Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

Kaka unajaribu kubadili fikra kuwa uhalisia. Mfumo wa serikali kufanya biashara ulifeli Dunia nzima miaka ya '80
Na nchi za ulaya zote walianza kuamini na kusapoti sekta binafsi kabla ya Karne ya 10.
Kampuni kubwa duniani NI za watu binafsi. Zio za ndege Wala za vinywaji.
Tanzania tunawatu wehu kweli. Simba inaajili kocha na wachezaji kutoka kila Kona wenye vipaji ndio wa kapata mafanikio.
Nmb manajment yote wazungu wenye vipawa vya usimamizi wa fedha na taaluma ndio maana imesimama.
Sisi wasomi wetu NI wasaka fursa sio talented. Mtu anakipawa Cha kuwa dokta anasoma uinjinia Sasa akija kwenye utendaji Hana Cha kuongezsa zaidi ya aliyoyasoma pindi akiwa chuo.
Eeenh Heeee, mchango wako 'serious', lakini ulivyouwasilisha imenibidi nicheke, hasa huko mwisho kwa 'dokta kuwa injinia"!

Mkuu, kama unanielewa vizuri, mimi sikatai ushiriki wa sekta binafsi sehemu yoyote katika biashara. Sikatai kabisa.

Ila naomba unielewe: unavyoliweka hapa wazo lako, ni kama huko kwenye sekta binafsi biashara hazianguki, na kana kwamba watu walioko huko ni kama malaika wenyewe walioshuka toka mbinguni.
Hali haipo hivyo hata kidogo

Na kwa maoni kama uliyotoa hapa, sijui unashindwa kitu gani kuhitimisha kabisa kwamba hata serikali yenyewe inafaa tuiondoe, tuwape sekta binafsi waiendeshe!
Labda nikutahadharishe kidogo unaponogewa na fikra zinapotiririka ukiandika; kwa mfano unaandika: "Na nchi za ulaya zote walianza kuamini na kusapoti ekta binafsi kabla ya karne ya 10". Kweli? Histyoria hii unayo? Na una uhakika nchi zote hizo hakuna kinachofanywa na serikali katika baadhi ya mashirika katika nchi hizo, badala ya kuiachia sekta binafsi ifanye, nchi zote za Ulaya?
 
Serikali haiwezi kufanya biashara. Hasa hizi za kwetu.

Kama Waziri Mkuu anaona madudu kwenye mradi wa mwendokasi.

Kama Serikali imeshindwa kufanya miradi ya reli ya Kati na TAZARA, vivuko, ndege na sasa Mabasi ya mwendokasi kujiendesha ni wakati wa kubadili mtazamo.

Wajiondoe waruhusu sekta binafsi iviendeshe yenyewe ichukue Kodi na idili na kutoa huduma kwa wananchi.
Wengi hawana elimu ya ujasiriamali
 
Serikali haitakiwi kufanya biashara, full stop. Serikali kazi yake ni kutunga sera na kuweka mazingira rafiki kwa watu ili wavutiwe kufanya biashara.
Huwezi kuwa na serikali inayoshindana na raia wake, lazima raia atashindwa tuu na mwisho wa siku serikali nayo itaboronga.
 
Kifupi wanaofanikiwa kwenye biashashara NI watu wenye vipawa vya UBUNIFU na kufanya biashara na sio wasomi. Wao ndio hubuni mbinu mpya za kutafuta masoko, kuvutia wateja na kusimAmia mitaji na kuchungulia fursa. Serikali haiwezi kuajili watu hao. Huajili kwa kuangalia vyeti na vyama vyao vya siasa.
Bodi za wakurugenzi kwa Kampuni kubwa huwa NI watu wenye hisa kubwa kwenye kampuni husika. Ikitokea limefilisika NI wao huwa wa kwanza kuumia.
Ila bodi ya wakurugenzi kwa mashirika ya Uma NI wateule wa Raisi au waziri. Wengi NI wanasiasa wastafu. Hawajui lolote kuhusu biashara na uenda uko kupokea posho tu sio kushauri.

Sio biashara tu vitu vya serikali vyote Hadi shule, hospital huduma NI mbovu kwa kukosa UBUNIFU.
Mchango wako huu umenifikirisha kweli kweli!

