Kamati: Kinyesi na Mikojo ya Mifugo ndiyo chanzo cha kufa samaki mto Mara, sio sumu ya maji ya Migodini

Kamati: Kinyesi na Mikojo ya Mifugo ndiyo chanzo cha kufa samaki mto Mara, sio sumu ya maji ya Migodini

Acha hizoo...!
Hao ng'ombe wameanza leo kufaulisha kinyesi mto Mara?
Tunaongelea mambo mengi sana kwa wakati mmoja..

Kama kinyesi / mbolea inaweza kupelekea vifo vya viumbe hai kwenye maji haimaanishi kwamba ndicho kilichotokea Mara..., Na kama sicho kilichotokea Mara haimaanishi kwamba wingi wa mbolea / samadi kwenye vyanzo vya maji hakuwezi kuleta madhara...

Tuongelee vitu katika utenganisho ama sivyo tunaweza kujikuta tunakataa theory fulani sababu haikutokea sehemu fulani wakati hio theory ina ukweli (inaweza kutokea)
 
Kwamba ng'ombe mara wanakula sumu ndiyo maana kinyesi kina sumu?
Sumu ni nini ?

Mbolea kwenye mimea ni chakula, mbolea kwenye maji pia ni chakula cha algae ambacho baadhi ya samaki mfano Tilapia wanakula..., sasa mbolea ikizidi algae wakazidi wakati hakuna jua la kutosha (photosynthesis) ili algae watengeneze oxygen dissolved oxygen kwenye maji inapungua..., Oxygen ikipungua nadhani you know what will happen
 
Ngombe hawa hawa wa mara mmoja anakunya kinyesi cha kg 25 na mkojo lita 21..???

Hivi wanaficha nini kwa manufaa ya nani?..hivi hiyo mifugo imeanza kufungwa mwaka huu maeneo hayo..mbona hayakuwahi kutokea hayo.?

Nadiriki kusema hii ni moja ya kamati za michongo...hivi wanadhani watanzania wasasa ni vilaza sana kwamba hawajui kuhoji au ku reason.

Eti mwenyekiti wa kamati ni professor..daah hii nchi kuna mambo yanakera sana..

Hivi hamna huruma na wananchi kansa kila uchwao zinaongezeka kanda ya ziwa..magonjwa ya ajabu ajabu..sasa hadi samaki wanakufa..ila mnaleta ngonjera.

#MaendeleoHayanaChama
Mimi pia nimeshangaa sana kusoma ripoti hii ya ajabu ya Profesa

Na mimi kiasili natoka jamii ya wafugaji kanda ya ziwa

Ila hili la ng'ombe kunya kilo 25 na kukojoa mkojo lita 21 kwa siku HAKIKA NI UONGO wa mchana kweupe!

Hakuna ng'ombe wa kunya kilo 25 na mkojo lita 21 kwa siku huku kanda ya ziwa. Huyu profesa ni mwongo. Kuna kitu hakiko sawa, wanaficha jambo hawa!!

Hawa ng'ombe wamekuwa ni tembo wanye mavi ya namna hiyo kwa siku?

Na ina maana profesa huyu anataka kutuambia kubwa hawa ng'ombe walikuwa wananyea mavi na kukojolea mkojo huo ndani ya mto kila siku?

Na hizo mvua ndo zimeanza kunyesha mwaka huu huko Mara? Miaka mingine hakujawahi kuwa na mvua? Kwanini hakukutokea maafa ya namna hii?

Na hao ng'ombe 300,000 tu ndiyo wameanza kufugwa mwaka huu huko Mara?

Ni kweli kabisa hii ripoti ni ya uongo. Ni ya kupika na kuuficha ukweli halisi ambao wameuona.

Kuna mawili kuihusu kamati hii;

AIDHA
Hawana utaalamu wa kuchunguza jambo hili

AU

Kwa sababu aidha kuhongwa na wahalifu hao, wameamua kuuficha ukweli wa jambo hili kwa maslahi yao na ya wahalifu hao wa mazingira!
 
Sumu ni nini ?

