Kamati: Kinyesi na Mikojo ya Mifugo ndiyo chanzo cha kufa samaki mto Mara, sio sumu ya maji ya Migodini

Kamati: Kinyesi na Mikojo ya Mifugo ndiyo chanzo cha kufa samaki mto Mara, sio sumu ya maji ya Migodini

Musoma. Kamati maalum ya kitaifa iliyoundwa na serikali kuchunguza mabadiliko ya maji ndani ya mto Mara, imetoa taarifa ya chanzo cha mabadiliko katika mto huo yaliyosababisha maji kuwa meusi na kutoa harufu, huku samaki wakifa ambapo chanzo kimeelezwa kuwa ni shughuli za binadamu pamoja na nguvu za asili.

Akitoa matokeo ya uchunguzi leo Jumamosi Machi 19, 2022 mjini Musoma, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Samuel Manyele amesema kuwa hali hiyo imetokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kinyesi cha mifugo mtoni pamoja na uozo wa mimea ndani ya mto hasa mimea vamizi kama vile magugu maji na matete.

Amesema kuwa hali hiyo ilisababisha kupungua kwa kiasi kikubwa kiwango cha oksijeni ndani ya mto na hivyo maji kubadilika rangi na kuwa na harufu mbaya huku samaki wakikosa chakula na hivyo kusababisha vifo vyao.

Hata hivyo, amekanusha picha zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zilizokuwa zikionyesha samaki wakiwa wamekufa kwa wingi, akisema sio kutoka mkoani Mara.

Amesema kuwa kwa mujibu wa uchunguzi waliofanyana walibaini kuwa mabadiliko hayo ni matokeo ya mvua kubwa iliyonyesha ghafla kwa muda mfupi katika kipindi cha mwezi huu hivyo kutibua uchafu uliokuwa umejikusanya chini ya mto kwa muda mrefu.

"Mvua zingeendelea kunyesha hali hii ingeisha kwani uchafu ungetiririshwa lakini kwa vile mvua zimenyesha na kukatika ghafla ina maana uchafu ule unatoka taratibu na hii hali inaweza kudumu kwa zaidi ya miezi mitatu hadi minne endapo mvua hazitanyesha hapa katikakati," amesema.

Profesa Manyele amesema kuwa mto huo umeathiriwa kuanzia katika kijiji cha Marasibora wilayani Rorya na kijiji cha Wegero wilayani Butiama huku akisema kuwa mgodi wa dhahabu wa Barrick North Mara hauhusiki na uchafuzi huo.

"Mgodi upo mbali sana na maeneo yaliyoathirika na hata kama uchafu unaozalishwa mgodini pale ungezidishwa mara ishirini na kumwagwa mtoni maji yasingebadilika rangi wala kuwa katika hali iivyo sasa na maji ya mto kelekea kule mgodini ni masafi na hayana shida yoyote," amesema.

Amesema kuwa wamebaini uwepo wa kinyesi cha ng'ombe zaidi ya tani 1.8 milioni pamoja na mkojo wa ng'ombe lita 1.5 bilioni uchafu uliotokana na kuwepo kwa ng'ombe zaidi ya laki 3 waliokuwepo katika eneo oevu la mto Mara kwa kipindi cha miezi minane mwaka jana wakati wa kiangazi.

"Ng'ombe mmoja ana toa kilo 25 za kinyesi kwa siku moja na mkojo lita 21 kwa siku kwahiyo ukizidisha kwa idadi hiyo ya ng'ombe mara miezi minane utapata kiwango hicho na hapo bado hatujaweka kinyesi na mkojo wa kondoo, mbuzi na punda," amesema.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Suleiman Jafo ametoa muda wa siku mbili kwa kamati hiyo kuandaa taarifa kamili yenye mpango kazi juu ya nini kifanyike na muhusika ni nani kisha taarifa hiyo ikabidhiwe kwake kwaajili ya utekelezaji.

