Kama umewahi kutumia hivi vitu, wewe ni legend

Kama umewahi kutumia hivi vitu, wewe ni legend

Vyombo vya usafiri

1. DCM (Japo siku hizi bado chache zipo)
2. Mabasi ya Leyland
3. Chai maharage hii mnakaa mnatazamana Kama mnacheza draft
4. Peugeot
5. Datsun N.k
Nb: zilikua ndio luxury pindi hizo, nyingine ongeza.

Vyakula
1. Sambusa za ubwabwa ( shuleni)
2. Kachori za chachandu ya machicha ya Nazi
3. Koni za kwenye vikopo vya bati
Nyingine mtaongeza wadau.

Vinywaji
1. Juice ya kutengenezwa kutokana na unga wa kwenye vipakti, siku hz zipo jusi cola lakini hz zilikua noma pakti moja inatolewa ndoo mbili au tatu afu zinawekwa barafu...kumbuka hyo ni sikukuu wakubwa wanapiga soda watoto mnaishi na hzo ndude af mna enjoy sana.
2. Kuna soda flani ilikua ya njano inatengenezwa na kampuni ya coca nadhani jina nimeisahau
3. Chai ya chai jaba Nk.

Mavazi and accessories
1. Suruali za kodrai zikipigwa jua zinawakawaka Kama gold ya geita, sikuuu mnaeza jikuta mtaa mzima mmevaa Aina moja.
2. Magauni ya spesheli.
3. Njumu flani za mpira Kuna wajomba wameenda nazo Hadi shule zipo kama raba flani
4. Mifuko ya sports
5. Viroba vya unga kufanywa mfuko wa kubebea daftari

N.k
Matusi na matukano hasa ya wazazi
1. Nyau kasoro mkia ww
2. Nyambafu
3. Macho kumchuzi ww
4. Shenzi type

Ongezeeni na ya kwenu maana nimekumbuka nimecheka sana
Ngoja wahenga waje walete mrejesho mjarabu
 
Vyombo vya usafiri

1. DCM (Japo siku hizi bado chache zipo)
2. Mabasi ya Leyland
3. Chai maharage hii mnakaa mnatazamana Kama mnacheza draft
4. Peugeot
5. Datsun N.k
Nb: zilikua ndio luxury pindi hizo, nyingine ongeza.

Vyakula
1. Sambusa za ubwabwa ( shuleni)
2. Kachori za chachandu ya machicha ya Nazi
3. Koni za kwenye vikopo vya bati
Nyingine mtaongeza wadau.

Vinywaji
1. Juice ya kutengenezwa kutokana na unga wa kwenye vipakti, siku hz zipo jusi cola lakini hz zilikua noma pakti moja inatolewa ndoo mbili au tatu afu zinawekwa barafu...kumbuka hyo ni sikukuu wakubwa wanapiga soda watoto mnaishi na hzo ndude af mna enjoy sana.
2. Kuna soda flani ilikua ya njano inatengenezwa na kampuni ya coca nadhani jina nimeisahau
3. Chai ya chai jaba Nk.

Mavazi and accessories
1. Suruali za kodrai zikipigwa jua zinawakawaka Kama gold ya geita, sikuuu mnaeza jikuta mtaa mzima mmevaa Aina moja.
2. Magauni ya spesheli.
3. Njumu flani za mpira Kuna wajomba wameenda nazo Hadi shule zipo kama raba flani
4. Mifuko ya sports
5. Viroba vya unga kufanywa mfuko wa kubebea daftari

N.k
Matusi na matukano hasa ya wazazi
1. Nyau kasoro mkia ww
2. Nyambafu
3. Macho kumchuzi ww
4. Shenzi type

Ongezeeni na ya kwenu maana nimekumbuka nimecheka sana
Na tulio vaa chcchcchc tunaitwaje?
 
Kama uliwahi kutumia stendi ya mabasi ya kwenda mikoani ilipokuwa MNAZI MMOJA hapa Dar yatosha kusema wewe ni LEGEND pia
 
😁😁 FANTASTIC!
unnamed (2).jpg
 
Mkuu umezisahau Chacha Cha tena tulikua tunachagua rangi ya kijani...hiyo Peugeot 505 ndio gari ndogo niliyopata Control nayo sana maana nilijifunzia kuendesha Isuzu injection ilikua tunapaki kwenye ka mlima kwa sababu ya kustua...
 
Kama umewahi kusoma gazeti liitwalo Mfanyakazi basi inabidi uwe kwako!

Kama uliwahi kuwaona O-level students wa Tambaza hama kwenu haraka.

Kama Uliwahi kusikia shule ya sekondari Forodhani hupaswi kuendelea kumtegemea babako.

Kama uliwahi kunywa juice ya sun vita basi wewe mkongwe.

