Kama Tanzania ingeshindwa vita ya Kagera: Je, Rwanda na Uganda zingefika hapa zilipofika leo?

Kama Tanzania ingeshindwa vita ya Kagera: Je, Rwanda na Uganda zingefika hapa zilipofika leo?

Usilinganishe kitu kimoja tu. Kwenye bandiko nalisema uzuri TISS wapo macho hivyo ukichanganya na ukubwa wa nchi hali inakuwa nafuu. TISS ya DRC unaijua, kuna serikali inayofanyakazi nchi nzima? Kuna loyality kwa viongozi wa nchi kwa nchi yao au ni mamluki. Kwetu ukubwa wa nchi ni faida kulingana na mazingira yetu.

Hata hivyo DRC ingekuwa kama Rwanda unadhani PK asingekuwa anaitawala yaani angekuwa Mkoloni wa DRC. Ukubwa wake umemfanya PK ashindwe kuitawala wala kuiteka yote

Bazazi
Anhaaaaaa. Sawa mkuu
 
Hii kitu ipo mkuu,kuna dada miaka kama 7 nyuma alikua anajitangaza mrwanda,hadi kwenye profile yake ya facebook aliweka from gisenyi,ninavyokuambia hivi sasa ni diwani simiyu huko,na yuko close sana na baadhi ya waheshimiwa wa CCM, kipindi cha bunge umkosi mitaa ya Dodoma
Mkuu, siwezi kukukatalia kabisa kwasababu mimi ni mwanafunzi mzuri wa historia. Nilichojifunza ni kwamba historia ni sayansi ya mambo ya mbele na siyo mambo ya nyuma: Hivyo katika kusoma kwangu historia mpaka kufika umri huu naamini lolote lile linaweza kutokea kama wanadamu wataamua.

Mwaka 1862 mtu alikuwa akisema nchi ndogo kama Prussia itakuja kutawala Ulaya yote hakuna aliyeamini. Lakini ndani ya miaka tisa tu waliweza kuunganisha mataifa zaidi ya 39 yanayozungumza Kijerumani na kuyapiga kijeshi mataifa yenye nguvu Ulaya kama Ufaransa, Austria na Denmark.

Miaka ya 1897 Theodor Herlz alivyoanzisha harakati za Uzayuni ili kurudi Mashariki ya Kati na kutengeneza taifa la kiyahudi hakuna aliyekuwa anaamini hasahasa ukiangalia nguvu ya dola la Uturuki kwa wakati huo. Wayahudi walikuwa wanakaa na Wapalestina kama ndugu tena kwa amani: Kiufupi walikuwa hawana madhara, lakini kuanzia mwaka 1917, 1919, 1946 na 1948 kuelekea Six Days War na Yom Kippur hakuna Mwarabu aliyeamini yaliyotokea.

Siwezi kukupuuza kabisa mkuu, hasahasa nikiangalia mwenendo wa Tanzania siku hadi siku. Muhimu tu tupate taarifa za ukweli wa yanayoendelea na siyo hadithi za kupikwa.
 
Aisee !!!
Ni hatari pale dini au kabila au jamii moja linapotaka kuwa juu ya makundi au jamii nyingine huku vitu kama rangi, umbo LA pua, imani, kimo, ukubwa wa macho, urefu wa shingo, urefu wa miguu vikiwa vigezo

Yaani Ukiwa mweusi hata uwe Na uwezo kiasi gani kwa brain yako wewe ni sifuri tu mbele ya mjerumani - kisa rangi. Hata uwe Na uwezo kiasi gani lakin kama pua yako ni bapa kama sambusa wew aisee ni sifuri tu mbele ya MTU mwenye pua iliyochongoka kama ya 'mrembo wa kiitaliano'. Teh teh teheee

Kua uyaone

Ni rahisi tu. Unawafanya kama nkurunzinza tu. Network zao zote zitakuwa hazishiki tena
 
Ndugu yangu Malcom Lumumba,

Pamoja na mambo mengine, umetaja yale yaliyotokea baada ya Museveni kuingia madarakani, kisha ukahoji:-
Kwanza, mimi naomba nianze na Museveni mwenyewe!

Je, Museveni alipiga kambi Tanzania ili kuvuta nguvu ya kumuondoa Iddi Amin madarakani au alipiga kambi Tanzania kuvuta nguvu ili hatimae yeye aingie madarakani?

