Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

Kwa nini serikali haiwezi kufanya biashara ambazo kupata faida ni muhimu kwa mafanikio kama sekta binafsi.

1.Serikali zinaongozwa na wanasiasa sio wafanyabiashara.Kawaida ya mwanasiasa ni kuangalia mambo kwa vipindi vifupi vifupi.Mwanasiasa anafanya mambo akiangalia uchaguzi unaofuata kwa mfano miaka mitano ijayo.

Haijalishi kama serikali inao watu wenye ujuzi wa biashara au inaweza kuchukua watu kutoka nje ya mfumo wake.Mara zote katika kuajiri,kuongeza mtaji, kutafuta soko n.k itatanguliza maslahi yake ya kisiasa kwanza na kile inachoamini ni sahihi kwake na lazima kifanyike.

Biashara zenye ufanisi huwa hazifanyiwi kwa mtindo huo wa serikali bali kwa kungalia uhitaji na ya hali ya upatikanaji bidhaa sokoni pamoja na bei.Kwa mtazamo huo kampuni binafsi inaamua objectively wakati huu niongeze au nipunguze wafanyakazi, nisikope tena, niongeze au nisoongeze bidhaa au huduma.Kampuni ya serikali haiwezi kuwa objectively hivi itakuwa subjectively siku zote ikisikiliza upepo wa kisiasa unapovuma.
Lakini si serikali ipo vipindi vyote mkuu Yoda?

Wanasiasa watakuja na kuondoka, lakini serikali haiondoki!

Labda tuseme tu kwamba nchi zetu hizi hazina taratibu nzuri za uendeshaji serikali.

Wanasiasa wanapoondoka, hawaondoki na serikali wanapomaliza ngwe zao au wanapoachishwa kazi.

Kama mwanasiasa kakuta shirika linajiendesha vizuri na linaingiza faida, ataanzia wapi kuliua?
 
Watu ndio wanaendesha serikali. Na ndio wanaamua kipi kinafanyika na kipi hakifanyiki kwa muda upa.
Biashara haiwezi kuongozwa kwa katiba, ni maamuzi yanayotegema hali halisi ya wakati husika.
Huko kwenye nchi zilizoendelea ndio huwezi kukuta kabisa serikali zake zikifanya biashara.
Lakini si serikali ipo vipindi vyote mkuu Yoda?

Wanasiasa watakuja na kuondoka, lakini serikali haiondoki!

Labda tuseme tu kwamba nchi zetu hizi hazina taratibu nzuri za uendeshaji serikali.

Wanasiasa wanapoondoka, hawaondoki na serikali wanapomaliza ngwe zao au wanapoachishwa kazi.

Kama mwanasiasa kakuta shirika linajiendesha vizuri na linaingiza faida, ataanzia wapi kuliua?
 
2.Serikali inatumia pesa ambazo sio zake kufanya biashara. Pesa ambazo serikali inatumia kufanya biashara ni kodi za wananchi hivyo hata faida isipopatikana kwa uzembe wa kawaida kabisa hali ya kujali sio kubwa kwa sababu kodi zipo siku zote, zitachotwa tu kutoka hazina.

Magufuli wakati anafanya maamuzi ya kutumia pesa zetu za kodi na wanajeshi kununua korosho alisema serikali haipati hasara! Na huo ndio mtazamo halisi kwa sehemu kubwa ya watumishi wa umma hata kama hawasemi wazi kama yeye.

Kampuni au mtu binafsi anatumia pesa zake mwenyewe, akifanya uzembe atalala njaa, atafilisika au kufilisiwa kabisa na benki kama amechukua mkopo. Katika hali kama hiyo ufanisi na kujiongeza kwa wafanyakazi wake lazima kuwe kwa hali ya juu kuliko watumishi wa umma kwenye kampuni ya serikali.
Unadhani nakukatalia hayo unayoyasema kuhusu hawa viongozi wetu kutojali? Ninakuelewa na kukubaliana nawe kabisa juu ya hilo.

Lakiniiii, hoja ya msingi hapa ni:je hawa ndio viongozi wa mfano? Ndio viongozi wazuri katika kuendesha serikali?

Hata huko kwa wafanya biashara, wewe huoni watu wakifilisika kutokana na kuwa na tamaa ya kuoa wake (huu ni mfano tu, wa aina ya udhaifu wa binaadam).

Kwenye siasa pia hali ni hiyo hiyo. Tukipata viongozi wenye 'commitment' na dhamira ya kweli ya kuliinua taifa letu, kwa nini mashirika yake yasifanye vizuri?
 