Kama uliwahi kuhadithiwa kuwa Nyerere aliwahi kupigwa mtama na bodyguard wake basi unapaswa uwe na wajukuu...
Dah hii ya nyerere kupigwa mtama tulikua tunajazwa sana upepo
 
Nawaza tu Peni za Bic au Speedo zipo kweli?

Zile juice za Samvita za pakti mnazikumbuka?

Dawa za meno Aha? juzi kati hapo walikuwa wanauza mpaka 50 wale waliweza
Maji ya pakti ya bakhresa
 
Nilisahau Mkuu halafu hapo kwenye Isuzu journey hiyo ilikua new model baada ya ile yenye tairi za mbele zimeingia ndani utasema inadondoka pale mbele ikatapo kona
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] hiyo unayosema nishaijua
Hata mm nilikuwa naziogopa kupanda kwenye kona nahisi ni kama zigapindukq
Km wewe legend wa kkoo hiyo ISUZU ilipaki ilikuwa pale mtaa TANDAMTI karibu na msikiti wa idrisa pembezoni mwa OFISI YA STAR TIME miaka ya 2013 lilikuwa bovu lilikaa pale karibu miaka 3 au miwili hivi
Sema zile hazikuwa JOURNEY
zile nhisi zilikuwa modified kama unavyoona hizi TX hapa BODI ya kuchonga
images%20(59).jpg
 
Kuna Land Rover zilikua hazina automatic ignition zinaingizwa chuma kama bpedal ya baiskeli kwenye fan ya rejeta inazungusha kwa nguvu ndio ziwake ...ukiwa mzembe zinaeza vunja mkono... Kama kick ya Honda 110 ilikua na tabia hiyo nayo
Hizo LONDO za kupiga ENDEL km Jafongo za mchina toleo la kwanza
 
Kama umewahi kusoma gazeti liitwalo Mfanyakazi basi inabidi uwe kwako!

Kama uliwahi kuwaona O-level students wa Tambaza hama kwenu haraka.

Kama Uliwahi kusikia shule ya sekondari Forodhani hupaswi kuendelea kumtegemea babako.

Kama uliwahi kunywa juice ya sun vita basi wewe mkongwe.

Kama uliwahi kuhadithiwa kuwa Nyerere aliwahi kupigwa mtama na bodyguard wake basi unapaswa uwe na wajukuu...
Kwenye kuchagua shule primary Mtihani starndard 7
Edhi hizo masomo matatu MAARIFA YA JAMII LUGHA na HESABU
Unachagua shule tatu uzipendazo
Forodhani chaguo la kwanza
Kibasira chaguo la pili
Kambangwa kipindi hicho ndo inaanza nikaiweka ya tatu

Asikwambie mtu edhi zetu DAR ES SALAAM nzima shure za SECONDARY ZA hazikuzidi 8
Na wanafunzi tulikuwa wengi balaa
kama kuna mtu humu kasoma JAMUHURI ya edhi hizo nakusalimu sana LEGEND mana ilikuwa shule ya MALEGEND wanasona lkn hawana uhakika kama watafanya paper ya TAIFA ya FORM 4 malegend wa edhi hizo watanielewa

Forodhani ni shule waliosoma BRO zangu nikawa naipenda sana hiyo SHULE
 
Kama ushawahi kula askirim (ice cream) za vijiti uwe una watoto watatu na zaidi

Kama unajua maana ya peremende uwe na wajukuu wawili

Kwa miaka ya 2000 kama ulivaa viatu vya alichoki hakikisha unatakiw uwe na na watoto wawili

Kama ulishawahi kunywa soda inaitwa Fahari unatakiwa uwe na wajukuu sasa

Kama ulishiriki uchaguzi wa kwanza wa Demokrasia jiandae kufa tu ushakula chumvi nyingi hii awamu ya sita na mnakuwa wajuaji sana humu ndani.
Hahahaaa nipo hapo kwenye kuvaa viatu vya Alichoki umenikumbusha mbali sana [emoji23][emoji23][emoji23]. Inshallah mtoto wa pili anakuja soon
Peni ya speedo ndio peni yangu pendwa ilikuwa unanifanya naandika mwandiko mzuri sana .
View attachment 2519123
 
Kama ushawahi kula askirim (ice cream) za vijiti uwe una watoto watatu na zaidi

Kama unajua maana ya peremende uwe na wajukuu wawili

Kwa miaka ya 2000 kama ulivaa viatu vya alichoki hakikisha unatakiw uwe na na watoto wawili

Kama ulishawahi kunywa soda inaitwa Fahari unatakiwa uwe na wajukuu sasa

Kama ulishiriki uchaguzi wa kwanza wa Demokrasia jiandae kufa tu ushakula chumvi nyingi hii awamu ya sita na mnakuwa wajuaji sana humu ndani.
Sikiza LEGEND
kama uliwekewa CHIPSI na tomato ya kwenye CHUPA ya kioo na ukashushia na hii juisi nakusalimu LEGEND
FB_IMG_1667561575929.jpg
 
Back
Top Bottom