"Hii taarifa imenipa faraja baada ya uchunguzi kubaini kuwa hakuna kemikali mtoni maana kama kungekuwa na kemikali hii ingekuwa ni habari mbaya sana lakini taarifa hii inaonyesha kuwa tuna kazi kubwa sana ya kufanya ili mto uweze kuendelea kuwepo na tusipochukua hatua za haraka mto unaweza kupotea," amesema Jafo.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma;

1).Vifo vya Samaki Mto Mara: Kamati ya Dharura yaundwa kuchunguza Samaki wanaodaiwa kufa kwa Sumu

2). Madai ya sumu Mto Mara kutoka migodini, wananchi wazuiwa kutumia maji, kula samaki, uvuvi, Serikali yatoa tamko
View attachment 2157025
Hii ni taarifa mchongo.
 
Muafrika hata afike level gani ya elimu, atabaki kuwa mpumbavu tu.

Wewe fikiria hapa Tz unamtofautishaje Kishimba au Msukuma na Chenge au Lipumba?? Kwa kipi yani??
Vyeti vya kitaaluma na urefu wa C.V zao.
 
Za kuambiwa changanya na zako!!

Kuna maslahi ya umma na maslahi ya watu wachache.

Ni ngumu wakati mwingine kung'amua umma ndio akina nani!!
 
Endapo Ng'ombe mmoja wa kienyeji atafanikiwa kuzalisha kilo 25 za kinyesi na lita 21 za mkojo Kwa SIKU kipindi Cha kiangazi, je atatoa uchafu kiasi Gani kipindi Cha kiangazi?

Je, uchafu huu uzaliwa ukanda mmoja tu wa mto mara au Hali hii IPO Katika maeneo mengine nchini? Mbona hakuna rekodi ya Matokeo ya utafiti kama huu Toka kuumbwa Kwa Dunia?

Kupitia tafiti hizi za maprofesa: Kwako wewe msomaji, unadhani Profesa ni mtu wa aina gani? Ungetamani kuitwa profesa?

Unadhani kwanini Dr. Jafo kaelekeza kamati ikaandae Taarifa badala ya kupokea Taarifa? Je, profesa amewasilisha Taarifa ambayo haijakamilika? Findings zake amezitoa wapi? Vipi kuhusu recommendations?
Kwa muktadha huo, ina maana ng'ombe wote wa Mkoa wa Mara wamefunzwa kuwa sehemu pekee ya kujisaidia ni mtoni tu.

Hivyo wakiwa machungani huko huwa wanatunza vinyesi mikojo yao hadi wafike mtoni!

What a joke!
 
Ukitaka kujua uwezo wao uwapime kwa kuwaangalia propesa Lipumba, Mruma na Ossoro...

Mwafrika hata asome vipi huwezi mtofautisha na mshenzi.
Nafuta kauli.

Sema siasa na wanasiasa ktk bara letu la Africa ni kansa na virusi hatari ustawi ya jamii yetu ya kiafrika
 
Hii ni decomposition formula. Vipi kuhusu quantity?.... weka namba ya simu tukutafutie uteuzi
Ha ha ha aaaaa! Namba tena?
Binafsi nilihitaji prof ashushe madini rahisi tunayoweza kuelewa kwa urahisi.

Kutumikia wananchi ni jambo muhimu, lakini jambo hilo liambatane na baraq za Allah.
 
Ngombe hawa hawa wa mara mmoja anakunya kinyesi cha kg 25 na mkojo lita 21..???

Hivi wanaficha nini kwa manufaa ya nani?..hivi hiyo mifugo imeanza kufungwa mwaka huu maeneo hayo..mbona hayakuwahi kutokea hayo.?

Nadiriki kusema hii ni moja ya kamati za michongo...hivi wanadhani watanzania wasasa ni vilaza sana kwamba hawajui kuhoji au ku reason.

Eti mwenyekiti wa kamati ni professor..daah hii nchi kuna mambo yanakera sana..

Hivi hamna huruma na wananchi kansa kila uchwao zinaongezeka kanda ya ziwa..magonjwa ya ajabu ajabu..sasa hadi samaki wanakufa..ila mnaleta ngonjera.

#MaendeleoHayanaChama
Kinachotafutwa hapa siyo uchafu wa maji ya mto Mara ila ni sababu ya kuondoa wafugaji na mifugo bonde la mto mara tu
 
Ni up.umbavu wa hali juu kufikiria kuwa eti kuna sumu za mgodini zingesababisha samaki kufa mto Mara. Ni fikra za kijinga kabisa kutoka kwa wajinga wasiojua chochote kuhusiana na shughuli za mineral processing.