Natamani niukalie kidogo na kuutafakari ili nitoe mawazo ya kina juu yake; lakini najua nikiondoka sasa bila kujibu kitu, ninaweza nisipate nafasi tena ya kurudi.
Ngoja nijaribu kuujibu kwa kuukata vipande vipande:

1. Vipawa vya Ubunifu wa wafanya biashara ambao wasomi hawana ubunifu huo - sijui ukweli wa hili jambo. Kwani maana ya kuwa msomi ni nini hasa? Si inahitaji kujua vizuri eneo unalosomea na mbinu mbalimbali zinazotumika katika eneo hilo? Sasa kama umesoma vizuri na kujua mbinu za eneo hilo, kwa nini usiweze kujua mbinu na ubunifu katika eneo hilo?
Kwangu mimi, naamini, sio ukosefu wa kuwa mbunifumbinu, bali ni mchango wa mambo mbalimbali yanayokwamisha mashirika, ikiwemo na hizo siasa na ufisadi na mambo chungu nzima yanayoyakabili mashirika ya umma. Kama vikwazo hivi vingeondolewa, ufanisi kwenye mashirika ungepatikana.

2. "Bodi za wakurugenzi kwa kampuni kubwa huwa ni watu wenye hisa kubwa kwenye kampuni husika"
Na kama ulivyosema, bodi za mashirika ni watu walioteuliwa na wanasiasa, ambao hutumia vigezo ambavyo hata havina manufaa yoyote kwa shirika.
Swali ninalojiuliza hapa, ikiwa ni pamoja na kukuuliza wewe, kwa nini iwe hivi; na kwa nini wenye shirika (wananchi) na waoo wakubali hali hiyo? Hawa wanasiasa tunawachagua sisi wananchi; lakini tunashindwa kuwawajibisha?
Kwa hiyo jibu lipo hapa. Kushindwa kwa mashirika yetu kunatokana na sisi wenyewe wananchi kutowawajibisha wahusika ili watambue kuwa kazi wanazofanya hazikidhi matakwa yetu.

3. "Sio biashara tu, vitu vyote vya serikali, hadi shule, hospitali huduma ni mbovu kwa kukosa UBUNIFU."(?)

Huu mstari wako wa mwisho ndio uliotoa mhitasari mzuri sana wa mengine yote yaliyoandikwa hapo juu.
Siamini kwamba sababu ya ubovu wa shule, hospitali, n.k., ni ukosefu wa UBUNIFU.
Ni kutotimiza wajibu ipasavyo kwa wahusika, ikiwa ni pamoja na waajiriwa wa sehemu hizo na wasimamizi wao wote tokea ngazi za juu serikalini.
Kama serikali inawanyima watumishi wake nyenzo za kufanikisha kazi zao, huko sio kukosa 'UBUNIFU'.
 
Jibu la hoja yako lipo kwenye hiyo aya ya mwisho.

Kwa kifupi kabisa, pitia historia ya uchumi ya Tanzania tangu kupata uhuru kisha toa pendekezo la uhakika jinsi Tanzania itakavyoweza kuwapata hao “viongozi wenye commitment na dhamira ya kweli ...” na kuwapa madaraka stahiki ya uongozi wa mashirika ya serikali.

Ukitoa jibu thabiti kuhusu changamoto hilo basi hakika hoja yako ya serikali kufanya biashara kwa ufanisi/ushindani haitakuwa na ubishi.

Nyerere alishindwa na alieleza kuwa tatizo kubwa lililoua mashirika ya umma ni “kutotilia umuhimu mkubwa kwenye suala la management”. Ukweli ni kwamba isingewezekana kwa jinsi serikali ilivyokuwa ikiendeshwa huku malengo ya kisiasa yakiwa na kipaumbele namba moja ilhali yakikinzana na ya kibiashara/kiuchumi mara kwa mara.
Mchango mzito huu.
Sitoweza kuutendea haki kujibu harakaharaka hapa.
Lakini niseme tena hapa. Mimi, Kalamu1, sisemi kwamba serikali ijihusishe na kila aina ya biashara yoyote iwayo; lakini nasema bila kumung'unya maneno, serikali inawajibu, na ni lazima, haiwezi kujitoa moja kwa moja katika baadhi ya maeneo, kama elimu, kama afya, kama mashirika muhimu yanayotoa huduma kwa wananchi, kama umeme, na hata maji.

Na hasa hasa kwa wakati huu wa maendeleo ya nchi yetu.

Ila, naisihi serikali yetu, ifanye kazi zake kwa ufanisi ili mashirika haya yatoe huduma stahiki kwa wananchi.
 
