Kama watoto ni Malaika kwa nini wana roho mbaya na tabia chafu

Kama watoto ni Malaika kwa nini wana roho mbaya na tabia chafu

Watoto wanazaliwa wakiwa na minds pure, hii hupelekea kuona vitu vya ulimwengu wa kiroho pasipo sisi kuviona. Kadri wanakuwa minds zao zinaanza kudaka yale yanayofanywa na watu wanaowazunguka hasa wazazi. Hapa ndipo hutegemea sasa, wanarekodi mabaya au mazuri toka kwa hao wanaowazunguka?
Kutokana na bongo zao zimerekodi mambo machache compare to matured ones hufikia muda akili zao zinare-load yale waliyokuwa wanayasikia.
Kwakuhitimisha jamii imzungukayo mtoto ndio huamua mtoto huyo awe wa aina gani.
 
Biblia inasema,mlee mtoto katika njia impasayo,naye hatoiacha ata ajapokuwa mtu mzima,

Kumbe jamii na wazazi tunajukumu la kumlea/kumpandikizia mtoto Yale mema yatakiwayo,
Tusipowapandikiza mema,shetani uja na kupanda vitu/tabia ovu mioyoni mwao.
 
Mmh hiki kikombe kimumeupeka na kiendelee kumuepuka mwanangu,ana upendo,adabu,anapenda watoto wenzie na akiona wanapigana analia anawaamulia na yule anayempenda sana anaenda mkumbatie,ni furaha yetu hapa home,akiona na mawazo anakuja kunkumbatia,ana miaka chini ya miwili
Mlee vema na kumuombea ili Mungu amtunze na kuzidi kumpa moyo huo halisi wa Mungu mwenyewe
 
Ndugu yangu hapa umechanganya madesa tu, ila ukweli ni kuwa watoto hawana roho mbaya hata kidogo. Ni kwamba hayo matendo yao yanayopelekea udhani kuwa wana roho mbaya, yanadhihirisha asili ya mwanadamu namna anavyotakiwa aishi hapa duniani, baada ya kuwa ameumbwa na Mungu. Kuna mambo mawili tu makubwa na ya msingi ambayo kwayo binadamu aliumbwa ili ayafanye. MOJA Ibada kwa ajili ya kumwabudu Mungu aliyeumba na PILI kufurahia maisha yake hapa duniani.
Kinachotokea sasa kwa mtoto kwa mfano umemununulia kitumbua halafu ukajaribu kumuomba akakunyima, ni kwamba kile kitumbua kinamfurahisha, iwe na kwa kukila au kwa kukivuruga kwenye mchanga bila hata kukila, hasa anapokuwa ameshiba tayari. Kwa hiyo kitendo cha mtoto kukunyima wewe kitu,hakunyimi kwa sababu anakuchukia au kwa sababu ni mchoyo, hapana, ila anakunyima kwa sababu kitendo cha wewe kukupa kile alichonacho kitamfanya akose kitu cha kumfurahisha tena, na yeye kusudi lake mojawapo kubwa ambalo kwalo aliumbwa ni aliumbwa ili afurahi. Kwa hiyo akikupa wewe automatically atakuwa amepoteza kitu cha kumfurahisha, na ukizingatia kuwa yeye hajui kuwa na wewe pia ni mhitaji kama alivyo yeye pia.

Ni kama wewe hapo ulipo una gari lako ukaamue kulidumbukiza mtoni liende na maji wakati mto hauhitaji hilo gari lako, haitamaanisha kuwa unaupenda mto huo au unauchukia. Hivyo ndivyo yalivyo mahusiano yetu sisi na watoto hasa hawa ambao hawajajua chochote. Kwa hiyo mtoto anapokunyima kitu, hakunyimi kwa sababu anakuchukia na anapokupatia pia, hakupatii kwa sababu anakupenda hapana, ni matendo ambayo yako automated tu katika maisha yao.

Mimi siyo daktari wa binadamu lakini maoni yangu kwa mfano mtoto anapozaliwa huwa ni lazima alie kama yuko kawaida. Mimi ninavyodhani ni kuwa huwa analia baada ya mwili wake kukukutana na hali ya hewa nyingine nje ambayo hakuwa ameizoea pindi alipokuwa tumboni mwa mama yake. Hali hii huwa inamghasi na ukirudi kweye point yetu kwamba binadamu aliumbwa ili afurahi, hali hiyo huwa inamnyang'anya furaha yake na hivyo kumsababisha alie. kwa sbabu huwa inamnyang'anya furaha yake.

