Kama mlikuwa hamjui: CCM imeliongoza hili Taifa kwa uongo tangu ikiwa TANU hadi sasa.

Kama mlikuwa hamjui: CCM imeliongoza hili Taifa kwa uongo tangu ikiwa TANU hadi sasa.

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Ni vile tu Watanzania wengi ni wajinga na sio wasomaji sana wa vitabu na wafuatiliaji wa masuala ya nchi yao.

Mlioshtuka leo kuhusu habari ya Tanzania kununua umeme nje kwa ajili ya matumizi ya mikoa ya Kaskazini wakati Serikali imekuwa ikijisifu kuzalisha umeme kuzidi matumizi yetu nawashangaa sana.

Kwa wale msiofahamu hakuna Chama cha siasa Afrika hii na nadhani duniani kinachoishi kwa uongo kama CCM. Na uongo wa CCM haujaanza leo, ulianza tangu ikiwa TANU na uliasisiwa na aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Tanganyika na Tanzania , Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Vitabu vya dini vinasema Shetani ni Baba wa Uongo ila kwa hapa Tanzania, baba wa uongo ni CCM.

Yafuatayo ni maeneo ambayo TANU na CCM waliwadanganya/Wamewadanganya Watanzania na wao wakaamini.

1. Suala la Oscar Kambona kutangazwa kuwa mhaini na ameolewa Uingereza. Jambo hili lilitangazwa na Serikali ya Nyerere mwaka 1967 baada ya Kambona kuamua kujiuzuru nafasi zote za Uongozi ndani ya Serikali na Chama baada ya kupingana na Nyerere kuhusu sera za Ujamaa. Watanzania kama mazuzu tuliamini huu uongo wa Nyerere na hadi tukatungishwa nyimbo mashuleni kuwa kambona Kaolewa Uingereza. Huu ulikuwa uongo wa Nyerere ili kuwarubuni Watanzania na kuwa label vibaya wanaompinga.

2. Suala la Nyerere kung'atuka kutangazwa ni kwa sababu eti ni Kiongozi mzuri na hataki kung'ang'ania madaraka. Mwaka 1985 CCM walitangaza na kueneza uongo unaoaminika hadi leo kuwa Nyerere aling'atuka kwa sababu hakuwa na tamaa ya madaraka wakati kiukweli kilichomkimbiza Nyerere ikulu ni mfululizo wa majaribio ya mapinduzi dhidi yake hasa ya mwaka 1981/1982 na lile la kutekwa kwa ndege ya ATCL kutokana na kushinikiza aondoke madarakani kwa sababu ya hali mbaya ya kimaisha/ kiuchumi iliyotokana na kufeli kwa sera zake za ujamaa.

3. Suala la kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 kuwa ni busara za Nyerere wakati ukweli ni kwamba baada ya kuanguka kwa Shirikisho la Kikokumunisti (USSR) nchi zote zilizokuwa zinaitegemea Urusi ziliamua kuchukua sera zinazofanana na za kimagharibi ili kuendelea kupata misaada kutoka Mataifa ya Magharibi.

4. Suala la Nyerere kuwa alikuwa kiongozi bora na hakuwa dikteta wakati kiuhalisia hakuna Kiongozi aliyekuwa dikteta nchi hii kama Mwalimu Nyerere. Kipindi cha Uongozi wake ndipo Watanzania wengi waliotofautiana nae kimawazo kama kina Bibi Titi Mohamed na Oscar Kambona walifunguliwa kesi za Uhaini na wengine wengi kuwekwa vizuizini chini ya Sheria ya kuweka watu kizuizini. Waliopona wachache walikimbia nje ya nchi na kurudi baada ya Nyerere kuondoka madarakani.

5. Suala la vita vya Uganda kuwa ilitokana na Iddi Amini kutaka kuuchukua mkoa wa Kagera wakati ukweli ni kwamba ugomvi wa Iddi Amini na Nyerere ulitokana na Nyerere kumpa hifadhi Obote aliyepinduliwa na Iddi Amini. Amini aliamini vikundi vinavyompinga ambavyo vingi vilikuwa vinashambulia Uganda kutokea Mkoa wa Kagera nchini Tanzania vinakuwa supported na Nyerere hivyo kuanza kuleta chokochoko mpakani na kuivamia Tanzania.

