Kama una stress pitia hapa, usiache kutupia na wewe maneno yako

* Habari zenu *
Ndugu zangu ninapenda kuwataarifu kuwa siku ya jumatatu kijana mwenzenu ntachukua jiko. Japo imekua ghafla hili ni jambo la kheri la kumpendeza mungu niliamua kuchukua uwamuzi huu baada ya kuona mama yangu akipata shida kupikia kuni hivyo keshokutwa ntachukua jiko la gesi na kumpelekea nyumbani
*sitaki mother apate tabu*
 
*KWA STAILI HII WIZI HAUTAISHA TZ*
*Katika zoezi la kupata vitambulisho vya shule mpiga picha alimwambia mwalimu mkuu kuwa kwa kila picha gharama yake ni sh.500, mwalimu mkuu akamwambia mwalimu wa darasa awaambie wanafunzi walete sh.1000 kwa ajili ya picha, mwalimu wa darasa akawaambia wanafunzi mkawaambie wazazi wenu wawape sh.1500 ya picha, mwanafunzi alipofika nyumbani akamwambia mamake tumeambiwa tupeleke sh.2000 ya picha shuleni, mama akamfuata baba akamwambia mtoto kaambiwa apeleke sh. 5000 ya picha shuleni nipe haraka nimpe maana wamesema mwisho kesho...!!!!!.Dah Magufuli Anayo Kazi*
 
kama kawaida chawa hawakosekanagi kuharibu threads za watu
 
JINSI YA KURUDISHA UPYA NGUO YAKO ILIYOCHAKAA AU KUPAUKA!!!

WATU wengi hukosa raha haswa pale nguo zao wanazozipenda zinapochakaa au kupauka;;

Fanya kama ifuatavyo
1:chemsha maji yachemke kwa (100C°)
2:weka nguo yako kisha iache ichemke ndani ya dakika50
3:itoe nguo yako!!
4:weka mafuta,kitunguu,nyanya na chumvi kidogo
5:chukua nguo yako,iweke na ukoroge kisha ufunikie!!
Ona unavyonifatilia kwa makini,kama nguo imepauka kanunue nyingine kwani madukani zimeisha??
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Pana demu namtongoza hapa cha ajabu kahamaki na kuniuliza kwanini namtongoza wakati anamjua mke wangu? nami kwa upole kabisa nimemuuliza kwani ukienda kununua nguo unakwenda uchi? naona anacheka na kung'oa ng'oa nyasi sijui ng'ombe watakula nini!
Hahaaaa
 
Vita baridi ni nini?

Vita baridi no pale ambapo we we na baba yako mnabishana kuhusu mpira yeye anasema Giroud mkali kuliko messi..halafu we we ukajisahau ukadhani upo kibandani unaropoka "msikieni huyu matako" [emoji23] [emoji23]
Hahahaha
 
Hahaha we jamaaa ujue unaonekana
 
Naomba siku yangu ya kufa ikifika nife kimya kimya usingizini kama marehemu babu yangu...

Sio kufa napiga mikelele kama wale abiria wake waliokuwemo kwenye gari lake hapo alipopitiwa na kifo usingizini nyuma ya usukani
 
Jamaa alienda kanisani ku confess makosa yake kwa mchungaji..

Jamaa: Mchungaji nimekuja ku confess dhambi zangu, nimelala nje ya ndoa na binti wa miaka 18 aliyekuwa bikira.

Mchungaji: Kata ndimu 10 ukamue kikombeni ... changanya na maji ya limau 10 humo kikombeni kisha unywe.

Jamaa: Hii ndio itaniondeshea dhambi zangu?

Mchungaji: Hapana... itaondoa hilo tabasamu lako hapo usoni kwako
 
Lala uache dirisha wazi usiku wa leo....

Mbu 1400 watabonyeza likes
Mbu 510 watacomment
Mbu 210 watashare event kwenye page zao

Mbu mmoja atajibu mualiko
Mbu laki moja watahudhuria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…