[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD="colspan: 2"]
KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 676, bgcolor: transparent, colspan: 2"]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 187, bgcolor: transparent"]
Uhuru wa mtu
kuamini dini
atakayo Sheria
ya 1984
Na.15 ib.6
Sheria ya 1992
Na.4 ib
[/TD]
[TD="width: 489, bgcolor: transparent"]
19.-(1) Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani
na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu
kubadilisha dini au imani yake.
(2) Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya
Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza
dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na
shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya
shughuli za mamlaka ya nchi.
(3) Kila palipotajwa neno "dini" katika ibara hii ifahamike
kwamba maana yake ni pamoja na madhehebu ya dini, na
maneno mengineyo yanayofanana au kuambatana na neno hilo
nayo yatatafsiriwa kwa maana hiyo.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]