Kamati ya bunge yampongeza rais Samia kwa fedha za miradi ya REGROW

Kamati ya bunge yampongeza rais Samia kwa fedha za miradi ya REGROW

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
590
Reaction score
807
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ikiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Timotheo Mnzava (Mb)imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajenda yake ya kukuza utalii ikiwemo katika miradi ya ujenzi wa kituo cha utalii kwa gharama ya shilingi bilioni 21.4 na kituo cha utafiti kwa shilingi bilioni 1.55 chini ya mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW), Kihesa Kilolo Mkoani Iringa.

Ameyasema hayo leo Septemba 7, 2024 wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika miradi hiyo mkoani Iringa.

“Kwa ujumla kama Kamati tunaendelea kuipongeza Serikali, kumpongeza Rais Samia kwa namna ambavyo anaendelea kusimamia na kutekeleza shughuli mbalimbali za nchi yetu ikiwemo ajenda yake kubwa ya kukuza utalii” amesisitiza Mhe. Mnzava.

Amefafanua kuwa kamati imeishauri Serikali kusimamia miradi hiyo ili ikamilike kwa ufanisi wa hali ya juu na kwa wakati ambapo kwa upande wa Kituo cha utafiti amesema sehemu kubwa ya kazi ya ujenzi wa kituo hicho inakwenda vizuri huku akimuelekeza mkandarasi wa ujenzi wa kituo cha utalii kutimiza wajibu wake ili kukamilisha kazi hiyo.

Naye, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa fedha za miradi hiyo huku akisisitiza kuwa ni wajibu wa Wizara ya Maliasili na Utalii kusimamia miradi hiyo itekelezwe kwa wakati.

Mhe. Chana ametoa rai kwa Wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kusimamia mikataba yao na kukamilisha miradi kwa wakati.

“Nitoe angalizo kwa Wakandarasi walio kwenye miradi ya Wizara ya Maliasili na Utalii ni muhimu sana kutekeleza miradi kutokana na mikataba tuliyowekeana ili ikamilike kwa wakati” amesema.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Malisili na Utaklii iko Mkoani Iringa kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa miradi iliyo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.
IMG-20240908-WA0015.jpg
IMG-20240908-WA0013.jpg
IMG-20240908-WA0012.jpg
IMG-20240908-WA0011.jpg
IMG-20240908-WA0009.jpg
IMG-20240908-WA0010.jpg
IMG-20240908-WA0006.jpg
 
Kwamba news ni kupongeza na sio pro / cons au faida ya mradi deadline na vipi itanuifaisha na kwanini mradi huu na sio mwingine

Kila kitu kimekuwa propaganda
 
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ikiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Timotheo Mnzava (Mb) imeridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali iliyo chini ya Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW) inayotekelezwa ndani ya Hifadhi ya Taifa Ruaha huku ikiitaka Wizara ya Maliasili na Utalii na Menejimenti ya Ruaha kuwa wabunifu kufanya maboresho yatakayoiongezea mapato Hifadhi ya Taifa Ruaha.

Ameyasema hayo leo Septemba 8, 2024 wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ya kukagua miradi ya ujenzi wa kituo cha ikolojia- Ibuguziwa, kituo cha utoaji taarifa kwa wageni,uwanja wa ndege wa Kiganga, ujenzi wa malazi ya watalii (cottage), malazi ya madereva na hosteli za wanafunzi za hifadhi hiyo Mkoani Iringa.

"Kutokana na ukubwa na umuhimu wa hifadhi hii, tuongeze ubunifu na maarifa ili kurahisisha watalii kufika kwa kuboresha miundombinu ya barabara na kuongeza njia za kuingilia hifadhini" amesema Mhe. Mnzava.

Aidha, ameweka msisito katika usimamizi wa miradi hiyo kuhakikisha inakamilika kwa wakati.

Naye, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) ameishukuru kamati hiyo kwa maoni ya kuboresha hifadhi hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi.

Mhe. Chana ameendelea kutoa rai kwa wakandarasi wote waliokabidhiwa miradi iliyo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kukamilisha miradi hiyo kwa wakati kama ilivyo katika mikataba yao.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii inaendelea na ziara ya kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW).
IMG-20240909-WA0013.jpg
IMG-20240909-WA0012.jpg
IMG-20240909-WA0011.jpg
IMG-20240909-WA0010.jpg
IMG-20240909-WA0009.jpg
IMG-20240909-WA0008.jpg
IMG-20240909-WA0007.jpg
IMG-20240909-WA0006.jpg

 

KAMATI YA BUNGE YAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA FEDHA ZA MIRADI YA REGROW

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ikiongozwa na Mwenyekiti, Mhe. Timotheo Mnzava (Mb)imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajenda yake ya kukuza utalii ikiwemo katika miradi ya ujenzi wa kituo cha utalii kwa gharama ya shilingi bilioni 21.4 na kituo cha utafiti kwa shilingi bilioni 1.55 chini ya mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW), Kihesa Kilolo Mkoani Iringa.

Ameyasema hayo leo Septemba 7, 2024 wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika miradi hiyo mkoani Iringa.

“Kwa ujumla kama Kamati tunaendelea kuipongeza Serikali, kumpongeza Rais Samia kwa namna ambavyo anaendelea kusimamia na kutekeleza shughuli mbalimbali za nchi yetu ikiwemo ajenda yake kubwa ya kukuza utalii” amesisitiza Mhe. Mnzava.

Amefafanua kuwa kamati imeishauri Serikali kusimamia miradi hiyo ili ikamilike kwa ufanisi wa hali ya juu na kwa wakati ambapo kwa upande wa Kituo cha utafiti amesema sehemu kubwa ya kazi ya ujenzi wa kituo hicho inakwenda vizuri huku akimuelekeza mkandarasi wa ujenzi wa kituo cha utalii kutimiza wajibu wake ili kukamilisha kazi hiyo.

Naye, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa fedha za miradi hiyo huku akisisitiza kuwa ni wajibu wa Wizara ya Maliasili na Utalii kusimamia miradi hiyo itekelezwe kwa wakati.

Mhe. Chana ametoa rai kwa Wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kusimamia mikataba yao na kukamilisha miradi kwa wakati.

“Nitoe angalizo kwa Wakandarasi walio kwenye miradi ya Wizara ya Maliasili na Utalii ni muhimu sana kutekeleza miradi kutokana na mikataba tuliyowekeana ili ikamilike kwa wakati” amesema.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Malisili na Utaklii iko Mkoani Iringa kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa miradi iliyo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.


WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.48.jpeg

WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.49.jpeg
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.51(1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.51(1).jpeg
    315.7 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.51.jpeg
    WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.51.jpeg
    584.2 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.50(1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.50(1).jpeg
    438.6 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.50.jpeg
    WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.50.jpeg
    666.8 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.49(1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.49(1).jpeg
    465.9 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.52.jpeg
    WhatsApp Image 2024-09-07 at 18.51.52.jpeg
    108.9 KB · Views: 2
Back
Top Bottom