masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,207
- 13,839
Bado huelewi the spirit of free enterprise na innovativeness of private business.'Masopya...' vuta pumzi, kwa sababu hapa ni serious discussion, na tambua unanijibu mimi, huwa sitaki upuuzi..., mbona hukumbuki?
Hayo mashirika nayajua sana na nimeyapanda sana, na huwezi kuniambia chochote juu yake.
Soma vizuri unielewe: kama ni nyinyi, sijui kama nawe uko kwenye biashara hizo za kutafuta kila mara kuangusha juhudi za serikali, bado hamjampata kiongozi anayeweza kuwakomesha.
Magufuli kama angeacha upuuzi wa kuonea watu wasiostahiri kuonewa, na akashughulika na wahujumu waliopo humo humo serikalini na huko kwenu kwenye sekta binafsi, angeacha heshima kubwa sana katika jamii ya kumkumbuka kwayo.
Sasa hapa nimemzungumzia Magufuli moja kwa moja kukuchokoza kama wewe ni mtu mwenye kumbukumbu, kwa sababu tulishawashiana moto juu yake wewe na mimi na pacha wako 'Jidu' humu humu JF.
Kwa hiyo wewe kuniita mimi kuwa na "...akili za mbuni" inakufanya wewe uwe kama kichaa fulani.
Katika nchi zetu hizi, na hasa kwa Tanzania, baada ya kuona Magufuli aliyofanya, dawa ya kuyafanya hayo mashirika kufanya kazi ipaswavyo ni kuacha kucheka cheka na wapuuzi wanayoyaendesha.
Ikilazimu, baadhi yao ni kufungwa jela maisha na hao wanaohujumu hata kifo ni haki yao.
Ndiyo, nyinyi watu mnatia hasira sana na hivi vimambo vyenu.
Mnashiriki kuyaua mashirika ya wananchi, halafu mnarudi hapo pembeni na kuchekelea..., kuna usaliti zaidi ya huo?
Huu ndio usaliti unaotakiwa kunyongwa na kufilia mbali, kwa maslahi mazima ya taifa, sio kwenda kuhangaika na akina Lissu!
Nimejaribu kila njia ya kujieleza nieleweke, naona sieleweki na wengi hapa. Maslahi ya waTanzania ni kila kitu, hayawezi kuchezewa na mtu yeyote, iwe serikalini au huko kwenye sekta binafsi.
Naomba sana utulie unisome vyema, usinirukie tu kujibu bila kuelewa ninakotokea.
Mnachosha sana.
Serikali kufanya biashara ni sawasawa na paka kukata mawimbi kuogelea pale Feri!
Ni ukweli usiopingika kuwa huwezi kukuta ati “mzalendo” akabidhiwe mabilioni ya wananchi halafu ayachekee bila kuchota kiasi.
Mwisho sisi wenyewe kwa ujinga wetu tunamkabidhi mabilioni halafu tunamwita mhujumu.
Huyo mtu hana uchungu wowote na mtaji au mali ya umma iliyopo pale , wala hajawekeza chochote pale zaidi ya ajira!
Halafu tunategemea afanye wonders!
Hapo ni kutegemea yule paka aogelee toka Feri hadi Kigamboni.
Tatizo mko wengi msiojua principles hizo, na wasiojua kwa kiwango cha lami wanafikiri msomi zaidi hasa mwenye PhD ndio watakuwa enterprising zaidi.
Experience is proving them wrong!
Mwalimu alitengeneza mashirika zaidi ya 400, yalikufa YOOOTE!
Na hilo somo wenye vichwa vigumu hawalielewi.............!