Mwanzoni ilikuwa rahisi sana kuamini pasipo na shaka kwamba alipiga kambi Tanzania ili kuondoa utawala kandamizi wa Iddi Amin! Na kwavile tayari Mwalimu alishakuwa against Amin, kwake Museveni ilikuwa ni rahisi sana kuuzika kwa zana ya kutaka kuuondoa utawala wa Amin!

Tanzania ikaingia vitani na Uganda, huku ikishirikiana na wafuasi wa Obotte pamoja na Museveni! Iddi Amin akang'olewa madarakani, na baada ya hili na lile, hatimae uchaguzi unafanyika Uganda unaomrudisha Obotte madarakani!

Historia inatukumbusha kwamba, muda mfupi baadae Museven anagoma kukubaliana na matokeo ya uchaguzi kwa hoja zile zile ambazo hadi karne ya 21 bado zinaendelea kutamalaki Afrika... kwamba uchaguzi uliomwingiza Obotte madarakani ulijaa udanganyifu!

Kufuatia tuhuma hizo, Museveni akishirikiana na akina Fred Rwigyema bila kumsahau PK hatimae wanaingia msituni kupambana na serikali ya Obotte!

Hapo ndipo ulipo msingi wa swali langu la awali kwamba, Museveni alipiga kambi Tanzania ili kumuondoa Dikteta Iddi Amin au ili aingie madarakani?! Na hapa tukumbuke kwamba, pamoja na Museven kupiga kambi Tanzania, pia alishakuwa na uzoefu wa kivita aliyokuwa anapigana huko Msumbiji!

Kwa maoni yangu, Museven hakupiga kambi Tanzania ili kumuondoa Amin bali alipiga kambi Tanzania ili kuhakikisha anaiongoza Uganda "no matter what!" Madai yake kwamba uchaguzi ulijaa fraud ni bullshit kwa sababu, tangu aingie madarakani hata mwenyewe hajawahi kufanya uchaguzi usio na mizengwe hata kwa chaguzi alizoitisha kwenye karne ya 21!

Ninachotaka kusema ni kwamba, endapo Tanzania ingeshindwa vita ile bado isingekuwa ndo mwisho wa Museven kutaka kuitawala Uganda!

Na kushindwa kwa Tanzania kungetengeneza " a More Aggressive and Notorious Idd Amin!"

Huyu More Aggressive and Notorious Iddi Amin angekuwa more brutal nchini kwake na matokeo yake angetengeneza wimbi jipya la Wakimbizi wa Uganda ambao majority kama ilivyokuwa wale wa awali ambao ni wafuasi wa Obotte, hawa nao wangeingia Tanzania na kujiunga na Waasi chini ya Museven!

Wimbi hili bila shaka lingehusisha na Wanywaranda waliokuwa Uganda ambao nao walipigana bega kwa bega na Museven ili kumuondoa Obotte madarakani!

Kwa kuangalia hilo, it would be a matter of time kabla Museven na wafuasi wake hawajarudi tena Uganda kama ambavyo wafuasi wa Obotte walivyofanya majaribio kadhaa ya kuingia Uganda kumpiga Iddi Amin ili kumrudisha Obotte madarakani... nazungumzia matukio ya kabla ya 1979 Uganda-Tanzania War!

Hata hivyo, kushindwa kwa Tanzania huenda kungefanya Kagera kusipitike tena! Sasa wangepitia wapi?! Tayari hapa tuna Waasi wa Uganda na Waasi wenye asili ya Rwanda!

Pia tusisahau nchini kwetu tulikuwa na "muasi" mwingine anayeenda kwa jina la Laurent Kabila wa Zaire aliyekuwa na lengo la kumng'oa Mabotu madarakani!

Tukiacha upande wa Mashariki na Kaskazini ya Uganda, Uganda pia ingeingilika ama kupitia Tanzania, Rwanda au Zaire!!

Kwa maana nyingine, it's also a matter of time kwa huu "Utatu Mtakatifu" wa Museven, PK na Kabila kabla haujapanga uanzie wapi! Kwamba, walianzishe Rwanda ili wapate " a playing ground" kama ambavyo PK alivyokuwa ameipata Uganda as a playing ground, au waanzie Kivu ambako Kabila alikuwa na ushawishi kama njia ya kuingia Uganda!

