Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

'Masopya...' vuta pumzi, kwa sababu hapa ni serious discussion, na tambua unanijibu mimi, huwa sitaki upuuzi..., mbona hukumbuki?
Hayo mashirika nayajua sana na nimeyapanda sana, na huwezi kuniambia chochote juu yake.

Soma vizuri unielewe: kama ni nyinyi, sijui kama nawe uko kwenye biashara hizo za kutafuta kila mara kuangusha juhudi za serikali, bado hamjampata kiongozi anayeweza kuwakomesha.

Magufuli kama angeacha upuuzi wa kuonea watu wasiostahiri kuonewa, na akashughulika na wahujumu waliopo humo humo serikalini na huko kwenu kwenye sekta binafsi, angeacha heshima kubwa sana katika jamii ya kumkumbuka kwayo.

Sasa hapa nimemzungumzia Magufuli moja kwa moja kukuchokoza kama wewe ni mtu mwenye kumbukumbu, kwa sababu tulishawashiana moto juu yake wewe na mimi na pacha wako 'Jidu' humu humu JF.

Kwa hiyo wewe kuniita mimi kuwa na "...akili za mbuni" inakufanya wewe uwe kama kichaa fulani.

Katika nchi zetu hizi, na hasa kwa Tanzania, baada ya kuona Magufuli aliyofanya, dawa ya kuyafanya hayo mashirika kufanya kazi ipaswavyo ni kuacha kucheka cheka na wapuuzi wanayoyaendesha.
Ikilazimu, baadhi yao ni kufungwa jela maisha na hao wanaohujumu hata kifo ni haki yao.

Ndiyo, nyinyi watu mnatia hasira sana na hivi vimambo vyenu.

Mnashiriki kuyaua mashirika ya wananchi, halafu mnarudi hapo pembeni na kuchekelea..., kuna usaliti zaidi ya huo?

Huu ndio usaliti unaotakiwa kunyongwa na kufilia mbali, kwa maslahi mazima ya taifa, sio kwenda kuhangaika na akina Lissu!

Nimejaribu kila njia ya kujieleza nieleweke, naona sieleweki na wengi hapa. Maslahi ya waTanzania ni kila kitu, hayawezi kuchezewa na mtu yeyote, iwe serikalini au huko kwenye sekta binafsi.

Naomba sana utulie unisome vyema, usinirukie tu kujibu bila kuelewa ninakotokea.

Mnachosha sana.
Bado huelewi the spirit of free enterprise na innovativeness of private business.
Serikali kufanya biashara ni sawasawa na paka kukata mawimbi kuogelea pale Feri!

Ni ukweli usiopingika kuwa huwezi kukuta ati “mzalendo” akabidhiwe mabilioni ya wananchi halafu ayachekee bila kuchota kiasi.

Mwisho sisi wenyewe kwa ujinga wetu tunamkabidhi mabilioni halafu tunamwita mhujumu.
Huyo mtu hana uchungu wowote na mtaji au mali ya umma iliyopo pale , wala hajawekeza chochote pale zaidi ya ajira!

Halafu tunategemea afanye wonders!
Hapo ni kutegemea yule paka aogelee toka Feri hadi Kigamboni.

Tatizo mko wengi msiojua principles hizo, na wasiojua kwa kiwango cha lami wanafikiri msomi zaidi hasa mwenye PhD ndio watakuwa enterprising zaidi.

Experience is proving them wrong!
Mwalimu alitengeneza mashirika zaidi ya 400, yalikufa YOOOTE!
Na hilo somo wenye vichwa vigumu hawalielewi.............!
 
Experience is proving them wrong!
Mwalimu alitengeneza mashirika zaidi ya 400, yalikufa YOOOTE!
Na hilo somo wenye vichwa vigumu hawalielewi.............!
Hii mnapenda sana kuiimba kama kasuku, lakini hamuelewi chochote mnachoimba.

Inaelekea unasoma, lakini ubongo wako umeganda palepale ulipogandia toka mwanzo.

Kuna biashara inayoweza kuzifanya serikali kwa mafanikio makubwa kwa manufaa ya wananchi. Kama wewe hutaki kukubali hilo, hiyo ni shida yako, baki nayo hivyo hivyo.
 
