Kama una mpango wa kuoa, jifunze hapa

Kama una mpango wa kuoa, jifunze hapa

Dawa yenu ni wanawake kukataa kuzaa kabla ya ndoa, anayetaka watoto aoe simple tu, hili nalo tutalianzishia kampeni soon "mwanamke kamwe usikubali kuzaa kabla ya ndoa"
Labda huwafamu vizuri wanawake wa kibongo eti wakatae kuzaa hawana hiyo jeuri
 
Subirini tu wakiona hawaolewi na wanazidi kutukanwa na kuitwa single mothers akili zitajireset zenyewe na kujua hapa kinatakiwa nini

Na mwanamke anayekubali kuzaa kabla ya ndoa ni mpumbavu hivyo nashangaa mwanaume anakosaje utu kiasi cha kutaka watoto wake wazaliwe na mama mpumbavu

Anyway tutafika tu
Daa!!! hivi kumbe kuitwa single mother ni tusi?
 
Mkuu kama mwanaume unajifanya mbabe, msaliti, mnyanyasaji au eti unarudi nyumbani muda unaotaka na mwanamke anyamaze avumilie tu, na upumbavu mwingine kama huo, eti kisa tu wewe ndio kichwa cha familia (na wanaume wengi ndio mnataka hivi), tegemea tu lazima atavumilia kwa muda ila atakapopata nafasi ya kuondoka kwenye hiyo ndoa lazima ataondoka tu, hakuna binadamu anaweza kuvumilia hayo mnayoita "kumheshimu mume" bila sababu tena kwa maisha yake yote


Hakuna upumbavu ambao sitakuja kufanya kama kurudi mapema nyumbani.

Kuanzia baba mzazi, kaka zangu na wanaume wote wa mazingira niliyokulia sikuwahi kuona wanarudia mapema kisa shinikizo la mwanamke.

Mwanaume anarudi nyumbani pale anapoona ni muda mwafaka kwake kurudi nyumbani.

Kwangu halafu nipangiwe muda wa kurudi??? PUMBAVUUU!!!
 
Kwa umri wangu huu (nimekula chumvi kiasi) nimeona na kujifunza mengi kuhusu mahusiano ya kimapenzi na ndoa. Nimeshuhudia vijana wengi waliokimbilia maisha ya ndoa wakipoteza muelekeo wa maisha muda mfupi tu baada ya kuianza hiyo safari ya ndoa!

Kutokana na mikasa na vitimbwi vya wanandoa wengi nilijipa muda wa kufanya utafiti mdogo usio rasmi kuhusu maisha ya ndoa na mwisho wa siku nikaibuka na majibu haya;-

1. Ndoa ni gereza la kiroho, kimwili na kiuchumi kwa mwanaume (ndomana inaitwa pingu za maisha)

2. Ndoa ni mtego wa wanawake kuwatawala wanaume.

3. Ndoa ni chanzo cha magonjwa mengi kwa wanandoa hasa wanaume yanayopelekea vifo vyao (tuna mifano mingi ya wanaume waliopoteza maisha au kupata magonjwa mazito muda mfupi baada ya kuoa)

Kutokana na utafiti wangu huo usio rasmi nimeona niwashauri vijana wenzangu na wanaume kwa ujumla, Hakuna maisha ya furaha na amani ndani ya ndoa kama mnavyohubiriwa.

Ukitaka furaha tafuta pesa ujipe furaha mwenyewe (ukiwa na pesa utapata kila utakacho ikiwa ni pamoja na huduma zipatikanazo ndani ya ndoa)

Achaneni na upuuzi wa ndoa, yaani umtolee mahari, umtunze, uwatunze watoto, umlinde asikusaliti, umridhishe kitandani na bado mkiachana abebe mali zako?

Wabobevu mniambie ndoa ina faida gani kwa mwanaume? Je ni ngono tu au kuna kipi special?

#KATAANDOA
Kipindi taasisi hii ya ndoa inaheshimika tulikuwa tukishuhudia watoto katika familia wakiwazika wazazi wao katika uzee wao kwa kiwango cha asilimia 98 wazee na asilimia 2 vijana.
Sasa hivi baada ya taasisi hi hii ya ndoa kuchukuliwa poa na vijana kutafuta raha ya ndoa kwa kurukaruka kwa kila msichana ajipitishae mambo yamegeuka.
Sasa wazazi( wazee katika ndoa) ndio wanawazika vijana wao kwa asilimia 90vijana na asilimia 10wazee.
Ndoa ni uzio unaokinga na kulinda familia kiakili, kiafya na kiroho.
Huna ndoa halafu ni kitombi, ukitoboa 55 yrs katoe sadaka ya kushukuru.
 
