Kamati ya Mambo ya Nje ya Umoja wa Ulaya (EU) wataka kujua msaada wa Euro Mil. 27 za COVID-19 kwa Tanzania uliahidiwa kwa vigezo gani?

Sijaona hata kilichokufurahisha hapo! Tanzania ni nchi huru, tusipangiane vitu vyakufanya! Ukoloni ulikoma tarehe 9.12.1961!
Unaefurahia hayo, hutokuwa salama kabisa siku yakija mabaya!
Kama wewe ni huru ungeenda kutembeza bakuli kwao kudai unaomba hela za covid wakati umetangaza kuwa huna covid kilaza wewe??😂😂😂
 
Nikikuambia watu wanadaiwa kuwa ni "Wanyonge" ndio "wanaonyongwa" na Ndio mtaji wa Mwenye kupenda kutumia tabaka hilo kufanya yake kwa maslahi yake Utaidigest vipi?
Sisi wanyonge tunafurahia kuongezeka kwa fursa za biashara, na kutokusumbuliwa pale tu tunapokuwa tuna
Kama wapinzani walienda na kura fake kwenye vituo vya kupigia kura hiyo ni very serious crime,sasa kwa nini serekali haikuwachukulia hatua?
Ndio maana walikamatwa na kuondolewa kwenye vituo, wakatumia ubinadamu na kuwaachia huru 😀
 
Tangu lini Dona kantri inalilia misaada? Tujiandae Tu maana wanywa ARV wengi wako mjengoni.
ARV za watu wa mjengoni ni Made in Spain na Italy....ghali sana na ndio maana haziletwi kwa msaada wa watu wa Marekani...shemeji yako na Baba Mkwe wako na mimi ndio tutaumia tunaotumia ARV made in India za bei ya chini!
 
Rafiki mkubwa na mdau mkubwa wa maendeleo wa Tanzania kwa sasa hivi eti ni Zimbabwe![emoji1782]

Hii ni wazi sasa hata kwa mtoto wa chekechea kuwa Tanzania inaongozwa na goigoi
 
Nasubiri tamko la Kalamaganda Kabugi dhidi ya MABEBERU UCHWARA WA MAULAYA!
😅
👊 ✌️✌️✌️💥
 
Wazungu wanatulegeza kwa kutumia misaada. Marekani na Ulaya wanategemea mataifa mengine ku survive, wakiisusia Tanzania wanaacha nafasi kwa China na uturuki kunufaika, sio wajinga wa hivyo, wataleta tu hata kama sio kama EU lakini watakuja kama Ujerumani, Ubelgiji, ufaransa, uholanzi, uingereza, sweden, nk.
 
Wazungu wanatulegeza kwa kutumia misaada. Marekani na Ulaya wanategemea mataifa mengine ku survive, wakiisusia Tanzania wanaacha nafasi kwa China na uturuki kunufaika, sio wajinga wa hivyo, wataleta tu
China huyu mliyekamata bank yake Leo?? Au yupi???
 
Ukiangalia kuanzia 1995 mpaka 2015 tulikuwa tunakwenda vizuri na huko Unguja ikafika hata Serikali ya Umoja wa kitaifa.

Kwa huku bara tulihitilafiana lakini hatukufikia kiwango hiki.

Wote waliopita hakuna aliyeomba ya kuwa Upinzani ufe,kote tulikopita hakuna aliyetamani kuifunga mitandao ya kijamii (zilitunga sheria kuhakikisha ya kuwa uhuru huu hautumiki vibaya).

Leo kupata habari za mrengo tofauti na serikali ni labda uingie twitter na JF kidogo.TV station zote zipo upande mmoja.

Kama umechora graph utagundua ya kuwa tunaelekea katika kuporomoka katika baadhi ya mambo ya msingi.

Yoyote anayeona mbali ni lazima astuke, hii si dalili nzuri
 
Wachukue kwani bilioni 70 kitu gani?
Nilizani utasema tirioni kadhaa kumbe ni billioni?
Mbona wlikataa kutupa hiyo pesa kipindi caha corona na hatukufa kama walivyotaka?
 


Sasa kama ni hivyo , waambie hao jiwe na kokoto zake wajiuzulu waitishe mkutano na vyama vyote na taasisi za kijamii na viongozi wa dini zote , iundwe tume huru na waitishe uchaguzi mpya ,
 
Sasa kwa taarifa yako jiandae. Wewe na hao mabwana zako. Mtajuta kuiba uchaguzi mwaka huu.

Eti Tanzania haijawai kuwalamba miguu wakati kila siku mbatembeza bakuli kwao kuomba hela za misaaada na mikopo.

Na jiandaeni kula jeuri yenu. Bado ICC sasa
Kwa taarifa zako ni kwamba Tanzania kufuata masharti ya mabwana zenu ndiyo kuliua uchumi wa Tanzania. Wakati JK Nyerere Tanzania ilikuwa ni nchi ya viwanda kuliko sasa, tulikuwa na Tanganyika Packers Dar, Arusha na Shinyanga. Tulikuwa na textile industries Dar, Mwanza, Moro na Mbeya. Mikoa Mwanza na Shinyanga kila wilaya ilikuwa na cotton ginnery zaidi ya moja kwa ajili ya kusindika pamba. Bwana zenu zenu wakaja na sera za Structural Adjustment Program wakashinikiza ubinafsishaji wa mali za umma kwa private sector. Baada ya muda mfupi Bwana zenu waliua viwanda ajira zikapotea, viwanda vikageuka kuwa magodani.
Tumeanza kuweka viwanda wanaanza fyokofyoko. Hatugeuki nyuma sasa hivi. Tuna hela za kutosha kujisimamia bajeti yetu. Sehemu kuuza bidhaa zetu ni nyingi hata tusipoouza US na Ulaya. Kuna India na China.

Sent from my Infinix X655 using JamiiForums mobile app
 
Wachukue kwani bilioni 70 kitu gani?
Nilizani utasema tirioni kadhaa kumbe ni billioni?
Mbona wlikataa kutupa hiyo pesa kipindi caha corona na hatukufa kama walivyotaka?
kitu gani kiliwafanya mzitafune hamkuzirudisha ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…