Mgodi wa North Mara, mahali uliko halafu eti ukasababishe vifo vya samaki mto Mara, hata akili ndogo ya kawaida inakataa.

Kwanza ni sumu gani ambayo ingeweza kutembea toka mgodi wa North Mara mpaka ikafike mto Mara ikiwa bado ina nguvu ya kuua viumbe majini? Chemical pekee yenye sumu kali inayotumika kwenye mineral processing ni Sodium cyanide, ambayo kwa muda mfupi ikiwa exposed kwenye hewa hupoteza nguvu yake. Chemicals nyingine ni acids, ambazo zingeingia majini zingekuwa diluted kutokana na uwingi wa maji.
Kwahiyo kinyesi cha Ng'ombe ndiyo kimesababisha maji kubadilika rangi na kuua samaki mtoni ?
 
Sitaki tena kusoma ikiwa nikisoma kufikia level ya uprofessor ninapoteza Uzalendo na utu kama huyu.
Kifupi tunaomba tume huru iundwe kuchunguza jambo hili na kuchunguza tume hii pia
 
Musoma. Kamati maalum ya kitaifa iliyoundwa na serikali kuchunguza mabadiliko ya maji ndani ya mto Mara, imetoa taarifa ya chanzo cha mabadiliko katika mto huo yaliyosababisha maji kuwa meusi na kutoa harufu, huku samaki wakifa ambapo chanzo kimeelezwa kuwa ni shughuli za binadamu pamoja na nguvu za asili.

Akitoa matokeo ya uchunguzi leo Jumamosi Machi 19, 2022 mjini Musoma, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Samuel Manyele amesema kuwa hali hiyo imetokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kinyesi cha mifugo mtoni pamoja na uozo wa mimea ndani ya mto hasa mimea vamizi kama vile magugu maji na matete.

Amesema kuwa hali hiyo ilisababisha kupungua kwa kiasi kikubwa kiwango cha oksijeni ndani ya mto na hivyo maji kubadilika rangi na kuwa na harufu mbaya huku samaki wakikosa chakula na hivyo kusababisha vifo vyao.

Hata hivyo, amekanusha picha zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zilizokuwa zikionyesha samaki wakiwa wamekufa kwa wingi, akisema sio kutoka mkoani Mara.

Amesema kuwa kwa mujibu wa uchunguzi waliofanyana walibaini kuwa mabadiliko hayo ni matokeo ya mvua kubwa iliyonyesha ghafla kwa muda mfupi katika kipindi cha mwezi huu hivyo kutibua uchafu uliokuwa umejikusanya chini ya mto kwa muda mrefu.

"Mvua zingeendelea kunyesha hali hii ingeisha kwani uchafu ungetiririshwa lakini kwa vile mvua zimenyesha na kukatika ghafla ina maana uchafu ule unatoka taratibu na hii hali inaweza kudumu kwa zaidi ya miezi mitatu hadi minne endapo mvua hazitanyesha hapa katikakati," amesema.

Profesa Manyele amesema kuwa mto huo umeathiriwa kuanzia katika kijiji cha Marasibora wilayani Rorya na kijiji cha Wegero wilayani Butiama huku akisema kuwa mgodi wa dhahabu wa Barrick North Mara hauhusiki na uchafuzi huo.

"Mgodi upo mbali sana na maeneo yaliyoathirika na hata kama uchafu unaozalishwa mgodini pale ungezidishwa mara ishirini na kumwagwa mtoni maji yasingebadilika rangi wala kuwa katika hali iivyo sasa na maji ya mto kelekea kule mgodini ni masafi na hayana shida yoyote," amesema.

Amesema kuwa wamebaini uwepo wa kinyesi cha ng'ombe zaidi ya tani 1.8 milioni pamoja na mkojo wa ng'ombe lita 1.5 bilioni uchafu uliotokana na kuwepo kwa ng'ombe zaidi ya laki 3 waliokuwepo katika eneo oevu la mto Mara kwa kipindi cha miezi minane mwaka jana wakati wa kiangazi.

