Kama tunaaminishwa kuwa Mungu hakosei inakuwaje hakuna kiumbe mkamilifu chini ya jua?

Kama tunaaminishwa kuwa Mungu hakosei inakuwaje hakuna kiumbe mkamilifu chini ya jua?

Kuna mchangiaji mmoja nimeona amejaribu kuweka tofauti vizuri tunapo taka kujadili kuhusu Mungu ni lazima kuwepo na utengano wa uhalisi na kiroho.
Mjadala wa uweza wa Mungu hauwezi pimwa kwa muonekano wa uumbaji wake kwa kuwa kwenye maandikao mengi amekuwa ana kumbusha moja ya sababu ya tofauti ambazo tunaziona ndio ukumbusho wa uwepo wake kwani ana sema hufanya vile anavyo take yeye kama muumba lakini sisi kama waumbwaji tunataraji rehma zake yeye kutimiza ukamilifu wetu.

Nikirejea kwenye hoja naona mtoa hoja amerejea maneno ya Mungu kama uubwaji wetu sisi ni kwa mfano wake yeye
"tufanye maneno hayo kuwa ni sahihi je ni kweli kitu ambacho kipo wa mfano wa kitu kingine ni lazima kuwa na ubora sawa na kinacho pigiwa mfano? Nijuavyo kwenye lugha yetu ya kiswahili neno mfano lipo wazi sana na kushabihisha kitu kimoja na kingine bila kujali ubora wake ulivyo
Mfano. Mbio zake ni mfano wa duma but sentensi hiyo haiwezi kutupa uhalisia wa kitu husika kuwa ni kweli kina ubora wa mbio za duma
 
Ni kweli hakuna binadamau aliyekamilika kwani kila binadamu (hata awe mzuri au/na akili kiasi gani) mara zote hujiona hajakamilika. Naunga mkono hoja 100%.
 
Ukisoma vizuri sifa za Mungu wakati alipo muumba Adam utaona kwanini Adam alichaguliwa kuwa kiongozi wa dunia kwa kuwa baada ya Adam kuumbwa Mungu alimrudhuku Adam kwa kumpatia akili pamoja na yakini.

Sasa akili ndio hii ambayo inatupa utashi wa maamuzi kwenye matendo yetu ya kila siku kwenye maisha tukiwa hai.

Lakini yakini hii ndio inayo tupa nafasi ya kuhoji na kubainisha uwezo wa Mungu kutokana na kuwa na nafasi ya kujiuliza na kupata majibu yale ambayo haya hitaji hesabu au elimu ya shule
ndio maana linapo kuja swala la imani siyo lazima kujua kusoma na kuandika ili kuweza kuamini kwani jambo muhimu hata kwa mtu mjinga ni kuwa na yakini ndio inampa uwezo wa kujiuliza nini asili yake na kwanini yeye? na mengine ya kiimani
 
Mkuu ivi Mungu anaitaji asihojike ndo awe Mungu yani watu msijiulize ndo anakuwa Mungu kwa iyo Mungu akihojika uyo si Mungu aseeeh very interested story

Kwamba Mungu anaitaji asihojike asifikiriwe asiulizwe ndo anakuwa Mungu and vice versa is true
Ongea na Mungu kwenye sala na maombi yako.
Unapata wapi uwezo wa kumhoji Mungu?.. tena kuhusu nini?
 
Suala la Mungu ni la kiimani.Ama uchague kuamini uwepo wake ama uchague kuamini vitu unavyopenda wewe.

Ukianza kuhoji masuala ya Mungu utaishia kuchanganyikiwa kama Kiranga.Mungu alikuwepo kabla yako na ata ukifa ataendelea kuwepo.
Amina
 
When did sin came on earth
Satan started it through its rebellion, And through Adam and Eve sin entered the world. We all know where and how sin started, we don know when it started. We no longer perfect creatures EVER SINCE.
 
Majibu yake ni mafupi sana...

Mwenyezi Mungu hakosi,hajakosea na hua hakosei.... ina maana kwamba chochote unachokiona ndani au nje ya uso wa dunia kipo kwa sababu na kimetengenezwa kwa makusudi wala siyo bahati mbaya, na ndiyo unavyokiona ndivyo kinavyotakiwa kiwe au kuonekana...



Hakuna Binadamu aliyekamilika chino ya jua, mwezi au Dunia... maana yake ni kwamba vile ulivyo ndivyo unavyotakiwa uwe au kuonekana ila lolote linaweza kukutokea na either ukabadilika au kubadilishwa na kua tofauti na ulivyozoeleka kuonekana au kua...


Cc: mahondaw
 
Kana kumbuka "God has no religion" the issue is to believe on its existence only.

Sio biblia tu hata ukisoma Quran au Shinto holy book zina mianya mingi wanayoitumia akina kiranga kugaragazia watu.

Be God centred-person and not religious oriented.

The truth is God exist.
Hivi kwanini wakristo wengi wamekuwa wakitenganisha dini na Mungu,yani wanaona dini haina msaada wowote na husema Mungu hana dini?
 
