Kama mtu anakopa benki 5 tofauti za Tanzania na akaweza kukimbia nchi bila kugundulika ni ishara kwamba TISS na vyombo vingine vimelala

Kama mtu anakopa benki 5 tofauti za Tanzania na akaweza kukimbia nchi bila kugundulika ni ishara kwamba TISS na vyombo vingine vimelala

loan-image.jpg

Jana, raisi wa Jamhuri ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benki 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti za watu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini aweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Mnakuja na theorise za kiajabuajabu wakati mama kaweka very clear, kuwa game ni ya wafanyakazi wa mabenki. Nini ambacho hamjakielewa kwenye kukopa?
 
loan-image.jpg

Jana, raisi wa Jamhuri ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benki 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti za watu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini aweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Ila uyu kaishayakanyaga izo pesa atazilipa
 
Tiss wajishughulishe na mikopo? Hili mbona ni kosa la benki? Benki inakopeshaje mtu ambaye haimjui? Dhamana anazoweka kwanini hawazihakiki? Huu ni mchongo wa benki na TISS unawaonea bure. Hujui hata inavyofanya kazi pengine.
Mkuu labda humjui mleta mada. Jamaa ni Tiss tena wa muda mrefu.
 
Hao wanaopaswa kufanya maamuzi ndio wanapaswa wajikague tena.
 
TISS kwani wapo tena? sio kwamba nao walifutwa baada ya kuonekana hawana tija kwa Taifa?
Wangekuwepo haya ya ushoga yasingekuwawepo kwa kaisi hiki na pia uteuzi wa viongozi hadi wenye matatizo ya akili!
 
Tatizo na changamoto kubwa ni TISS kutumika kisiasa za ndani tu badala pia ya kiuchumi na kiutamaduni dhidi ya mataifa ya kigeni kwa maslahi mapana ya kitaifa.
Mabadiliko ya fikra, kutoka kwenye mapambano ya ndani kwenda kimataifa yanahitajika .
 
Mkuu huyo Nolle Prosequl ni mke alipewa?
Hapana mkuu🙂

Hilo ni neno la kilatini (likimaanisha kutokuwa tayari kuendelea na mashtaka) la kisheria ni ile "notice" ambayo mwendesha mashitaka hutoa kufuta mashitaka dhidi ya mshtakiwa ama yote au sehemu yake.
 
Mnakuja na theorise za kiajabuajabu wakati mama kaweka very clear, kuwa game ni ya wafanyakazi wa mabenki. Nini ambacho hamjakielewa kwenye kukopa?
Hao wafanyakazi wapo nchi gani si hapahapa
 
loan-image.jpg

Jana, raisi wa Jamhuri ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benki 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti za watu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini aweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Kuna mambo mengine tunayajadili kiujumla sana na kuvitwisha mzigo vyombo vya usalama bila mantiki. Mtu kakopa huko benki na kakutana na Meneja mikopo na DG wa benki kaidhinisha, TISS, Polisi au FIU wanahusikaje?

Hivyo vyombo vya usalama vinahusika na mikopo benki? Nilidhani hoja ingekuwa ma CEO wa benki husika wakamatwe na chain yote iliyoidhinisha mikopo. Pili, Interpol kama walipewa taarifa ya jinai walipaswa kutuma warrant mtuhumiwa arejeshwe.

Kukiwa na hoja lazima tufikiri kabla ya kunyooshea vidole taasisi zetu pendwa. Mimi na wewe na wageni wanafurahia nchi yenye usalama wa hali ya juu ni TISS. Uhuru na mipaka yetu iko salama ni JWTZ. Usalama wa raia uko juu ni Polisi. 🙏🙏🙏
 
Kuna mambo mengine tunayajadili kiujumla sana na kuvitwisha mzigo vyombo vya usalama bila mantiki. Mtu kakopa huko benki na kakutana na Meneja mikopo na DG wa benki kaidhinisha, TISS, Polisi au FIU wanahusikaje? Hivyo vyombo vya usalama vinahusika na mikopo benki? Nilidhani hoja ingekuwa ma CEO wa benki husika wakamatwe na chain yote iliyoidhinisha mikopo. Pili, Interpol kama walipewa taarifa ya jinai walipaswa kutuma warrant mtuhumiwa arejeshwe. Kukiwa na hoja lazima tufikiri kabla ya kunyooshea vidole taasisi zetu pendwa. Mimi na wewe na wageni wanafurahia nchi yenye usalama wa hali ya juu ni TISS. Uhuru na mipaka yetu iko salama ni JWTZ. Usalama wa raia uko juu ni Polisi. 🙏🙏🙏
Mkuu, raisi Samia kasema mwizi kakopa pesa benki kwa kutumia dhamana za kughushi na kakimbia nchi, hIyo ni kauli ya raisi mwenyewe na ipo tafuta uisikilize.

Sasa raisi akija na kauli kama hiyo yamaanisha nini?

Yaani benki zilipogundua mtu kachukua mkopo benki 5 au 6 tofauti na kasepa na pengine polisi wamejulishwa, uhamiaji pale uwanja wa ndege na idara zingine wewe wafikiriaje?

Kitendo cha raisi kuja na kauli kama hiyo yaonyesha wazi kuna tatizo katika mfumo mzima kuanzia benki kwenyewe hadi kwa wale ambao wana wajibu wa kuhakikisha mtu anakamatwa.

Mbona huko nyuma watu wamekamatwa JNIA wakitaka kupanda ndege?
 
Usisingiz TISS kwenye mambo ya mkopo , Hizo ni terms tuu za mkopeshaji ndio zinamapungufu
 
Mkuu, raisi Samia kasema mwizi kakopa pesa benki kwa kutumia dhamana za kughushi na kakimbia nchi, hIyo ni kauli ya raisi mwenyewe na ipo tafuta uisikilize.

Sasa raisi akija na kauli kama hiyo yamaanisha nini?

Yaani benki zilipogundua mtu kachukua mkopo benki 5 au 6 tofauti na kasepa na pengine polisi wamejulishwa, uhamiaji pale uwanja wa ndege na idara zingine wewe wafikiriaje?

Kitendo cha raisi kuja na kauli kama hiyo yaonyesha wazi kuna tatizo katika mfumo mzima kuanzia benki kwenyewe hadi kwa wale ambao wana wajibu wa kuhakikisha mtu anakamatwa.

Mbona huko nyuma watu wamekamatwa JNIA wakitaka kupanda ndege?
Yaani taarifa yoyote inayotoka kwa Mhe. Rais wala haihojiwi. Ni sahihi kwa asilimia 100. Rais ni mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu. Ila hakuna sehemu Mhe. Rais amekisema hiki kilichoandikwa hapa kutuhumu TISS na Polisi.

Nikasema; hii mikopo ni taratibu za kibenki. Mikopo mikubwa kama hii naamini hadi bodi zinajua. Sasa kusema kila mkopo taasisi za usalama zijue huko ni kuwaonea. Kuhusu hoja mtuhumiwa alipitaje airport au border yoyote ya nchi inategemea taarifa zilitolewa muda gani?

Kama tukio hadi kabaini CAG usikute ma CEO wa benki walikuwa wanapambana kimya kimya. Naamini kabisa kutoka rohoni vyombo vya usalama visingeshindwa kuzuia hata ndege kama ilianza kupaa.

Nina imani kubwa mno na vyombo vyetu pendwa vya usalama. Nchi hii iko vizuri jamanii. Hapa ni watu wa benki wanapaswa kukamatwa tu. Benki kuna michezo mingi ya money loundering. 🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom