Kama Saudi Arabia na Vatican wameweza kufanya ibada majumbani sisi tuliopokea dini toka kwao tunashindwa nini?

Kama Saudi Arabia na Vatican wameweza kufanya ibada majumbani sisi tuliopokea dini toka kwao tunashindwa nini?

Jana nilimsikia Prof Lipumba akisema yeye ameanza kuswalia nyumbani ili kuepuka misongamano inayoweza kusababisha maambukizi ya Covid 19.

Binafsi nikawa nimemwelewa vilivyo.

Ndipo nikaanza kutafakari, kama Waislamu kule Saudia wanaswalia nyumbani Bakwata wanashindwa nini?

Kama Wakristo kule Vatican, UK na Germany wanasalia majumbani hawa Katoliki, Anglican na KKKT wanafeli wapi?

Kama Walokole huko USA wanasalia majumbani hawa kina Kakobe, Gamanywa, Gwajima, Mwingira wanashindwa nini?

Kuna wakati yatupasa kutumia busara hata kama mamlaka za juu zimewaachia hiyo fursa bado mnatakiwa kutumia hekima ya Mungu kutenda jambo sahihi.
Serikali haiwezi kuwakataza directly lakini nyie mmebarikiwa macho ya rohoni na mwilini na hata hao wagonjwa 88 waliotangazwa hadi sasa ni waumini wenu.

Hekima ya Mungu wa mbinguni na iwe juu yenu!
Masikini huficha ujinga na uzembe wake kwenye dini? Eti viongozi wanaotuhumiwa kufuja Mali zetu,kuteka na kuua watu wasio na hatia eti ndo hao hao Leo wanajifanya wacha Mungu
 
Ninachokijua tu ni kwamba ukiwa na Imani ya kweli kwa Mwenyezi Mungu / Allah hata ukisalia Sebuleni au Chumbani Kwako au Bustanini Kwako au hata Stoo basi Dua yako inakubaliwa na unabarikiwa vizuri tu. Huko kwenda Makanisani na Misikitini mara nyingine huwa ni Mbwembwe tu zilizochanganyika na Unafiki mwingi ndani yake.

Kama kuna Jambo ninaloilaumu Serikali yetu na sipendezwi nalo hata kidogo ni Kitendo cha Kuruhusu Ibada za Misikitini na Makanisani iendelee. Nina uhakika kama wasipoliangalia hili kwa marefu na mapana yake Waumini wengi wanaojazana huko / humo wataanza Kufa Siku si nyingi. Yaani Serikali inashindwa Kuzuia Ibada huko katika Nyumba za Ibada kwa sasa kwasababu inahofia Kuchukiwa na Kupoteza kama pia si Kuyimwa Kura nao.

Siasa inaharibu utaratibu mzima wa Kiafya hasa mbele ya Janga hili baya na hatari la COVID-19. Asante sana Mdau kwa hili Bandiko lako kwani ni zuri, sahihi na uliyoyaanisha hapa yana ukweli mtupu. Hongera Umenena!
Serikali inataka huruma baada ya kufanya uzembe wa kiwango cha SGR
 
Hata kupokea, hatukupokea dini yoyote nkutoka Saudi Arabia.

Saudi Arabia imeanza 1932. Dini zote zilizopo Tanzania zipo kwa miaka mingi sana kabla ya Saudi Arabia.a

Sifahamu Ukristo ulipokelewa kutoka wapi lakini Uislam hapa kwetu haukupokelewa kutoka Saudi Arabia.
Tuliupokea kutoka wapi? Wao waliouleta wanakusanyika?
 
Tatizo ni akili za viongozi wetu wa serikali. Waliidharau covid wakidhani ni "kagonjwa kanakowahusu mabeberu" tu.

Viongozi wa dini si kwamba hawajui nini cha kufanya, bali wanadhani wakifanya tofauti na serikali inavyotaka ni kumpinga Magu na serikali yake.

Ndio maana hotuba za pasaka ziliishia kumpongeza Magu kwa maamuzi ya kuruhusu mikusanyiko ya ibada kana kwamba ametoa garantii corana haitaingia kwenye nyumba za ibada na waumini watapata nafuu ya maambukizi.
Viongozi wa dini wamewatoa kafara kondoo wa bwana.
 
Kama serikali imeweza kufunga shule na vyuo hadi vya hayo makanisa na misikiti,inashindwaje kupiga stop hizo ibada?
 
