Kama mipakani COVID19 iko hivi, Tanzania yenyewe hali iko vipi?

Kama mipakani COVID19 iko hivi, Tanzania yenyewe hali iko vipi?

Nachokiwaza au kufikiria huu ugonjwa naona tutaishi nao tu kama maralia, ukimwi na magonjwa mengine tu maana sioni dalili ya kuondoka tutakunywa dawa za Madagascar kuvipooza vijidudu tu alafu tutachapa kazi kama kawaida tu.
 
Habari wakuu
Hali ya maambukizi ya corona hapa nchini kwa sasa haifahamiki zaidi ya sintofahamu tu huku watu wakiendelea kufanya shughuli zao kama kawaida

Watanzania tuko njia panda sasa tusielewe hali ya nchi hii kwa vita ya covid19 mpaka kujiuliza maswali kama hali ya mipaka ya nchi iko hivi, Tanzania yenyewe hali hali ikoje? I mean huko Dar es salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha na kwingineko kwingi maambukizi yakoje

Kwa sasa tunashuhudia mipaka ikifungwa na nchi zote jirani kututenga Rwanda, Uganda, Kenya, Zambia zote zimetutenga kwa sababu watanzania tunasambaza corona katika nchi hizo

Tuendelee kujiuliza yaani dereva wa lori ambaye anafika bandari tu kupakia mzigo huku akiwa ajajichanganya sana huko mitaani anapata corona je wale kutwa wanapambana na usafiri wa daladala, mishe za kariakoo, dereva bodaboda watakuwa na hali gani?

Tanzania tuna hali gani ikiwa wasafiri wa malori tu wasio na mizunguko na mchanganyiko mkubwa wa watu wanaathirika vibaya dhidi ya corona?

muanzisha thread, usiende mbali sana

huwa nauliza hivi mtaani kwako wewe, au kitaani kwako wewe wangapi wamekufa na corona? umeshuhudia au kusikia unapoishi hapo? kazini

kujua extent ya tatizo anza na kuona wewe

ushakutana na maiti ngapi barabarani zimelala kwa sababu ya corona?


usipelekeshwe na mitandani na news, have time to think
 
Nachokiwaza au kufikiria huu ugonjwa naona tutaishi nao tu kama maralia, ukimwi na magonjwa mengine tu maana sioni dalili ya kuondoka tutakunywa dawa za Madagascar kuvipooza vijidudu tu alafu tutachapa kazi kama kawaida tu.

HII NI KWA DUNIA NZIMA, sio Tanzania tu kaka
 
muanzisha thread, usiende mbali sana

huwa nauliza hivi mtaani kwako wewe, au kitaani kwako wewe wangapi wamekufa na corona? umeshuhudia au kusikia unapoishi hapo? kazini

kujua extent ya tatizo anza na kuona wewe

ushakutana na maiti ngapi barabarani zimelala kwa sababu ya corona?


usipelekeshwe na mitandani na news, have time to think
Mpaka sasa sijakutana na hayo mazingira unayoyasemea hapo
lakini kwa hivyo unataka kutuaminisha kuwa nchi jirani zinaihujumu tanzania na huenda madereva wetu wanazushiwa?
 
Siku baba yako au mama yako akifa ndio utajua kuna corona na hapo ndipo utaacha huu upumbvu na ujinga. Unajua kuna wapumbavu kama wewe wataamini kauli zako za kijinga na waje kufa.

Sent using Jamii Forums mobile app

naona umeambiwa ukweli ndio unakasirika sasa, unaoenda kusikia habari mbaya

kuna ajali, kisukari, ukimwi, covid, cancer n.k na hata wewe baba yako na mama yako watakufa kwa ugonjwa fulani au washakufa

Tanzania msimamoa wake kila mtu anajua kuna corona na tunavaa barakoa, kunawa, sanitizing our hand, social distancing n.k ndio measures ya dunia nzima, na hata uko duniani waliokufa ni so innocent, hawakupenda ila imetokea

umeulizwa swali specific wwe kwa mfano mtaani kwenu hali ikoje??? umeona, sikia au kuona maiti ziko barabarani kwa corona?? wingi wa vifo vya corona tunavipimaje?? maana rate ya kufa kwaida kila siku nchi hata bila corona wanakufa watu si chini ya 200, kila siku kwa sababu zote

posting ya vifo sasa imechagizwa na issues za corona, well

mtaani kwenu hali ikoje??? tupe maelezeo usitishe watu hapa na kutukana
 
HII NI KWA DUNIA NZIMA, sio Tanzania tu kaka
Juzi siuliona Huwan, Denmark, France shule zinafunguliwa, Italy jana watu wapo nje wameanza kutoka bila vibali league ndio kama hivyo zitaanza kuchezwa Epl, Laliga na Bundesliga.