Kwa hiyo Watoto hawana roho mbaya, na ukirudi kwenye imani utafiti wangu mimi umeshanionyesha kuwa siri zote za binadamu wakubwa kwa wadogo, kweye ulimwengu wa roho, zimebebwa na watoto, na ikitokea mtu yeyote asiyekuwa ana dhamira nzuri au ana mambo ya giza na akawa anajaribu kuwatumia ili wazifiche, kadri anavyojitahidi kuwafanya wazifiche, ndivyo kadri anavyowafanya wazidi kuzi-expose kwa kiwango cha juu zaidi ya kile ambacho alitaka wakifiche. Sharti moja linalohitajika hapa ili uweze kuvuna to the maximum kutoka kwa watoto, ni lazima uwe uko na Mungu tu na hauna mchanganyiko wa kitu kingine chochote, na siri watakazokuwa wanakulete ni zote nzuri na mbaya ila zote zimeunganika katika kusudi moja la kukufanya ujilinde na mwovu Ibilisi. Watoto huwa hawaangushi kwa hili na HAYUPO anayeweza kuwafanya wafanye otherwise, ni NATURAL GIFT yao kutoka kwa Mungu na HAYUPO BINADAMU ANAYEWEZA KUIPOKONYA

Mwisho, bunadamu aliumbwa ili afurahi,..., kwa hiyo hakikisha kuwa kila siku unaponyanyua mguu wako kutoka nyumbani kwako, mguu huo siyo wa kwenda kuondoa furaha ya mwingine, ila kuongeza. Pia hakikisha kuwa una Ibada na Mungu mmoja wa kweli, na ni Mungu mmoja tu anayetakiwa kuabudiwa, miungu hawana haki wala hadhi ya kuabudiwa, kwa sababu huwa wanafanya kazi kinyume na Mungu mmoja wa kweli
Natanguliza shukrani zangu!
Uzi umeishia hapa no addition [emoji122] [emoji122]
 
wasalaam wakuu,kwenye jamii yetu tumeaminishwa kuwa watoto ni Malaika hawana dhambi wala hatia yoyote(hata mimi nakubali hili).sasa mimi nauliza kama kweli watoto ni Malaika kwa nini wana roho mbaya na tabia za ovyo?Mfano unakuta mtoto wa miaka chini ya miwili ni mchoyo na mbinafsi yaani kitu chake hatoi kabisa,watoto wengine wana wivu kama wanawake kwa mfano ulimweka chini na kubeba mwingine yeye anaumia na kuanza kulia(hapa nazungumzia wale wa chini ya miaka miwili,tabia nyingine ni ukorofi,matusi(nimeshuhudia mtoto wa chini ya miaka 2 anatukana),na tabia kubwa ni kiburi na dharau.naomba kujuzwa au shetani anawapa mafunzo ya uovu huko tumboni kwa mama zao tabia hizi nimezifanyia uchunguzi.Nawasilisha
%by Sir Khan.born 2 win%


Watoto wadogo kweli hawana dhambi na mfano wake. Ila kiwaita malaika ni uongo na ni uchache wa elimu juu ya viumbe wa Mola mlezi.
 
kusemwa yeye ni malaika si ukweli wa uhalisia lkn ni tafsiri kwani mtoto anakuwa hajua hili wala lile hata hivyo mtoto wa nyoka ni nyoka


Unaweza kutuorodheshea japo sifa mbili za malaika au tabia mbili za malaika ? Ili tufaidike ?
 

Jitahidi sana katika maisha yako usikuzie mtoto uswahilini.
 
Tungo za kuwapo kwa malaika, ni characters katika hadithi ya kubuni tu.

Hawapo kiukweli.


Kaka kwako wewe naona kitu kimoja kati ya vitatu au zaidi.

1. Una matatizo ya akili

2. Mjinga sanaaaaa !

3. Umekariri mawazo ya watu bila kumakinika kwayo.
 
Ulidanganywa sana na ulipewa chai...mtoto sio malaika
 
Kaka kwako wewe naona kitu kimoja kati ya vitatu au zaidi.

1. Una matatizo ya akili

2. Mjinga sanaaaaa !

3. Umekariri mawazo ya watu bila kumakinika kwayo.
Yote matatu hayo, hata kama ni kweli yote kwa pamoja au moja tu kati ya hayo, itakuwa ni uthibitisho zaidi kwamba Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingeumba ulimwengu ambao lolote kati ya hayo matatu yanawezekana.
 
Hujanijua vizuri bado.

Sio tu siamini, sitaki kuamini, nataka kujua.

Tafadhali usinishushe ngazi na kunipeleka kituo kisicho changu.


Kaka kauli zako huwa zinaenda kinyume sana na unachotenda. Mtu anayetaka kujua hana sifa kama zako,na ndio maana hujui mambo mengi sana.

Mola amekupa akili aisee,itumie vizuri ikufae.
 
Yote matatu hayo, hata kama ni kweli yote kwa pamoja au moja tu kati ya hayo, itakuwa ni uthibitisho zaidi kwamba Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye uoendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingeumba ulimwengu ambao lolote kati ya hayo matatu yanawezekana.