Watu ndio wanaendesha serikali.Na ndio wanaamua kipi kinafanyika na kipi hakifanyiki kwa muda upa.
Biashara haiwezi kuongozwa kwa katiba,ni maamuzi yanayotegema hali halisi ya wakati husika.
Huko kwenye nchi zilizoendelea ndio huwezi kukuta kabisa serikali zake zikifanya biashara.
Najua serikali haifanyi biashara hizi za kuuza pipi.

Lakini, hata huko unakosema walikoendelea, kuna vitu ambavyo serikali haiwezi ikajitoa moja kwa moja na kuwaachia watu binafsi ndio waendeshe shughuli hizo.
Hawa wachina hadi juzi juzi walikuwa wamejifungia ndani. Mashirika yao mengi yalikuwa ya kiserikali, yakiendesha shughuli na kutoa huduma kwa wananchi wake.
Leo hii mashirika hayo ndiyo yanayofanya shughuli dunia nzima! Na ndiyo yaliyoijenga China na kuibuka hivi sasa kuwa kama ilivyo.
 
Katika suala la biashara sio viongozi wetu Tanzania tu, serikali zote duniani zinakabiliwa na hali hiyo hiyo.Nchi nyingi zilizopiga hatua kwa haraka ziligundua haya mapema zikaachana na zile biashara zinazoweza kufanywa kwa ufanisi na sekta binafsi.
Unadhani nakukatalia hayo unayoyasema kuhusu hawa viongozi wetu kutojali? Ninakuelewa na kukubaliana nawe kabisa juu ya hilo.

Lakiniiii, hoja ya msingi hapa ni:je hawa ndio viongozi wa mfano? Ndio viongozi wazuri katika kuendesha serikali?

Hata huko kwa wafanya biashara, wewe huoni watu wakifilisika kutokana na kuwa na tamaa ya kuoa wake (huu ni mfano tu, wa aina ya udhaifu wa binaadam).
Kwenye siasa pia hali ni hiyo hiyo. Tukipata viongozi wenye 'commitment' na dhamira ya kweli ya kuliinua taifa letu, kwa nini mashirika yake yasifanye vizuri?
 
Utasema mengi lakini ukweli ndio huo ..

Serikali haiwezi kufanya biashara! Tokea tupate uhuru mpaka leo hakuna sehemu ilipofanikiwa ni madudu tu kila siku.

Ni bora wajiweke pembeni wajikite kwenye kukusanya kodi tu

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Sasa si hata huko kukusanya kodi uliona wakiwa wanashindwa?

Sikubaliani nawe kamwe juu ya hayo mawazo ya kusema "Tokea uhuru mpaka leo hakuna sehemu linapofanikiwa..., ni madudu tu kila siku."

Unachanganya mambo mengi hapa pengine bila kujua.

Kushindwa kwa mambo mengi yaliyofanyika hapa tokea uhuru sababu zipo nyingi sana, hata zisizohusu maamuzi ya serikali. Kama wewe huwezi kulitambua hilo, basi maana yake ni kwamba mawazo yako umeyagandisha sehemu moja tu, na huna uwezo wa kupambanua hali zinazohusiana katika kufifisha mafanikio.
Ni vigumu sana kujadili jambo na mtu wa aina hiyo.
 
Pia waliona mwelekeo wabdunia wakaona ni vyema sekta binafsi iwe ni mshirika na sii adui kama ilivyokuwa kwetu.
Mkuu, unadhani hilo nalikataa? Silikatai kamwe, hali ndivyo ilivyo sasa duniani kote. Sekta binafsi inao mchango mkubwa sana katika taifa lolote, kama ilivyo kwa serikali kushiriki katika baadhi ya mambo kufuatana na hali ya nchi ilivyo.
 
Sio kwamba serikalini hakuna watu wenye ubunifu, ila hakuna mazingira yanayohamasisha waajiriwa kuwa wabunifu kila kitu mpaka bodi ya wakurugenzi ikae na maazimio ya kikao lazima yapelekwe kwa waziri ili yapatiwe solution
Sasa nikuulize.
Kuna katazo gani huko serikalini kufanya ubunifu?

Huo muundo ndio unaokataza ubunifu?

Mimi naona kinyume kabisa, kwa sababu kama Bodi ni ya watu waelewa na inafanya kazi vizuri, ubunifu huo ndio wangekuwa wanauchochea kabisa?