Aidha kushindwa kwa Tanzania huenda kungesababisha tu kutoendesha tena "all-out war" dhidi ya Amin lakini huenda kungeanzisha " a Covert Army" ambayo inge-team up na akina Museven dhidi ya Amin!!

Na kama nilivyosema hapo kabla, Waasi Uganda wangeongezeka, Iddi Amin kiburi kingeongezeka, Ushenzi wa Amin kwa raia wa Uganda hususani wale wa kabila la akina Museven na Obotte ungeozeka, na matokeo yake, huenda Amin angekuwa na maadui wengi zaidi ambao ni Waganda kuliko ilivyokuwa kabla ya 1979 Uganda-Tanzania War!

Na kutokana na hayo, sioni ni namna gani Amin angeweza kufika in 1990's kabla hajafurumushwa!

Hapa ninachoona ni kama ile miaka 6 ya Uganda's Bush war iliyomwingiza Museven madarakani dhidi ya wafuasi wa Obotte, ingekuwa ni miaka ya kumuondoa Amin madarakani baada ya Tanzania kushindwa!

Kwa maana nyingine, haya ya sasa ya akina Kagame huenda yangechelewa tu lakini yangetokea!

Swali lako la pili kwamba:-Kwa maoni yangu, YES, wangekuwapo, kwa kuangalia niliyoeleza hapo juu! Na kwamba:-Hapa naomba niwe makini kidogo ili nisihamishe mjadala! Nitaongea kwa uchache sana kwa hofu ile ile ya kuhamisha mjadala... Tanzania hatupo innocent kutokana na Vita vya Uganda!

By 1979 Tanzania ilikuwa LAZIMA iingie vitani dhidi ya Amin lakini ukiangalia matukio tangia kuondolewa Obotte madarakani na Iddi Amin, Tanzania tukaanza kuitengeneza ile vita "in favor of our beloved Obotte"!

Tukam-provoke Kichaa Iddi Amin, nae akaitikia provocation yetu!!

Hivyo basi, hatukuwasaidia, bali ile vita ilikuwa ni ya kwetu wenyewe! Museven nae akatumia fursa kuonesha lengo lake ni kumuondoa Kichaa Iddi Amin kumbe alikuwa anatutumia tu ili aende kuitawala Uganda!!

Mwalimu alishindwa kuliona hili kwa sababu akili yake yote ilikuwa dhidi ya Amin! Na kama alishaliona lakini akasimamia nadharia ya "adui wa adui yako ni rafiki", well and good.
Nakubaliana na wewe kabisa lengo la M7 lilikuwa nikuongoza Uganda na ndio maana sasa hivi kuna kauli kule kuwa "

"wakati tukikuwa tunaoigana msituni mlikuwa wapi?"

Yaani kule kuna watu hawaguswi kabisa ukitaka kuwagusa unakutana na hiyo kauri hapo juu.
 
Huo msemo upo hadi Leo na Mwalimu pamoja na Wazanaki wenzake waliutumia kuwagandamiza wajita kwa kuwanyima huduma muhimu kama shule. Maeneo ya kuzunguka wajita shule zilikuwa chache sana.
Inawezekana Ndio. Wazanaki ni jina walilopewa na Wajita. Ukilitamka kwa sauti ya kikabila za kibantu ina maanisha "Ulikuja na nini". Wajita waliwadharau kwa kuwauliz walikuja na nini zaidi ya mifugo?

Bazazi
 
Ni kweli mkuu & the point to note huu ukanda toka enzi za mwalimu jk ulijengwa ktk misingi ya matabaka ya wahima au nilotics na wabantu ambapo hawa kina mwalimu walitaka kuzitawala Tz , Brndi , Rwnda, Congo ,Ugnda then Kenya na kwa ushahidi tu wa hilo 1.Idd Amin mwalimu hakumpenda kwakua bantu 2.Marais wakibantu toka Burnd & Rwnda walidunguliwa wakitokea Tz na walipandishwa ndge moja ili mpango uende vizuri 3. Rais Kabila 'bantu'wa Congo aliuliwa na kina kagame na m7 sababu zile zile ili waishike nchi NDADAYE wa Burndi alichinjwa mchango wa kagame upo 4. Juzi Nkurunziza aliandaliwa mapinduz kwakua tu ni mhutu walio andaa zoezi likashindwa walikimbilia kwa kagame mpaka leo wamehifadhiwa huko 5. kagame huyo alitaka kumkagame Mh JK Kikwete n.k n.k hivyo kifupi hima empire ni mpango ulikuwepo ila kwa neema ya MWENYEZI tu.
Sasa hapa niweke wazi na Nyerere alikuwa ni sehem mpango wa Hima empire dominance au alikuwa akichezeshwa ngoma asiyoijua?
 
