Kama Saudi Arabia na Vatican wameweza kufanya ibada majumbani sisi tuliopokea dini toka kwao tunashindwa nini?

Kama Saudi Arabia na Vatican wameweza kufanya ibada majumbani sisi tuliopokea dini toka kwao tunashindwa nini?

Lakini ukiomba msamaha si unasamehewa?

Si wote mnakubali kua Mungu ni mwenye huruma na husamehe endapo utafanya toba?

Na hawa watoto wadogo wanaokufa kwa corona imekuaje waambukizwe hadi kufikia hatua wanakufa je wao wamefanya mahasi gani mbele za Mungu?

Hadi chui wanapata corona, sasa nao hawa tunawaweka katika kundi gani? Chui nao wanafanya maasi?

It's Scars
Kwa nilivyoelewa ni kwamba maasi hufanya kuletwa kwa mabalaa kama hayo maradhi ya corona hivyo hoja si nani limempata hilo balaa na nani limemkosa.
 
Sadaka zenu ni muhimu sana
Jana nilimsikia Prof Lipumba akisema yeye ameanza kuswalia nyumbani ili kuepuka misongamano inayoweza kusababisha maambukizi ya Covid 19.

Binafsi nikawa nimemwelewa vilivyo.

Ndipo nikaanza kutafakari, kama Waislamu kule Saudia wanaswalia nyumbani Bakwata wanashindwa nini?

Kama Wakristo kule Vatican, UK na Germany wanasalia majumbani hawa Katoliki, Anglican na KKKT wanafeli wapi?

Kama Walokole huko USA wanasalia majumbani hawa kina Kakobe, Gamanywa, Gwajima, Mwingira wanashindwa nini?

Kuna wakati yatupasa kutumia busara hata kama mamlaka za juu zimewaachia hiyo fursa bado mnatakiwa kutumia hekima ya Mungu kutenda jambo sahihi.
Serikali haiwezi kuwakataza directly lakini nyie mmebarikiwa macho ya rohoni na mwilini na hata hao wagonjwa 88 waliotangazwa hadi sasa ni waumini wenu.

Hekima ya Mungu wa mbinguni na iwe juu yenu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa nilivyoelewa ni kwamba maasi hufanya kuletwa kwa mabalaa kama hayo maradhi ya corona hivyo hoja si nani limempata hilo balaa na nani limemkosa.
As long as umesema "kwa namna ulivyoelewa" litabakia kua swala lako binafsi kulingana na uelewa wako hivyo hupaswi kuhitimisha kua "hoja si nani"
 
Jana nilimsikia Prof Lipumba akisema yeye ameanza kuswalia nyumbani ili kuepuka misongamano inayoweza kusababisha maambukizi ya Covid 19.

Binafsi nikawa nimemwelewa vilivyo.

Ndipo nikaanza kutafakari, kama Waislamu kule Saudia wanaswalia nyumbani Bakwata wanashindwa nini?

Kama Wakristo kule Vatican, UK na Germany wanasalia majumbani hawa Katoliki, Anglican na KKKT wanafeli wapi?

Kama Walokole huko USA wanasalia majumbani hawa kina Kakobe, Gamanywa, Gwajima, Mwingira wanashindwa nini?

Kuna wakati yatupasa kutumia busara hata kama mamlaka za juu zimewaachia hiyo fursa bado mnatakiwa kutumia hekima ya Mungu kutenda jambo sahihi.
Serikali haiwezi kuwakataza directly lakini nyie mmebarikiwa macho ya rohoni na mwilini na hata hao wagonjwa 88 waliotangazwa hadi sasa ni waumini wenu.

Hekima ya Mungu wa mbinguni na iwe juu yenu!
Maendeleo hayana Chama...!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ni akili za viongozi wetu wa serikali. Waliidharau covid wakidhani ni "kagonjwa kanakowahusu mabeberu" tu.

Viongozi wa dini si kwamba hawajui nini cha kufanya, bali wanadhani wakifanya tofauti na serikali inavyotaka ni kumpinga Magu na serikali yake.

Ndio maana hotuba za pasaka ziliishia kumpongeza Magu kwa maamuzi ya kuruhusu mikusanyiko ya ibada kana kwamba ametoa garantii corana haitaingia kwenye nyumba za ibada na waumini watapata nafuu ya maambukizi.
Usiwape ufahamu kiasi hicho. Viongozi wengi wa dini hawana ufahamu unaofaa kwa hali tuliyonayo. Ndo maana akina Gwajima wakisoma lolote mtandaoni, wanawalisha wafuasi wao bila hata kuchuja.

