Kama mtu anakopa benki 5 tofauti za Tanzania na akaweza kukimbia nchi bila kugundulika ni ishara kwamba TISS na vyombo vingine vimelala

Kama mtu anakopa benki 5 tofauti za Tanzania na akaweza kukimbia nchi bila kugundulika ni ishara kwamba TISS na vyombo vingine vimelala

Yaani taarifa iliyotoka kwa Mhe. Rais wala haihojiwi. Ni sahihi kwa asilimia 100. Ila hakuna sehemu Mhe. Rais amekisema hiki kilichoandikwa hapa kutuhumu TISS na Polisi.

Nikasema; hii mikopo ni taratibu za kibenki. Mikopo mikubwa kama hii naamini hadi bodi zinajua. Sasa kusema kila mkopo taasisi za usalama zijue huko ni kuwaonea. Kuhusu hoja mtuhumiwa alipitaje airport au border yoyote ya nchi inategemea taarifa zilitolewa muda gani?

Kama tukio hadi kabaini CAG usikute ma CEO wa benki walikuwa wanapambana kimya kimya. Naamini kabisa kutoka rohoni vyombo vya usalama visingeshindwa kuzuia hata ndege kama ilianza kupaa.

Nina imani kubwa mno na vyombo vyetu pendwa vya usalama. Nchi hii iko vizuri jamanii. Hapa ni watu wa benki wanapaswa kulamatwa tu. Benki kuna michezo mingi ya money loundering. 🙏🙏🙏
Mkuu, kusema wamelala ni lugha inomaanisha kuwa wawe tayari masaa 24.

Ni kweli vyombo vyetu vimekuwa macho masaa 24 hilo halina ubishi kabisa.

Lakini kauli ya raisi yamaanisha kwamba huyo mwizi hayupo nchini.

Na kama hayupo nchini amepitapita vipi hadi kutoroka?
 
Mkuu, kusema wamelala ni lugha inomaanisha kuwa wawe tayari masaa 24.

Ni kweli vyombo vyetu vimekuwa macho masaa 24 hilo halina ubishi kabisa.

Lakini kauli ya raisi yamaanisha kwamba huyo mwizi hayupo nchini.

Na kama hayupo nchini amepitapita vipi hadi kutoroka?
Nimereply juu. Ume establish taarifa kwa vyombo vya usalama zilitolewa muda gani baada ya huyo bilionea kukopa na kuondoka nchini? Taarifa zingetolewa mapema asingefika hata Vingunguti pepsi angetiwa mbaroni. Mabenki ndani ipo syndicate ya baadhi ya wahalifu. 🙏🙏🙏
 
Nimereply juu. Ume establish taarifa kwa vyombo vya usalama zilitolewa muda gani baada ya huyo bilionea kukopa na kuondoka nchini? Taarifa zingetolewa mapema asingefika hata Vingunguti pepsi angetiwa mbaroni. Mabenki ndani ipo syndicate ya baadhi ya wahalifu. 🙏🙏🙏
Mkuu, kauli ya raisi kwamba mwizi kakopa benki tano au sita tofauti kwa kutumia fake documents na kakimbia nje weye waielewaje?

Mimi nimezungumzia kauli ya raisi na ndo msingi wa mada yangu kwamba ikiwa raisi kakiri kuwa huyo mwizi amekimbia nchi hilo ni tatizo.

Auweye umemwelewavipi raisi Samia?
 
huyo mkopaji lazima alikuwa anashirikiana na wafanyakazi wa hizo benki. Benki ni taasisi binafsi kwa asilimia kubwa na wao ndiyo wanatakiwa kuwachunguza wateja wao. Hiyo mikopo haikuwa na securities zo zote au amepewa tu kienyeji (labda kwa kuwa mzungu au muhindi).
Amna hiyo ina security ya serikal ndo maana analalamika
 
huyo mkopaji lazima alikuwa anashirikiana na wafanyakazi wa hizo benki. Benki ni taasisi binafsi kwa asilimia kubwa na wao ndiyo wanatakiwa kuwachunguza wateja wao. Hiyo mikopo haikuwa na securities zo zote au amepewa tu kienyeji (labda kwa kuwa mzungu au muhindi).
Huyo kaja kaa mwekezaji
 
loan-image.jpg

Jana, raisi wa Jamhuri ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benki 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti za watu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini aweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Mimi sitaki kuilaumu Tiss nawalaumu watawala je Tiss imewezeswa kwa kiasi gani?
Je Tiss ni idara ya nani ikiwa Rais anaweza pangua na kuweka mtu wake? What If akiweka mtu wakupiga naye nani atatoa hiyo taarifa?
Sheria zetu zipoje maana tusilaumu chombo tukasahau Kuna mfumo unao ruhusu haya.
Tiss yetu hakuna asie jua ina hitaji a big reforming iwe idara isio ingiliwa na siasa na ndipo tutaona maajabu.
 