Binadamu wote waliumbwa wakamilifu kwa mtazamo wa aliyewaumba.kwani alipomaliza kuwaumba aliwapumuzia pumzi yake,akastep aside akaridhika kisha akaenda kupumzika kwa kazi alitoifanya.
Sema tu ibilisi ni mharibifu dhidi ya uumbaji huo kwa wale wanaomruhusu awatawale,pia kwa wenye mashaka na ukamilifu wa uumbaji wake mwenyeenzi Mungu.
 
Kiimani na hata mahala pengi tu utawasikia Watu wakisema kwamba Mwenyezi Mungu hakosei, hajakosea na kwamba huwa hakosei na wengi wetu ama Kiuwoga au ' Kimbumbumbu ' tu au kwa kuwa wa ' hovyo hovyo ' katika Kufikiri tayari tumeshaaminishwa hivyo.

Sawa kama kweli Mungu hakosei sasa inakuwaje kila mara huwa tunaisikia hii Kauli ambayo nainukuu hapa " Hakuna Binadamu aliyekamilika chini ya Jua, Mwezi au Dunia hii ". Je hapa tushike lipi au tuelewe lipi?

Na kama Wote tunakiri kwamba Mwenyezi Mungu hakosei katika ' Uumbaji ' wake na Sisi Wanadamu ni mfano wake tosha iweje tena leo tunasema hadi kwa msisitizo kabisa kwamba Binadamu wote hatujakamilika?

Tujadili na Karibuni katika huu ' mjadala ' ambao nawahitaji tu wale ambao wamebarikiwa Critical Thinkig na Logical Reasing ya kutosha wachangie na nimetahadharisha mapema tu katika ' Headline ' kama unajijua au kujihisi huna huo uwezo tafadhali tusichoshane na pita zako tu mia.

Nawasilisha.
Ngoja nikavute ikikolea kichwani nitarudi na kuuchangia Uzi huu
 
Mungu ametuumba kwa ukamilifu mkuu wa kimaumbile mapungufu ya mwanadamu yanatokana na ubinadamu wake.

Mungu ametupa hekima kuu kupita viumbe vyote, mwanadamu ajua jema na baya pasipo kufunzwa, ila yeye hutenda maovu kwa kiburi na jeuri ilhali akijua matokeo yake yalivyo.

Mkamilifu ni Mungu pekee kwa maana yeye hutenda kwa haki na kwa upendo mkuu jambo ambalo mwanadamu haliwezi, nalo ndilo lampunguzia ukamilifu mwanadamu aliye kiumbe cha Mungu.

Kutokukamilika kwa mwanadamu kunadhihirika kupitia maovu anayotenda na si kwa maumbile. Tunaposema binadamu hajakamilika tunazungumzia mapungufu kupitia matendo yake na si vinginevyo.
 
" Hakuna Binadamu aliyekamilika chini ya Jua, Mwezi au Dunia hii ".

We kiswahili sio lugha mama kwako I guess,..teh teh teh!!!
 
Unataka kum challenge Mungu? unashindwa kuli challenge jiwe linavyoboronga na kufukarisha watu unakuja mbio kum challenge Mungu?
Ok, sasa umeshapata mwongozo wa kujua hakuna Binadamu aliyekamilika, je unakubali kwamba MUNGU hakosei?
 
Mungu ametuumba kwa ukamilifu mkuu wa kimaumbile mapungufu ya mwanadamu yanatokana na ubinadamu wake.

Mungu ametupa hekima kuu kupita viumbe vyote, mwanadamu ajua jema na baya pasipo kufunzwa, ila yeye hutenda maovu kwa kiburi na jeuri ilhali akijua matokeo yake yalivyo.

Mkamilifu ni Mungu pekee kwa maana yeye hutenda kwa haki na kwa upendo mkuu jambo ambalo mwanadamu haliwezi, nalo ndilo lampunguzia ukamilifu mwanadamu aliye kiumbe cha Mungu.

Kutokukamilika kwa mwanadamu kunadhihirika kupitia maovu anayotenda na si kwa maumbile. Tunaposema binadamu hajakamilika tunazungumzia mapungufu kupitia matendo yake na si vinginevyo.
Naona wewe umechangia ki critical thinker
 
"Mwenyezi Mungu hakosei " ni kauli tu ya kiutukuzaji basi. They are just words na hayana impact yeyote kwetu na tumekuwa tukiaminishwa hivyo hivyo miaka nenda miaka rudi. Sisi binadamu ni lazima tufanye makosa maana makosa yameumbwa ndani yetu, ni sawa kama vile mbwa anvyobweka au jogoo anavyowika. Huwezi kumzuia mbwa kubweka, tunatakiwa tu tujikubali na hali yetu kuwa tutafanya makosa popote any time
 
mfano hakiwezi kuwa sawa sawa na kitu hasilia in hivyo tu
 
Back
Top Bottom