Kama watoto ni Malaika kwa nini wana roho mbaya na tabia chafu

Kama watoto ni Malaika kwa nini wana roho mbaya na tabia chafu

wasalaam wakuu,kwenye jamii yetu tumeaminishwa kuwa watoto ni Malaika hawana dhambi wala hatia yoyote(hata mimi nakubali hili).sasa mimi nauliza kama kweli watoto ni Malaika kwa nini wana roho mbaya na tabia za ovyo?Mfano unakuta mtoto wa miaka chini ya miwili ni mchoyo na mbinafsi yaani kitu chake hatoi kabisa,watoto wengine wana wivu kama wanawake kwa mfano ulimweka chini na kubeba mwingine yeye anaumia na kuanza kulia(hapa nazungumzia wale wa chini ya miaka miwili,tabia nyingine ni ukorofi,matusi(nimeshuhudia mtoto wa chini ya miaka 2 anatukana),na tabia kubwa ni kiburi na dharau.naomba kujuzwa au shetani anawapa mafunzo ya uovu huko tumboni kwa mama zao tabia hizi nimezifanyia uchunguzi.Nawasilisha
%by Sir Khan.born 2 win%
Acha watoto, hao "malaika" wenyewe si malaika.
 
1)Waacheni watoto waje kwangu msiwazuie kwa maana walio mfano wa hao ufalme wa mbinguni ni wao, by Yesu.

2)Waacheni watoto wadogo waje kwambu maana ufalme wa mbinguni ni wao. by Wachungaji au Wahubiri.

Point namba mbili ndio chanzo cha watoto kuitwa malaika.
 
Mmh hiki kikombe kimumeupeka na kiendelee kumuepuka mwanangu,ana upendo,adabu,anapenda watoto wenzie na akiona wanapigana analia anawaamulia na yule anayempenda sana anaenda mkumbatie,ni furaha yetu hapa home,akiona na mawazo anakuja kunkumbatia,ana miaka chini ya miwili
Hongera amu
 
Kumbuka mtoto mdogo hilo ni umbo tu ila tabia ni ile ile kama ya MTU mzima,ndo maana mtoto akifa hukumu yake ni kwa mzazi kama alikuwa safi anahesabiwa haki kama mwovu mtt ata awe na siku moja anahesabiwa uovu wa mzazi wake. Tafsiri ya bible ya kuwa acheni watoto wadogo waje kwangu haikumaanisha kwa umri noooo maana yake wenye dhambi ndo watoto wadogo maana hawajakua kiimani,walio act sinema alidanganya kuonesha eti anamnyanyua mtt mdogo na watu walikalili ivo mpaka kesho." Kumbuka hakufundisha pasipo mfano" na mfano sio halisi ya kile husika ni ili watu waelewe. Ivo tabia zote mtoto anazaliwa nazo ila akija akakuta jamii iko active zinaonekana wazi ila kama ni ya wacha Mungu zinashindwa na nguvu hy na haziinuki. Mfano mzuri Cane na Abel hakukuwa na jamii ovu ila dhambi ilionekana kwa mmoja wao means unazaliwa Nazo. Nawasilisha tu.
 
Ila mod aliyetembeza ban siku ile ana roho ngumu sana aliwezaje kupiga ban wezere kama lile?kama si mwanamke yule sijui
Haaaaaahaaaaaaa....we demu bana mbavu zangu, ngoja nikae kimya siropoki tena asee[emoji40] [emoji40] [emoji40] [emoji40]
 
Mkuu,
Kuku huzaa kuku, bata huzaa bata na hata binadamu huzaa binadamu. Watoto si malaika bali kwakuwa sisi wazazi wao ni wadhambi basi nao dhambi i ndani yao kama vile ilivyo ndani yetu.
 
1)Waacheni watoto waje kwangu msiwazuie kwa maana walio mfano wa hao ufalme wa mbinguni ni wao, by Yesu.

2)Waacheni watoto wadogo waje kwambu maana ufalme wa mbinguni ni wao. by Wachungaji au Wahubiri.

Point namba mbili ndio chanzo cha watoto kuitwa malaika.
nimegundua watu wanatafsiri Bible kama wanavyotaka wao(kwa mahaba)kuanzia leo watoto ni watoto tu ova
 
Kwa nini ujitoe? Tunakoelekea wapi?Unajitoa vipi kwa kuweka habari inayoleta maswali zaidi?
mimi naamini Malaika wapo wewe hauamini na kwa jinsi ninavyokujua hatuwezi kuelewana kabisa mkuu
 
mimi naamini Malaika wapo wewe hauamini na kwa jinsi ninavyokujua hatuwezi kuelewana kabisa mkuu

Hujanijua vizuri bado.

Sio tu siamini, sitaki kuamini, nataka kujua.

Tafadhali usinishushe ngazi na kunipeleka kituo kisicho changu.
 
Wewe una umri gani?

Maana inawezekana mtoto kaanzisha uzi kulalamikia utoto wa watoto wenzie!
 
Roho mbaya na tabia mbaya lakini hawajui wafanyalo bado hawajui baya na zuri, anaweza kumtoboa mwenzake jicho bila kujijua. Ni malaika kwa kuwa hawana nia ya kufanya kitu hivyo hawana dhambi na ufalme wa mbinguni ni wao.Hata nabii Issa anajua hilo.
 
Back
Top Bottom