Wewe unaangalia uongozi mbaya, halafu unahitimisha kwamba hapawezi kuwepo na uongozi unaoweza kuendesha mashirika haya kwa ufanisi.
 
Serikali haiwezi kufanya biashara. Hasa hizi za kwetu.

Kama Waziri Mkuu anaona madudu kwenye mradi wa mwendokasi.

Kama Serikali imeshindwa kufanya miradi ya reli ya Kati na TAZARA, vivuko, ndege na sasa Mabasi ya mwendokasi kujiendesha ni wakati wa kubadili mtazamo.

Wajiondoe waruhusu sekta binafsi iviendeshe yenyewe ichukue Kodi na idili na kutoa huduma kwa wananchi.
Mabadiliko makubwa yanakuja.. Serikali itabaki na huduma tuu, biashara zitapelekwa sekta binafsi
 
Kuanzia mwaka 1950 hadi 1980 China ilikuwa na uchumi wa kijamaa haswa. Ule ujamaa wa serikali kumiliki kila biashara,rasilimali na kila kitu. Hapo mwanzoni waliua hadi matajiri viwanda vyao na ardhi zao zikachukuliwa na serikali ya Kikomunisti ya Mao.

Kipindi cha mapinduzi ya kiutamaduni kati ya mwaka 1966 hadi 1976 Hadi CocaCola zilipigwa marufuku China, suti za ulaya ilikuwa marufuku, kila kitu ilibidi ununue cha nchini kwako na sio kutoka kwa mabeberu.
Na sisi tukiamua kuua ushindani namna hiyo kwa sekta binafsi ya ndani ili biashara za serikali zifanikiwe tunaweza kufanikiwa ila kwa sekta binafsi ya nje haiwezekani kwa sababu hatuna soko la watu billion moja kama china kuweza kuuza kila kitu chote humu ndani mataifa mengine watakapoanza kutuwekea vikwazo na wao.
Najua serikali haifanyi biashara hizi za kuuza pipi.

Lakini, hata huko unakosema walikoendelea, kuna vitu ambavyo serikali haiwezi ikajitoa moja kwa moja na kuwaachia watu binafsi ndio waendeshe shughuli hizo.
Hawa wachina hadi juzi juzi walikuwa wamejifungia ndani. Mashirika yao mengi yalikuwa ya kiserikali, yakiendesha shughuli na kutoa huduma kwa wananchi wake.
Leo hii mashirika hayo ndiyo yanayofanya shughuli dunia nzima! Na ndiyo yaliyoijenga China na kuibuka hivi sasa kuwa kama ilivyo.
 
zikaachana na zile biashara zinazoweza kufanywa kwa ufanisi na sekta binafsi.
Haswaaaa.
Umetumia maneno ninayokubaliana nayo moja kwa moja.
Serikali haiwezi ikajiingiza kwenye kila aina ya biashara.

Lakini hilo sio sawa na kusema kwamba hakuna maeneo, kwa sababu mbalimbali, isipoweza kushiriki katika biashara yoyote.
 
Najua serikali haifanyi biashara hizi za kuuza pipi.

Lakini, hata huko unakosema walikoendelea, kuna vitu ambavyo serikali haiwezi ikajitoa moja kwa moja na kuwaachia watu binafsi ndio waendeshe shughuli hizo.
Hawa wachina hadi juzi juzi walikuwa wamejifungia ndani. Mashirika yao mengi yalikuwa ya kiserikali, yakiendesha shughuli na kutoa huduma kwa wananchi wake.
Leo hii mashirika hayo ndiyo yanayofanya shughuli dunia nzima! Na ndiyo yaliyoijenga China na kuibuka hivi sasa kuwa kama ilivyo.
Na ndio maana China haindelei kulinganisha na rasilimali ilizo nazo kutokana na mifumo mibovu kama hii ya Serikali ki hodhi kila kitu na kufanya Biashara.

Kutokana na mambo hayo itachukua Miaka 1000 China kuizidi U.SA huku kimsingi kutoka na Rasilimali zake pamoja na Idadi kubwa ya watu ambao ni Mara 4 ya Idadi ya Watu wa U.S.A alitakiwa awe amisha mpita U.S.A kiuchumi.
 
Sasa si hata huko kukusanya kodi uliona wakiwa wanashindwa?

Sikubaliani nawe kamwe juu ya hayo mawazo ya kusema "Tokea uhuru mpaka leo hakuna sehemu linapofanikiwa..., ni madudu tu kila siku."

Unachanganya mambo mengi hapa pengine bila kujua.