"Ng'ombe mmoja ana toa kilo 25 za kinyesi kwa siku moja na mkojo lita 21 kwa siku kwahiyo ukizidisha kwa idadi hiyo ya ng'ombe mara miezi minane utapata kiwango hicho na hapo bado hatujaweka kinyesi na mkojo wa kondoo, mbuzi na punda," amesema.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Suleiman Jafo ametoa muda wa siku mbili kwa kamati hiyo kuandaa taarifa kamili yenye mpango kazi juu ya nini kifanyike na muhusika ni nani kisha taarifa hiyo ikabidhiwe kwake kwaajili ya utekelezaji.

"Hii taarifa imenipa faraja baada ya uchunguzi kubaini kuwa hakuna kemikali mtoni maana kama kungekuwa na kemikali hii ingekuwa ni habari mbaya sana lakini taarifa hii inaonyesha kuwa tuna kazi kubwa sana ya kufanya ili mto uweze kuendelea kuwepo na tusipochukua hatua za haraka mto unaweza kupotea," amesema Jafo.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma;

1).Vifo vya Samaki Mto Mara: Kamati ya Dharura yaundwa kuchunguza Samaki wanaodaiwa kufa kwa Sumu

2). Madai ya sumu Mto Mara kutoka migodini, wananchi wazuiwa kutumia maji, kula samaki, uvuvi, Serikali yatoa tamko
View attachment 2157025
Hapo Kwenye Tani 1.8 za kinyesi Cha Ng'ombe patamu
 
Mtu na pesa zake eeh
Anaweza kuhamisha mito milima na mabonde
Lakini akumbuke Mungu hapokei rushwa
Ujinga kama huu usingetokea kama Baba Yetu wa kisiasa Dkt Magufuli angekuwepo. Ila basi ndiyo hivyo, wananchi wataendelea kufa huku chanzo hatukijui.
 
Alichoficha mwenyekiti wa ripoti na hii timu yake ni kuwa chanzo cha hayo mavi ya ng’ombe kuwa contaminated ni nini???

“The study by Jadavpur University's School of Environmental Studies says the region's groundwater is contaminated with the cancer-causing chemical which gets into paddy through contaminated water. Cattle that feed on contaminated paddy husk and water produce dung that is likely to contain arsenic.”

Inaonekana chemical ambazo ni hatari kutoka migodini zinaingia kwenye mifumo ya maisha ya maeneo husika kama kwenye nyasi na hizo nyasi zikiliwa na hao ng’ombe hatimaye wanazitoa kupitia kinyesi ambacho kinaenda kwenye maji. Ila watoa reporti wamehongwa hela waseme tu uhusika ule wa mwisho. Kumbukeni pia tofauti na Dkt Magufuli aliyekuwa anahakikisha haki za watanzania zinalindwa, Mama yeye anahakikisha haki za muwekezaji zinalindwa kwanza hata kama watanzania itabidi wafe. Hiyo ripoti imetengenezwa kulinda muwekezaji.
 
Najiuliza tu kama huo mto Mara unamwaga maji mahali ambapo ni muhimu sio tu kwa uchumi wa nchi yetu bali hata jirani zetu, je tume haikuona kuwa majibu fulani yanaweza kudraw public attention na hata watu/soko letu kutilia shaka kuwa kuna kitu kinafichwa?

Au tume haikufuata taratibu na kukimbilia kutoa report kwa wanasiasa!!
 
Haingii akilini.
Kwani wakurya wameanza kufuga ng'ombe Jana au juzi.
Hizi rushwa ndogo ndogo hizi zitawapeleka jehanum.
Mabeberu wamewaambia semeni ni mifugo ili wakurya wahame na mifugo Yao.
A full professor could not see this trick because of two million shillings.
Kumbe 2m ndio imefanya awauze watanzania wenzake..insikitisha sana.

#MaendeleoHayanaChama
 
Samadi ( ni biomass) ikiwa na C H O na trace element Ikivunda bila hewa uzalisha gesi ukaa ch4. Gesi hii nyepesi, upaa mawingu ki urahisi! Pia samadi ikiingia mtoni usababisha uwepo wa wadudu walao hewa ya o2 iliyomo majini na ambayo utumiwa na samaki... sijui nimechanganya madesa!
Uko sawa..ila tambua huo ni mto sio bwawa..manake flow ya maji mapya kila mda so hilo la samadi haliwezi kuwa tatizo..inshu hapo inawezekana ni utando wa mafuta juu ya maji ama kemikali.

Ila kuhusu samadi inayo decompose hapo tumepigwa na kitu kizito.


#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom