Kama una mpango wa kuja South, zingatia mambo haya sita kabla ya kuanza safari yako

Kama una mpango wa kuja South, zingatia mambo haya sita kabla ya kuanza safari yako

Ulimshauri vizuri mi mchana kabisa colored walinizunguka kama watatu kibindoni Nina almost ten thousand rand na mfuko wa kawaida twenty rand
Dah nilishtuka ila nikawaza fasta nikawatolea Ile twenty wakaondoka
Kule kupigana telo mchana kawaida
Na hii huwa wanaangalia mwonekano wa mhusika. Wakinusa una hela na wanona utaleta utata, bakubeka ku-radar bese uyabulawa.
 
Binafsi huwa nina uwezo wa kusoma mawazo ya mtu na kumuelewa.
Nilichomuelewa jamaa alivyosema foreigner hawezi pata kazi alimaanisha kazi rasmi sio hizi za day work. Nikisema rasmi namaanisha kazi uliyosomea.

Ulichokielezea ni sahihi, ndio ukweli ulivyo. Kazi ngumu ni za fani yako ila za kawaida tu zinapatikana coz wa SA ni wavivu na wanazikimbia.
Ni kweli nimekuelewa mkuu.
 
Anatoboa tena vizuri sana si Bora huyu hata anaweza kuweka sentence ikaeleweka Kuna wengi wanajua thank you na sorry na baada ya mda Wana master na maisha yanaendelea
SA kwa kingereza mtaani wana pidgin Yao ukiwa mwepesi ndani ya miezi 3 hakuna shida
English ni lugha rahisi kuijua. Mimi kiukweli hizi lugha za kiafrika zimenishinda kabisa kuziweza... kibemba, Nyanja na Lingala nimeanza kujifunza muda ila kuongea kiusahihi bado sana.
 
Mkuu kwani kwa kiswahili chako neno kazi linamaana gani?
Unaposema South Africa hakuna kazi kwa foreigners huku ukikiri tena mwenyewe kuwa wazimbabwe (ambao ni foreigners) wana kazi za hovyo unamaanisha nini?

Je kama hizo kazi wanazofanya wazimbabwe zingekuwa za hovyo kama unavyojaribu kuaminisha watu, unafikiri wazawa wangeingia barabarani kuanzisha fujo na kudai kuwa wageni hasa wazimbabwe wanachukua kazi zao? Kuna vitu ambavyo ndugu zangu wabongo wengi hawavifahamu kuhusu hii country na mmoja wao ni wewe.

Let me tell you something that you don't know about it. Mwaka 2009 hadi 2015, nilikuwa nafanya kazi katika restaurant moja maarufu hapa SA inaitwa Spur, ipo ndani ya RandPark Ridge mbele ya Cresta jijini Johannesburg. Yani 98% ya wafanya kazi wa pale walikuwa wazimbabwe, huku mbongo nikiwa peke yangu na wazawa wa3. Waiters tulikuwa tunakunja R6500 ya kipindi kile kila mwezi, na keep change ambayo tulikuwa tunaachiwa na wazungu ndo ilikuwa kufuru. Mtu ulikuwa unaondoka na R400 au 500 kila siku, na weekends unaondoka mpaka na R800.

Wazimbabwe wengi walijenga kwao, walinunua mifugo, magari nk. Hata mimi pale ndo nilipopatia akili ya kununua kiwanja changu cha kwanza bongo na kuanza kujenga nyumba yangu ya kwanza. Mwaka 2015, nikarudi bongo kuweka mambo sawa, ila nilichelewa kurudi hivyo nafasi yangu kuchukuliwa na mtu mungine.

Sasa unaweza kuangalia mwenyewe kima cha mshahara wa R6500 plus R300 au 400 ya kila siku, kama una akili ya kuweka ukizijumlisha kwa mwezi unakuwa na bei gani? Ni Wa South wangapi ambao wanaweza kupata kima hicho cha pesa kila mwisho wa mwezi. Kuna msemo wa kiswahili unaosema kuwa usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Hizi kazi watu wengi au naweza kusema wote kutoka East Africa hawazijui ndo maana wewe unaita eti kazi za hovyo. Maana hata mimi nilitafutiwa kazi hiyo na demu wangu wa kishona (mzimbabwe) ambae alikuwa ni manager pale Spur.

Hiyo ni moja kati ya kazi nyingi zinazowapa maisha wazimbabwe. Na sasa wamegeukia kwenye Uber, Bolt nk, huku wabongo tukiendelea kusimama kwenye kona za barabara kuuza vikete viwili vitatu vya bangi na hapo hapo wazee wapite uwaungie na kubaki na ela ya kula. Maisha hayo mtu utaishi mpaka lini?
Temana na huyo jomba huwa ana ubishi wa kipuuzi sana.
 