Ni Ujinga kila saa kutolea mfano wa china, Tanzania mtu anaiba na afanywi chochote kwa sababu tu ni kada wa chama na alikua mteule wa rais
Mkuu 'Science Priest', mimi nimekwishatoa mfano wa China kuwa na mashirika yaliyofanikiwa, lakini sikugusia hayo uliyoyaweka hapo ya kuwaondoa uhai wabadhirifu, sio kwamba sikujua. Hilo nililiacha maksudi, na kwa kweli sioni tatizo ikifanyika hivyo hata hapa, mradi haki inatendeka.

Magufuli angeelekeza ukali wake huko, na kutoonea wapinzani wake, hata mimi ningekuwa shabiki wake mkubwa.

Hatuwezi kuendelea kuwachekeachekea hawa washenzi wanaoturudisha nyuma, halafu hao hao wanarudi hata humu JF na kutucheka na kusema serikali haiwezi kufanya biashara!
Inaudhi sana!

Nakushukuru kwa kuwa muwazi, na ningependa sasa tuwaambie hawa watu ukweli bila kuficha kitu kwamba tunataka viongozi serikalini wenye uchungu na mali za nchi hii. Ukihujumu, kama wewe ni mfanya kazi, au mfanya biashara, kukwamisha maslahi ya wananchi, haki yako ni adhabu kali, ikiwa ni pamoja na kuondoa uhai wako.

Utakubaliana nami tuipigie kelele kampeni hii humu JF?
 
View attachment 1764619


Nilishakuwekea jibu hapo ☝️hizo grants ni mkopo kutoka serikalini wanalipa sio bure. Umeona mkopo wa £1.3 billion kwa jiji GLA (greater London authority) inayoendesha TfL; na TFL yenyewe imepokea £750 directly na umeambiwa kabisa ni loan from DfT (Department for Transport; wizara ya uchukuzi).

Kama umesoma biashara utakuwa unaelewa sources of investment finance; government grants ikiwa moja wapo na wanufaika includes private organization.

Anyway mada inasema serikali aiwezi endesha biashara na mabeberu hawafanyi ivyo; jambo ambalo si la ukweli.

Kumbe huelewi kwamba hela ya serikali ni hela ya walipa kodi. London Underground ambayo asilimia 41% ya hela za kuindesha zinatoka kwa walipa kodi tuseme ni government program siyo biashara.
 
Watendaji na wezi kwenye hayo mashirika si ni sisi hawa hawa; inakuwaje tunailaumu serikali inayotuwezesha?
Sioni logic ya kuilaumu serikali wakati tunaoua hayo mashirika ni sisi wenyewe!
 
Miradi ya serikali wanaiendesha bila ya kuwa na uchungu wao hawajali kuhusu pesa
Anglia mradi akiuwendesha mtu binafsi lazima awe na uchungu,mfano tu mtu kama baresa etc ona wanavyoendesha biashara zao
Ila serikali wao wanajua hata mradi ukifa itatafutwa pesa nyingine tu

Ova
 
Ninachokubaliana nawe moja kwa moja katika hoja yako ni hayo hapo juu niliyonakili.

Hii ina maana, hata mengine yasiyo ya biashara huko serikalini yapo hivyo hivyo. Je, na yenyewe tuyabinafsishe?
Hili ni swali halisi ninalouliza, wala sio katika kujibu hoja yako.

Sasa swali ni hili. Tufanyeje?

Tunaweza tukawapata viongozi wenye 'commitment' ya kuliendeleza taifa hili, pamoja na udhaifu wa ubinaadam walionao kila mmoja wao? Tufanyeje?
Hawa makampuni binafsi, tuwakodishe watuendeshee serikali pia?

Maswali ni mengi.

Nimeeleza nini cha kufanya ktk post yangu uliyoikwoti...

Taasisi na mashirika ya umma yaachwe yajiendeshe yenyewe kwa kuzingatia professionalism huku serikali ikisimama kama mlezi mkuu ili wakikosea tuwe na nguvu kuwauliza na kuwahoji...

Kwa sasa sina hakika kama serikali (viongozi hawa PM, Rais, wabunge nk ) wana audacity ya kukemea hasara na failures ktk uendeshaji wa mashirika na taasisi hizi za umma huku wenyewe wakiwa ni sehemu ya tatizo/failures hizo...

