Kamati kuu ya CCM yakutana Mwanza: Yampongeza Rais Magufuli, Walio hama vyama vya Upinzani waongeza Ruzuku ya chama hadi Bil 13

Kamati kuu ya CCM yakutana Mwanza: Yampongeza Rais Magufuli, Walio hama vyama vya Upinzani waongeza Ruzuku ya chama hadi Bil 13

Pinda ni hovyo sana...kumbe CCM WAMENUNUA MADIWANI NA WABUNGE ILI KUONGEZA RUZUKU KWENYE CHAMA CHAO....CCM FANYENI BIASHARA SIASA ZIMEWASHINDA KABISAAAAAA
 
Kamati kuu ya CCM imekutana jijini Mwanza na kuongozwa na Mwenyekiti wake Dr Magufuli.

Kamati kuu imempongeza Rais Magufuli na serikali yake kwa ujenzi wa miradi mikubwa inayoendelea nchini.
Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru amesema kwa sasa hakuna kikwazo chochote kinachoweza kupunguza kasi ya chama na serikali yake katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Dr Bashiru amewataka watanzania kuendelea kuwa na umoja huu tulionao sasa kwani umoja na amani iliyopo ndio vimewezesha kupatikana kwa haya maendeleo makubwa tunayoyashuhudia.

Source Uhuru

Maendeleo hayana vyama!
Ujinga mtupu wa kale. Yaan kamati inaitishwa kwa ajili ya kupongezana
 
Mwenyekiti wa CCM Dr Magufuli amewashukuru wajumbe wa halmashauri kuu ya chama hichi kwa maamuzi mbalimbali waliyoyachukua katika kuleta mabadiliko.

Kwa mfano kamati ya kufuatilia mali za chama iliyoongozwa na Dr Bashiru iligundua ufisadi mkubwa kwenye mali za chama.

Baada ya kamati ya Dr Bashiru kumaliza kazi yake tumefanikiwa kurejesha mali nyingi mikononi mwa chama na kurekebisha baadhi ya mikataba ikiwemo ya Vodacom na jengo la HQ ya UVCCM.

Pia kituo cha habari cha Channel ten kimerejeshwa chamani.

Kwa sasa mapato ya CCM ni zaidi ya sh bilioni 59 kwa mwaka na thamani ya mali zake ni zaidi ya sh bilioni 900

Kadhalika Dr Magufuli amewapongeza wanaccm kwa kuwapokea wabunge na madiwani waliotokea upinzani kwani ujio wao umeiongezea ruzuku CCM kutoka sh bilioni 12 mwaka 2015/16 hadi zaidi ya sh bilioni 13 mwaka 2018/19

Dr. Magufuli anaihutubia NEC ya CCM jijini Mwanza muda huu na tukio liko mubashara Channel ten.

Mzee Pinda amesema japo katiba hairuhusu lakini kutokana na utendaji uliotukuka wa Rais Magufuli anamuomba Rais Magufuli atawale walau kwa miaka 15 badala ya ile 10 ya kikatiba.......japo anaamini kuwa Dr Magufuli hawezi kukubali.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama
Na CCM imetumia sh.ngapi kuwanunua tujue kama tumepata faida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazee ni hazina kwa taifa..

Mzee Pinda katoa dira..Watanzania tumuunge mkono.

Kwa hakika watanzania tumebarikiwa sana
 
Mwenyekiti wa CCM Dr Magufuli amewashukuru wajumbe wa halmashauri kuu ya chama hichi kwa maamuzi mbalimbali waliyoyachukua katika kuleta mabadiliko.

Kwa mfano kamati ya kufuatilia mali za chama iliyoongozwa na Dr Bashiru iligundua ufisadi mkubwa kwenye mali za chama.

Baada ya kamati ya Dr Bashiru kumaliza kazi yake tumefanikiwa kurejesha mali nyingi mikononi mwa chama na kurekebisha baadhi ya mikataba ikiwemo ya Vodacom na jengo la HQ ya UVCCM.

Pia kituo cha habari cha Channel ten kimerejeshwa chamani.

Kwa sasa mapato ya CCM ni zaidi ya sh bilioni 59 kwa mwaka na thamani ya mali zake ni zaidi ya sh bilioni 900

Kadhalika Dr Magufuli amewapongeza wanaccm kwa kuwapokea wabunge na madiwani waliotokea upinzani kwani ujio wao umeiongezea ruzuku CCM kutoka sh bilioni 12 mwaka 2015/16 hadi zaidi ya sh bilioni 13 mwaka 2018/19

Dr. Magufuli anaihutubia NEC ya CCM jijini Mwanza muda huu na tukio liko mubashara Channel ten.

Mzee Pinda amesema japo katiba hairuhusu lakini kutokana na utendaji uliotukuka wa Rais Magufuli anamuomba Rais Magufuli atawale walau kwa miaka 15 badala ya ile 10 ya kikatiba.......japo anaamini kuwa Dr Magufuli hawezi kukubali.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama
viva jonh
 
Back
Top Bottom