Kama una mtaji fanya biashara ya Mbuzi, utakuja kunishukuru

Nitalifanyia kazi hili wazo.Ahsante sana mkuu
 
Nzuri. Kwa anaye anza mdogo mdogo nunua mbuzi chinja. Ya ndani pika supu. Ya nje kata mapande, uza 4,000 weka kibanda karubu na kituo kikubwa cha mabasi. Kaa karibu na mtu wa chapati. Chukua na ndizi iwe karibu.
 
Nafatilia mkuu,ntatia neno

Ova

Uko salama lakini mkuu? Umepotea sana.
Hivi viwanda kama kweli wananunua kiasi chochote utakachopeleka na hawako na usumbufu kwenye malipo, watakua wazuri.

Hapo kwenye mzigo kupimwa bila uwepo wako ndio naona kuna mushkel kidogo.
 
Simple, kama huwaamini unachukua mbuzi wako unaenda kupambana na madalali Vingunguti 😅 ndio ukaone vibweka sasa kama hujarudi mbio mbio hapo kiwandani!

Bora ya hawa hata kama wanakupiga lakini uhakika na mfumo wao umekaa sawa kidogo. Madalali unaweza kujikuta umegeuka Hamza na pesa yako hauipati.
 
Wangenunua mbuzi akiwa hai ingekuwa nzuri zaidi, bei iwe 6,000 ao 6,500 /KG kuliko wanunue nyama 6,800 ao 7,000/KG. AMINI NAKWAMBIA!!!!! WANAPIGA KWENYE UZITO WA NYAMA
 
Ahsante sana kwa kua muazi mkuu japo umesema baada ya wewe kupata kazi nyingine. Ila mtririko wa wa biashara ni mzuri, ila hiki kipanda ndo kimeharibu hiyo biashara bepari an exoploit hapa kwa nini asiwe muazi?

"......Unapofikisha mzigo kiwandani unaandikisha idadi ya mbuzi, na label uliyowawekea. Kisha unawaachia bank account au namba ya simu kama utapenda malipo yafanyike kwa njia ya simubank. Baada ya siku moja au mbili maximum unatumiwa kiasi cha uzito uliopatikana baada ya kuchinja mzigo wako na kisha account yako inasoma....."

Bepari anapata faida ×3 ya muangaikaji polini hapo ngozi ya mbuzi ni sh 7000 kwa open market, utumbo wa mbuzi unakausha na kutegeneza chakula cha [emoji241] kilo gharama ni 5000, kama mzani ni wake mpimaji niyeye mnunuzi niyeye duh hiyo sio fair play. Ata akipunguza 0.5kg kwa kila mbuzi ni faida kubwa sana.... wanyonge tutabaki hivo hivo paka pale tutakapo pigania fair trade na matajiri. Hiyo biashara ni nzuri kwa kujikimu ila kutajirika ujenge apartment au mall sio.
 
Yah hawa ndio watu wanaotakiwa wawe wengi nchini ili tusonge mbele ila kibaya wamejaa wachoyo, roho mbaya na wazandiki tu! Mtu anakwambia tafta hela wewe ila mbinu hakupi 😅 shwaini kabisa kwani zinaokotwa hizo hela?
Mtu mweusi akiacha ubinafsi tutafika mbali sana,

Wengi tunaamini tulikuja duniani kukusanya tunasahau kuwa tulikuja kufanikisha mambo, ukitoa hata mawazo tu ni sadaka kubwa sana.
 
Mtu mweusi akiacha ubinafsi tutafika mbali sana,

Wengi tunaamini tulikuja duniani kukusanya tunasahau kuwa tulikuja kufanikisha mambo, ukitoa hata mawazo tu ni sadaka kubwa sana.
Yeah mtu mweusi roho mbaya la kinyongorilo
 
Nimejikuta naingia kwenye profile yako kukagua thread zingine mana umeiandika kiufundi sana thread hii.. binafsi pia nimewahi fanya japo haikuwa kwa mfumo wa viwanda ila sioni chakuongezea mana pote umeenea na nimependa zaidi ulivyomalizia..
 