Hivyo vyombo unavovishangaa ni vya kabatani ama?
Kama ni vile vya ulinzi na Usalama TZ asee... Vipo kwa ajili ya kuthibiti upinzani! Huyo mkopaji angekuwa upinzani wangemdaka kabla hata ajakopa benki ya kwanza!
 
Mkuu, kauli ya raisi kwamba mwizi kakopa benki tano au sita tofauti kwa kutumia fake documents na kakimbia nje weye waielewaje?

Mimi nimezungumzia kauli ya raisi na ndo msingi wa mada yangu kwamba ikiwa raisi kakiri kuwa huyo mwizi amekimbia nchi hilo ni tatizo.

Auweye umemwelewavipi raisi Samia?
Sikiliza bhana, mimi siwezi kutaja taja mamlaka ya Mhe. Rais naiheshimu kwa kiwango cha juu. Nimekueleza naona unataja taja tu mamlaka kuu ya nchi. Nimekuuliza ni wapi Mhe. Rais alizotaja hizo taasisi? Mhe. Rais kazungumzia benki kumkopesha mtu kwa docs fake na akawatoro hao benki. Huo ni udhaifu wa kibenki siyo vyombo vya usalama. Usiviingize na kutaja taja mamlaka ya Amiri Jeshi Mkuu. Msikilize vizuri utaelewa. 🙏🙏🙏
 
Sikiliza bhana, mimi siwezi kutaja taja mamlaka ya Mhe. Rais naiheshimu kwa kiwango cha juu. Nimekueleza naona unataja taja tu mamlaka kuu ya nchi. Nimekuuliza ni wapi Mhe. Rais alizotaja hizo taasisi? Mhe. Rais kazungumzia benki kumkopesha mtu kwa docs fake na akawatoro hao benki. Huo ni udhaifu wa kibenki siyo vyombo vya usalama. Usiviingize na kutaja taja mamlaka ya Amiri Jeshi Mkuu. Msikilize vizuri utaelewa. 🙏🙏🙏
Mkuu, please stop being condescending, yaani kuwa na tabia ya kuonyesha ubabe au kutoa vitisho hiyo naamini huna.

Na hii tabia mara nyingi sisi waafrika ndiyo tabia yetu sisi.

Nimemsikiliza uzuri tu na nimerudia hiyo sehemu (dak ya 33) nimechambua na nimeweka analysis yangu.

Nawe una uwezo huo kutumia akili yako kuchambua hotuba ya mheshimiwa raisi Samia na kuja na hitimisho lako, hivyo ndivyo mambo huwa.

Na katika mada utangulizi wangu umeanza uzuri kwa kumtaja kwa heshima raisi wetu.

Pia kutajwa mamlaka ya juu ni kitu cha kawaida sana kisikutishe.

Mradi mtu havunji sheria.

Kama waona washindwa kuweka "counter argument" kimantiki basi wacha na pita, huja haja ya kuzogoa.
 
loan-image.jpg

Jana, raisi wa Jamhuri ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benki 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti za watu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini aweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Serikali itawakamata tu maana ina mkono mrefu, hivyo namna ya kuwafuatilia itafuatwa na kukamatwa warudishe hela wazokopa na waliowasaidia nao washughulikiwe.
 
Serikali itawakamata tu maana ina mkono mrefu, hivyo namna ya kuwafuatilia itafuatwa na kukamatwa warudishe hela wazokopa na waliowasaidia nao washughulikiwe.
Na wakikamatwa watangazwe kwa watanzania ili tuelewe kwamba vyombo vyetu vimefanya kazi yao.
 
Wewe huwezi kuwa na kuhakikishia. Usitishie watu ubwana shamba wako eti wewe Tiss. Labda ungekuwa chizi flan hivi.
Kwani kuwa TISS ndiyo nini? Mbona una inferiority complex mbaya sana? Nyie ndiye matapeli wanawatishia kuwa wao ni TISS mnaishia kuwapa fedha. Hao ni binadamu kama wengine tu na hawana cha ziada.
 
Kwani kuwa TISS ndiyo nini? Mbona una inferiority complex mbaya sana? Nyie ndiye matapeli wanawatishia kuwa wao ni TISS mnaishia kuwapa fedha. Hao ni binadamu kama wengine tu na hawana cha ziada.
Wewe siyo TISS. Tulia wewee
 
loan-image.jpg

Jana, raisi wa Jamhuri ya Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania kaeleza kwamba kuna mtu amekopa benki 5 au 6 tofauti za Tanzania na hajulikani alipo, yaani amekimbia na kutoka nchini.

Sasa huu ni mtihani kwa TISS, vyombo vya fedha, uhamiaji na wizara ya mambo ya ndani kwa ujumla.