6. Suala la Corona kutokuwepo Tanzania kipindi cha awamu ya 5 (mwaka 2020/21) wakati kipindi hicho maelfu kama sio mamia ya watanzania walikuwa wanakufa kwenye hospitali zetu kwa ugonjwa wa Corona.

Kutokana na mifano hii michache, napenda kuwaambia Watanzania, CCM hawajawahi kuongoza hii nchi kwa ukweli. Kama wanashangaa leo kuambiwa tutanunua umeme Ethiopia wakati waliambiwa tunazalisha umeme unaozidi matumizi yetu basi watakuwa hawaijui CCM vizuri.

Ukweli uliopo kwenye suala la umeme ni kwamba matumizi yetu yanazidi kuongezeka kila kukicha hivyo hata huo Umeme wa Bwawa la Nyerere hautoshi. Pia pamoja na kuanza kazi kwa Bwawa la Nyerere, mabwawa mengine yanazidi kupunguza uzalishaji kila siku kutokana na kujaa matope na mabadiliko ya tabia nchi yaliyopunguza uwezo wa mabwawa hayo kuzalisha umeme kwa kiwango kinachopaswa. Ila ukweli huu kamwe Watanzania hamtaambiwa mtaletewa uongo wa kila na post za watu mbalimbali kutengeneza hoja uchwara kuutetea huo Uongo (Spinning)

Ikitokea CCM ikaanguka kwenye taifa letu jambo la kwanza watakalotakiwa kulifanya Viongozi wapya wa Tanzania ni kufanya maombi ya toba kwa Taifa kutokana na nchi hii kuendeshwa kwa uongo kwa miongo mingi sana.

Lord denning.
 
KWELI TUPU.
163192.jpg
 
lile la corona kusema tumeomba kwa mungu pale magufuri alichemka sababu wizara ya afya ilikuwa uchi.

Uongo mwingine ni kutumia watu wasiojulikana kuzima ukweli ambao watu wasishtuke.

Bado watu wanaishi kwa uongo wa ccm kuchuma mali na kuitafuna nchi ndio maana kila mwizi na mshenzi anakuwepo ccm.
 
Miaka 2 iliyopita ulimalizika mradi mkubwa wa kujenga nji a ya umeme kutoka Singida kwenda Arusha.Tuliaminishwa pia kuwa njia hii itaongeza kama sio kuondoa tatizo la umeme Mikoa ya Kaskazini!😭
Kumbe sakata la Simba kugomea mechi juzi halikuwa la bahati mbaya!
 
Ni vile tu Watanzania wengi ni wajinga na sio wasomaji sana wa vitabu na wafuatiliaji wa masuala ya nchi yao.

Mlioshtuka leo kuhusu habari ya Tanzania kununua umeme nje kwa ajili ya matumizi ya mikoa ya Kaskazini wakati Serikali imekuwa ikijisifu kuzalisha umeme kuzidi matumizi yetu nawashangaa sana.

Kwa wale msiofahamu hakuna Chama cha siasa Afrika hii na nadhani duniani kinachoishi kwa uongo kama CCM. Na uongo wa CCM haujaanza leo, ulianza tangu ikiwa TANU na uliasisiwa na aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Tanganyika na Tanzania , Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Vitabu vya dini vinasema Shetani ni Baba wa Uongo ila kwa hapa Tanzania, baba wa uongo ni CCM.

Yafuatayo ni maeneo ambayo TANU na CCM waliwadanganya/Wamewadangana Watanzania na wao wakaamini.