Sayansi ni ya wachache, wengine walistahili kulazimishwa kufuata.
 
As long as umesema "kwa namna ulivyoelewa" litabakia kua swala lako binafsi kulingana na uelewa wako hivyo hupaswo kuhitimisha kua "hoja si nani"
Ulitaka nitumie maneno kama ya wanasayansi ambao watakwambia hili ndio sahihi kabisa kwa ushahidi wa kisayansi lakini baada ya muda utafiti mwengine wa kisayansi kupiga jambo la mwanzo na kuonekana kumbe halikuwa sahihi.

Nimejibu kile ulichokuwa unauliza au ulichotaka kujua kuhusu watoto na hadi wanyama kupata corona,tunatofautiana uelewa na elimu na ndiyo maana nikasema kwa nilivyoelewa.
 
Ulitaka nitumie maneno kama ya wanasayansi ambao watakwambia hili ndio sahihi kabisa kwa ushahidi wa kisayansi lakini baada ya muda utafiti mwengine wa kisayansi kupiga jambo la mwanzo na kuonekana kumbe halikuwa sahihi.

Nimejibu kile ulichokuwa unauliza au ulichotaka kujua kuhusu watoto na hadi wanyama kupata corona,tunatofautiana uelewa na elimu na ndiyo maana nikasema kwa nilivyoelewa.
Na hakuna mahali nimeku-recommend utumie maneno ya wanasayansi

Uko sahihi kwa uelewa wako, ila hautakua sahihi kutoa jibu la hitimisho kua ndio jibu sahihi kwa uelewa wako ulivyoelewa
 
Viongozi wa dini ni wanafiki Sana na hawana upendo kwa waumini kinachofanya wasiambie watu watulie majumbani ni wao wanataka sadaka basi,pia serikali na yenyewe inawaogopa kisa mwaka wa uchaguzi viongozi eti wanawaumini wengi wakikataza wataudhi wapiga kura, maandiko yenyewe yasema watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa huku tumeletewa dini tunajifanya wacha Mungu kuliko Vatican au huko sijui Macca, I wish corona ingewapiga viongozi wa dini ili raia wagutuke kuwa corona ni hatari, wengine badala ya kuelimisha wananchi wajilinde eti watoe sadaka ili wasipate corona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu waombee corona majumbani huko dawa za ki science zipo watu hawafati huko ka si kukosa akili Nini, akili tunazo Ila hatutumii ipasavyo kukabiliana na changamoto Sasa hivi tunapambana na corona ka enzi za Vita vya majimaji eti ukipigwa risasi itayeyuka
Waafrica tunaweka siasa hata kwenye mambo ya majanga.......wacha tupukutuke ili tutie adabu......

eti makanisa yasifungwe sababu yanaombea Corona.....yale yale ya Kibwetele.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na hakuna mahali nimeku-recommend utumie maneno ya wanasayansi

Uko sahihi kwa uelewa wako, ila hautakua sahihi kutoa jibu la hitimisho kua ndio jibu sahihi kwa uelewa wako ulivyoelewa
Mkuu hakuna sehemu niliyosema kuwa jibu langu mie tu ndio sahihi na ndiyo maana nimesema kwa nilivyoelewa,sasa wewe umeuliza swali na mie nikajaribu kujibu kwa kukuelewesha kwa nilivyoelewa sasa sijui wewe ulikuwa unataka vp.
 
Viongozi wa dini ni wanafiki Sana na hawana upendo kwa waumini kinachofanya wasiambie watu watulie majumbani ni wao wanataka sadaka basi,pia serikali na yenyewe inawaogopa kisa mwaka wa uchaguzi viongozi eti wanawaumini wengi wakikataza wataudhi wapiga kura, maandiko yenyewe yasema watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa huku tumeletewa dini tunajifanya wacha Mungu kuliko Vatican au huko sijui Macca, I wish corona ingewapiga viongozi wa dini ili raia wagutuke kuwa corona ni hatari, wengine badala ya kuelimisha wananchi wajilinde eti watoe sadaka ili wasipate corona

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hata hao viongozi wa dini nao ni waumini kama lawama zipelekwe kwa serikali.
 
Back
Top Bottom