Mkuu kama mwanaume unajifanya mbabe, msaliti, mnyanyasaji au eti unarudi nyumbani muda unaotaka na mwanamke anyamaze avumilie tu, na upumbavu mwingine kama huo, eti kisa tu wewe ndio kichwa cha familia (na wanaume wengi ndio mnataka hivi), tegemea tu lazima atavumilia kwa muda ila atakapopata nafasi ya kuondoka kwenye hiyo ndoa lazima ataondoka tu, hakuna binadamu anaweza kuvumilia hayo mnayoita "kumheshimu mume" bila sababu tena kwa maisha yake yote

Mkuu kama babako alikuwa anashinikizwa kurudi nyumbani mapema, na akichelwa anagombezwa basi babako alikuwa/ni zwazwa.

Yaani mwanaume unarudi nyumbani mapema muda mke ndo yuko anapika Ili iweje? Mke aanze kukutuma "niletee hilo sahani. Nisogezee hiyo ndoo"

Huo si ni utahira
 
Mzee wangu naye alikuwa kama wewe hivyo hivyo, bahati nzuri hakuna aliyewahi kumuuliza wala kumshauri chochote si mama wala sisi watoto wake, cha ajabu sasa hivi analalamika eti mkewe na watoto tumemtenga ndicho anachonishangaza


Na baba yangu mzazi nae alikuwa hivyo, na sasa ni mzee sana. Wanae tunakoenda sana yeye na mke wake (mama yetu) na kuwatunza sana.


Hivyo inaonekana kwenu kuanzia wewe na mama yenu wote MAJANGA, na atakaeoa kwenu/alieoa kwenu KAZI anayo.
 
Na baba yangu mzazi nae alikuwa hivyo, na sasa ni mzee sana. Wanae tunakoenda sana yeye na mke wake (mama yetu) na kuwatunza sana.


Hivyo inaonekana kwenu kuanzia wewe na mama yenu wote MAJANGA, na atakaeoa kwenu/alieoa kwenu KAZI anayo.
Mtoto wa kike huyo hawezi kuelewa na tusimlaumu sana naona wanamkomoa mzee wao,hawajui sababu kwa nini mzee wao alikuwa anachelewa kurudi. Hapo unaweza ukakuta wanakula vizuri,wanavaa vizuri na mahitaji yote ya msingi wana yapata,sijui hawajiulizi haya mahitaji yalikuwa yanatoka wapi na ni nguvu ya nani.

Sasa uoe mwanamke kama huyo ambaye hamthamini baba yake aliye mtimizia mahitaji yake ya msingi yaani damu yake then ndioo utegemee aje kukuthamini ww. Vifua vya wanaume vimebeba mengi sana na ndio maana Mungu katupa makoromeo.

Hawajui sisi wanaume tuna sacrifice vitu vingi sana ili mradi familia ipate mahitaji yake ya msingi.
 
Mtoa mada sijakuelewa unachoogopa ni kipi haswa kwenye ndoa.

1.Kuchapiwa mke ?

2.Mkeo kutumia Mali zako? Sasa na Baadae , ukifa.

3. Uchumi wako mdogo kuhudumia kama wajibu na haki ya wategemezi ?

4. Magonjwa ya ngono ?...

5. Mkiachana mtagawana Mali na huyo mke ?

Em funguka Kaka maana mpaka Sasa nna hints tatu
:Ww ni mtu mzima wa 40+ (nahisi)
: Una stress na shinikizo juu ya ndoa kutoka kwa jamii na familia.


Swali la Uzushi.
Je ww ni mtoto wa nje ya ndoa, kwa mama ako ?
 
Mzee wangu naye alikuwa kama wewe hivyo hivyo, bahati nzuri hakuna aliyewahi kumuuliza wala kumshauri chochote si mama wala sisi watoto wake, cha ajabu sasa hivi analalamika eti mkewe na watoto tumemtenga ndicho anachonishangaza
Kwa hiyo mna mnyoosha mzee wenu daah.Yaani baba yako aliye kuleta duniani na kukupatia mahitaji yote ya msingi unamfanyia hivyo je huyo mume wako utamfanyiaje. Unajua sababu ya kwa nini alikuwa anachelewa kurudi?.

Daah hizi ndizo type zenyewe zilizopo....... kweli kazi tunayo.(ukiingia tu umeyakanyaga kama Shabani Kaoneka).

Huyo mzee wako na muonea huruma nahisi Sonona inaweza chukua hata uhai wake..........ila kama ni kweli mnamfanyia hivyo na yeye inamuumiza kaeni mkijua hamtabaki salama.
 