Nakuuliza swali dogo. Ukiwa unakula huwa una tumia mkono gani ?
 
Nakuuliza swali dogo. Ukiwa unakula huwa una tumia mkono gani ?
Swali lako linaonesha ufinyu wa mawazo yako na utovu wa maarifa ya tamaduni.

Unafikiri kwa sababu kijijini kwenu watu wanakula kwa mkono fulani, basi watu wote wanakula kwa mkono fulani tu.
 
Kaka kauli zako huwa zinaenda kinyume sana na unachotenda. Mtu anayetaka kujua hana sifa kama zako,na ndio maana hujui mambo mengi sana.

Mola amekupa akili aisee,itumie vizuri ikufae.
Thibitisha Mola yupo.

Nataka kujua hilo. Usihubiri. Usiniambie habari za imani. Thibitisha yupo.
 
Swali lako linaonesha ufinyu wa mawazo yako na utovu wa maarifa ya tamaduni.

Unafikiri kwa sababu kijijini kwenu watu wanakula kwa mkono fulani, basi watu wote wanakula kwa mkono fulani tu.


Kaka acha kuwa na wasi wasi na kuwa na dhana,unapoulizwa swali jibu swali sio unaleta dibaji.

Kama utakuwa una kumbukumbu nilishawahi kukwambia hivi " Kutokana na mtiririko wako wa ujengaji hoja na mitazamo yako,huwa najua kifuatacho utasema nini,japokuwa sio neno kwa neno bali hata kwa maana huwa sikukosi". Sasa inabidi ujitathmini mara mbili mbili mzee.

Sio kwamba nina uwezo wa kujua yajayo la ! la ! bali fikra zako nyepesi kiasi hicho. Mfano wako wewe ni mfano wa mtoto mdogo ambaye nikimpa shilingi 50 ya kitanzania,najua ataenda kununua nini,kabla hajaenda kununua.

Kaka ukiukizwa swali jifunze kujibu swali. Nakuuliza tena "WEWE UKILA HUWA UNATUMIA MKONO GANI ?"
 
Kaka acha kuwa na wasi wasi na kuwa na dhana,unapoulizwa swali jibu swali sio unaleta dibaji.

Kama utakuwa una kumbukumbu nilishawahi kukwambia hivi " Kutokana na mtiririko wako wa ujengaji hoja na mitazamo yako,huwa najua kifuatacho utasema nini,japokuwa sio neno kwa neno bali hata kwa maana huwa sikukosi". Sasa inabidi ujitathmini mara mbili mbili mzee.

Sio kwamba nina uwezo wa kujua yajayo la ! la ! bali fikra zako nyepesi kiasi hicho. Mfano wako wewe ni mfano wa mtoto mdogo ambaye nikimpa shilingi 50 ya kitanzania,najua ataenda kununua nini,kabla hajaenda kununua.

Kaka ukiukizwa swali jifunze kujibu swali. Nakuuliza tena "WEWE UKILA HUWA UNATUMIA MKONO GANI ?"
Kwa nini unafikiri natumia mkono maalum kula?
 
Thibitisha Mola yupo.

Nataka kujua hilo. Usihubiri. Usiniambie habari za imani. Thibitisha yupo.


Hujawahi kutaka kujua hilo. Siku ukitaka kujua kama tukiwa hai,nitajua tu na nitakuwa nakukumbusha wapi niliwahi kukuthibitishia uwepo wa Mola,hata kama si neno kwa neno hata kwa maana ya ujumla.

Turudi kwenye mada husika. Nilikuuliza swali kama unakataa malaika sio malaika,basi malaika ni nani hasa au kina nani hasa ?
 
Hujawahi kutaka kujua hilo. Siku ukitaka kujua kama tukiwa hai,nitajua tu na nitakuwa nakukumbusha wapi niliwahi kukuthibitishia uwepo wa Mola,hata kama si neno kwa neno hata kwa maana ya ujumla.

Turudi kwenye mada husika. Nilikuuliza swali kama unakataa malaika sio malaika,basi malaika ni nani hasa au kina nani hasa ?
Thibitisha Mola yupo kabla ya yote.

Kama huwezi kuthibitisha Mola yupo, na Mola ndiye kaumba mpaka malaika, basi hujakanusha kwamba malaika ni hadithi tu na hawapo.
 
Kwa nini unafikiri natumia mkono maalum kula?


Tatizo muoga sana kaka,jibu swali. Ukiwa unakula huwa unatumia mkono gani ? Kama unatumia yote wewe jibu. Ila si unajua hata Birika pia lina mkono ila sio kama mkono wako ? Tafakari kidogo juu ya kauli yangu utahisi au utaona ishara japo kwa mbali kwanini nimekuuliza swali hili dogo.

Nataka nikufundishe jinsi ya kufikiri vile unavyooaswa ufikiri.
 
Back
Top Bottom