Rais amesema kagonjwa ni kadogo mbele ya Yesu hivyo hakuna haja ya kutishika tuenderee kwenda kwenye nyumba za ibada. Shida ya viongozi wetu mpaka tatizo liwe kubwa ndipo akili huwa zinawarudia.

Ugonjwa ulipoingia akatokea kiongozi mmoja mpumbavu wa chama akasema wapinzani ni sawa na korona. Hapo ndio kaanza kuupiga vita ugonjwa huo. Hatuja kaa sawa akatokea mjinga mwingine bwana masifuri gavana wa jimbo kuu. Yeye akasema anamshukuru Mungu kuwa mtoto wa kiongozi wa upinzani naye kapata korona.

Wapinzani waliposhauri kuwa tuzuie wageni viongozi wakajibu tupo vizuri tunahitaji pesa za watalii. Tukaendelea kupokea watalii kutoka China ulipoanzia ugonjwa. Baada ya mambo kuzidi wamefuata ushauri ule ule walioukataa

Wagonjwa walipoanza kuongezeka kiongozi mmoja wa upinzani akashauri badala ya kuwaweka karantini kwenye hoteli za gharama wanaotoka nje wawekwe kwenye mabweni kwani siyo wote wanauwezo wa kulipa gharama za hoteli. Wakatokea wabwatukaji wa chama wakamzodoa kiongozi. Hali ilipo zidi wakaanza kuwapeleka watu kwenye hostels za chuo wakati mwanzo walijia vichwa maji.

Wapinzani wameshauri tena tufunge makanisa na misikiti watu wasali nyumbani ili kuepuka maambuzi. Baba mkubwa amesema hapana huko ndiko kuna uponyani. Wakati wa Pasaka tumeona wenzetu waliotuletea hizi dini wakiendesha misa bila waumini kwa kutumia video. Sisi tunaojifanya tuko karibu sana na Mungu kuliko wao tukajazana makanisani. Sasa wagonjwa wanaongezeka na vifo vinaongezeka. Je wataendelea kusisitiza kutofunga makanisa na misikiti au akili zitawarudia baada ya tatizo kuongezeka? Baadhi ya makanisa yamesitisha huduma mbali mbali za shamra shara kama ndoa na vipaimara. Sasa hivi hata Sunday Schools zinaambiwa siyo sehemu ya kujaza wanafunzi waliopo likizo ya korona. Nini kinashindikana watu kumwomba Mungu wakiwa makwao mpaka waende makanisani na misikitini?
Asante kwa kuweka kumbukumbu sawa! Ccm na serikali yake wanahisi wakitekeleza ushauri watawapa credit "wapinzani" na kuonekana wamekosa maarifa na kwahiyo waanaendeshwa kwa "remote controller".
 
Jana nilimsikia Prof Lipumba akisema yeye ameanza kuswalia nyumbani ili kuepuka misongamano inayoweza kusababisha maambukizi ya Covid 19.

Binafsi nikawa nimemwelewa vilivyo.

Ndipo nikaanza kutafakari, kama Waislamu kule Saudia wanaswalia nyumbani Bakwata wanashindwa nini?

Kama Wakristo kule Vatican, UK na Germany wanasalia majumbani hawa Katoliki, Anglican na KKKT wanafeli wapi?

Kama Walokole huko USA wanasalia majumbani hawa kina Kakobe, Gamanywa, Gwajima, Mwingira wanashindwa nini?

Kuna wakati yatupasa kutumia busara hata kama mamlaka za juu zimewaachia hiyo fursa bado mnatakiwa kutumia hekima ya Mungu kutenda jambo sahihi.
Serikali haiwezi kuwakataza directly lakini nyie mmebarikiwa macho ya rohoni na mwilini na hata hao wagonjwa 88 waliotangazwa hadi sasa ni waumini wenu.

Hekima ya Mungu wa mbinguni na iwe juu yenu!
Vipi kuhusu sadaka?..
 
Jana nilimsikia Prof Lipumba akisema yeye ameanza kuswalia nyumbani ili kuepuka misongamano inayoweza kusababisha maambukizi ya Covid 19.

Binafsi nikawa nimemwelewa vilivyo.

Ndipo nikaanza kutafakari, kama Waislamu kule Saudia wanaswalia nyumbani Bakwata wanashindwa nini?

Kama Wakristo kule Vatican, UK na Germany wanasalia majumbani hawa Katoliki, Anglican na KKKT wanafeli wapi?

Kama Walokole huko USA wanasalia majumbani hawa kina Kakobe, Gamanywa, Gwajima, Mwingira wanashindwa nini?

