Kamera za ulinzi kufungwa Kariakoo kwa gharama ya Tsh Milioni 514

Kamera za ulinzi kufungwa Kariakoo kwa gharama ya Tsh Milioni 514

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Katika kuhakikisha biashara zinafanyika saa 24, Jiji la Dar es Salaam limeingia mkataba na Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) unaogharimu jumla ya shilingi milioni 514 wa usimikaji wa mifumo ya kamera za ulinzi katika barabara na maeneo ya Kariakoo ambapo jumla ya kamera 40 zitakazofanya kazi kwa saa 24 zitafungwa katika awamu ya kwanza ya mpango huo kwa ajili ya ufuatiliaji wa hali ya usalama na udhibiti wa matukio ya kihalifu.

Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo amesema lengo la mpango huo ni kuimarisha usalama wa wanachi na wafanyabiashara na kuongeza ufanisi wa shughuli za kibiashara.

Amesema, kamera hizo hizo zitasaidia kurahisisha utambuzi wa matukio, kuimarisha ufuatiliaji wa wahalifu na kutoa ushahidi wa haraka inapohitajika.

My take:

Hawa watu wanaliibia sana hili Taifa na ifike wakati wenye akili kwenye vyombo vya dola waungane na Wananchi Wazalendo wachukuliwe hatua.

Baada ya Wizi mkubwa uliofanywa kwa kuongeza gharama za ujenzi wa viwanja vya michezo, leo umesainiwa mkataba kufunga Kamera 40 tu Kariakoo kwa gharama ya milioni 514.

Acha niendelee kuwaamini CHADEMA kuwa No Reform No Election. Nchi hii inaibiwa sana


FB_IMG_1739887889767.jpg
 
Umoja, amani na utulivu wa waTanzania wote Taifa katika kila kona na pembe ya nchi yetu, vitalindwa kwa nguvu na gharama yoyote bila kujali kelele au mdomo wa kibaka au tapeli yoyote wa kisiasa nchini. :NoGodNo:
Kulinda umoja na amani kwa kuliibia Taifa? Kweli mpo vizuri. Kamera 40 tu kwa Milioni 514?

Kweli CCM mpo vizuri kuliibia Taifa.
 
Kulinda umoja na amani kwa kuliibia Taifa? Kweli mpo vizuri. Kamera 40 tu kwa Milioni 514?

Kweli CCM mpo vizuri kuliibia Taifa.
nadhani ilifaa kua 1 billion kabisa,
kwasababu usalama wa Taifa na wananchi wake ni muhimu sana na gharama yake haipimwi kwa fedha

ni muhimu ikafahamika kwamba kwa nguvu na gharama yoyote ile usalama wa waTanzania utazingatiwa na serikali sikivu ya CCM gentleman bila mbambamba yoyote:NoGodNo:
 
nadhani ilifaa kua 1 billion kabisa,
kwasababu usalama wa Taifa na wananchi wake ni muhimu sana na gharama yake haipimwi kwa fedha

ni muhimu ikafahamika kwamba kwa nguvu na gharama yoyote ile usalama wa waTanzania utazingatiwa na serikali sikivu ya CCM gentleman:NoGodNo:
Sawa pigeni tu pesa za walipakodi wa nchi hii.

Muda utaongea!
 
Tunaposema ni lazima Serikali ya CCM iondolewe madarakani kwa njia zozote zile zinazowezekana tunamaanisha.

Hawa watu wanaliibia sana hili Taifa na ifike wakati wenye akili kwenye vyombo vya dola waungane na Wananchi Wazalendo CCM iondolewe na wachukuliwe hatua.

Baada ya Wizi mkubwa uliofanywa kwa kuongeza gharama za ujenzi wa viwanja vya michezo, leo umesainiwa mkataba kufunga Kamera 40 Kariakoo kwa gharama ya milioni 514.

Acha niendelee kuwaamini CHADEMA kuwa No Reform No Election. Nchi hii inaibiwa sana
View attachment 3240879View attachment 3240880
Kikosi Cha wahuni waliohalalishwa kula
Tunaposema ni lazima Serikali ya CCM iondolewe madarakani kwa njia zozote zile zinazowezekana tunamaanisha.

Hawa watu wanaliibia sana hili Taifa na ifike wakati wenye akili kwenye vyombo vya dola waungane na Wananchi Wazalendo CCM iondolewe na wachukuliwe hatua.

Baada ya Wizi mkubwa uliofanywa kwa kuongeza gharama za ujenzi wa viwanja vya michezo, leo umesainiwa mkataba kufunga Kamera 40 Kariakoo kwa gharama ya milioni 514.

Acha niendelee kuwaamini CHADEMA kuwa No Reform No Election. Nchi hii inaibiwa sana
View attachment 3240879View attachment 3240880
Kikosi Cha wahuni kilichohalalishwa kujibinafsisha uchumi wa nchi hii.
 
Sawa pigeni tu pesa za walipakodi wa nchi hii.

Muda utaongea!
pesa haina maana wala thamani yoyote kwenye kulinda uhai na maisha ya watu hususani kwenye maene ya makazi na biashara za wananchi gentleman,

hakuna mbamabamba kwenye hilo.
halafu ni vizuri wananchi kuepuka na undumilakuwile,

mtu akifa mnlalamika,
usalama wa watu na makazi yao ukiimarishwa mnlalamika,

nini sasa mnataka? :NoGodNo:
 
Ni jambo la uzuri kuweka hapa mchanganuo wote na proposal ilopelekea huyo mzabuni kushinda zabuni.

Pia hata tukifahamu gharama ya kamera moja.

Nani atasimamia hizo CCTV masaa 24?

Ujuzi wao kusimamia CCTV na kadhalika.
 
Tunaposema ni lazima Serikali ya CCM iondolewe madarakani kwa njia zozote zile zinazowezekana tunamaanisha.

Hawa watu wanaliibia sana hili Taifa na ifike wakati wenye akili kwenye vyombo vya dola waungane na Wananchi Wazalendo CCM iondolewe na wachukuliwe hatua.

Baada ya Wizi mkubwa uliofanywa kwa kuongeza gharama za ujenzi wa viwanja vya michezo, leo umesainiwa mkataba kufunga Kamera 40 tu Kariakoo kwa gharama ya milioni 514.

Acha niendelee kuwaamini CHADEMA kuwa No Reform No Election. Nchi hii inaibiwa sana
View attachment 3240879View attachment 3240880
😿😿😿 nchi yangu Tanzania
 
Umoja, amani na utulivu wa waTanzania wote Taifa katika kila kona na pembe ya nchi yetu, vitalindwa kwa nguvu na gharama yoyote bila kujali kelele au mdomo wa kibaka au tapeli yoyote wa kisiasa nchini. :NoGodNo:
Tuichambue M514 alafu tujue zinafungwa kamera gani, watuonyeshe quotation ya hizo bidhaa. Yan kakubali
kabisa kamera million Mia tano?.
Umoja, amani na utulivu wa waTanzania wote Taifa katika kila kona na pembe ya nchi yetu, vitalindwa kwa nguvu na gharama yoyote bila kujali kelele au mdomo wa kibaka au tapeli yoyote wa kisiasa nchini. :NoGodNo:
 
Ni jambo la uzuri kuweka hapa mchanganuo wote na proposal ilopelekea huyo mzabuni kushinda zabuni.

Pia hata tukifahamu gharama ya kamera moja.

Nani atasimamia hizo CCTV masaa 24?

Ujuzi wao kusimamia CCTV na kadhalika.
Gharama za kufunga na kusimamia ni vitu viwili tofauti!

Huwezi kufunga Camera 40 tu kwa milioni 514. Huo ni wizi na dharau kubwa kwa walipa kodi wa Taifa hili.
 
Back
Top Bottom