Haiwezekani mtu mmoja akafanya jambo hilo zito na asepe kilaini hivyo hiyo ni ishara tosha kwamba idara yetu ya usalama na vyombo vingine vimelala au vimejiruhusu kupwaya kupita kiasi.

Lakini mimi ntaikosoa zaidi idara ya usalama kwani yenyewe ndio yaweza kuchagiza shughuli zote za ulinzi na usalama wa nchi.

Natambua idara hii ina uwezo mkubwa tu ina maofisa mahiri tu ambao wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi hivyo wana ueledi, umahiri, uerevu na kila aina ya mbinu za kimkakati na kimedani kuhakikisha nchi yetu ipo salama.

Leo hii shirika la ujasusi wa ndani la Russia la FSB limetangaza kumshikilia mwandishi wa jarida la Wall Street Journal kwa madai ya kujihusisha na ujasusi wa ndani yaani kwa kiingereza twasema "Espionage".

Hiyo ni kazi ya majasusi wa ndani ya Russia yaani "Counter Espionage Agents" ambao wapo macho masaa 24 kulinda nchi, mali zake au "Assets" na miundombinu yake na wananchi kwa ujumla.

Sasa ni wakati wa idara yetu ya usalama wa Taifa kujipambanua kumtafuta huyu mwizi wa fedha zetu ambazo zimehifadhiwa kwenye mabenki zikiwa ni akaunti za watu na mitaji pia. Ni wakati wa kushirikiana na vyombo ya ulinzi na usalama vya nchi jirani na pia ni wakati wa kumtambua mtu huyo ambae ni wazi atakuwa alikuwa na pasi ya kusafiria, makabrasha mbalimbali yanoonyesha anuani zake na kadhalika hata kama ni "fake documents".

Kuhusu mabenki yetu nina imani kwa wana taratibu zote kali ambazo ni lazima mkopaji azifuate na kwenye hili ni lazima iwe ni "inside job" wafanyakazi walohusika ni lazima wapatikane kabla ya Jumaa.

Niliwahi kutoa mapendekezo huko nyuma kuhusu kuifanyia mabadiliko idara ya usalama wa taifa Mapendekezo: Serikali ipitie upya Sheria ya Usalama wa Taifa na TISS iundwe upya kwa maslahi ya taifa na nikzaeleza kwa upana wake.

Pia niliwahi kueleza kwamba wapo watu watembea na wallet tu Mtu anaesafiri kwenda nje kila siku lakini anabeba wallet na passport tu, utamfikiriaje? na hawa huenda ni wale ambao huenda sehemu kufanya machafuko kama uporaji fedha katika taasisi za fedha bila kugundulika na hii ni hatari kwa taifa.

Na pia nikawahi kutoa wazo kama nchi yetu ipo tayari kwa vita vya kijasusi wa uchumi katika mada hii Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari ambapo yawezekana kabisa huyu mtu aliefanya wizi huu wa kughushi ni wale akina Carlos Jackal ambae alikuwa na uwezo wa kuingia katika nchi yoyote na kumaliza kazi kisha kujiondokea asijulikane.

Carlos alikuwa ni jasusi ambae alifunzwa kulelewa na kuwa alipwa ujira na idara ya kijasusi ya Russia ya wakati huo KGB na kazi zake hazikuwa na mfano.

Lakini mtu huyu ambae amehusika na wizi wa mabilioni ya shilingi si wa aina ya Carlos Jackal lakini aweza kuwa ni mhalifu wa kimataifa na huenda akarudi tena.

Hivyo Idara yetu ya TISS iamke isijisahau kwani majukumu yake si ya kisiasa bali ni ulinzi madhubuti wa nchi yetu vikiwemo vyombo vyetu vya fedha ambavyo kwa kushirikiana na vyombo vingine kama Uhamaji na hata huko nje Interpol tayari mtu huyu angekuwa yupo kwenye "Wanted List".
Sijui kigezo ya teuzi au ni shule gani wanaopitia!!
Wanadhani kazi yao kubwa ni kuandamana na Rais kuweka Usalama na Kwa Marais wanaokuja tu! KaI ya Hawa watu ni pana Kwa Taifa wanaotakiwa kujiongeza sana kila kona ya nchi.
Uhamiaji pale Kurasini Kuna kila namba ya Rushwa na ucheleweshaji wa huduma nyingi zinafanyika kwenye zile maduka na migahawa iliyopo mbele ya zile ofisi.
Ni Kwa Nini pakawekwa maduka pale mahali muhimu vile.

Ni wakati muafaka Serikali na Jiji Biashara kuhakikisha hakuna kuweka biashara kwenye maeneo muhimu ya ofisi za Serikali na uwe kama Ilivyo eneo la Uwanja wa ndege.
Sivyo basi na waweke biashara pale kwenye Kituo cha Polisi.
Biashara kwenye malls, Kariakoo mlimani city nk.
 
Back
Top Bottom