Tuwazuie wanasiasa kisheria kuingiza nepotism na siasa zao kwenye uendeshaji wa taasisi na mashirika haya. Tuziache management ziwe free kuendesha taasisi hizi...
 
Hao(sekta binafsi) hatuwaachii waendeshe tu kama wanavyoendesha TICTS bandarini. Serikali ikiamua kuindoa ATCL na mwendokasi mikononi mwake hayo mashirika yanakuwa kampuni binafsi kabisa za mtu mmoja au wanahisa wenye hisa nyingi waliokidhi vigezo vya kuuziwa.

Serikali inabaki kukusanya kodi au ushuru tu kama inavyokusanya kwenye mabasi ya watu binafsi mikoani, daladala na inavyokusanya fastjet na precision airways na kusimamia sheria.
Nchi kufaidika ni kukusanya kodi yake inavyotakiwa baada ya kuyauza hayo makampuni katika mchakato wa wazi na unaozingatia vigezo na kanuni, kama hata hiyo kazi yake ya msingi haiwezi basi iombe isaidiwe.
Lakini serikali yenyewe pia inaweza ikayaendesha mashirika hayo kwa ufanisi ikitaka kufanya hivyo. Hakuna kizuizi chochote kinachoifanya sewrikali isiweze kuyaendesha vizuri bila ya kutegemea sekta binafsi.
 
Taasisi na mashirika ya umma yaachwe yajiendeshe yenyewe kwa kuzingatia professionalism huku serikali ikisimama kama mlezi mkuu ili wakikosea tuwe na nguvu kuwauliza na kuwahoji...
Hakuna chochote ninachokataa hapa.
Kwa sasa sina hakika kama serikali (viongozi hawa PM, Rais, wabunge nk ) wana audacity ya kukemea hasara na failures ktk uendeshaji wa mashirika na taasisi hizi za umma huku wenyewe wakiwa ni sehemu ya tatizo/failures hizo...
Nadhani kinachotakiwa hapa ni kuwapata viongozi hao wa ngazi za juu wasiokubali uozo popote ndani ya serikali na mashirika yake.

Kutokubali huko ni pamoja na kujitambulisha wazi kabisa kwamba kila atakayevuruga popote hatoachwa hivi hivi. Sheria itamkumba na hata ikibidi adhabu mbaya zaidi ziwekwe kuwadhibiti hawa wakorofi.
Tuwazuie wanasiasa kisheria kuingiza nepotism na siasa zao kwenye uendeshaji wa taasisi na mashirika haya. Tuziache management ziwe free kuendesha taasisi hizi...
Nipo nawe sawia kabisa.

Unajua, hata huko kwenye sekta binafsi wanaohimiza serikali kujiondoa kwenye sehemu kadhaa za kimkakati, ni hawa hawa wanaochochea uozo huko serikalini, halafu wanageuka na kuanza kuhimiza wapewe wao.

Akina Roastam na wengine wamehimiza hapa kugawiwa karibu bure kabisa mali za serikali, halafu wanageuka na kuzifanya mtaji wa kukopa pesa za kufanya shughuli zao nyingine; halafu wanageuka na kuicheka serikali na kuwacheka wananchi.
 
Mada muhimu kweli kweli, lakini wachangiaji wanachungulia tu na kupita zao! Wanatafuta mada za CCM na CHADEMA!

Mimi sikubaliani na wewe juu ya hiyo dhana ya serikali haifanyi biashara.

Usiifanye kuwa 'dogma', au kama kitu ulichokaririshwa.

Hata kama ulisikia ikisemwa hivyo, kwa nini usiweke muda ujaribu kutazama uhalisia na ukweli wake ukoje?

Sasa mimi nakushauri uanze kulitazama hilo kwa jicho la pili; acha kufumba jicho moja, yafungue yote mawili ili upate picha nzuri.

Ni hivi: kuna kizuizi gani kinachofanya serikali isiweze kufanikisha kuendesha miradi hiyo yote uliyoitaja?

Kwani haina watu wenye uwezo wa kuifanya. Kama wapo, ni nini kinazuia wasifanye hiyo kazi kwa ufanisi?

Na kama hawapo, serikali haiwezi ikamwajiri, ndiyo kuajiri kampuni kwa mkataba inayoweza kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi? Sijasema serikali ibinafsishe, kama wewe unavyotaka.

Lakini la muhimu hapa ninalolisisitiza, ni hii dhana potofu ya kwamba serikali haiwezi kufanya mambo yake kwa ufanisi.

Kuna sababu zipi...., hizo sababu haziwezi kuondolewa?

Kila mara imekuwa ni kutafuta visingizio tuuu kwa kushindwa tu kutimiza wajibu mliopewa kuutimiza.

Hapa ndipo nilipopenda Magufuli apafanyie udikteta wake haswa haswa...! Hali ingebadilika tu baada ya muda.

Haya mashirika makubwa ya ujenzi na mengine toka China tunayoona yametapakaa duniani kote, mbona haya yalikuwa ni mashirika chini ya serikali?
Wao waliweza vipi?
Una akili ya mbuni kuinua mikia ya nyuma angani na kufukia kichwa shimoni.

Umeshawahi kuisikia UDA , DMT na hata KAMATA?

Ziliendeshwa na serikali kwa miongo zaidi ya mitatu, na serikali ikanyoosha mikono.

Sasa leo nini kimebadilika?
Wameendesha mradi kimagumashi na tunaona matokeo yake.
Amka ndugu!
 
Hakuna chochote ninachokataa hapa.

Nadhani kinachotakiwa hapa ni kuwapata viongozi hao wa ngazi za juu wasiokubali uozo popote ndani ya serikali na mashirika yake.

Kutokubali huko ni pamoja na kujitambulisha wazi kabisa kwamba kila atakayevuruga popote hatoachwa hivi hivi. Sheria itamkumba na hata ikibidi adhabu mbaya zaidi ziwekwe kuwadhibiti hawa wakorofi.

Nipo nawe sawia kabisa.

Unajua, hata huko kwenye sekta binafsi wanaohimiza serikali kujiondoa kwenye sehemu kadhaa za kimkakati, ni hawa hawa wanaochochea uozo huko serikalini, halafu wanageuka na kuanza kuhimiza wapewe wao.

Akina Roastam na wengine wamehimiza hapa kugawiwa karibu bure kabisa mali za serikali, halafu wanageuka na kuzifanya mtaji wa kukopa pesa za kufanya shughuli zao nyingine; halafu wanageuka na kuicheka serikali na kuwacheka wananchi.
1. Ishu si "kuwapata wapi viongozi wa kuwakabidhi taasisi/mashirika haya" ili wayaendeshe. Viongozi ni hawahawa waliopo wanatosha na wana sifa zote..

2. Kinachokosekana kwa viongozi hawa ni Job security zao. Hatima yao iko controlled na wanasiasa. Hawana uhakika wa kesho yao. Wanachofanya ni kutafuta mwanya wa kuchukua chao mapema tena mara nyingi wakishirikiana na wanasiasa - watawala hao hao kuyafilisi na kuyala mashirika haya. Katika mazingira haya, huwezi kuwa na management bunifu kuendeleza taasisi/shirika...

3. Unawalaumu bure kina Rostam na wengine waliopewa viwanda na kushindwa kuviendeleza...

Sababu ni zilezile, SIASA CHAFU ambazo zinazalisha viongozi waovu na mafisadi..

Hawa daima ni walaji na hawana uchungu wala hawaangalii maslahi ya nchi bali matumbo yao na familia zao...

Kupewa viwanda hivyo na kisha kushindwa kuendelezwa, ni deal kati ya wafanya biashara hao na baadhi ya wanasiasa - watawala kujipatia fedha kwenye mabenki kwa dhamana ya serikali kisha kutumika kufanyia mambo mengine...

Na ikitokea hivi hakuna hatua zinazochukuliwa kwa wafanyabiashara hawa kwa kuwa viongozi wenyewe are part of the deal...
 
Una akili ya mbuni kuinua mikia ya nyuma angani na kufukia kichwa shimoni.

Umeshawahi kuisikia UDA , DMT na hata KAMATA?

Ziliendeshwa na serikali kwa miongo zaidi ya mitatu, na serikali ikanyoosha mikono.

Sasa leo nini kimebadilika?
Wameendesha mradi kimagumashi na tunaona matokeo yake.
Amka ndugu!
'Masopya...' vuta pumzi, kwa sababu hapa ni serious discussion, na tambua unanijibu mimi, huwa sitaki upuuzi..., mbona hukumbuki?
Hayo mashirika nayajua sana na nimeyapanda sana, na huwezi kuniambia chochote juu yake.

Soma vizuri unielewe: kama ni nyinyi, sijui kama nawe uko kwenye biashara hizo za kutafuta kila mara kuangusha juhudi za serikali, bado hamjampata kiongozi anayeweza kuwakomesha.

Magufuli kama angeacha upuuzi wa kuonea watu wasiostahiri kuonewa, na akashughulika na wahujumu waliopo humo humo serikalini na huko kwenu kwenye sekta binafsi, angeacha heshima kubwa sana katika jamii ya kumkumbuka kwayo.

Sasa hapa nimemzungumzia Magufuli moja kwa moja kukuchokoza kama wewe ni mtu mwenye kumbukumbu, kwa sababu tulishawashiana moto juu yake wewe na mimi na pacha wako 'Jidu' humu humu JF.

Kwa hiyo wewe kuniita mimi kuwa na "...akili za mbuni" inakufanya wewe uwe kama kichaa fulani.

Katika nchi zetu hizi, na hasa kwa Tanzania, baada ya kuona Magufuli aliyofanya, dawa ya kuyafanya hayo mashirika kufanya kazi ipaswavyo ni kuacha kucheka cheka na wapuuzi wanayoyaendesha.
Ikilazimu, baadhi yao ni kufungwa jela maisha na hao wanaohujumu hata kifo ni haki yao.

Ndiyo, nyinyi watu mnatia hasira sana na hivi vimambo vyenu.

Mnashiriki kuyaua mashirika ya wananchi, halafu mnarudi hapo pembeni na kuchekelea..., kuna usaliti zaidi ya huo?

Huu ndio usaliti unaotakiwa kunyongwa na kufilia mbali, kwa maslahi mazima ya taifa, sio kwenda kuhangaika na akina Lissu!

Nimejaribu kila njia ya kujieleza nieleweke, naona sieleweki na wengi hapa. Maslahi ya waTanzania ni kila kitu, hayawezi kuchezewa na mtu yeyote, iwe serikalini au huko kwenye sekta binafsi.

Naomba sana utulie unisome vyema, usinirukie tu kujibu bila kuelewa ninakotokea.

Mnachosha sana.
 
3. Unawalaumu bure kina Rostam na wengine waliopewa viwanda na kushindwa kuviendeleza...

Sababu ni zilezile, SIASA CHAFU ambazo zinazalisha viongozi waovu na mafisadi..
Huwezi kuwaondoa hao wafanya biashara katika muungano wao na siasa chafu. Kwani historia zao hapa Tanzania hazipo wazi? Walijazana bungeni kufanya nini?

Wanaowachochea hao wenye siasa chafu ni akina nani kama siyo hawa hawa!

Wote wapo kwenye chungu kimoja.
 
Kupewa viwanda hivyo na kisha kushindwa kuendelezwa, ni deal kati ya wafanya biashara hao na baadhi ya wanasiasa - watawala kujipatia fedha kwenye mabenki kwa dhamana ya serikali kisha kutumika kufanyia mambo mengine...

Na ikitokea hivi hakuna hatua zinazochukuliwa kwa wafanyabiashara hawa kwa kuwa viongozi wenyewe are part of the deal..
Sasa mkuu, 'The Palm Tree', mbona uliwaondoa kwenye lawama kwenye mchango wako huko juu?

Huwezi kurekebisha chochote kwenye siasa bila kuwagusa hawa wafanya biashara wahujumu wakubwa wa nchi zetu hizi.
 
Again!!

Acha porojo nitajie shirika moja tu la serikali linaloendeshwa kwa faida

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Sasa nikisema hakuna, utachukua huo kama ushahidi kuonyesha kwamba serikali haiwezi kuendesha mashirika yake kwa ufanisi?

Mimi sikubaliani na hiyo dhana ya kwamba serikali haiwezi kuendesha mashirika yake, SIKUBALI.

Sitaki kurudiarudia mambo niliyokwishaandika hapa.

Ubovu wa watendaji, wanaoua mashirika, sio sababu ya kuhitimisha kwamba serikali haiwezi kufanya kazi hizo.

Inaweza sana, kwa kuwashughulikia wahujumu wake wote, waliopo kwenye mashirika hayo, na walio nje, hasa kwenye hizo sekta binafsi.

Bado tu hajapatikana mtu sahihi wa kuwanyoosha wote.

Ukitaka kunielewa, utaelewa ninachoandika hapa, ukitaka kuona kuwa ni porojo, sawa, jifurahishe.
 
Back
Top Bottom