Kama unataka kupunguza umasikini fuga kuku chotara na kama unataka kufanya biashara fuga Kisasa

Mkuu unatumia majogoo wa nje?( Yaani umri tofauti na hao tetea )
Maana nikifuga Sasso ila matetea walipofika umri wa kutaga changamoto ikawa majogoo walikuwa Bado hawajapevuka

Kuchi ni aina gani?
Sasso wanaanza kutaga wakiwa na umr gani?
 
Mleta mada ni aina ya watu wanaoamini anajua kila kitu, hayupo tayari kujifunza kwa wengine lakini pia kufunza wengine, kwa ufupi mbinafsi. Au pengine tusimalize maneno, hajui namna ya kufikisha ujumbe. Moja kati ya hayo linamhusu.

Ukisoma mada yake utaona anapoint fulani, ila hajaiwakilisha kifasaha, ameandikaa juu juu tu kwa kujiamini yeye anajua na wengine wote hamjui kitu na hayupo tayari kufafanua.

Huyu ni kuachana naye tu, binafsi sina uzoefu mkubwa wa ufugaji lakini ninashauri watanzania kwny mijadala yetu tujiepushe sana kutoka nje ya mada. Yaani usipoteze muda nje ya mada kama ninavyofanya hapa. Ongelea Kuku, tetea upande unaouamini kwa hoja imara na vielelezo halisi, hiyo ni faida sana kwa wote.

Siku njema
 
Kwa nini usiiwakilishe wewe?.acha ujuha wa kutafuta sifa za kijinga humu. Unaweza anzisha Thread yako na ukaelezea.
 
Consumption yao ikoje? Angalia Consumption power.

Dar ndo watumiaji namba 1 wa kuku wakifuatiwa na Miji mingine kama Arusha then Mwanza na Mbeya.

Hiyo niji wanakula kuku siku ya sikukuu hiyo sio biashara. Yaani ufuge kuku kusubilia sikukuu?
 
Kula like mkuu.. Umemaliza kila kitu
 
Habari watanzania wenzangu

Napenda sana kujituma na huwa silazi damu nikiona fursa....



Juzi kati nilikua mtaa fulani hivi nikakuta mtu mfanyabiashara (yeye huuza vifaranga chotara) wenye week na kuendelea.


Nilivutiwa na vifaranga wake mno nikawaza na mimi siku zijazo ninunue nifuge ila nikikimbuka mara nyingi vifaranga wanavyoanzaga kufa hadi naogopa

Kasema keshawapa chanjo ya gumboro na kideri


Nafikiria kuanza na 20 hivi ila kuna wakati moyo unasita.


Hebu tuambiane ukweli wakuu kwa wale walowahi kufuga vifaranga mliwapa nini wasife?Chakula sio tatizo kwangu ila nataka kujua mbinu mliotumia ili vifaranga wasife
 
Moderators naomba muhamishie huu uzi jukwaa la kilimo na ufugaji pls


Asante
 
Biashara ya kukusaidia ku maintain Umaskini
 
Kaa mbali na hii biashara, utawatumikia madalali tu. Unless una uhakika wa supply ya vifaranga bora saa yoyote unapovitaka kwa bei nzuri na pia una soko la direct, kwa mkataba.
Pia, kaa nayo mbali kama unataka kufuga less tha 1000.
Hii biashara madalali wameshaiharibu.
 
Sina hakika kama huu mradi utalipa sana;kwani changamoto naona ni nyingi
 
Hakuna fursa utakayoifanya ikakosa changamoto cha msingi kusanya maarifa kisha anza. Mimi nilitafuta maarifa hapa hapa JF nikaanza na tetea tano wa kienyeji mwezi wa saba mwaka huu nilipata vifaranga 49 wawili walikufa wakiwa na wiki sasa hivi nalea vifaranga 47 wa kienyeji wana mwezi mmoja na siku nane mama zao wameanza kukalia tena. Awamu hii ya pili nategemea kupata vifaranga sitini mwisho wa mwezi huu.
 

You must be a marketing Guru. I admire your IQ
 
Huu ndio ukweli
 
Kuku Layers.

Chukulia una kuku wa mayai 400. Hawa watakula average kilo 50 yaani mfuko mmoja wa Layers.

Bei ya mfuko kwa sasa ni 52,000.

Utapata average mayai 300 kila siku kama kuku wako watataga vizuri mno - Average 75% ya kuku wote ambazo ni tray 10.

Bei ya Trai moja kwa sasa ni Tshs 5,000.

Kwa hiyo ukiuza mayai yote Tray 10 utapata Tshs 50,000 kwa siku.

Kuku wanakua mfuko 1 kwa bei ya Tshs 52,000.

Piga hesabu mwenyewe, kisha hujaweka mshahara wa kijana kama 80,000 kwa mwezi.

Kazi kwako.

(Hesabu yangu hii si ya kufikirika bali ni ya kweli na current)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…