Kwa umri wangu huu (nimekula chumvi kiasi) nimeona na kujifunza mengi kuhusu mahusiano ya kimapenzi na ndoa. Nimeshuhudia vijana wengi waliokimbilia maisha ya ndoa wakipoteza muelekeo wa maisha muda mfupi tu baada ya kuianza hiyo safari ya ndoa!

Kutokana na mikasa na vitimbwi vya wanandoa wengi nilijipa muda wa kufanya utafiti mdogo usio rasmi kuhusu maisha ya ndoa na mwisho wa siku nikaibuka na majibu haya;-

1. Ndoa ni gereza la kiroho, kimwili na kiuchumi kwa mwanaume (ndomana inaitwa pingu za maisha)

2. Ndoa ni mtego wa wanawake kuwatawala wanaume.

3. Ndoa ni chanzo cha magonjwa mengi kwa wanandoa hasa wanaume yanayopelekea vifo vyao (tuna mifano mingi ya wanaume waliopoteza maisha au kupata magonjwa mazito muda mfupi baada ya kuoa)

Kutokana na utafiti wangu huo usio rasmi nimeona niwashauri vijana wenzangu na wanaume kwa ujumla, Hakuna maisha ya furaha na amani ndani ya ndoa kama mnavyohubiriwa.

Ukitaka furaha tafuta pesa ujipe furaha mwenyewe (ukiwa na pesa utapata kila utakacho ikiwa ni pamoja na huduma zipatikanazo ndani ya ndoa)

Achaneni na upuuzi wa ndoa, yaani umtolee mahari, umtunze, uwatunze watoto, umlinde asikusaliti, umridhishe kitandani na bado mkiachana abebe mali zako?

Wabobevu mniambie ndoa ina faida gani kwa mwanaume? Je ni ngono tu au kuna kipi special?

#KATAANDOA
Hii nyuzi
 
Mkuu kanali kama umeona shida imeanzia kanisani Sasa makasiriko ya nn kwa waliooa. Acha kuji-attach na hizo ethics za kikanisa we oa hata mara kama ukimshindwa mtoto wa watu unadisha kwao. Kuoa ni heshima .

Nimekuuliza kabla, je ww ni mtoto wa nje ya ndoa yaani zao la zinaa ? Naona una-skip swali tu.
 
Mkuu kwnn ufikirie kuachana na mkeo ? Hujaoa af ushafika kwenye kuachana ? Hofu ni nini haswa , amini mkuu kanuni ni hiyo hiyo utapata wa kufanana nae. Badala ya kushauri vijana wasioe, badili ushauri maana huo ni kwa wazinzi wezio .... UTAPATA WA KUFANANA NAE. Malaya hapati Gentle, na kama unahisi Kuna Gentle aliyepata Malaya huyo sio Gentle.
 
Mzee wangu naye alikuwa kama wewe hivyo hivyo, bahati nzuri hakuna aliyewahi kumuuliza wala kumshauri chochote si mama wala sisi watoto wake, cha ajabu sasa hivi analalamika eti mkewe na watoto tumemtenga ndicho anachonishangaza
Dah! [emoji23][emoji23][emoji23]sista unajua hapo ndio umechochea moto kabisa nasio kuuzima. Kweli hata nyie wenyewe hamjui mwanaume huangalia vitu gani mpaka aoe. Anyway mimi kuoa sitaacha hata kidogo, ila aisee mnajifungaga wenyewe sana. Hamjui kutetea hoja zenu[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hivi kwani siku hizi majukumu ya mwanamke kwenye ndoa hayaonekani au

Yani wewe mke akupikie, akufulie, akulee, akuzalie na akulelee watoto wako, akupe unyumba na vingine vingi halafu bado uone hastahili mali zako sasa unataka umpe kitu gani

Hizo mahari mnazotoa anachukua mke au wanachukua wazazi/walezi wake na umeshajiuliza ni kwanini kwenye jamii zetu mwanamke anatolewa mahari

Yani ukitoa huduma ya kiuchumi kuna kipi kingine mwanaume anachoweza kumpa mwanamke, maana mkae mkijua hizi kampeni zenu za kataa ndoa kisa kukimbia majukumu yenu hamuwakomoi wanawake, bali mnazidi kufanya wanawake wasione umuhimu wenu na hili limeshaanza hivi sasa kwa baadhi ya wanawake

Hayo mapungufu ya kibinadamu kwenye ndoa huwa yapo tu, hata wanaume mna mapungufu yenu ila ni vile ya kwenu mnayaona madogo hivyo mnalazimisha yavumiliwe, ila ya wanawake mnayaona makubwa hivyo mnaona hawastahili kuvumiliwa
Mahari inatolewa kama shukran kwa wazazi kwamba binti amejitunza ( bikra)
 
Back
Top Bottom