Mtu mweusi akiacha ubinafsi tutafika mbali sana,

Wengi tunaamini tulikuja duniani kukusanya tunasahau kuwa tulikuja kufanikisha mambo, ukitoa hata mawazo tu ni sadaka kubwa sana.
Kichwa kinauma toka niliposoma hapa mda huu Niko tu nimekaa sina cha kufanya nafsi inaumwa balaa...ningekua na 2m hapa mda huu Niko mbezi Nnapmshapaland KVC au Shabiby ya Dom niamkie Huko urangini ila ndo napambana hapa mpk kieleweke aseehh!kumbe tunapoteza tu mda kirahisi hivi ila bi idhn lllaah hii ntakomaa nayo hata mwisho wa mwezi huu!!
 
Nb: research ni muhim mnoo
 
kwwnye kutajirika na kujenga malls itategemea na mtaji wako na nidhamu kwa faida unayoingiza...kama mbuzi wawili mpk watatu wanaweza kulipa gharama zote ndogo ndogo...hlf kwa kila mbuzi lets say mbuzi 100, ukapata faida ya buku 5 - 6 nadhani sio faida mbaya kama una uhakika wa kuzungusha kila wiki.
 
Nafuga kondoo na mpka sasa Mimi ni mtaalamu mzuri ktk ufugaji kondoo...kuna kitu naona bado kinanitesa sana ktk maisha yangu kwa sababu sijakikamilisha ipasavyo nafuga kondoo wachache tu bado sijafikia lengo na bado sijaanda mazingira ya kufuga kondoo wengi hichi ndo kitu kinantesa
Naishi kijijini ila ni kijiji ambacho umeme upo,maji yapo, Barabara zinapitikaa na usafiri wangu wa boxer kwenda mjini na kurudi unanitosha sana...kijiji chetu naweza kufuga hata kondoo 900 na zikala majani mpka zikayaacha huwa napiga hesabu nikitimiza majike ya kondoo 300- 400 na madume 5 tu hapa kijijini... Mimi ni TAJILI uwezo wa kuwa nazalisha kondoo 900-1000 kwa mwaka upo...kondoo anazaa Mara 2 kwa mwaka anabeba mimba miezi mi3 je nkizalisha 800 na nkiwauza sh50000 kwa kila kondoo moja....hapa kijijini NTATAMBA si mchezo ngoja niandae mazingira.
 
Umeandika vizuri na umeeleweka ukiona mtu anauliza swali huyo Hana nia na hawezi mikiki mikiki ya hyo kazi sababu umeandika vitu muhimu na umenyoosha.

Binafsi nishafanya Ila ilkua n nguruwe mnadani unatakiwa uwe mjanja na mshapu Ila door to door n nzuri muhimu uwe unajua kwa macho kuwa huyu ukimuangalia hakosi KG kadhaa hvyo unakata hata 7kg ndo unaongea Bei na mnunuzi.

Changamoto ya Door to door unatakiwa ujue kuishi na watu ukikuta watu wanakula ugali wa mdama na dagaa wa kuchemsha unga usilete swaga, Kuna muda inabidi ulale hukohuko bush kwa wenyeji Kama n kulala chini lala Kama n kwenye ngozi lala faida yake utakuja kuiona baadae.

Ukiingia Kijiji unakutana na mjanja wao Sasa wewe kuwa mjanja zaidi yake wengi wanaongea kilugha hvyo jifunze kujua maneno muhimu kwenye Biashara yako katika sehemu unayokwenda kutafuta mifugo.

Jifunze kumsoma mtu usoni pindi mnaposalimiana tuu au akiongea maneno matatu hii itakusaidia kupata kwabei nafuu.

Vijana tupambane usisubiri mpaka ufike 1million ndo uanze Anza na hicho hicho ulichonacho Kama una Nia inakutoa bila shida hata Kama n laki moja we Anza na pale inapowezekana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…