Kamati ya Ulinzi na Usalama iliyompa silaha muuaji wa Lemax Bar iwajibike

Kamati ya Ulinzi na Usalama iliyompa silaha muuaji wa Lemax Bar iwajibike

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
20210718_12350890313.jpg

Moja kati ya sherehe zake akiwa hai​

Wengi wetu tumeona video na picha zilizosambaa za tukio la Mtu kupigwa risasi akiwa Baa Sinza kwa Remi Dar es salaam usiku wa July 17 2021.

Kwa mujibu wa shuhuda ambae pia ni Rafiki, Kijana aliyepigwa risasi na kufariki anaitwa Gift na alikua amekaa jirani na Alex na alisimama kumtuliza Alex baada ya kuona ameanza kutishia Watu kwa bastola yake, amesema Shuhuda huyu.

“Gift ni Kijana mwenzangu tukifanya kazi Ofisi moja, alikua ana muomba Alex asipige risasi kama vile na kupoteza amani, yani kitendo cha Gift kumsemesha yule Jamaa imekua kama kosa aligeuka akammiminia Gift risasi nyingi kama mbuzi, Gift kuona vile akakimbia lakini akaishiwa nguvu hatua chache tu”

“Tulishindwa kutoa msaada kwa Gift kwa sababu Jamaa mwenye Bastola (Alex) alikua kama amevurugwa Shetani kama amemuingia anageuka anaangalia nani mwingine ampige risasi.

My Take
Nimeambiwa jamaa Alex alipewa kibali cha kutumia bastola miezi kama mitatu iliyopita. Ni dhahiri kwamba kamati haikufanya uchunguzi wa kina kabla ya kutoa kibali. Tukio linaonyesha huyu mtu ana shida kichwani na mwepesi kuvurugwa. Kamati ya Ulinzi iwajibishwe
 
Hakuna haja ya kuilaumu kamati ya Ulinzi kwa hili, Kuna magonjwa ya akili huwa hayajionyeshi kirahisi hadi pale mtu anapokuwa ametumia kitu fulani.

Sasa hapo Kijana Alex huenda alikuwa hajawahi kutumia Kitu Cha Arusha before na amekitumia akili ikavurugwa. Sema Haya mambo ya kumiliki Silaha ni changamoto sana.
 
Huwa hawapimwi akili bali wanaulizwa tu maswali kama

Wewe siyo mwehu?

Hauna faili milembe?

Tukikupa hautopiga watu ovyo?

Mbu wakiingia kwako usiku nao utawapiga risasi?

Maswali kama hayo ndo wanayoulizwa na mengine mengi. Ukijibu yote unapewa kibari
Tanzania tunaishi simple sana
 
Kuna mmoja Sinza bar ya Dolphin anaitwa Wambura kuna siku miaka kadhaa nyuma alileta taharuki na bastola yake. Alimchapa mshkaji ya mkono.
 
Huwa hawapimwi akili bali wanaulizwa tu maswali kama

Wewe siyo mwehu?

Hauna faili milembe?

Tukikupa hautopiga watu ovyo?

Mbu wakiingia kwako usiku nao utawapiga risasi?

Maswali kama hayo ndo wanayoulizwa na mengine mengi. Ukijibu yote unapewa kibari

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wengi wetu tumeona video na picha zilizosambaa za tukio la Mtu kupigwa risasi akiwa Baa Sinza kwa Remi Dar es salaam usiku wa July 17 2021.

Kwa mujibu wa shuhuda ambae pia ni Rafiki, Kijana aliyepigwa risasi na kufariki anaitwa Gift na alikua amekaa jirani na Alex na alisimama kumtuliza Alex baada ya kuona ameanza kutishia Watu kwa bastola yake, amesema Shuhuda huyu.

“Gift ni Kijana mwenzangu tukifanya kazi Ofisi moja, alikua ana muomba Alex asipige risasi kama vile na kupoteza amani, yani kitendo cha Gift kumsemesha yule Jamaa imekua kama kosa aligeuka akammiminia Gift risasi nyingi kama mbuzi, Gift kuona vile akakimbia lakini akaishiwa nguvu hatua chache tu”

“Tulishindwa kutoa msaada kwa Gift kwa sababu Jamaa mwenye Bastola (Alex) alikua kama amevurugwa Shetani kama amemuingia anageuka anaangalia nani mwingine ampige risasi.

My Take

Nimeambiwa jamaa Alex alipewa kibali cha kutumia bastola miezi kama mitatu iliyopita. Ni dhahiri kwamba kamati haikufanya uchunguzi wa kina kabla ya kutoa kibali. Tukio linaonyesha huyu mtu ana shida kichwani na mwepesi kuvurugwa. Kamati ya Ulinzi iwajibishwe
Inauma sana aisee
 
Hakuna haja ya kuilaumu kamati ya Ulinzi kwa hili, Kuna magonjwa ya akili huwa hayajionyeshi kirahisi hadi pale mtu anapokuwa ametumia kitu fulani.

Sasa hapo Kijana Alex huenda alikuw hajawahi kutumia Kitu Cha Arusha before, na amekitumia akili ikavurugwa. Sema Haya mambo ya kumiliki Silaha ni changamoto sana.
Wa kulaumiwa ni Kamati ya Maendeleo ya Mtaa kwasababu wanaishi naye na ndiyo wanaotoa taarifa za awali apewe au asipewe...

Kisha ofisi ya Kata na OCD.

Sasa endeleeni kuchagua viongozi punguani wanaoiangalia pesa na siyo dhamana
 
Back
Top Bottom