Kama unaingiza faida ya Tsh. 30,000 na kuendelea kwa siku pita hapa

Kama unaingiza faida ya Tsh. 30,000 na kuendelea kwa siku pita hapa

150,000/= Mimi ninayo mawili ilinitoka laki tatu mana mm yangu nime weka matairi ya pikipiki yaliyo tumika ambapo fremu pekee nili tengeneza kwa 60,000/= hayo matairi mawili nilinunua 90,000/=

Return yake ikoje hii mkuu.....
 
Mtaji kuanzia laki moja na kuendelea ndo itakuwa fresh, lakini mimi nilianza na tsh 30k saiv naona faida hata ya 25k, had 50k siku nyingine kama faida.
Hapa parcel moja nauza tsh 2000 ..nikiwa na parcel 50 tu nikipita ofisi tano zinaisha zote..

Hili hii biz ..pia ongezea na value kidogo, yani kuwa mchangamfu, mchekeshaji hehehe hukosi wateja..

Wanaotafuta Ajira achezi kupoteza Muda hakuna ajira kwa sasa ila kazi zipo za kufanya. Ondoa aibu, mimi nakutana na wenzangu niliomaliza nao chuo, wapo tu eti wamejishkiza, kimshara chenyewe 3k,4k,5k, ukiotea sehemu nzuri ndo 10k hapo ujala, nauli, hujui ni lini utapata kazi ya kueleweka..

Nimegundua Kwamba watu ambao "hawajasoma" wanaingiza pesa nzuri sana kwa sababu hawana cha kupoteza. Wenzangu na mie wenye vi Degree vyetu tunachagua kazi za kufanya..

Mithali 10:4

Hongera sana nimeipenda 🤝
 
Wow huu ushauri ni mzuri mkuu, thank you itabidi nifanye hivo maana saving kwa hiari ni ngumu😐
Kuwa na account ambayo hauwezi kuiaccess muda wote, mie nna jr account.... Unajaza ile huduma ya kukatwa kiasi flani katika mshahara then inaingia huko, inategemea na kipato chako sasa ukikatwa laki mbili miezi mitano tu una 1m umepata mtaji wa kutosha kabisa kuanzia.
 
Kama unataka mtaji wa 30k-50k means kwa mwezi unakusanya 900k-1.5M
Basi jua iyo biashara ni kubwa inahitaji capital ya kuanzia 5M-10M na kuendelea

Kumbuka pikipiki kama boda boda na bajaji zinauzwa bei mkasi sana mfano boda boda 2.5M na wanarejesha kila siku 8000-10,000
Hivyo hivyo Bajaji inauzwa 7M wanarejesha kila siku 15,000-18,000

Uber yaani gari kama IST au tufanye vitz inacost approximatel 9M-13M
Wanarejesha 25k-30k

Hivyo unaweza ukachanganua ulicho nacho mfukoni kwako utaelewa iyo faida ya kila siku 30-50 unahitaji kuweka pesa kiasi gani

Na log out
Mkuu... Huyu mwamba anazungumzia faida ya 30K kwa siku. Boda ya 2.5m inakupa 10K kwa siku. Inakupasa uwe na boda 3 ili kupata 30K kwa siku... Hapo mtaji ni 7.5m

Kuna vibiashara vinaonekana vya kizembe lakini kwa hiyo 2.5m unakika 30K kiroho safi kabisa.

Hivi kwa mfano unajua kreti moja ya bia inakupa faida ya 5K? Kreti 6 tu unalamba 30K.

Ka grocery tu ambako unaweka na kajiko ka chipsi na mishikaki... Ukauza hata vikreti vitatu vya bia + Visoda + Vi-K Vant, nyagi, smart gin, maji na vitakataka vingine unaikunja 30K korahisi tu. Mtaji waweza usifike 4m.

Tatizo hivi vidigrii vinafanya wengi wabague kazi za kufanya...

Kuna kagrocery kanakunja faida mpaka nashangaa. Afu kuna mjasiriamali aliomba aweke shoeshine and repair pembeni na kuuza juice. Jamaa yule pia anaosha magari ya wateja kiaina anatengeneza mkwanja mpaka namwonea wivu natamani nimtoe pale lakini Roho wa Mungu ananikataza
 
Hakuna chenye faida kama Guest house.Tatizo ni mtaji tu...

