na yaliyo chini.Ikumbukwe siku moja kwa Mungu ni sawa na miaka elfu moja.Inavoonekana kabla ya kuumba mbingu na nchi shetani alikuwepo tayari Duniani.Nadhani kuna viumbe wengine tofaiti na wanadamu wenye sura ya Mingu ambao walikuwepo kwenye Sayari nyingine.Kabla ya Mwanzo moja nadhani kuna mambo ambayo tumefichwa wanadamu.Siku moja nilimsikiliza mtu mmoja (alikuwa mwabudi shetani) akasema;kabla ya kitabu cha mwanzo kulikuwa na civilization ambayo ilikuwa more advamced ambako shetani alikuwa kiongozi kama malaika nuru kwa kushirikiana na malaika wengine wa nuru kuoongoza hao viumbe kumwabudu Mungu.Badae kiburi kikachipuka ili aabudiwe kuliko Mungu ndipo vita ikapigawa.Mbinguni na Duniani umbali wake ni 'kufumba na kufumbua'.Ndipo Mungu akafutilia mbali hao viumbe na shetwani akatupwa Duniani ana Mungu akaanza upya uumbaji wa mtu wa kufanana nae.......Hakuna mwenye uhakika kwa haya.
Kweli asee.Pia Mungu hakuumba giza
 
Chanzo Cha dhambi sio shetani ni Moyo ata shetani dhambi yake ilianzia Moyoni baada ya kutamani kiti Cha enzi kwaiyo Moyo ndo chanzo Cha dhambi sio she
Sasa huo moyo wa dhambi ulitokana na nini ili hali huko binguni wanaishi watakatifu yaani ni mwiko kuwaza maovu. Inamaana Mungu hakujua kuwa atakuja kuasi ili amdhibiti?
 
Mbingu haipo, shetani hayupo na Mungu hayupo.

Biblia ni hekaya za kusadikika tu, kama ilivyo hekaya za Abunuwasi.
 
Kwenye Torah Mungu Hana mpinzani yaani Mungu Yuko peke yake hakuna huyo shetani, dini zlitengeneza shetani ili kupata wa kuangushia lawama. Utaniuliza Sasa nani analeta na kusababisha mambo mabaya. Nenda ukasome biblia Isaiah 45:7 . Naomba kuwasilisha,
Glory be to God the Creator of the universe.
 
Kwenye Torah Mungu Hana mpinzani yaani Mungu Yuko peke yake hakuna huyo shetani, dini zlitengeneza shetani ili kupata wa kuangushia lawama. Utaniuliza Sasa nani analeta na kusababisha mambo mabaya. Nenda ukasome biblia Isaiah 45:7 . Naomba kuwasilisha,
Glory be to God the Creator of the universe.
Nitakurudia mkuu acha niisome kwanza
 
Kwenye Torah Mungu Hana mpinzani yaani Mungu Yuko peke yake hakuna huyo shetani, dini zlitengeneza shetani ili kupata wa kuangushia lawama. Utaniuliza Sasa nani analeta na kusababisha mambo mabaya. Nenda ukasome biblia Isaiah 45:7 . Naomba kuwasilisha,
Glory be to God the Creator of the universe.
Mkuu naomba tafasiri yake hasa neno kulihuluku giza maana yake ni nini?
 
Mimi nami niongezee hapo kwenye hayo maswali, japo najua kabisa hakuna mwenye majibu zaidi ya talalila;

Kama kweli Mungu anatupenda kama tunavyoaminishwa, kwanini baada ya shetani kuasi akaamua tena kumtupa DUNIANI ambako alijua kabisa kuna viumbe vyake pendwa (sisi) na alijua kabisa huyu jamaa atakuja kutusumbua na kutupotosha? Kwanini hakumtupa hata PLUTO huko au VENUS, JUPITER nk ambako hakuna kiumbe kinachoishi? Yaani ni sawa na wewe upambane na nyoka huko nje, ushindwe kumuua halafu umtupie chumbani kwa watoto! Inaingia akilini?

Halafu huyo nyoka akiwauma watoto, unaanza kuwalaumu tena wale watoto. Kwamba kwanini wamekubali kuumwa na nyoka, unawalaani wao na vizazi vyao vyote, unawaambia waombe msamaha kwako kwa kuumwa na nyoka uliewatupia wewe, la sivyo wakifa utawachoma moto MILELE!!!

Hapa kuna mawili tu;

AMA hizi hadithi za kwenye biblia ni za UONGO kama alfu lela ulela, AU huyo Mungu muweza yote alietuumba na anaetupenda SIO HUYO wa kwenye maandiko!

Usikute hata haya maandiko ni mpango wa shetani kututenganisha na Mungu wa kweli? 🤔 Eeh manake shetani tunaambiwa ana akili sana na yeye ndio mfalme wa dunia so anaweza kufanya chochote.

Hapa.
 
Back
Top Bottom