Hahahahaaaaa sitakagi hata kukumbuka tulienda training na washikaji weekend tukaenda club sizaa wakati wa kurudi tuko wa tatu akapita jamaa mmoja ita kunjan atukujibu kilichofwata n kukutana hotelin. Mmmoja wakatokea 4 mbele nkahisi wako wapita njia kumbe walewale walitufokooaa sinahamuuh yaan


2.kule usitembeee nanpesà nyingi kama una sehemu ya kuhifadhi

Hifadhi hukoo

3 jifunze kutoa sadaka nono ukiwa nje ya nchi yaan kule...njenjee...

Mmoja wetu aligoma kutoa ushirikiano aisee walimpiga walimchapa badae nkamwambia ndugu wakikuuzunguka toa ushirikiano wale wakiona unazingua wanakuwaga na ma bonba[bastola] mfukoni ikitoka hairudi bure
Watu wengi huuwawa kwa sababu ya kugoma kutoa ushirikiano. Juzikati kuna mpopo fulani alikuwa anatoka kwake nafikiri kuelekea katika mizunguko yake.

Sasa ile anafungua gate atoke jamaa watatu wakamsogelea vizuri tu na kumuomba sim ili waondoke. Mpopo alipoona anaombwa sim akaleta mgomo. Jamaa wakataka watumie nguvu kuichukua. Yule mpopo kwa vile tayari alikuwa ashafunga gate, basi akairusha ile sim kwa ndani ili jamaa wasipate kitu.

Aisee kitendo kile walikichukulia kama dharau, wawili kati yao wakatoa bastola kila mmoja ya kwake. Basi wakawa wanapokezana. Mmoja kapiga ya paja, mungine akapiga kichwani, mungine tena kifuani, mungine akamalizia tumboni na kusepa zao kusikojulikana.
 
Kinyanja cha Zambia
Ok.. Sasa ulipoandika njanya nikaona bora nikuulize kama ulikuwa unamaanisha nyanja ya Zambia au ni lugha nyingine ya kiafrika.

Ila ukijua kuongea kichewa cha Malawi, basi asilimia kubwa ya maneno ya kinyanja utayajua na kuyasikia. Kichewa na kinyanja ni kama kiswahili cha Zanzibar na cha bara. Au cha Kenya na Tanzania.
 
Binafsi huwa nina uwezo wa kusoma mawazo ya mtu na kumuelewa.
Nilichomuelewa jamaa alivyosema foreigner hawezi pata kazi alimaanisha kazi rasmi sio hizi za day work. Nikisema rasmi namaanisha kazi uliyosomea.

Ulichokielezea ni sahihi, ndio ukweli ulivyo. Kazi ngumu ni za fani yako ila za kawaida tu zinapatikana coz wa SA ni wavivu na wanazikimbia.
Mungu mwema nilifika cape saa kumi jioni kesho saa Moja asubuhi nikaanza kazi JM mall customer assistant na kiingereza sijui wazungu walikuwa wanarudia nachowaambia mf go zea ' utasikia aah go zea !? In turn ikawa ndio lucky point kwangu ikawa kama nembo yangu
 
Watu wengi huuwawa kwa sababu ya kugoma kutoa ushirikiano. Juzikati kuna mpopo fulani alikuwa anatoka kwake nafikiri kuelekea katika mizunguko yake.

Sasa ile anafungua gate atoke jamaa watatu wakamsogelea vizuri tu na kumuomba sim ili waondoke. Mpopo alipoona anaombwa sim akaleta mgomo. Jamaa wakataka watumie nguvu kuichukua. Yule mpopo kwa vile tayari alikuwa ashafunga gate, basi akairusha ile sim kwa ndani ili jamaa wasipate kitu.

Aisee kitendo kile walikichukulia kama dharau, wawili kati yao wakatoa bastola kila mmoja ya kwake. Basi wakawa wanapokezana. Mmoja kapiga ya paja, mungine akapiga kichwani, mungine tena kifuani, mungine akamalizia tumboni na kusepa zao kusikojulikana.
Mkuuu m ushirikiano muhimuu sana kwangu hasa usikuuu asinivuee nguo tu
 
Mungu mwema nilifika cape saa kumi jioni kesho saa Moja asubuhi nikaanza kazi JM mall customer assistant na kiingereza sijui wazungu walikuwa wanarudia nachowaambia mf go zea ' utasikia aah go zea !? In turn ikawa ndio lucky point kwangu ikawa kama nembo yangu
Itakuwa ulikuwa na host.
Kuna ile hata wa kukupokea huna.
 
Ok.. Sasa ulipoandika njanya nikaona bora nikuulize kama ulikuwa unamaanisha nyanja ya Zambia au ni lugha nyingine ya kiafrika.

Ila ukijua kuongea kichewa cha Malawi, basi asilimia kubwa ya maneno ya kinyanja utayajua na kuyasikia. Kichewa na kinyanja ni kama kiswahili cha Zanzibar na cha bara. Au cha Kenya na Tanzania.
Kuzishika hizo lugha lazima uwe hujui kiingereza wala kiswahili. Waburundi ndo huwa ni ma-master wa kujua lugha za watu. Wenyewe wanasema french ni lugha ya kimaskini.
 
Back
Top Bottom