Nimebadilisha nyumba ya kupanga (ya urithi)ikawa guest house.Ilikua na room 12.Mbovu mbovu tu.kwa siku nilikua napata zaidi ya 90k.Saiv nimekarabati naingiza zaidi.Nina mpango wa kujenga ingine
Mbinguni utaenda kulala chooni
 
Nilianza kutengeneza capital nikawa na save kiasi kwenye salary (salary yangu ni 650000) ikafika mil 4 nikawekeza kwenye BIASHARA ya vipodozi income ya siku ilianza 10000/= ikafika mpaka 50000/= , nikatengeneza mtaji nikawa nanunua mahindi na fiwi nikawa nauza yakipanda , baadae nikawa nakopesha kwa sababu sina vibali , nakopesha wafanyakazi wenzangu kwa riba ndogo hadi 5% ambayo haipatikani kokote , kuhusu risk ya kupoteza nilitengeneza connection na mhasibu kwa hiyo mfanyakazi anaeenda kutemwa taarifa zake nakua nazo nakua najua jinsi ya kumtema…nikabadili jinsi ya ku-save nikatoa bank nikaweka UTT mwaka jana mwezi wa 5 ,mwaka sasa… NB , siko mwenyewe WIFE ni real hustler

Hapa kuna lesson ya mtaji, kuna watu hukimbilia kusingizia hatuna mitaji kumbe mitaji tunayo afu hatujui 😁

Hongera sana mkuu 👍👍 ahsante kwa mchango wako
 
Nilianza kutengeneza capital nikawa na save kiasi kwenye salary (salary yangu ni 650000) ikafika mil 4 nikawekeza kwenye BIASHARA ya vipodozi income ya siku ilianza 10000/= ikafika mpaka 50000/= , nikatengeneza mtaji nikawa nanunua mahindi na fiwi nikawa nauza yakipanda , baadae nikawa nakopesha kwa sababu sina vibali , nakopesha wafanyakazi wenzangu kwa riba ndogo hadi 5% ambayo haipatikani kokote , kuhusu risk ya kupoteza nilitengeneza connection na mhasibu kwa hiyo mfanyakazi anaeenda kutemwa taarifa zake nakua nazo nakua najua jinsi ya kumtema…nikabadili jinsi ya ku-save nikatoa bank nikaweka UTT mwaka jana mwezi wa 5 ,mwaka sasa… NB , siko mwenyewe WIFE ni real hustler
Hongera hapa kuna funzo kwamba ukipata mke sahihi ni rahis kufanikiwa.
 
Mkuu... Huyu mwamba anazungumzia faida ya 30K kwa siku. Boda ya 2.5m inakupa 10K kwa siku. Inakupasa uwe na boda 3 ili kupata 30K kwa siku... Hapo mtaji ni 7.5m

Kuna vibiashara vinaonekana vya kizembe lakini kwa hiyo 2.5m unakika 30K kiroho safi kabisa.

Hivi kwa mfano unajua kreti moja ya bia inakupa faida ya 5K? Kreti 6 tu unalamba 30K.

Ka grocery tu ambako unaweka na kajiko ka chipsi na mishikaki... Ukauza hata vikreti vitatu vya bia + Visoda + Vi-K Vant, nyagi, smart gin, maji na vitakataka vingine unaikunja 30K korahisi tu. Mtaji waweza usifike 4m.

Tatizo hivi vidigrii vinafanya wengi wabague kazi za kufanya...

Kuna kagrocery kanakunja faida mpaka nashangaa. Afu kuna mjasiriamali aliomba aweke shoeshine and repair pembeni na kuuza juice. Jamaa yule pia anaosha magari ya wateja kiaina anatengeneza mkwanja mpaka namwonea wivu natamani nimtoe pale lakini Roho wa Mungu ananikataza
Mkuu ulichosema ni sahihi mimi mara ya kwanza naona huu uzi mwaka 2021 nilipata wazo la biashara nikalifanyia kazi huku mkoani nilipo huwez amini mtaji hauzidi laki 2 lakini nakunja elfu 40 mpaka 50 kama faida kwa siku, nikikosa sana naambulia 25k mpaka 30k.... Hapa nataka nikitulia niweke goli kabsa maana pamechangamka!
 
Kuwa na account ambayo hauwezi kuiaccess muda wote, mie nna jr account.... Unajaza ile huduma ya kukatwa kiasi flani katika mshahara then inaingia huko, inategemea na kipato chako sasa ukikatwa laki mbili miezi mitano tu una 1m umepata mtaji wa kutosha kabisa kuanzia.
Ahsante sana ngoja nifanye hivyo pia, maana saving imekua shida pesa haikai
 
Mkuu ulichosema ni sahihi mimi mara ya kwanza naona huu uzi mwaka 2021 nilipata wazo la biashara nikalifanyia kazi huku mkoani nilipo huwez amini mtaji hauzidi laki 2 lakini nakunja elfu 40 mpaka 50 kama faida kwa siku, nikikosa sana naambulia 25k mpaka 30k.... Hapa nataka nikitulia niweke goli kabsa maana pamechangamka!
Biashara gani hiyo si muwe mnasema na biashara mnayofanya kwa faida ya wengi maana ndo dhumuni la huu uzi! Ukisema tu unakunja kiasi fulani kwa siku haimsaidii msomaji!
 
Back
Top Bottom