Mbolea kwenye mimea ni chakula, mbolea kwenye maji pia ni chakula cha algae ambacho baadhi ya samaki mfano Tilapia wanakula..., sasa mbolea ikizidi algae wakazidi wakati hakuna jua la kutosha (photosynthesis) ili algae watengeneze oxygen dissolved oxygen kwenye maji inapungua..., Oxygen ikipungua nadhani you know what will happen
Labda uniambie Huwaga watu wanabeba malori ya kinyesi cha ngombe na mikojo kwenda kumwaga kwenye ule mto ila kinyesi cha ng'ombe wa malisho wa kawaida hawa wawe wengi vipi kamwe hakiwezi kuleta shida... maji yanamove muda wote accumulation ya kinyesi mpaka kuleta hio athari inatokea wapi??? Ni upuuzi wa hali ya juu wazri kupokea na kukubali ripoti ile
 
Labda uniambie Huwaga watu wanabeba malori ya kinyesi cha ngombe na mikojo kwenda kumwaga kwenye ule mto ila kinyesi cha ng'ombe wa malisho wa kawaida hawa wawe wengi vipi kamwe hakiwezi kuleta shida... maji yanamove muda wote accumulation ya kinyesi mpaka kuleta hio athari inatokea wapi??? Ni upuuzi wa hali ya juu wazri kupokea na kukubali ripoti ile
Sijibu issue iliyotokea mto Mara, najibu watu wanaosema Kinyesi hakiwezi kuleta madhara..., Ndio maana nikasema kuanzia mwanzo huyu Bwana apingwe specifically kulingana na sehemu aliyofanya hio Kazi ila sio kupinga uwezekano wa jambo kama hilo kutokea.... Na hapa nilikuwa najibu Uzi kwamba Kinyesi cha Mifugo ya Mara kina Sumu....
 
Musoma. Kamati maalum ya kitaifa iliyoundwa na serikali kuchunguza mabadiliko ya maji ndani ya mto Mara, imetoa taarifa ya chanzo cha mabadiliko katika mto huo yaliyosababisha maji kuwa meusi na kutoa harufu, huku samaki wakifa ambapo chanzo kimeelezwa kuwa ni shughuli za binadamu pamoja na nguvu za asili.

Akitoa matokeo ya uchunguzi leo Jumamosi Machi 19, 2022 mjini Musoma, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Samuel Manyele amesema kuwa hali hiyo imetokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kinyesi cha mifugo mtoni pamoja na uozo wa mimea ndani ya mto hasa mimea vamizi kama vile magugu maji na matete.

Amesema kuwa hali hiyo ilisababisha kupungua kwa kiasi kikubwa kiwango cha oksijeni ndani ya mto na hivyo maji kubadilika rangi na kuwa na harufu mbaya huku samaki wakikosa chakula na hivyo kusababisha vifo vyao.

Hata hivyo, amekanusha picha zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zilizokuwa zikionyesha samaki wakiwa wamekufa kwa wingi, akisema sio kutoka mkoani Mara.

Amesema kuwa kwa mujibu wa uchunguzi waliofanyana walibaini kuwa mabadiliko hayo ni matokeo ya mvua kubwa iliyonyesha ghafla kwa muda mfupi katika kipindi cha mwezi huu hivyo kutibua uchafu uliokuwa umejikusanya chini ya mto kwa muda mrefu.

"Mvua zingeendelea kunyesha hali hii ingeisha kwani uchafu ungetiririshwa lakini kwa vile mvua zimenyesha na kukatika ghafla ina maana uchafu ule unatoka taratibu na hii hali inaweza kudumu kwa zaidi ya miezi mitatu hadi minne endapo mvua hazitanyesha hapa katikakati," amesema.

Profesa Manyele amesema kuwa mto huo umeathiriwa kuanzia katika kijiji cha Marasibora wilayani Rorya na kijiji cha Wegero wilayani Butiama huku akisema kuwa mgodi wa dhahabu wa Barrick North Mara hauhusiki na uchafuzi huo.

"Mgodi upo mbali sana na maeneo yaliyoathirika na hata kama uchafu unaozalishwa mgodini pale ungezidishwa mara ishirini na kumwagwa mtoni maji yasingebadilika rangi wala kuwa katika hali iivyo sasa na maji ya mto kelekea kule mgodini ni masafi na hayana shida yoyote," amesema.

Amesema kuwa wamebaini uwepo wa kinyesi cha ng'ombe zaidi ya tani 1.8 milioni pamoja na mkojo wa ng'ombe lita 1.5 bilioni uchafu uliotokana na kuwepo kwa ng'ombe zaidi ya laki 3 waliokuwepo katika eneo oevu la mto Mara kwa kipindi cha miezi minane mwaka jana wakati wa kiangazi.

