Anayejifanya kuzijua siasa za marekani si wewe uliyekwenda hadi kujifanya kudadavua numbers, sababu uchwara na majimbo ndani?
Umetambua hakuna tulichoandika sisi zaidi ya:
1. Kuonyesha wapinga vita marekani walimpa miadi Kamala ya kumtia adabu kama hatabadilika mapema ya kutosha.
2. Kwamba hatimaye alikwenda kuwaangukia akiwa kachelewa mno nao wakakaza:
Kamala Harris alikumbuka shuka kukiwa kumekucha!
3. Baada ya kumtia adabu wamekwenda mbele kumkumbusha miadi yao kwa kuangusha party.
Hapo kipi kipya tumeandika sisi kuhusu siasa za marekani ndugu?
Kukurejea binafsi, unaonekana una makasiriko sana baada ya Kamala kutiwa adabu vilivyo.
"Kama Kamala angeshindwa tu kwa hizi sababu uchwara zako ulizoorodhesha, kumbe:"
1. Kwa nini alikuwa anagombea au kufanya kampeni?
2. Vipi Marais wote hai wa democrats kasoro Carter wa miaka 100+ kuambatana naye kumnadi na kumpiga kampeni vilivyo?
3. Vipi vigogo wakiwamo wa republican kama kina Dick Cheney na wengi wengine kum endorse Kamala?
4. Kulikuwa na haja gani ya kimwondoa Biden ulingoni?
5. Vipi kwenda kuwaangukia wapinga vita hawa?
6. Vipi Marais wote hai republican kumsusa Trump majukwaani na kukampeni kama yatima?
7. Nk.
Ujuaji wenu uchwara huu mngeuelekeza Narung'ombe ndani ndani huko, siyo huku kwenye utandawazi ambako dunia ni Kijiji!
Zaidi sana nikufahamishe hauko na data zozote kuwahusu wapinga vita ambamo humo wamo Arab Americans na sympathizers wao.
Kwamba wewe una makasiriko nao kivyao vyako unadhani kila mtu ndugu?
Jasmoni Tegga na wale wasayuni wengine habari ndiyo hiyo.
Kinyungu,
Proved,
Bwana Utam na ndugu waungwana hebu oneni hizi ngombe.
Ninakazia:
"Ngombe si ng'ombe!"