Kamati: Kinyesi na Mikojo ya Mifugo ndiyo chanzo cha kufa samaki mto Mara, sio sumu ya maji ya Migodini



Ripoti ya kijinga sana maji ya mto yanatembea sasa vinyesi haviendi na maji??
 
aibu na fedheha sana kwa taifa hili sijui Lissu anasemaje katika hili na waandani wake wamempa ubuyu gani na Chadema chini ya Heche wanasemaje ukanda huo
 
Usicheze na wahuni, kabla kamati haijaanza Kazi vikatafutwa vinyesi vikaenda kumwagwa. Ujanja Kazi ingefanyika kimya kimya ingesaidia, Hii serikal kila kitu siasa. Utaalamu uko pemben
 
Ngombe hawa hawa wa mara mmoja anakunya kinyesi cha kg 25 na mkojo lita 21..???

Hivi wanaficha nini kwa manufaa ya nani?..hivi hiyo mifugo imeanza kufungwa mwaka huu maeneo hayo..mbona hayakuwahi kutokea hayo...
Watendaji Kazi wabovu muda wote wanawaza rushwa
 
Pinga maeneo mengine yote, lakini sio hilo la daily quantity ya huo uchafu. It’s a googleable fact!
Hizo fact za Google ndo hatueitaki. Ng'ombe tunaongelea hapa ni Ng'ombe ambao eneo la mto hukaa kwa dk 5 mpaka 10 wakinywa maji. Utafiti unatuletea kiasi cha uchafu anaotoa Ng'ombe kwa saa 24. Najiuliza jambo moja huo mto umetumika kunywesha Ng'ombe maji tangu Enzi hizo na wakazi wa maeneo husika wakiwa na kiasi kikubwa kuliko hivi Sasa.
 
Sasa tunaahangaa nini hao ma PhD wakimpasua mtu kichwa badala ya mguu?
 

Umedandia train kwa mbele. Alichohoji ni uwezo wa ng’ombe kuzalisha kiasi hicho cha uchafu kwa siku moja. In this context, mahali anapozalishia huo uchafu is irrelevant!
 

Proffesor ni Proffesor kulingana MA vigezo vya uprofessor, labda tu jadili vigezo vya u Proffesor wa mtu

Na ondoa utendaji wa mtu kuupima na u Proffesor Wake, havina mahusiano, Kuna mtu anaweze kuwa pastor, lakini mzinzi.

Kwa hiyo kuna Kujua na utashi wa kutumia ujuzi, au utaalam mtu alio nao, ni vitu tofauti.
 
Jamani hayo ndo majibu ya utafiti Sasa nyie mnaokataa mmefanya utafiti?

Mimi sikubaliani na hiyo report ila siikatai report yao.
 
Point yako ya pili (2) upo correct mkuu,kwa kufanya oxidation ili ku degrade cyanide level ni gharama sana...hata method nilioanisha mimi ya kufanya dilution nayo cost yake sio ndogo...Kama wanaepuka na kuchepusha hizo tailings kwenye mazingira basi watakua hawatutendei haki
Napenda watu wa aina yako tunajadili mambo kwa hoja
 
Ukitaka kujua uwezo wao uwapime kwa kuwaangalia propesa Lipumba, Mruma na Ossoro...

Mwafrika hata asome vipi huwezi mtofautisha na mshenzi.
Teh teh teh πŸ˜‚πŸ˜‚ we jamaa acha dharau bhana.... heshimu wasomi wenzako.
 
Study nyingi zinaonesha kgs 9 mpaka 15 za kinyesi na lita 7 mpaka 10 za mkono kwa ng'ombe mmoja. Sasa sijui hao ng'ombe wa Mara wakoje?
Sasa hpo ukijumlisha 15 za kinyesi na 10 za mkojo hatupati 25 kweli?
 
Nyie mnaopinga hii ripoti ya utafiti Inabidii mtoe utafiti wenu maana kupinga kwa hisia zenu tu haitoshi.
 
Profesa ni kilaza mwenye makaratasi yanayoitwa vyeti
 
Muafrika hata afike level gani ya elimu, atabaki kuwa mpumbavu tu.

Wewe fikiria hapa Tz unamtofautishaje Kishimba au Msukuma na Chenge au Lipumba?? Kwa kipi yani??

Elimu kwa kigezo cha kuelimika hawawezi kuwa sawa ila Chenge na Lipumba na wasomi wengine wameweka maslahi binafsi mbele na wako override na wanasiasa..

Chenge kama mwanasheria kwenye taaluma yake ni nguli kweli na amewaacha hao wengine km nyingi sana, Lipumba naye ni mwanauchumi kwenye taaluma yake na dunia inafahamu kazi yake kama mwanauchumi..

Linapokuja suala la ujanja ujanja wa mjini na utafutaji wa hela kwa mbinu za kihuni basi kila mtu atatumia taaluma yake kwenye kufanikisha uhuni wake...

Huyo Kishimba unayemsema au Msukuma sidhani kama unafahamu background zao kabla ya kuingia kwenye siasa zetu hizi za kisanii...
Kishimba aliishi sana Zimbabwe akikimbia Tanzania miaka fulani, bila shaka unaifahamu sukita mali ya CCM ilivyofilisika....Huyu Msukuma huhitaji kumuelezea sana anajulikana kila kona..

Kwa hali hiyo unataka Chenge na Lipumba waishi kama Malaika kwenye shamba lililojaa mashetani kuanzia Makanisani, misikitini, Serikalini, mitaani kila mahala, nao ni binadamu wanahitaji kuishi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…