Kama una mpango wa kuja South, zingatia mambo haya sita kabla ya kuanza safari yako

kumbe wa south sio wajanja sasa hiyo ni upuuzi kwanini wasiajili mtu yani vitu vyengine vimekaa kifala sana!
 
Usela mavi, duh hatari sana..
 
Aisee , Ile nchi imeharibiwa na ANC na Sera zao za uhamiaji holela .
Criminals wakaanza kukimbilia huko.
South ilikuwa nchi nzuri sana , mimi nina Bro wangu alikuwa huko tangia mwaka 2003 , mwaka 2020 akarudi Bongo na hajarudi huko mpaka leo .
Anasema pia nchi ile imeharibika kabisa ,crimes everywhere , Yaani kuna mahayawani hayaoni kuua kwa kitu kidogo tu .
 
Noma sana aisee
 
kumbe wa south sio wajanja sasa hiyo ni upuuzi kwanini wasiajili mtu yani vitu vyengine vimekaa kifala sana!
Swala la kuajiri mtu ili amlipe, hilo ndo hawataki kulisikia. Kunakuwa na wapiga debe kwenye kituo kikuu cha daladala. Hao ndo wanaita watu kariakoo kariakoo, au ubungo ubungo. Abiria mkishaingia na kuanza safari, yule mpiga debe anabaki kujaza daladala lingine.

Sasa pale dereva anakuwa ashajua idadi ya abiria kupitia viti vyake. Hivyo anajua ni kiasi gani cha hela ambacho atapata kupitia nauli yake. Mfano nauli ni sh100 hivyo kila siti mkikaa watano ni 500. Na kama gari zima lina siti 15 atapata 1500.

Hakunaga cha watu kusimama na kubanana kama bongo, hivyo ni lazima ajue udadi yenu tu, na kiasi cha fedha atachopata. Ni vigumu sana mtu akose kulipa maana mnachangishana wenyewe kila siti halaf mnazipeleka kwa jamaa aliekaa siti ya mbele ya dereva. Nae anazihesabu, kama kuna mtu au watu wametoa hela kubwa anawarudishia chenji zao, zinazibaki anamkabidhi dereva ambae nae anazihesabu akiona zimetimia anazichimbia chimbo lake. Na zisipotimia kimbembe kwako mpokeaji na muhesabuji.
 
 
Na dunia iliyoendelea Ulaya na marekani hakuna conductor mkusanya hela ni unalipia kwenye mlango kwa driver kwa kadi au cash japo wengi ni kwa card tena unakuta ni ya mwezi mzima (kama kwenye train au hizo bus za town ) hii ya konda na abiria ni huku kwetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…