Kushindwa kwa mambo mengi yaliyofanyika hapa tokea uhuru sababu zipo nyingi sana, hata zisizohusu maamuzi ya serikali. Kama wewe huwezi kulitambua hilo, basi maana yake ni kwamba mawazo yako umeyagandisha sehemu moja tu, na huna uwezo wa kupambanua hali zinazohusiana katika kufifisha mafanikio.
Ni vigumu sana kujadili jambo na mtu wa aina hiyo.
Ni ukweli ulio bayana kuwa Serikali imeshindwa kufanya biashara na nibusara waukubali ukweli huu ili either waiachie private sector ifanye biashara wao wabaki kukusanya kodi au washirikiane na private sector through PPP.
Historia siku zote ni mwalimu. Tulikuwa na mashirika ya umma lukuki kama - NASACO, TRC, UFI, URAFIKI, TANGANYIKA PECKASE, ALAF, UDA , ATC ,TRC etc yote hayo tuliyazika kaburini kutokana na mapungufu ya namna ambavyo Serikali haiwezi kuendesha biashara.
 
Ubunifu huwa unachochewa na faida ambayo inaenda kwa mmiliki na wafanyakazi wake moja kwa moja. Shirika la serikali likipata faida au hasara mshahara wa mkuregenzi na wafanyakazi ni ule ule unaopangawa na utumishi au kuongezwa kwa pamoja na watumishi wengine wote mei mosi. Kwa mantiki hiyo kwa nini Mkuregenzi wa shirika la serikali afanye juhudi yoyote kuongeza ubunifu??
Sasa nikuulize.
Kuna katazo gani huko serikalini kufanya ubunifu?

Huo muundo ndio unaokataza ubunifu?

Mimi naona kinyume kabisa, kwa sababu kama Bodi ni ya watu waelewa na inafanya kazi vizuri, ubunifu huo ndio wangekuwa wanauchochea kabisa?

Wewe unaangalia uongozi mbaya, halafu unahitimisha kwamba hapawezi kuwepo na uongozi unaoweza kuendesha mashirika haya kwa ufanisi.
 
Kuanzia mwaka 1950 hadi 1980 China ilikuwa na uchumi wa kijamaa haswa. Ule ujamaa wa serikali kumiliki kila biashara,rasilimali na kila kitu. Hapo mwanzoni waliua hadi matajiri viwanda vyao na ardhi zao zikachukuliwa na serikali ya Kikomunisti ya Mao.

Kipindi cha mapinduzi ya kiutamaduni kati ya mwaka 1966 hadi 1976 Hadi CocaCola zilipigwa marufuku China, suti za ulaya ilikuwa marufuku, kila kitu ilibidi ununue cha nchini kwako na sio kutoka kwa mabeberu.
Na sisi tukiamua kuua ushindani namna hiyo kwa sekta binafsi ya ndani ili biashara za serikali zifanikiwe tunaweza kufanikiwa ila kwa sekta binafsi ya nje haiwezekani kwa sababu hatuna soko la watu billion moja kama china kuweza kuuza kila kitu chote humu ndani mataifa mengine watakapoanza kutuwekea vikwazo na wao.
Mkuu Yoda, hakuna serikali yoyote wakati huu 2021, hata ile ya kijana Kim Jong Un, wala Cuba, wanaofikiria kurudi kwenye enzi za miaka hiyo, sembuse sisi?

Lakini wakati huo huo, hata hawa Wamarekani, Waingereza, au Wajerumani, hakuna serikali inayokataa kata kata kuwa na mchango wowote katika uendeshaji na usimamizi wa baadhi ya maswala yanayogusa maisha ya wananchi wao moja kwa moja.
 
Na ndio maana China haindelei kulinganisha na rasilimali ilizo nazo kutokana na mifumo mibovu kama hii ya Serikali ki hodhi kila kitu na kufanya Biashara.

Kutokana na mambo hayo itachukua Miaka 1000 China kuizidi U.SA huku kimsingi kutoka na Rasilimali zake pamoja na Idadi kubwa ya watu ambao ni Mara 4 ya Idadi ya Watu wa U.S.A alitakiwa awe amisha mpita U.S.A kiuchumi.
Aiiseee, wewe unaishi dunia yako kama unaona hivyo ulivyoandika.
Sina lolote la kujibu hapo.
 
Suala la muhimu zaidi ni siku ya uzinduzi kukata utepe na kujipongeza....huko kwingine ni juu yenu🤣
 
Back
Top Bottom