1. Suala la Oscar Kambona kutangazwa kuwa mhaini na ameolewa Uingereza. Jambo hili lilitangazwa na Serikali ya Nyerere mwaka 1967 baada ya Kambona kuamua kujiuzuru nafasi zote za Uongozi ndani ya Serikali na Chama baada ya kupingana na Nyerere kuhusu sera za Ujamaa. Watanzania kama mazuzu tuliamini huu uongo wa Nyerere na hadi tukatungishwa nyimbo mashuleni kuwa kambona Kaolewa Uingereza. Huu ulikuwa uongo wa Nyerere ili kuwarubuni Watanzania na kuwa label vibaya wanaompinga.

2. Suala la Nyerere kung'atuka kutangazwa ni kwa sababu eti ni Kiongozi mzuri na hataki kung'ang'ania madaraka. Mwaka 1985 CCM walitangaza na kueneza uongo unaoaminika hadi leo kuwa Nyerere aling'atuka kwa sababu hakuwa na tamaa ya madaraka wakati kiukweli kilichomkimbiza Nyerere ikulu ni mfululizo wa majaribio ya mapinduzi dhidi yake hasa ya mwaka 1981/1982 na lile la kutekwa kwa ndege ya ATCL kutokana na kushinikiza aondoke madarakani kwa sababu ya hali mbaya ya kimaisha/ kiuchumi iliyotokana na kufeli kwa sera zake za ujamaa.

3. Suala la kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 kuwa ni busara za Nyerere wakati ukweli ni kwamba baada ya kuanguka kwa Shirikisho la Kikokumunisti (USSR) nchi zote zilizokuwa zinaitegemea Urusi ziliamua kuchukua sera zinazofanana na za kimagharibi ili kuendelea kupata misaada kutoka Mataifa ya Magharibi.

4. Suala la Nyerere kuwa alikuwa kiongozi bora na hakuwa dikteta wakati kiuhalisia hakuna Kiongozi aliyekuwa dikteta nchi hii kama Mwalimu Nyerere. Kipindi cha Uongozi wake ndipo Watanzania wengi waliotofautiana nae kimawazo kama kina Bibi Titi Mohamed na Oscar Kambona walifunguliwa kesi za Uhaini na wengine wengi kuwekwa vizuizini chini ya Sheria ya kuweka watu kizuizini. Waliopona wachache walikimbia nje ya nchi na kurudi baada ya Nyerere kuondoka madarakani.

5. Suala la vita vya Uganda kuwa ilitokana na Iddi Amini kutaka kuuchukua mkoa wa Kagera wakati ukweli ni kwamba ugomvi wa Iddi Amini na Nyerere ulitokana na Nyerere kumpa hifadhi Obote aliyepinduliwa na Iddi Amini. Amini aliamini vikundi vinavyompinga ambavyo vingi vilikuwa vinashambulia Uganda kutokea Mkoa wa Kagera nchini Tanzania vinakuwa supported na Nyerere hivyo kuanza kuleta chokochoko mpakani na kuivamia Tanzania.

6. Suala la Corona kutokuwepo Tanzania kipindi cha awamu ya 5 wakati kipindi hicho maelfu kama sio mamia ya watanzania walikuwa wanakufa kwenyw hospitali zetu kwa ugonjwa wa Corona.

Kutokana na mifano hii michache, napenda kuwaambia Watanzania, CCM hawajawahi kuongoza hii nchi lwa ukweli. Kama wanashangaa leo kuambiwa tutanunua umeme Ethiopia wakati waliambiwa tunazalisha umeme umaozidi matumizi yetu basi watakuwa hawaijui CCM vizuri.

Ikitokea CCM ikaanguka kwenye taifa letu jambo la kwanza watakalotakiwa kulifanya Viongozi wapya wa Tanzania ni kufanya maombi ya toba kwa Taifa kutokana na nchi hii kuendeshwa kwa uongo kwa miongo mingi sana.

Lord denning.
Wenda hili ni andiko bora kabisa jf kwa mwaka 2025, mkuu umenyooka kama rula, hii ndo jf sasa ,

Mayalla aje ajifunze kitu cha msingi
 
SGR wana lalamika ngedere na bundi wanahujumu shirika.
Hata siku moja usije kuamini data au takwimu zozote zile zinazotolewa na Serikali ya Tanzania iliyo chini ya CCM.

Amini maneno yangu. HATA SIKU MOJA USIZIAMINI, maana almost 99.9% ni za kupika, kutengenezea kwa nia na maslahi wanayojua wao.
 
lile la corona kusema tumeomba kwa mungu pale magufuri alichemka sababu wizara ya afya ilikuwa uchi.

Uongo mwingine ni kutumia watu wasiojulikana kuzima ukweli ambao watu wasishtuke.

Bado watu wanaishi kwa uongo wa ccm kuchuma mali na kuitafuna nchi ndio maana kila mwizi na mshenzi anakuwepo ccm.
Hilo la Corona ni dogo sana mbona. Kuna mambo hadi yameandikwa kwenye vitabu vya historia vya nchi hii na yanafundishwa kwa watoto wetu wakati ni uongo na hayana ukweli wowote ule.

Wakija Viongozi wapya Tanzania hatuna budi tuwaambie wa re-write upya historia yq nchi yetu. Tumelishwa matango pori sana na sie kama majinga tunaamini tu bila kuhoji.
 
SGR wana lalamika ngedere na bundi wanahujumu shirika.
Tena kuna wakati wakatoa taarifa kuwa watu wanaiba miundombinu kumbe ukweli ni kwamba kulikuwa na shida ya umeme kwenye njia zao kulikotokana na kutoweka umeme wa kutosha kwenye njia na ku u balance vizuri kwenye njia zao.
 
Amini maneno yangu. Nchi yetu shida ya umeme haitokuja kamwe kupungua au kuondoka kabisa as long as tunategemea vyanzo vya maji.

China pamoja kuwa na Mabwawa mengi ya Umeme alafu bado anazalisha Umeme wa Nyuklia sio wajinga.

Mataifa ya Marekani, Canada, Uingereza na mengine makubwa kuanza tena kuwekeza kuzalisha umeme wa nyuklia sio wajinga.

Sie tuna madini ya Uranium Bahi na Lindi pale ila haujawahi kusikia hata siku moja wajinga wa CCM hata wakiongelea Jmeme wa nyuklia wakati Kenya tu hapo juu amepata kibali cha kuanza kutengeneza Umeme wa Nyuklia na sasa anahamisha watu kwenye moja ya Pwani zake ili aanze ujenzi wa mradi huo.

Miaka 2 iliyopita ulimalizika mradi mkubwa wa kujenga nji a ya umeme kutoka Singida kwenda Arusha.Tuliaminishwa pia kuwa njia hii itaongeza kama sio kuondoa tatizo la umeme Mikoa ya Kaskazini!😭
Kumbe sakata la Simba kugomea mechi juzi halikuwa la bahati mbaya!
 
Vitabu vya dini vinasema Shetani ni Baba wa Uongo ila kwa hapa Tanzania, baba wa uongo ni CCM.
Utakapoanza kuisifia CCM kwa mapambio km zilivyokua nyuzi zako za zamani nitakutukana JF nzima mpaka uikimbie ID yako, maana nakujua wewe hauna tofauti na Mayor Quimby mpo kimkakati zaidi hamchelewi kubadirisha uelekeo leo utasema hivi kesho kile kile ulichokiponda unakuja kukisifia unajisahaulisha
 
Utakapoanza kuisifia CCM kwa mapambio km zilivyokua nyuzi zako za zamani nitakutukana JF nzima mpaka uikimbie ID yako, maana nakujua wewe hauna tofauti na Mayor Quimby mpo kimkakati zaidi hamchelewi kubadirisha uelekeo leo utasema hivi kesho kile kile ulichokiponda unakuja kukisifia unajisahaulisha
CCM chama

Hiko ndio cha msingi wewe kuelewa, flip-flops za michango ya watu humu zisikuzumbue.

MaCCM yanajua matusi ya wanachama wao, neutral party, wapinzani na kadhalika (raia wenye hasira tu) wasio na vyama

Mimi nipo katika hizo sehemu zote nne usinipe label.
 
Back
Top Bottom