Trump mwenye analalama tu wako ndani lakini bado wanakufa tu muda sio mrefu atawaachi watu uraiani tutaendelea kuna mikono na kuvaa groves huku tukifanya shughuli zetu tena ndio mm nachokiona maana chanjo hapa mpaka miaka iende ndio tupate.
 
Mpaka sasa sijakutana na hayo mazingira unayoyasemea hapo
lakini kwa hivyo unataka kutuaminisha kuwa nchi jirani zinaihujumu tanzania na huenda madereva wetu wanazushiwa?

wanachofanya nchi jirani wana take measures za DUNIA NZIMA, kuwa wawe na lockdown, it is okay with them


wala hawafanyi hujuma yeyote, waache wajilinde

ila nani atataka mipaka ifunguliwe lini? na corona itaisha?

Nchi zote dunian inaanza kufungua kazi na maisha yanaendelea, corona itaishi kama magonjwa mengine

hizo nchi jirani hawawezi bila kupelekea mizigo; hivyo hakuna namna watahitaji tu mipaka kufunguliwa


Ndani ya nchi zao wanaoata pressure na hizi social media kuwa fungeni mipaka ''watanzania wana corona'' ishafungwa

kesho maisha yakiwa magumu na hawapati supplies watasema ''fungueni mipaka' kazi itaanzia hapo.Kumbuka mizigo yao inatoka nje, ita suffer port charges kubwa, itarundikana hapo bandarini na watapata hasara wao kwa sababu wameruhusu kupepeswa na upepo wa social media zao

Just wait and see
 
Madereva wenye corona wanaweza kupiga gear toka Dar hadi mipakani bado watu wanaona corona ni tishio?

Kama hawataki watz waende kwao kwanini wao wanaendelea kuja TZ? Ni watz pekee ndo wanaweza kusambaza corona ila wao hawasambazi?

Corona ni mafua "makubwa" hayaishi leo wala kesho, anayetaka kukaa ndani hadi chanjo ipatikane akae hakatazwi, kama tumeshindwa kuzuia mafua ndo tutaweza corona! Approach ya lockdown ni uzwazwa popote pale.
 
Makaburi yanaenda kujaa muda si mrefu kuna sehemu maiti 50 zinazikwa deilee halafu ninyi mnaleta siasa
kwani ulikuwa unadhani haitafika siku makaburi yajae mjomba???

au yakijaa ndio corona??
 
Kwanza unatakiwa kujua Kenya na Tanzania zina vita ya bandari, Mombasa na Dar Port. So wanafanya kila wanaloweza kuonyesha Tanzania ni tatizo kiusalama na kiafya. Usifungie fikira zako kwenye Covid19 pekee kuna zaidi ya Covid19....

Watu weusi tunasahau haraka sana, tunashida ya kushindwa ku connect dots.., we are ending up in speculation and assuming and leave the fact away.

Ukienda mbali zaidi utaona wakati huu Kuna vitu vingi vitaendelea kuanzia kisasi, political gain, biashara, kufirisika, marumbano, kuyumba uchumi nk.
 
Juzi siuliona Huwan, Denmark, France shule zinafunguliwa, Italy jana watu wapo nje wameanza kutoka bila vibali league ndio kama hivyo zitaanza kuchezwa Epl, Laliga na Bundesliga.

Trump mwenye analalama tu wako ndani lakini bado wanakufa tu muda sio mrefu atawaachi watu uraiani tutaendelea kuna mikono na kuvaa groves huku tukifanya shughuli zetu tena ndio mm nachokiona maana chanjo hapa mpaka miaka iende ndio tupate.

kaka kukaa ndani kazi jamani

kumbuka TZ 80% YA RAIA wanaishi kwa kutegemea kipato cha siku

serikali ina waajiriwa kama laki saba tu, private sector ajira rasmi imeajiri watu milion tatu tu, population yetu ni 56m, ukitoa hawa waajiriwa rasmi wa serikali na private unabaki na watu kama 50m, nusu ya hawa ni wazee na watoto

una watu watu karibu 20m hawana ajira za kueleweka..na wahawa wabeba karibu wategemezi 15m ya wazee na watoto

DSM kwa mfano ina wasiojariwa na sekta sio rasmi kama 2.5 !!!


Lockdown kwetu isingewezekana hata kama JPM angeamua iwepo RAIA wangeingia barabarani, POLISI wanaongeka!!! Kenya polisi wanapewa hela wanaachiwa watu kidogo na maisha yanaendelea

swali ni je mpaka lini watu watakaa ndani??
experts wamekisikia corona inaisha lini?? -Hamna majibu
 
1589274841149.png
 
Back
Top Bottom