Kuna wakati yatupasa kutumia busara hata kama mamlaka za juu zimewaachia hiyo fursa bado mnatakiwa kutumia hekima ya Mungu kutenda jambo sahihi.
Serikali haiwezi kuwakataza directly lakini nyie mmebarikiwa macho ya rohoni na mwilini na hata hao wagonjwa 88 waliotangazwa hadi sasa ni waumini wenu.

Hekima ya Mungu wa mbinguni na iwe juu yenu!
Ndugu yangu kwanza ninakupongeza sana kwa andiko zuri. Ni Serikali pekee ndiyo inayoweza kuepusha wananchi na hili janga. Sihitaji kurudia
Jana nilimsikia Prof Lipumba akisema yeye ameanza kuswalia nyumbani ili kuepuka misongamano inayoweza kusababisha maambukizi ya Covid 19.

Binafsi nikawa nimemwelewa vilivyo.

Ndipo nikaanza kutafakari, kama Waislamu kule Saudia wanaswalia nyumbani Bakwata wanashindwa nini?

Kama Wakristo kule Vatican, UK na Germany wanasalia majumbani hawa Katoliki, Anglican na KKKT wanafeli wapi?

Kama Walokole huko USA wanasalia majumbani hawa kina Kakobe, Gamanywa, Gwajima, Mwingira wanashindwa nini?

Kuna wakati yatupasa kutumia busara hata kama mamlaka za juu zimewaachia hiyo fursa bado mnatakiwa kutumia hekima ya Mungu kutenda jambo sahihi.
Serikali haiwezi kuwakataza directly lakini nyie mmebarikiwa macho ya rohoni na mwilini na hata hao wagonjwa 88 waliotangazwa hadi sasa ni waumini wenu.

Hekima ya Mungu wa mbinguni na iwe juu yenu!

Sihitaji kurudia andiko zuri uliloandika na majibu mazuri kabisa ya wanajamii forum. Ni serikali pekee ndiyo itaweza kuepusha wananchi na hili janga kwa kutoa uamuzi sahihi kama ulivyosema. Mungu wetu anaabudiwa katika Roho na Kweli. Siyo majengo! Viongozi wa dini kamwe hawatasema ibada zisifanyike kwenye majengo kwa sababu zao. Na shetani hupenda kuanza na viongozi kwanza na siyo waumini wa kawaida kusambaratisha makanisa.
 
Kiislam ibada ni popote na misikitini tunaifata jamaa (kujumuika pamoja) na Kwa ajilinya sala za Ijumaa ambazo ni maagizo ya Allah kutoka kwenye Qur'an kuwa inaponadiwa sala siku ya Ijumaa basi twende tukajumuike pamoja. Lakini kama kwenda huko msikitini kutaleta madhara kwako au kwa wengine basi sali hata peke yako nyumbani kwako.
Nimekuelewa!
 
Acha upotoshaji wewe !!

Aliyekwambia waanzilishi wa Saudia ndio waanzilishi wa Israel nani?

Ibn Al Saud alianzisha ufalme wa Saudia wakati David Ben Gurion alianzisha dola ya Israel huko Mashariki ya Kati mwaka 1948.

Unataka kusema Ibn Al Saud alikuwa myahudi?
Hapa napata elimu, ahsante mkuu!
 
Serikali za Saudi Arabia na Italia zimetoa amri za kufungwa misikiti na Makanisa.
Kwa nini serikali yako haitoi amri hiyo?
Jana nilimsikia Prof Lipumba akisema yeye ameanza kuswalia nyumbani ili kuepuka misongamano inayoweza kusababisha maambukizi ya Covid 19.

Binafsi nikawa nimemwelewa vilivyo.

Ndipo nikaanza kutafakari, kama Waislamu kule Saudia wanaswalia nyumbani Bakwata wanashindwa nini?

Kama Wakristo kule Vatican, UK na Germany wanasalia majumbani hawa Katoliki, Anglican na KKKT wanafeli wapi?

Kama Walokole huko USA wanasalia majumbani hawa kina Kakobe, Gamanywa, Gwajima, Mwingira wanashindwa nini?

Kuna wakati yatupasa kutumia busara hata kama mamlaka za juu zimewaachia hiyo fursa bado mnatakiwa kutumia hekima ya Mungu kutenda jambo sahihi.
Serikali haiwezi kuwakataza directly lakini nyie mmebarikiwa macho ya rohoni na mwilini na hata hao wagonjwa 88 waliotangazwa hadi sasa ni waumini wenu.

Hekima ya Mungu wa mbinguni na iwe juu yenu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom