Kamati kuu ya CCM yakutana Mwanza: Yampongeza Rais Magufuli, Walio hama vyama vya Upinzani waongeza Ruzuku ya chama hadi Bil 13

Kamati kuu ya CCM yakutana Mwanza: Yampongeza Rais Magufuli, Walio hama vyama vya Upinzani waongeza Ruzuku ya chama hadi Bil 13

Rais Magufuli anahitaji pongezi na sio kwa CCM tu, hata wapinzani, na Watanzania wote hata wasioukua na mlengo wowote kichama.
Kwa sasa anapongezwa Afrika yote, ametenda, anatenda na atatenda, tunamuombea kwa Mungu ampe nguvu na uwezo maana kazi iliyo mbele yake inamuhitaji kwa sana, leo hii akiamua kuachia madaraka, sitegemei kama kunaye atakuja mwenye utashi wa kutekeleza haya ya leo.
Kipofu kama wewe utakuta hajawahi kukubambikiza hata kakesi kamoja!

Kuna vipofu wenzio boarders walikuwa waimba mapambio kama wewe wiki tatu/nne zilizopita kaenda kuwapora hela! Pambio zoote kwisha zimebaki laana tuu!

Ngozi nyeusi INA matatizo, usipoguswa unaona wanao onewa wanastahili, tatizo ni akili ndogo, ukiguswa wewe tuu unaanza laana!
 
CCM.jpg

Mwenyekiti wa CCM Dr Magufuli amewashukuru wajumbe wa halmashauri kuu ya chama hichi kwa maamuzi mbalimbali waliyoyachukua katika kuleta mabadiliko.

Kwa mfano kamati ya kufuatilia mali za chama iliyoongozwa na Dr Bashiru iligundua ufisadi mkubwa kwenye mali za chama.

Baada ya kamati ya Dr Bashiru kumaliza kazi yake tumefanikiwa kurejesha mali nyingi mikononi mwa chama na kurekebisha baadhi ya mikataba ikiwemo ya Vodacom na jengo la HQ ya UVCCM.

Pia kituo cha habari cha Channel ten kimerejeshwa chamani.

Kwa sasa mapato ya CCM ni zaidi ya sh bilioni 59 kwa mwaka na thamani ya mali zake ni zaidi ya sh bilioni 900

Kadhalika Dr Magufuli amewapongeza wanaccm kwa kuwapokea wabunge na madiwani waliotokea upinzani kwani ujio wao umeiongezea ruzuku CCM kutoka sh bilioni 12 mwaka 2015/16 hadi zaidi ya sh bilioni 13 mwaka 2018/19

Dr. Magufuli anaihutubia NEC ya CCM jijini Mwanza muda huu na tukio liko mubashara Channel ten.

Mzee Pinda amesema japo katiba hairuhusu lakini kutokana na utendaji uliotukuka wa Rais Magufuli anamuomba Rais Magufuli atawale walau kwa miaka 15 badala ya ile 10 ya kikatiba.......japo anaamini kuwa Dr Magufuli hawezi kukubali.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama
 
Chadema inaomba maridhiano ya nini sasa wakati nihaki yao,yani mtu anakuzuia kufanya mikutano ya siasa bado makesi kibao wamewabambikia kinyume na sheria afu unaomba maridhiano ya kitu gan sasa
 
johnthebaptist,
Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi ndiye Rais wa nchi, kwa hiyo anaposimama automatically CCM nayo ipo hapo hapo na inachanja mbunga... hii kidogo inaleta ukakasi.

Katiba yetu iwe wazi kwamba mgombea kiti cha Urais asiwe mwenyekiti wa chama chochote cha siasa....hii itaondoka kitu kinachoitwa conflict of interest. Huyu anatakiwa kututumika sisi wananchi kwa 100%.

Hata kwenye katiba yetu hakuna kifungu kinasema Rais atawajibika kwa kukiongoza chama chake cha siasa.
 
Kwa sisi tulioishi miaka ya muuaji Idd Amin, haya hatuyashangai. Inafika mahali dikiteita anaua watu na kupandikiza hofu kiasi kwamba kila moja anakuwa kama mbwa katika kufikiri. Lumumba wote na 98% ya watanzania ni kama mbwa anavyotingisha mkia kama ishara ya utii kwa boss wake
Nachompea Rais wetu anayaanyoosha hadi ma CCM menyewe yamebaki yanaimba nyimbo za pongezi huku yanatukana kimoyo moyo teh tehe tehe huu mwaka tumekamatika wote.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hotuba ya jiwe a.k.a jitabonga' kuhusu demokrasia kwa wale walioomba maridhiano bora wafanye mengine maana hakuna kitakachobadirika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kamati ya kijani imekutana ili walipane posho pesa za walipakodi walalahoi
 
Rais Magufuli anahitaji pongezi na sio kwa CCM tu, hata wapinzani, na Watanzania wote hata wasioukua na mlengo wowote kichama.
Kwa sasa anapongezwa Afrika yote, ametenda, anatenda na atatenda, tunamuombea kwa Mungu ampe nguvu na uwezo maana kazi iliyo mbele yake inamuhitaji kwa sana, leo hii akiamua kuachia madaraka, sitegemei kama kunaye atakuja mwenye utashi wa kutekeleza haya ya leo.
Hivi ni hao hao CCM wa awamu ya pili , ya tatu na nne ndo wanapongeza ama wengine? Maana sijawahi kiwaelewa walivyokuwa wanagawana mali za nchi hadi mafuriko yakawatia adabu .mie ni kindakindaki na Magufuli ila huwa sina imani na kijani labda baadhi ya wateule wa Magu kama Bashiru na baadhi tu ila as a whole CCM siwaelewagi kabisa
 
JPM bhana anaogpe mpka na kuku majuzi yale mkurugezi hati aliapia kwa jila na Mwenye ulimwangu wake(MUNGU) kuwa atapeleka matofali siku inayofuata mbele ya magu nachofurahi wote tunateseka kasoro konda boy(daby)

Sent from my TECNO LC6 using Tapatalk
 
Back
Top Bottom