Hii mnapenda sana kuiimba kama kasuku, lakini hamuelewi chochote mnachoimba.

Inaelekea unasoma, lakini ubongo wako umeganda palepale ulipogandia toka mwanzo.

Kuna biashara inayoweza kuzifanya serikali kwa mafanikio makubwa kwa manufaa ya wananchi. Kama wewe hutaki kukubali hilo, hiyo ni shida yako, baki nayo hivyo hivyo.
Srikali inafanya biashara kama zipi kwako wewe ubongo uliozibuka!
Zitaje!
 
Hujui biashara zinazofanywa na serikali?

Sasa hapa unalalamikia nini juu ya serikali kujiingiza kwenye biashara!
Usikwepe kwepe swali.
Zaidi ya kodi tupe shirika linaloendeshwa kibiashara na kwa faida ya "kizalendo" kama ulivyohamasika!
 
UshU
Mchango wako huu umenifikirisha kweli kweli!

Natamani niukalie kidogo na kuutafakari ili nitoe mawazo ya kina juu yake; lakini najua nikiondoka sasa bila kujibu kitu, ninaweza nisipate nafasi tena ya kurudi.
Ngoja nijaribu kuujibu kwa kuukata vipande vipande:

1. Vipawa vya Ubunifu wa wafanya biashara ambao wasomi hawana ubunifu huo - sijui ukweli wa hili jambo. Kwani maana ya kuwa msomi ni nini hasa? Si inahitaji kujua vizuri eneo unalosomea na mbinu mbalimbali zinazotumika katika eneo hilo? Sasa kama umesoma vizuri na kujua mbinu za eneo hilo, kwa nini usiweze kujua mbinu na ubunifu katika eneo hilo?
Kwangu mimi, naamini, sio ukosefu wa kuwa mbunifumbinu, bali ni mchango wa mambo mbalimbali yanayokwamisha mashirika, ikiwemo na hizo siasa na ufisadi na mambo chungu nzima yanayoyakabili mashirika ya umma. Kama vikwazo hivi vingeondolewa, ufanisi kwenye mashirika ungepatikana.

2. "Bodi za wakurugenzi kwa kampuni kubwa huwa ni watu wenye hisa kubwa kwenye kampuni husika"
Na kama ulivyosema, bodi za mashirika ni watu walioteuliwa na wanasiasa, ambao hutumia vigezo ambavyo hata havina manufaa yoyote kwa shirika.
Swali ninalojiuliza hapa, ikiwa ni pamoja na kukuuliza wewe, kwa nini iwe hivi; na kwa nini wenye shirika (wananchi) na waoo wakubali hali hiyo? Hawa wanasiasa tunawachagua sisi wananchi; lakini tunashindwa kuwawajibisha?
Kwa hiyo jibu lipo hapa. Kushindwa kwa mashirika yetu kunatokana na sisi wenyewe wananchi kutowawajibisha wahusika ili watambue kuwa kazi wanazofanya hazikidhi matakwa yetu.

3. "Sio biashara tu, vitu vyote vya serikali, hadi shule, hospitali huduma ni mbovu kwa kukosa UBUNIFU."(?)

Huu mstari wako wa mwisho ndio uliotoa mhitasari mzuri sana wa mengine yote yaliyoandikwa hapo juu.
Siamini kwamba sababu ya ubovu wa shule, hospitali, n.k., ni ukosefu wa UBUNIFU.
Ni kutotimiza wajibu ipasavyo kwa wahusika, ikiwa ni pamoja na waajiriwa wa sehemu hizo na wasimamizi wao wote tokea ngazi za juu serikalini.
Kama serikali inawanyima watumishi wake nyenzo za kufanikisha kazi zao, huko sio kukosa 'UBUNIFU'.
Ushauri NI kuwa serikali idili na vitu vichache tu. Huwezi kung'ang'ania vitu ambavyo sekta binafsi Inaweza kuvifanya vizuri.
 
UshU
Ushauri NI kuwa serikali idili na vitu vichache tu. Huwezi kung'ang'ania vitu ambavyo sekta binafsi Inaweza kuvifanya vizuri.
Hata sasa hivyo inavyovifanya bila ufanisi ni vichache; lakini haina maana kwamba haiwezi kuvifanya kwa ufanisi. Inaweza sana.
 