Malcom Lumumba,

Watu hawatengenezi historia, ni historia inayoandaa watu wa kuja kuitengeneza. Hivyo kuna kuwepo na future then mchakato wa kuitengeneza future au kuandaa watu wa kuja kuitengeneza hiyo future huanza.
Kama Uganda angeishinda Tanzania basi huenda British na France zingepigana ili yaliyopo hivi sasa yawe.
 
Hongera Mkuu huu Uzi sikuupitia ,umechambua vzr ila in sehemu nadhani ni namba 4 ,hapo kdg wapanga mipango nadhani walifichana taarifa ya lengo lao
Huyu ni Martin Meredith tena: Anaelezea mambo yalivyotokea kwenye uvamizi wa Congo DRC.

Screenshot_20191209-083836.jpeg
Screenshot_20191209-083846.jpeg
 
With reference mkuu
lini Tz ilikuwa na influence over other African states ?
Hadi kufika miaka ya themanini mwishoni Tanzania ilikuwa na ushawishi mkubwa sana kwa mataifa mengi ya Afrika. Hebu tuangalia machache tu kwenye uwanja wa diplomasia.

Mosi, Tanzania ilileta kitu kinachoitwa Nyerere's Doctrine of State Succession ambacho kilielekeza jinsi gani nchi inaweza kushughulika na mikataba yote ambayo ilisainiwa na wakiloni. Mwalimu Nyerere alisema litakuwa ni jambo la kipuuzi kama mikataba ya Kikoloni iliyosainiwa na Serikali za kikoloni itaendelea kuwa na nguvu hata baada ya Uhuru.

Utaratibu wa kanuni hii ni kwamba ni kwamba nchi ikishapata Uhuru inatoa miaka miwili ya neema kwa nchi ambazo zilisaini mikataba ya kikoloni kuamua kama zinataka kuendelezea hiyo mikataba au kutoendeleza kwa kuandika barua (Exchange of Notes). Miaka miwili ikipita na hakuna kilichofanyika mikataba inakufa.

Sasa mpaka kufika mwaka 1973 nchi sita za Afrika ikiwemo Kenya zilifuata hii kanuni ya Nyerere's Doctrine of State Succession katika kishughulikia mikataba ya kikoloni.

Pili, mwaka 1963 Mwalimu Nyerere ndiye aliyeshauri nchi za Afrika zifuate kanuni inayoitwa The Doctrine of Intangibility of Frontiers ambayo iliseme nchi za Afrika zisibadilishe mipaka iliyochorwa na mkoloni ili kudumisha amani barani Afrika. Hii kanuni iliheshimiwa na nchi nyingi huru za Afrika. Kanuni hii waliiga kutoka nchi za Amerika Kusini, na Nyerere ndiyo aliyependekeza itumike hapa Afrika.

Natumai hizi rejea zimekutosha kwa leo !
 
Hata hivyo DRC ingekuwa kama Rwanda unadhani PK asingekuwa anaitawala yaani angekuwa Mkoloni wa DRC. Ukubwa wake umemfanya PK ashindwe kuitawala wala kuiteka yote

Bazazi
Labda nikumbushe tu Kagame amewahi Iteka Congo nzima wakati wa 1st congo war ya kumng'oa mobutu kutokea ziwa kivu mpaka port matadi!!

Sio hivyo tu alipotaka kumng'oa Kabila aliiteka tena congo na alifika mpaka kinshasa kabisa na kama sio msaada wa Angola basi angekua ameiteka Congo nzima ndani ya wiki 2 pekee.

Kwenye vita za kileo ukubwa wa nchi hauna maana yeyote sababu vita inapiganwa kwa teknolojia nyingi mfano matumizi ya ndege na makombora ya masafa marefu kwahiyo unaweza zingirwa kwenye anga na kumalizwa ndani ya wiki tu kabla hata majeshi ya ardhini hayajafika Dodoma.
 
Back
Top Bottom