"Ng'ombe mmoja ana toa kilo 25 za kinyesi kwa siku moja na mkojo lita 21 kwa siku kwahiyo ukizidisha kwa idadi hiyo ya ng'ombe mara miezi minane utapata kiwango hicho na hapo bado hatujaweka kinyesi na mkojo wa kondoo, mbuzi na punda," amesema.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Suleiman Jafo ametoa muda wa siku mbili kwa kamati hiyo kuandaa taarifa kamili yenye mpango kazi juu ya nini kifanyike na muhusika ni nani kisha taarifa hiyo ikabidhiwe kwake kwaajili ya utekelezaji.

"Hii taarifa imenipa faraja baada ya uchunguzi kubaini kuwa hakuna kemikali mtoni maana kama kungekuwa na kemikali hii ingekuwa ni habari mbaya sana lakini taarifa hii inaonyesha kuwa tuna kazi kubwa sana ya kufanya ili mto uweze kuendelea kuwepo na tusipochukua hatua za haraka mto unaweza kupotea," amesema Jafo.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma;

1).Vifo vya Samaki Mto Mara: Kamati ya Dharura yaundwa kuchunguza Samaki wanaodaiwa kufa kwa Sumu

2). Madai ya sumu Mto Mara kutoka migodini, wananchi wazuiwa kutumia maji, kula samaki, uvuvi, Serikali yatoa tamko
View attachment 2157025
Watanzania kweli watawala wanatuona wasenge na mazoba hivi kweli
 
Sumu ni nini ?

Mbolea kwenye mimea ni chakula, mbolea kwenye maji pia ni chakula cha algae ambacho baadhi ya samaki mfano Tilapia wanakula..., sasa mbolea ikizidi algae wakazidi wakati hakuna jua la kutosha (photosynthesis) ili algae watengeneze oxygen dissolved oxygen kwenye maji inapungua..., Oxygen ikipungua nadhani you know what will happen
Kwa hiyo ni kwa ajili ya Mara pekee?
 
Wananchi hapo wangemnywesha kwanza hayo maji kama kweli hayana sumu,na kiongozi wa nchi hana habari ...........................
 
Kwa hiyo ni kwa ajili ya Mara pekee?
Again siongelei kilichotokea Mara naongelea kama jambo kama hilo linaweza kutokea..., In short animal waste ni moja ya chanzo kikubwa sana katika uharibu wa vyanzo vya maji duniani (ingawa hii inaletelezwa sana na concentrated animal farming) kwenye free grazing hili sio tatizo kubwa as kinyesi kinakuwa absorbed kama mbolea hata kabla ya kufikia water bodies
 
Again siongelei kilichotokea Mara naongelea kama jambo kama hilo linaweza kutokea..., In short animal waste ni moja ya chanzo kikubwa sana katika uharibu wa vyanzo vya maji duniani (ingawa hii inaletelezwa sana na concentrated animal farming) kwenye free grazing hili sio tatizo kubwa as kinyesi kinakuwa absorbed kama mbolea hata kabla ya kufikia water bodies
Sawa mkuu
 
Ni up.umbavu wa hali juu kufikiria kuwa eti kuna sumu za mgodini zingesababisha samaki kufa mto Mara. Ni fikra za kijinga kabisa kutoka kwa wajinga wasiojua chochote kuhusiana na shughuli za mineral processing...
Comment ya mchongo.
 
Tunaongelea mambo mengi sana kwa wakati mmoja..

Kama kinyesi / mbolea inaweza kupelekea vifo vya viumbe hai kwenye maji haimaanishi kwamba ndicho kilichotokea Mara..., Na kama sicho kilichotokea Mara haimaanishi kwamba wingi wa mbolea / samadi kwenye vyanzo vya maji hakuwezi kuleta madhara...

Tuongelee vitu katika utenganisho ama sivyo tunaweza kujikuta tunakataa theory fulani sababu haikutokea sehemu fulani wakati hio theory ina ukweli (inaweza kutokea)
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, mtu akikuambia mambo ya ovyo, na wewe unajua ni ya ovyo, na yeye anajua amakumbia ya ovyo, basi mtu huyo amekudharau sana.
 
Umekazana ni "Matusi kwa Rais,"

Mimi nakwambia hayo ni Matusi kwa wananchi ambao wanategemea mto huo kwenye maisha yao ya kila siku.

Rais wako ategemei chochote kutoka kwenye huo Mto.


Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa mkuu wananchi hata wakionewa hawana cha kufanya kamati imetoa majibu ya kipuuzi wakiamini Rais ni wa kumtania na kumchukulia poaa...!! Na kweli ametaniwa na kuchukulia poa amebaki anashangaa tuu
 
Back
Top Bottom