Serikali haiwezi kufanya biashara. Hasa hizi za kwetu.

Kama Waziri Mkuu anaona madudu kwenye mradi wa mwendokasi.

Kama Serikali imeshindwa kufanya miradi ya reli ya Kati na TAZARA, vivuko, ndege na sasa Mabasi ya mwendokasi kujiendesha ni wakati wa kubadili mtazamo.

Wajiondoe waruhusu sekta binafsi iviendeshe yenyewe ichukue Kodi na idili na kutoa huduma kwa wananchi.
Mfumo wa uendeshaji mashirika ya umma Una mapungufu,watendaji wangeajiliwa kwa kutuma maombi na pawepo na vipengele vya uwajibikaji kwa watumishi pia,CEO awe na mkataba na si mtumishi wa umma na apewe malengo ya shirika akishindwa anaondolewa kama makocha wa mpira .
 
Kama inaweza sana kufanya kwa ufanisi, then tatizo ni nini?
Tatizo ni serikali, kwani serikali haiwezi kufanya kazi zake kwa ufanisi? Inazuiwa na nani kufanya hivyo.

Hivi serikali zinakuwepo ili zifanye mambo bila ufanisi; hiyo ndiyo kawaida?
 
Hii mnapenda sana kuiimba kama kasuku, lakini hamuelewi chochote mnachoimba.

Inaelekea unasoma, lakini ubongo wako umeganda palepale ulipogandia toka mwanzo.

Kuna biashara inayoweza kuzifanya serikali kwa mafanikio makubwa kwa manufaa ya wananchi. Kama wewe hutaki kukubali hilo, hiyo ni shida yako, baki nayo hivyo hivyo.
Biashara ipi na kwa mfano upi dhahili?
 
Mada muhimu kweli kweli, lakini wachangiaji wanachungulia tu na kupita zao! Wanatafuta mada za CCM na CHADEMA!

Mimi sikubaliani na wewe juu ya hiyo dhana ya serikali haifanyi biashara.

Usiifanye kuwa 'dogma', au kama kitu ulichokaririshwa.

Hata kama ulisikia ikisemwa hivyo, kwa nini usiweke muda ujaribu kutazama uhalisia na ukweli wake ukoje?

Sasa mimi nakushauri uanze kulitazama hilo kwa jicho la pili; acha kufumba jicho moja, yafungue yote mawili ili upate picha nzuri.

Ni hivi: kuna kizuizi gani kinachofanya serikali isiweze kufanikisha kuendesha miradi hiyo yote uliyoitaja?

Kwani haina watu wenye uwezo wa kuifanya. Kama wapo, ni nini kinazuia wasifanye hiyo kazi kwa ufanisi?

Na kama hawapo, serikali haiwezi ikamwajiri, ndiyo kuajiri kampuni kwa mkataba inayoweza kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi? Sijasema serikali ibinafsishe, kama wewe unavyotaka.

Lakini la muhimu hapa ninalolisisitiza, ni hii dhana potofu ya kwamba serikali haiwezi kufanya mambo yake kwa ufanisi.

Kuna sababu zipi...., hizo sababu haziwezi kuondolewa?

Kila mara imekuwa ni kutafuta visingizio tuuu kwa kushindwa tu kutimiza wajibu mliopewa kuutimiza.

Hapa ndipo nilipopenda Magufuli apafanyie udikteta wake haswa haswa...! Hali ingebadilika tu baada ya muda.

Haya mashirika makubwa ya ujenzi na mengine toka China tunayoona yametapakaa duniani kote, mbona haya yalikuwa ni mashirika chini ya serikali?
Wao waliweza vipi?
Mnapenda kukifananisha na China lakini hamtaki hata kidogi kuishi kama wachina. Lakini hata serikali ya China haifanyi biashara japo inatoa huduma ya usafiri mijini kama hiyo ya mwendo kasi.
Tatizo letu ni moja, UBINAFSI.
Magu nae aliteswa na ubinafsi ,, kile kituko cha kuipaisha chato kwa nguvu huku akitumia kodi zetu kilimtoa kabisa sifa za kuweza kusimamia mali zetu vizuri.
Hivyo njia inayobaki ni serikali kutojiingiza kwenye biashara au la iamue kutoa huduma.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hii mnapenda sana kuiimba kama kasuku, lakini hamuelewi chochote mnachoimba.

Inaelekea unasoma, lakini ubongo wako umeganda palepale ulipogandia toka mwanzo.

Kuna biashara inayoweza kuzifanya serikali kwa mafanikio makubwa kwa manufaa ya wananchi. Kama wewe hutaki kukubali hilo, hiyo ni shida yako, baki nayo hivyo hivyo.
Biashara ipi na kwa mfano upi dhahili?
Hutaki kuelewa ninachoeleza, siwezi kukulazimisha uelewe na ukubali.
Wewe hujui mifano ya mashirika inayoyaendesha? Unataka nikupe mifano?
Mashirika yote yanayoendeshwa na selikali kwa 100% uendeshwa kwa hasara, hutegemea ruzuku tu kujiendesha na hayana UBUNIFU na mshindani. Mfano NI Tanesco, Posta, TLA,
Using'ang'anize hoja zisizo na uhalisia
 
Mnapenda kukifananisha na China lakini hamtaki hata kidogi kuishi kama wachina. Lakini hata serikali ya China haifanyi biashara japo inatoa huduma ya usafiri mijini kama hiyo ya mwendo kasi.
Tatizo letu ni moja, UBINAFSI.
Magu nae aliteswa na ubinafsi ,, kile kituko cha kuipaisha chato kwa nguvu huku akitumia kodi zetu kilimtoa kabisa sifa za kuweza kusimamia mali zetu vizuri.
Hivyo njia inayobaki ni serikali kutojiingiza kwenye biashara au la iamue kutoa huduma.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Siyo lazima tuishi kama wachina, lakini tunaweza kutumia baadhi ya njia zao zinazofanikisha katika mazingira yetu. Kwa nini tuishi kama wao; kwani sisi hatuna akili za kufikiri na kupanga mambo tunayoona yanafaa?

Una maana unamwona mchina bora kuliko ulivyo wewe, hadi upende kuishi maisha yake?

Serikali zote dunia hutoa huduma, sio China pekee...

Hata hivyo, unaangalia tu huduma za mwendo kasi hapo, kwani huduma zinapotolewa hazipashwi kufanywa ili ziwe huduma bora?

Sikubaliani na wewe juu ya serikali ya china kutofanya biashara. Mashirika yote yaliyotapakaa duniani kote yanayojenga kila aina ya miundo mbinu yanatoa huduma?
TTCL hapa kwetu haiwezi kufanya biashara, kwa nini?
 
Mashirika yote yanayoendeshwa na selikali kwa 100% uendeshwa kwa hasara, hutegemea ruzuku tu kujiendesha na hayana UBUNIFU na mshindani. Mfano NI Tanesco, Posta, TLA,
Using'ang'anize hoja zisizo na uhalisia
Kwa nini kwa mfano, Tanesco iwe biashara ya hasara, hebu nieleze wewe? Na kwa nini hiyo biashara inatakiwa ifanywe na shirika binafsi ndipo liwe na faida, kwa nini?
Hapa ndipo ninapotaka ufafanue kwa nini iwe hivyo.

Usiseme tu kwa kuwa ni serikali haiwezi kufanya biashara, hiyo siyo sababu.

Ndio, kuna aina za biashara/huduma zinazohitaji kupewa ruzuku, lakini si zote.
 
Kwa nini kwa mfano, Tanesco iwe biashara ya hasara, hebu nieleze wewe? Na kwa nini hiyo biashara inatakiwa ifanywe na shirika binafsi ndipo liwe na faida, kwa nini?
Hapa ndipo ninapotaka ufafanue kwa nini iwe hivyo.

Usiseme tu kwa kuwa ni serikali haiwezi kufanya biashara, hiyo siyo sababu.

Ndio, kuna aina za biashara/huduma zinazohitaji kupewa ruzuku, lakini si zote.
Serikali uajili kwa vyeti. Sio uwezo nA UBUNIFU. Haina uwezo wa kuongeza tija. Unaweza ukaws mbunifu ukaongeza mapato ya kampuni lkn mshahara unabak vile vile
 
Back
Top Bottom